Whistleblower: Kashfa nzito suala la sukari, wamo vigogo wazito

Whistleblower: Kashfa nzito suala la sukari, wamo vigogo wazito

Sema Majaliwa ni mkurupukaji sana.sijui ni kwa sababu gani.yaani naweza kuamini kwamba hizi tuhuma zinamhusu.maana toka ameanza kuunda tume hakuna iliyowahi kuleta mrejesho.Ananyamazishaga watu kwa kuwambia anaunda tume ichunguze
Kifupi hakuna jambo lolote tangible alishawahi fanikisha kama waziri mkuu. Yupo yupo tu as long as mambo yake yanamwendea.
 
Utakapoandika hayo mengine ukumbuke pia kuwa unayemwandikia ni Mwana CCM...anayajua nje ndani ila sijasema anaweza kuwa pia sehemu yake
Hata sielewi mwandishi anapata wapi ufahamu na uhakika wa kujuwa kwamba anayemwandikia ni tofauti na hao anaoandika juu yao!

Mwandishi anajuaje kwamba anayemwandikia siyo sehemu ya mpango mzima anaounanga?

Kama Magufuli, na hasa Mkapa kawahusisha kwenye mipango hiyo, ni kipi hasa kinachomtofautisha Samia kiasi kwamba mwandishi aamini kuwa yeye yupo tofauti?

Majaliwa, Jenister, na wengine wafanye anayoyasema mwandishi, huyo anayemwandikia asiwe hata na chembe ya taarifa yoyote juu yao?

Wakati sukari ya Uganda imekataliwa Kenya mara kadhaa kwa kujuwa kwamba ni sukari inayotoka nje ya nchi hiyo, Samia yeye bila shaka yoyote kaikubali..., na hana shaka nayo na wala hana haja ya kusisitiza uzalishaji wa ndani ya nchi! Hapo kuna matumaini kweli?
 
Wewe jamaa ni liongo na linafiki. Yaani ktk kujiita mnyetishaji ni muongo kabisa. Huo mradi kwanza ulikwama kwa sababu kuna watu walileta feasibility study ya kubumba na ya kifisadi serikali ikaamua kufumua na kufanya upya. Na hiyo ndiyo sababu ya prof kuondolewa kwa sababu alitoa kazi ya kuandaa plan kishikaji na hao ma prof wa udsm walijifungia ndani na kuandika andiko. So ujue serikali ya Dkt Magufuli ilikuwa makini sana. Acha kupotosha. Huu ujinga wako ni wakitoto sana, kila ulichoandika ni cha kutunga na ni uongo. Nimepuka tu hint kidogo ya kilichoanza mi najua mpaka mwisho wewe muhuni muhuni usipotoshe. Mnataka Mama kumjaza uongo ili afanye kama kwenye mkataba wa meli, wahuni nyie.
Leta bandiko lako la ukweli tulione.
 
Umeandika kwa urefu ila umeharibu tu pale ulipomtaja :MAGUFULI' hapo umedhihirisha uongo wako ma conspiracy theory zako.Hakuna asiyefahamu kwamba Magufuli alikuwa mzalendo wa kweli asiyeyumbishwa na mafisadi.Haya bhn kwa hiyo hizo Trilion alizopiga alipeleka wapi? Mbona maisha yake ya kawaida tu
 
Kesi ya Ngedere anapelekewa nyani, Ila sijui kwa nini namuamini sana mama kweli yeye ni mnyenyekevu Ila kazungukwa na majenerali wa ufisadi na Hivi vitu ndivyo vya kujadiliwa

Je inawezekana ile " NONSENSE" aliyoitoa mama kwa waziri wa Kilimo ilikuwa baada ya kupata taarifa hizi?
 
Hujamuelewa mleta uzi. Ni kuwa yeye mleta uzi katumwa na genge la wezi na mafisadi. Prof. Mkenda alifafanua vizuri sana. Nyie mafisadi hamuwezi kutudanganya hata iweje. Dkt Magufuli alikuwa mzalendo alifanya vitu vyenye tija na faida kwa taifa. Acheni uhuni wa kutunga. Maana unaposema eti wanaamua wazalishe kiasi gani wakati waziri aliwahi kusema na inajulikana capacity ya viwanda vyetu ni ndogo. Halafu mnavyotaka vibali vitolewe ili mlete na sukari oliyo isha muda ili watanzania wafe??? Kipindi cha JK watu walikula bidhaa za ovyo ovyo cheki watu wanavyokufa na cancer. Kwa ufupi huo mlango wa ufisadi hautafunguliwa!

Haya makundi mawili ya ccm yanagombania ulaji na hapo kazi ya Mama Samia ndio itakapokuwa ngumu kwani genge zote mbili anazikumbatia!!!
Ukweli ni kwamba Majaliwa na Jenista Mhagama sio wasaidizi wa kuwategemea na hilo JIWE alikwisha liona na ndio maana alimwambia Majaliwa kuwa asidhani angekuwa waziri mkuu kwa miaka kumi!!! Samia alikuwepo kwenye huo mkutano JIWE alipomuwashia Majaliwa taa nyekundu!!!
 
