Who is INDO Power Solutions na ni nani Bw. Brian Mutembei?

Who is INDO Power Solutions na ni nani Bw. Brian Mutembei?

Ki uhalisia kufunguliwa kwa kampuni hakuko sawa kisheria ,kampuni haiwezi kuwa na wakurugenzi au wanahisa mizimu,waliokufa,serikali lazima iingie.mikataba na makapuni yaliyo sahihi kisheria

Sent using Jamii Forums mobile app
Hamna sheria iliyovunjwa mkuu.
Biashara ni Biashara na Siasa ni Siasa.
Kipi tulichague?
Wakati wakulima wetu wanahitaji malipo na tunahitaji hela?.
Najua unaujua msemo huu
"Ukimchunguza Kuku HUTAMLA "
 
Unafikiri kutumia nn? Kichwa au mavi? Umeelewa sheria ya nchi na mchakato wa manunuzi iliyotiwa saini? Huyu jiwe si ndiyo anaekataa wapiga deal? Hapa kimefanyika nini? Tafakari kwanza kabla ya kutoa huo ujinga wako.
Nyie uvccm mbona hamueleweki tatizo nn? Shule au njaa?
Lugha unayotumia INAKUSALITI kwamba unatatizo.
Deal ikliyopigwani ipi hapa?
Chuki hazitalusaidia.
MATUSI na lugha mbaya inaonyesha huelewi ni nini nilichokizungumzia .
 
Hapana huo ni uongo na unafiki, Wako watu tayari kununua kwa $1400 -1500/=, haiwezekani kwa robo bei. Korosho za Tz ni bora kwa ukubwa na uzito

Sent using Jamii Forums mobile app
Haitoshi kuwa "koro show" yetu ni kubwa na nzito bali kuchangamkia soko mapema na haraka, tukikumbuka kuwa sisi sio wakulima pekee wa korosho. Pia kwa kutumia tafiti, tusishangae kuwa baada ya miaka michache wenzetu watakuwa wanazalisha korosho bora kuliko zetu; sisi tuje kubaki na nyimbo yetu pendwa ya "Sisi ndio tulikuwa wa mwanzo".
 
Korosho zimekwisha chukuliwa 100,000 ton na hii kampuni? Au bado?
Koroshow nuksi kweli
Kweli mwanadamu ukiambiwa una roho ya koroshow ujue ni balaa[emoji23][emoji23]

Ova
 
Dah yametimia
===
ILANI:
Sina shida kabisa kama watu hawa wamelipa pesa walizosema watalipa ila endapo hawajatoa pesa na wamekuja kutafuta kiki kwetu ni vyema tuwachambue kwa umakini. Aidha, napata shaka kuwa kuna mtu nyuma ya kampuni hii ambaye soon tutamjua na tutajua lengo lake.
===

Mkuu Mkirindi,

Mimi Intelligence ya siku hizi inanishangaza inavyofanya kazi yake. Hakuna kitu kinasikitisha kama kuwa na Idara ya Usalama inayohangaika kudhibiti wananchi kwa maslahi ya 'tabaka tawala' badala ya kulinda maslahi mapana ya Taifa.

Ninachokijua mimi ni hiki:

1) Kampuni ya INDO Power Solutions imesajiliwa nchini Kenya mwaka 2016 ikionyesha inamilikiwa na watu wawili:
a) Joyce Waithira Gatoho na
b) Alice Wanjiku Gatoho

View attachment 1010458

Lakini, kinachoshangaza kidogo hapa ni kuwa pamoja na uchanga wa kampuni hii; Joyce anayedaiwa kuwa shareholder ni marehemu kitambo sana. Sasa, endelea kunisoma chini uelewe nini maana yake

View attachment 1010459

Ukisoma hapo juu utabaini kuwa Alice kwa mantiki hii ni sole shareholder ambaye akijua wazi kuwa Joyce hayupo hai (kwa nia ovu naweza kusema) aliamua kutumia jina lake ili atimize azma yake.

Taarifa za kampuni hii ambazo nimezipata ndani ya dakika 25 hivi nilitarajia vyombo vyetu vingeweza kuzipata kwa urahisi na kuepusha aibu mbeleni.

2) Twende kwa huyu ndugu Brian Mutembei

Namfahamu huyu jamaa kwa uzuri tu. Brian ni dalali maarufu na kwa waliokaa katika jiji la Nairobi watakuwa wanamfahamu.

Dalali huyu ni mtu wa karibu na Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto (ambaye wakenya wanamjua kama mmoja wa watu mafisadi wa kutupwa).

Brian ana rekodi ya makosa ya jinai na amewahi kufungwa. Kumbukumbu zake zipo kila sehemu (mtu akijiongeza):

View attachment 1010461

Aidha, dalali huyu anajulikana kwa mbwembwe zake za kumwaga mafedha kuonyesha 'jeuri ya pesa' hivyo siwezi kumtofautisha na kina "Ndama Mutoto ya Ng'ombe" au "Jackie Pemba" hivyo yeye kutumika kwenye hili deal haishangazi.

Simsingizii, soma hii story (event hii nzi wetu alikuwepo) na utaona maneno haya hapa:

View attachment 1010475

Naishia hapa kwa leo.

UPDATE, Feb 9, 2019

View attachment 1018644
 
Habari ya kwamba Indo Power Solutions ya Kenya ni fake lkn ndiyo imesaini deal la kununua tani laki moja za korosho hapa Tanzania, imetrend sana mitandaoni.

Nilitegemea kusikia AG wa Tanzania awe amejiuzulu. Anasubiri nn? Au jiwe ndiye aliwapigia simu?

1658210646374.png


Indo power Solutions ni kampuni iliyoshinda zabuni ya kuwa mnunuzi wa tani 100,000 za korosho za Lindi na Mtwara kwa bei ya Dola za kimarekani milioni 180. Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Prof. Joseph Buchweishaija alisema historia ya kibiashara haikuwa kigezo kikubwa cha kampuni kupewa zabuni.

Gazeti la Kenya la East African lilifanya uchunguzi dhidi ya kampuni hiyo na kubaini kuwa usajili wa Indo Power Solutions unaonesha ilisajiliwa 2016 hata hivyo haikuwahi kupata zabuni iliyozidi Dola milioni 10. Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo Brian Mutembei anajulikana zaidi kisiasa. Kamuni hiyo haijulikani, na ilibainika kuwa walikuwa ni madalali na sio wanununuzi.

Na hata baada ya kushinda zabuni hiyo kamuni hiyo ilienda kutangaza kuuza korosho kwenye tovuti ya Alibaba. Tangazo hilo waliliweka kabla ya kulipia korosho hali iliyoleta sintofahamu kwa watanzania.
 
Back
Top Bottom