Uchaguzi 2020 Why Bernard Membe is not a presidential material, at all!

Uchaguzi 2020 Why Bernard Membe is not a presidential material, at all!

download.jpg


Bernard Kamilius Membe ni waziri wa Mashauri ya Kigeni nchini Tanzania, ni mwanachama wa chama cha mapinduzi,

Historia ya Membe inaanzia mbali kidogo toka kusini mwa Tanzania katika mikono salama ya upadre, chini ya ukasisi wa Namupa Seminari.

Bernard Kamilius Membe kijana wa kati mwenye uso angavu akiketi dawati la Tatu kutoka kulia, alikuwa mtoto mwenye akili ya kawaida akiwa nyuma ya watoto wenye vipaji shuleni hapo, Kasisi Mariano anamueleza kama Bernard mvivu wakusimamiwa kila jambo,

Hayo ni ya Namupa Seminari na Itaga Seminari katika mapito yake kielimu. Bernard Membe kutoka Darasa la awali hadi High School yani kidato cha sita, hakuna mahali panapotaja uimara wake kiakili darasani wala hakuna tukio lolote la kishujaa la kukumbukwa, iwe katika mitiahani, michezo, uongozi shuleni ama sifa yoyote toka kwa wakufunzi wake.
Kwaujumla alikuwa ni mwanafunzi wa kawaida kabisa ambae hawezi kusonga mbele bila usimamizi wa walimu wake kinyume na wanafunzi wengine,

Mwaka 1978 Membe aliingia kwenye ajira ya serikali akihudumu Ofisi ya Rais Idara ya Usalama wa Taifa kitengo cha uchambuzi wa taarifa za kijasusi, Kazi hiyo amehudumu kwa mika kumi na mbili tu akahamishiwa Wizara ya Mashauri ya Kigeni na kwenda Ottawa Canada kuwa mshauri wa Kibalozi kutoka 1992-2000,

Utumishi wake ndani ya Idara ya Usalama haukuwa wa kutukuka na hakuna kumbukumbu lake na la mfano ndani ya idara kwa ujumla zaidi ya kuwa mmoja ya majasusi wa Tanzania waliopata mafunzo ya mda kuke Scotland Uk, Hakuna mission yoyote aliyowahi kupewa na akaifanya kwa ufanisi wenye kukubalika ndani ya Idara, anamshinda hata Eliamkim Maswi yule wa Escrow ambae yeye alipewa mission ya kuiua NCCR ya Mrema na akafanikiwa kwakujipenyeza mpaka kuwa mbeba mikoba wa Mrema enzi zile na kuizika NCCR MAGEUZI kabisa,

Mwaka 2000 aliingia kwenye siasa akawa Mbunge wa Jimbo la Mtama, nakisha tarehe 17/10/2006 hadi 1/11/2007 aliteuliwa kuwa naibu Waziri wa Nishati na Madini, na kisha 1/12/2007 mpaka sasa ni Waziri kamili wa Mashauri ya Kigeni,

Kulegalega kwa Diplomasia ya Tanzania kunatokana na udhaifu wa Bernard Membe katika wizara hii ya mashaiuri ya Kigeni, Diplomasia ya nchi imeshuka na sasa sio Tanzania ile yenye sauti ya UTU.

Katika kipiti cha utmishi wa Bernard Membe ndani ya Wizara taifa limeshuhudia migogoro mikubwa ya Kidiplomasia na mataifa ya kigeni, ambayo kimsingi ni ufinyu wa maarifa wa Bernard Membe katika kukabiliana nayo,

Mathalani Mgogoro na Malawi wa Ziwa Nyasa, Mgogoro na Rwanda, Mgogoro na Kenya, Mgorogoro na Uingeraza, Mgogoro na ummoja wa nchi wa Hisani wa Maendeleo za Ulaya,

Haya yote yametukia katika uongozi wa Bernard Membe katika wizara inayohusika na mashauri ya Kigeni, lakini hili linatokana na historia ya mtumishi huyu ambaye hajawahi kuwa kiongozi wala hajawahi kujiongoza yeye mwenyewe,

Je dhamana kubwa kabisa ya Urais wa Jamhuri anaweza ikiwa Wizara tu imemshinda?

Zingatia, Bernard Membe hajawahi kuwa kiongozi wa umma tangu AZALIWE 1953 mpaka 2000 alipoingia kwenye siasa, hivyo uongozi sio kipaji chake!
 
