Whozu ananunua gari baada ya kulipwa Tigo Fiesta..

Fiesta malipo yake haifiki milioni 1 labda amepiga show zingine huko na mapato ya YouTube
 
Huu uzi ushakuwa wa chai baridi kuna boya atapata sifa hapa kwa chai zake za stand
 
Hahaha humu Jf Kuna vituko sana. Haya dogo kula kulala.
 
Fiesta malipo yake haifiki milioni 1 labda amepiga show zingine huko na mapato ya YouTube
Hakuna mwenywe uhakika wa Malipo ya Fiesta wanaojua ni wasanii na Clouds yenyewe. Ila mwenyewe kasema ni kutokana na show alizofanya Fiesta, sasa mimi ni nani nipingane naye?
 
Mkuu sasa kosa ni kutegemea kazi yake kumiliki gari? Mziki ndo kazi yake na kama ndiyo kazi ianyomwezesha kununua gari mbona safi tu.
Halafu kuna watu kwa nature ya kazi wanazofanya na vipaumbele gari inabidi iwe kipaumbele cha kwanza then ndo nyumba. Maisha siyo kuigana maisha ni mipango siyo lazima kila mtu afuate formula ya mwenzake ndugu. Huenda hilo gari likampa michongo zaidi ya kushusha mjengo bila stress.
 
aisee naona mi si mzalenda wa nyimbo za kwetu maana hata sijawahi kumsikia huyu jamaa
 
Lakini cha ajabu akishazidi kupata mafanikio kuna siku atakuja kusema huwa anadhulimiwa
 
Wabongo bana ni sawa na mjasiliamali aliyefanikiwa baada ya kuuza unga kwa kusaga mahindi kwa kutumia jiwe kisha akanunua mashine ya umeme mtu anajitokeza anaponda eti kwanini asingejenga ghala.

Piga kazi Whozu wabongo tumeumbiwa fitna.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Follow
2. Gonga
3. Tunavesha
4. Huendi mbinguni
5. Usiombe

So far hizo ndo nyimbo zake hadi sasa, mimi namkubali sana hasa yale machepele yake.
 
Sasa wewe, umeona wapi mwanaume anasifiwa au kupostiwa kisa kanunua gari?

Shusha mjengo post ntamusaidia kushare,,

Halafu siyo kila michongo yake lazma utumie gari binafsi mbna bajaj zpo tena sana,

Unamiliki gari hata kununua mafuta unashndwa[emoji3]

#bado_sijanunua_gari_mjini_kuna_jam!
Sent from my TECNO-Y3+ using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…