Why blacks?

Why blacks?

Nani keshawahi kukutana na weusi wa kutoka visiwa vya Caribbean ambao wanajiona wao ni bora zaidi kuliko weusi wa Afrika?

Wamarekani weusi ndo usiseme kabisa. Wapo wengi tu wanaojiona kuwa wao ni bora zaidi kuliko Waafrika weusi (wa Afrika).

Huwa hawakawii kukwambia kuwa wao wamechanganya damu na Wahindi wekundu pamoja na Wazungu ili tu kukuonyesha kuwa wao wako tofauti.

Hao hao Wamarekani weusi, na wao huwa wanabaguana kati ya wenye ngozi nyeupe na wale wenye ngozi nyeusi.

Kwa ujumla watu weusi tuna matatizo mengi sana na hilo la uduni ni kubwa kati ya hayo.
 
If you employ some of "them" like I did, they will call you SIR. I am Sir to them, No low self esteem here. You got to be ahead of the game.

Kaka hawa viumbe wana matatizo hata kama umewaemploy wanajiona superior race
 
Nani keshawahi kukutana na weusi wa kutoka visiwa vya Caribbean ambao wanajiona wao ni bora zaidi kuliko weusi wa Afrika?

Wamarekani weusi ndo usiseme kabisa. Wapo wengi tu wanaojiona kuwa wao ni bora zaidi kuliko Waafrika weusi (wa Afrika).

Huwa hawakawii kukwambia kuwa wao wamechanganya damu na Wahindi wekundu pamoja na Wazungu ili tu kukuonyesha kuwa wao wako tofauti.

Hao hao Wamarekani weusi, na wao huwa wanabaguana kati ya wenye ngozi nyeupe na wale wenye ngozi nyeusi.

Kwa ujumla watu weusi tuna matatizo mengi sana na hilo la uduni ni kubwa kati ya hayo.

Mkuu kam tatizo ni hilo basi kazi ipo....na mtu mweupe ametu outsmart mpk kutujaza hiyo kasumba vichwani mwetu
 
Mtu mweusi anajishusha mwenyewe, anajibagua mwenyewe. Tatizo liko kwenye akili ya kitumwa kichwani mwa weusi. Mfano mzuri upo kwa viongozi weusi ambao wanajikomba na kuamuliwa na wazungu pamoja na mamlaka yote waliyopewa na watu wao.
Sikiliza kwa makini hotuba za viongozi weusi kwenye hadhara za kimataifa, zote za kuombaomba, kunyenyekea nyekea na mengine yanayofanana na hayo.
Hali hii itabadilika tu baada ya weusi kufanya mapinduzi ya fikra na waweze kujiona wao ni bora zaidi kwa nafasi yao!

Check with your political economy literature please!!!!!!
 
Thanx brothers !!!!!!!

You have given me a good starter!!!
 
Tatizo unaanzia kwenye era ya slavery, ungesema kwa nini mtu mweusi hapati heshima tangu slavery ungekuwa na hoja. Lakini huko nyuma mtu mweusi alifanya biashara na mtu mweupe on equal footing.

Karl Peters alivyokuja kuchukua nchi aliwekeana mikataba na masultani wa pwani ya Tanzania ya sasa. Hakuja na jeshi kuswaga watu tu. Admittedly mikataba ilikuwa ya treachery, lakini aliingia kwa heshima ya treaty.

Kabla ya hapo watu wa Azania walifanya biashara kama watu sawa na Wachina, Waliokaa Uingereza ya sasa walinunua chuma kutoka Afrika mashariki katika biashara iliyohusisha watu sawa, wao hawakujua kutengeneza chuma.

Hata hiyo biashara ya utumwa yenyewe mostly iliendeshwa na machifu wa Kiafrika waliokuwa wanawauza maadui zao na mateka wa vita. Wazungu waliokuja kununua watumwa walifanya biashara na hawa machifu kama watu sawa.

Mansa Musa alivyokwenda kuhiji Mecca mwaka 1324 alimwaga dhahabu hapo Cairo watu bado wanazungumzia habari zake mpaka leo, alifanya mpaka bei ya dhahabu ipungue. Huyu alikuwa mtu mweusi aliyeheshimika dunia nzima. Watu kutoka pande zote za dunia walikuwa wanakuja kwenye chuo kikuu cha Timbuktu kusoma na kukopi vitabu.

Contrary to popular belief, Waafrika wamefanya biashara kwa muda mrefu na sehemu nyingine za dunia kama watu sawa. Matatizo ya kudharauliwa mtu mweusi yameanza baada ya watu weusi kudharauliana wenyewe na kujifungia sana tusitoke huko Afrika.

Waafrika walikuwa majenerali walioheshimika katika majeshi ya Warumi. Wengine waliwapiga Warumi bado kidogo wauangushe ufalme huu mkubwa.

Someni kabla ya kutoa habari ambazo si timilifu.

