Who is INDO Power Solutions na ni nani Bw. Brian Mutembei?

Usomi unakomea hapo. Unaunga mkono juhudi za serikali kuwatetea wana wa nchi.

Unasema serikali imekurupuka, haikuweka mipango madhubuti ya kununua korosho. Mkulima leo hii amekuwa dhalili licha ya mavuno yake mazuri. Shida kwa mkulima imeongezeka. Utetezi gani huo? Waliteswa na watu binafsi sasa wanahangaishwa na serikali yao. Waweza amini kuwa mheshimiwa anawapiga shangazi zao.

Yule kijana Solomon Mihayo wa madini alimpeleka shule mheshimiwa. Ile ilikuwa thesis kuzidi ya maganda ya korosho. Unajiita authority lakini hutambuliki. Ushauri wa Solomon ungekuwa umechukuliwa na kutendewa haki usingekuwa hapa unajibizana na mimi. Ungekuwa unasaidia kurekebisha palipoenda fyongo kwenye korosho.

Unasema hujanielewa! Ni kweli. Huwezi kusema serikali inatetea wakulima wakati wanahangaika zaidi, ukanielewa. Serikali inatafuta wanunuzi ninyi iliowakataa. Unachoelewa wewe ni serikali kununua kwa wakulima kwa 3,300/= na kuuza kwenu kwa bei yenu ya 1,700/=? Mkulima hajapunjika. Serikali imefanya biashara kichaa. Serikali ni nini/nani? Kama unaangalia mbali zaidi na ncha ya pua utanielewa. CAG kwa biashara kama hii atazuiwa kutembelea huo mtaa. Madudu matupu. Mkirindi nakuelewa unataka kununua hizo korosho. Mark you at our expense!

Usomi unakosa maana hapa!!!
 
Nawashangaa Korosho zimeishanunuliwa maneno ya nini ajabu kabisa
 
Ndugu badi hujanielewa na hutanielewa. Anyway. Mimi ninachounga mkono ni kuwa wakulima walikuwa wanadhulumiwa na Cooperatives, Bodi na wafanyibiashara. Tulikuwa tunanunua korosho kwenye auction k.m. kwa TS 2000/= kg, mkulima analipwa 900/= hadi 1200/= tena jwa rejareja, na korosho nzuri wanapewa mashirika maalumu na qanalipa 2200/ hiyo 200 ni ya watu wa bodi na auction.

Serekali ilipoamua bei nikasema mkulima atafaidi. Lakini hii plan ingepangwa 6 months kabla ya msimu.

Kwa sasahivi bora najua mkulima chake ni 3000/=, serekali ikipata hasara kwa kuuza kwa bei che wanastahili hasara kwa ujinga, bora isimfikie mkulima.

Na usisahau hakuna mfanyi biashara asiyependa cha urahisi, hata mimi ni mmoja wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aliyenunua Korosho hizo ni mtanzania mwenzetu anakaa Kenya na huwa anafanya biashara hiyo ya korosho kwa kuwagawia watanzania wenzetu fedha kuja kununua hizo korosho, alivyoona hali ni ngumu korosho imebanwa na serikali akaja kupambana hapa kwa kumuona mzee baba kama unakumbuka hapo kati alikuja nchini na akafanya mazungumzo akaweka mambo sawa sasa amefanikisha hiyo biashara (Unganisha dots utamjua).
 
Mkuu kwa taarifa zilizopo ni kuwa wakubwa baada ya kuangukia pua kwenye operation koroshow wametafuta dalali wa kuuza hiyo korosho na tayari jamaa ameenda na wanunuzi fulani mtwara na pwani na wamekagua na kuambiwa kuwa watauziwa kilo moja grade 1kwa sh 4800 na grade 2 kilo moja kwa sh 3800 na hao wanunuzi wamesepa hivyo huyo siyo mnunuzi bali ni dalali
In God we Trust
 
Sisi tunataka korosho zisituozee gharani kuhusu uwezo wa kiwanda huko kenya watajijua wenyewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeona video clip ya kutiliana mkataba huko Arusha its amazing.
Watafanya transaction within a week according to waziri wa katiba prof Kabudi.
Na kama mambo yataenda as per plan Tanzania itakuwa imefanya biashara kubwa na Kenya itakuwa imepunguza trade imbalance,hivyo hata shillingi yetu itangara kiasi fulani kwa Kenya.
 
We have a cynicism problem amongst cynical politicians and followers alike in this country. The cashewnuts deal is a one off transaction, jetting money in our coffers, how and from where do you get such analogy with that doomed Richmond deal, which was designed to syphon money from our coffers?! It is crazy! Whether it is DP Ruto or Mutembei being crooks but they buy our commodity and pay us handsomely, where is the fuss? Unless architects behind this thread consider Tanzania or the government does not have goal just like them thus bring up this worthless discussion, they better get advised to rescind.
 
Hakuna 'surname' ya kimeru au ukoo unaoenda kwa jina la 'mutembei'...
Mutembei,mutembuzi,nk ni majina ya kihaya
This is a silly conclusion. Names have long crossed borders gentleman. Intermarriages have been on course and new born given names of parents choices. .
 
Kampuni ya RICHMOND iliyoingia mkataba na Serikali ya Tanzania kwani ilitokea wapi...??

Ukilijua hilo basi usiwe na hofu kwanini hiyo kampuni ya kununua hizo tani laki moja imekuja pasikojulikana....

Eaters are within us.

Sent using Nokia 8 Plus
Kama ni hivyo, basi mie ngachoka tena!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…