Haya makundi mawili ya ccm yanagombania ulaji na hapo kazi ya Mama Samia ndio itakapokuwa ngumu kwani genge zote mvili anazikumbatia!!!
Bora aangalia less evil, maana wamsogo hawafai bora kukumbatia waadilifu
 
Hata kama kuna 'gaps' katika stori hii, lakini 'core' ya stori ni sahihi. Kama ningekuwa rais at least ningepata 'second source' na siyo kuiacha tu kisa kuna majina makubwa yaliyotajwa.
 
Bora aangalia less evil, maana wamsogo hawafai bora kukumbatia waadilifu

Sasa hao unaosema hawafai ndio washauri wake wakuu nje na ndani ya serikali!!! Salama yake ni kufuata ushauri kutoka busara zilizobaki chamani MZEE MANGULLA.
 
Hahhahahahah
Ndio mkataba unavyosema mkandarasi afanye design na kujenga kiwanda chenye uwezo wa kuzalisha tonne 250 za sukari kwa siku (na kiwanda kidogo as far as sugar plants are concerned) lakini hakuna sehemu ya ununuzi wa mashine.

Ni ujenzi wa Kiwanda cha sukari; sasa TANROADS anaweza kapewa kazi ya usimamizi tu.
 
Huwa najiuliza tu kama kwa 1B mtu mzima wa umri wa miaka 40 tu anaweza kula maisha ya kawaida tu kula kulala mpaka akafa na still pengine akaiacha chenchi ya hio pesa kwa watoto.

Je, inakuwaje mtumishi anadokoa labda billion 20 na still bado ana tamaa tena ya mahela zaidi? Huyo mtu ikumbukwe analipiwa almost kila kitu na ofisi anapofanyia kazi!

Hayo mahela unaiba sijui billion 100 kesho tena unadokoa billion 50 hivi mahela yote huwa wanafanyia kitu gani? Au ndio wanajengea mahoteli labda!

Imagine umedokoa billion 100 tu inaweza kuwalisha familia yako na ukoo mzima mpaka mkapukutika kama hamuifuji! Na still pesa mtaiacha! Yani imagine kila mtoto aingiziwe 10B tu anaweza ikamsomesha mpaka akaoa na kulea familia na still pesa anayo tu.

Mi najiuliza kwa haya maisha dah unaiba trilion nzima na bado huriziki wakati expectancy ni miaka 60 tu kibongo bongo😂
Hii ndiyo ile wanasema nyama hatari akishaonja damu ndiyo basi tena, ataua sababu anaweza lakini mizoga ataiacha hamalizi.
 
Ukisoma andiko hili kisha ukaenda site kuona yanayoendelea kuna vitu utagundua haviko sawa. Kwa tuliobahatika kufika Dakawa,tumeshuhudia ujenzi wa kiwanda ukiendelea. Gharama zote za mradi inasemekana hazizidi 250billions. Hizo billion 500 zinazotajwa na mwandishi zinatoka wapi??
Umetumwa. Sema mzee wa deal kakuvutia ngapi
 
Ndio mkataba unavyosema mkandarasi afanye design na kujenga kiwanda chenye uwezo wa kuzalisha tonne 250 za sukari kwa siku (na kiwanda kidogo as far as sugar plants are concerned) lakini hakuna sehemu ya ununuzi wa mashine.

Ni ujenzi wa Kiwanda cha sukari; sasa TANROADS anaweza kapewa kazi ya usimamizi tu.
Sijasoma lugha lakini kiwanda kina mkusanyiko wa mashine mbalimbali zitakazochakata malighafi ili kupata zao/product inayotakiwa
 
Hata kama kuna 'gaps' katika stori hii, lakini 'core' ya stori ni sahihi. Kama ningekuwa rais at least ningepata 'second source' na siyo kuiacha tu kisa kuna majina makubwa yaliyotajwa.
Ni sahihi usemacho,shida katika uagizaji wa sukari ipo lakini tunachobishania ni gharama na uwepo wa ujenzi wa kiwanda
 
Inasemekana tatizo la kuhujumu uanzishaji wa viwanda vya sukari nchini ndo ulipelekea taasisi nunuzi kukaimisha ununuzi wa kiwanda kwa tanroad na ni kundi dogo sana la watu walijua hii kitu vinginevyo hakuna kiwanda ambacho kingejengwa
 
Sijasoma lugha lakini kiwanda kina mkusanyiko wa mashine mbalimbali zitakazochakata malighafi ili kupata zao/product inayotakiwa
Nimepitia tena posts number 1 naona mwandishi anachanganya mambo.

Kwanza serikalini consultant na Civil engineer awezi kuwa mtu mmoja; so inaonekana Tanroads kapewa tender ya kusimamia huo ujenzi wa kiwanda cha NSSF na yeye katafuta contractor wakufanya hiyo kazi; it is all part of Tanzania Gov requirement on infrastructure projects.

Lakini hakuna mahala huo mkataba unasema TANROADS wanunue machine, if anything contractor ndio anaweza propose mashine gani itafaa based on his design ya kiwanda na capacity waliyopewa.

Mbona kila kitu kiko wazi.
 
Back
Top Bottom