Shukurani kwa kuanzisha uzi tuweke record straight.

I am not saying this out of racial pride or black supremacy - which I think is just as bad as white supremacy - but historically sound accounts.

Mkuu tatizo historia yetu haijaandikwa hivi....na huko ndipo hata mitaala yetu inazidi kutubrainwash na kutufanya tuwe inferior
 
Mkuu tatizo historia yetu haijaandikwa hivi....na huko ndipo hata mitaala yetu inazidi kutubrainwash na kutufanya tuwe inferior

Nimeipenda point yako kuhusu mitaala. Asante sana Kiranga pia kwa somo zuri.

Education was very often used as a subtle means of our emasculation.

Kwa mfano, katika kipindi cha miaka ya karibu na uhuru, swali moja lililotoka sana kwenye somo la Jiografia lilikuwa hili:

"The weather around Nairobi is suitable for...." Jibu pekee lililokuwa linakubalika ni: "European settlement".

Swali lingine lililotoka sana lilikuwa: "The first man to see Mount Kilimanjaro was....". Jibu ilibidi liwe jina la Mjeruman (Kraft, I suppose; it has been a while). Sasa maana yake ni kwamba mababu zetu walioishi Uchagani aidha hawakuwa watu au walikuwa hawaoni!

Shida kubwa iliyoko sasa ni inferiority complex. It is overwhelming. Kitu kinafanya wadada wengi wajichubue na kuvaa mawigi ya kizungu ni inferiority complex. It is an unimaginably bad problem.
 
Tatizo unaanzia kwenye era ya slavery, ungesema kwa nini mtu mweusi hapati heshima tangu slavery ungekuwa na hoja. Lakini huko nyuma mtu mweusi alifanya biashara na mtu mweupe on equal footing.

Karl Peters alivyokuja kuchukua nchi aliwekeana mikataba na masultani wa pwani ya Tanzania ya sasa. Hakuja na jeshi kuswaga watu tu. Admittedly mikataba ilikuwa ya treachery, lakini aliingia kwa heshima ya treaty.

Kabla ya hapo watu wa Azania walifanya biashara kama watu sawa na Wachina, Waliokaa Uingereza ya sasa walinunua chuma kutoka Afrika mashariki katika biashara iliyohusisha watu sawa, wao hawakujua kutengeneza chuma.

Hata hiyo biashara ya utumwa yenyewe mostly iliendeshwa na machifu wa Kiafrika waliokuwa wanawauza maadui zao na mateka wa vita. Wazungu waliokuja kununua watumwa walifanya biashara na hawa machifu kama watu sawa.

Mansa Musa alivyokwenda kuhiji Mecca mwaka 1324 alimwaga dhahabu hapo Cairo watu bado wanazungumzia habari zake mpaka leo, alifanya mpaka bei ya dhahabu ipungue. Huyu alikuwa mtu mweusi aliyeheshimika dunia nzima. Watu kutoka pande zote za dunia walikuwa wanakuja kwenye chuo kikuu cha Timbuktu kusoma na kukopi vitabu.

Contrary to popular belief, Waafrika wamefanya biashara kwa muda mrefu na sehemu nyingine za dunia kama watu sawa. Matatizo ya kudharauliwa mtu mweusi yameanza baada ya watu weusi kudharauliana wenyewe na kujifungia sana tusitoke huko Afrika.

Waafrika walikuwa majenerali walioheshimika katika majeshi ya Warumi. Wengine waliwapiga Warumi bado kidogo wauangushe ufalme huu mkubwa.

Someni kabla ya kutoa habari ambazo si timilifu.

Shukurani kwa kuanzisha uzi tuweke record straight.

I am not saying this out of racial pride or black supremacy - which I think is just as bad as white supremacy - but historically sound accounts.

I am of your opinion,well elaborated
 
And these so called 'white people' made lot of bad things to sound black purposely...blackleg, blackmagic, blackmarket, blackmoney, blackhat(bad hacker), blackmail the list goes on. Good hackers are called whitehat...as of now english is the world's language.
Cheap tactics in the game of mental slavery...
 
tangu nilipoulizwa kwa nini hakuna mitume weusi na sikuwa na jibu basi tena!!!!!
kwa nini ulikosa jibu? Wapo wengi tu ...... Malisa, joshua wa nigeria, mzee wa upako, kakobe, na wengineo teh teh teh. Au unadhani kuwa mtume mpaka uwe marehemu? Mitume wetu weusi wa za zamani walikuwepo. Sema tu hawapo kwenye vitabu/simulizi za dini hizi za kimapokeo kutoka mashariki ya kati. Marasta wanaamini mfalme haile selasie ni mtume. Come out of the box bro.
 
Adui wa mtu mweusi ni mtu mweusi mwenyewe wala si wazungu. ukisimama sawa hakuna atakayekudharau hata kidogo.