Membe hovyo kabisa! anachokiweza ni kuwafitinisha wenzake tu! alianza kuwafitinisha akina Mudhihir na jamaa zake wote wa kusini waliokuwepo kwenye system! kwa kushirikiana na Sitta wameweza kupenyeza fitna ya kumchafua Lowassa ile mbaya! ilifikia mahla wakamwambia JK eti atatawala kwa kipindi kimoja tu kwani Edo amejiandaa kumvua madaraka 2010 kwa sababu za kiafya! Sendeka aliingizwa mkenge na sasa amekuwa mbogo ile mbaya! Membe amekuwa akiwashauri CCM mikakati ya kuidhoofisha UKAWA! Operesheni za kijinga za kukamata na kutesa wananchi ameziasisi yeye , wassira na Pinda! Jitihada za kuboresha Daftari la Wapiga kura siku zote zimekuwa zikififishwa na mikakati yake ya kijinga ... Membe si Mwanadplomasia mzuri kwani wataalam wanaweza kumsoma paji lake la uso kirahisi sana! No wonder sasa hivi tunapigwa bit kila upande ... Membe hafai kuwa kiongozi zaidi ya kusaidia kugawa Juice ....
 
So what?
Hiyo historia yote ya Membe umesimuliwa, umeisoma mahali au umetunga mwenyewe?

Bado sijajua lengo lako hasa. Kama ni suala la Membe kuwa rais wa Tanzania, hilo liko wazi kabisa. Kifupi Membe hafai kuwa rais wa Tanzania na kamwe hataweza kuwa rais.
 
Membe hovyo kabisa! anachokiweza ni kuwafitinisha wenzake tu! alianza kuwafitinisha akina Mudhihir na jamaa zake wote wa kusini waliokuwepo kwenye system! kwa kushirikiana na Sitta wameweza kupenyeza fitna ya kumchafua Lowassa ile mbaya! ilifikia mahla wakamwambia JK eti atatawala kwa kipindi kimoja tu kwani Edo amejiandaa kumvua madaraka 2010 kwa sababu za kiafya! Sendeka aliingizwa mkenge na sasa amekuwa mbogo ile mbaya! Membe amekuwa akiwashauri CCM mikakati ya kuidhoofisha UKAWA! Operesheni za kijinga za kukamata na kutesa wananchi ameziasisi yeye , wassira na Pinda! Jitihada za kuboresha Daftari la Wapiga kura siku zote zimekuwa zikififishwa na mikakati yake ya kijinga ... Membe si Mwanadplomasia mzuri kwani wataalam wanaweza kumsoma paji lake la uso kirahisi sana! No wonder sasa hivi tunapigwa bit kila upande ... Membe hafai kuwa kiongozi zaidi ya kusaidia kugawa Juice ....
Mkuu, unaweza kunieleza ni kwa namna gani Membe alimfitini Mudhihiri? Ninachojua ni kwamba Mudhihiri alishindwa kwenye siasa za ushindani na kijana Mtanda akatwaa jimbo na Mchinga
 
Hoja yako ipo kwenye mantiki gani mimi nikiangalia naiona kwenye umbea na unafiki mambo kama haya husemwa na watu waliochetuka pengine na wewe ni miongoni mwa watu hao.
 
Huyo jamaa ni mtu mnafiki kabisa yeye ndiye aliyeta kuliingiza Taifa kwenye migogoro ya Kidini kwa kushauri na kulazimisha hoja yake ya Taifa kujiingiza kwenye umoja wa nchi za kiislamu OIC wachungaji walimjia juu lakini yeye bado akakomalia msimamo wake mpaka Rais J Kikwete alipoingilia kati na kumaliza mzozo huo wachungaji na wakristo wengi hawataki hata kumsikia kutokana na kujifanya mjuaji wa kila jambo bila kutaka kusikia ushauri wa wengine leo anautaka urais,wakuu huyu jamaa hafahi hata kidogo ana majivuno,mjeuri,si msikivu wala ashauriki,hana hekima wala busara,ni mtu mwenye fitina na majungu kwa watuna viongozi wenzie amekuwa akibeba maneno ya uongo na kupeleka kwa wakubwa ili kuwachafua mawaziri na viongozi wenzie yani waswahili wanaita mbeya kwa uchambuzi mdogo tuhuo na ninavyomfahamu mimi Bernard Membe ni kweli hafahi hata kidogo kuwa rais hekima na busara zero tukimpa nchi ataliingiza taifa kwenye migogoro na matatizo badala ya kusonga mbele tutarudi nyuma kimaendeleo.
 
Leo Yericko yuko katika ubora wake..... Ingawa ni jambo la wazi Membe ni failure na mbumbumbu wa kisiasa...... Akaongoze WAMA organization, kuongoza nchi hasahau kabisa
 
Leo Yericko yuko katika ubora wake..... Ingawa ni jambo la wazi Membe ni failure na mbumbumbu wa kisiasa...... Akaongoze WAMA organization, kuongoza nchi hasahau kabisa
Naona unamuunga mkono kwa vile kampiga za uso adui wa bosi wako. Sisi tupo pembeni tunawachora tu
 
Back
Top Bottom