Tunajidharau wenyewe ndiyo maana tunadharaulika. Hatuthamini tulivyo na tulivyonavyo ambayo hao wazungu wangeweza wangesema tubadilishane. Tupo masikini mioyoni mwetu, Hivyo umasikini huu ndiyo unaochangia kujidharau. Na siku zote ukijidharau jua utadhauliwa ukijichukia utachukiwa.
 
Mkuu hoja yangu ni katika kujua kuna cha zaidi katika chuki ya mtu mweupe kwa mtu mweusi??kuna ovu gani ambalo mtu mweusi amelitenda kihistoria hadi kufikia hatua ya kudhaurika na kunyanyaswa na mtu mweupe??
KOSA NI UNYONGE. Walituteka, wakatutawala, wakatufanya tuzikane na kusahau dini na tamaduni zetu, tunajichukia wenyewe kwa kupenda lugha zao, kuichubua ngozi na kuvaa nywele bandia zinazofanana za za kwao, temeshindwa kutumia raslimali lukuki tulizo nazo kuendeleza nchi zetu. Kwa hayo yote nani anaweza kukuheshimu? Tutaheshimika tutakapojidhihirisha mbele ya mataifa mengine kuwa na sisi tuna hadhi ya kuwa kwenye kundi la bin-Adam. Watu weupe????? (wekundu? kahawia? njano?) hawatuchukii bali wanatudharau.
 
Wakuu habarini.....toka kuumbwa kwa huu ulimwengu mtu mweusi amekua akibaguliwa na mtu mweupe!!hivi nini asili ya chuki hii...tukikumbuka slavery...apartheid!!nadhani kuna la zaidi kwa hawa wenzetu kuhusu blacks...asanteni

Naona historia imekupita kando kidogo. Waingereza (weupe) kwa Waingereza (weupe) wanabaguana, soma historia ya 'Belfast Unrest'. Hio ni kabla hata biashara ya utumwa haijaanza. Ukimaliza uje nikupe mfano mwingne.
 
Nani keshawahi kukutana na weusi wa kutoka visiwa vya Caribbean ambao wanajiona wao ni bora zaidi kuliko weusi wa Afrika?

Wamarekani weusi ndo usiseme kabisa. Wapo wengi tu wanaojiona kuwa wao ni bora zaidi kuliko Waafrika weusi (wa Afrika).

Huwa hawakawii kukwambia kuwa wao wamechanganya damu na Wahindi wekundu pamoja na Wazungu ili tu kukuonyesha kuwa wao wako tofauti.

Hao hao Wamarekani weusi, na wao huwa wanabaguana kati ya wenye ngozi nyeupe na wale wenye ngozi nyeusi.

Kwa ujumla watu weusi tuna matatizo mengi sana na hilo la uduni ni kubwa kati ya hayo.
Nyani Ngambu usi-generalize. Nimekutana na diaspora Afrikans wengi ambao wanaona sifa kuwa na nasaba ya Afrika na wanaona gere kuwa hawakuzaliwa Afrika. Wapo hao wengine, wengi wao wenye elimu duni, wenye hizo superiority complexes lakini nadhani zinatokana na ignorance, low self esteem na hasiraya kuishi kwenye jamii za kibaguzi.
 
Nyani Ngambu usi-generalize. Nimekutana na diaspora Afrikans wengi ambao wanaona sifa kuwa na nasaba ya Afrika na wanaona gere kuwa hawakuzaliwa Afrika. Wapo hao wengine, wengi wao wenye elimu duni, wenye hizo superiority complexes lakini nadhani zinatokana na ignorance, low self esteem na hasiraya kuishi kwenye jamii za kibaguzi.

Wapi nime-generalize?
 
Kaka hawa viumbe wana matatizo hata kama umewaemploy wanajiona superior race
Kuna mmoja was like that in my firm. Lakini alipo gundua it is me ninaye lisha familia yake, ni pale nimpo mpa notice ya kumwachisha kazi, he bagged me like a kid, but I kicked him out of my firm.

Ingawa wapo wengi wanafikiria kuwa Weusi wote lazima wawe chini yao, hii imesababishwa na jinsi weusi wanavyo jihisi wanapo kutana na weupe. Kitu kibaya ni ile low self esteem. If you conquer that, you are the King of your own world.
 
kwa nini ulikosa jibu? Wapo wengi tu ...... Malisa, joshua wa nigeria, mzee wa upako, kakobe, na wengineo teh teh teh. Au unadhani kuwa mtume mpaka uwe marehemu? Mitume wetu weusi wa za zamani walikuwepo. Sema tu hawapo kwenye vitabu/simulizi za dini hizi za kimapokeo kutoka mashariki ya kati. Marasta wanaamini mfalme haile selasie ni mtume. Come out of the box bro.

Hao kina Joshua ni watoa fotokopi za hadithi za wayahudi.

Hata Selassie anasemwa ni mtume kama kijukuu cha Yesu wa Wayahudi, kwa hiyo si an authentic African prophet ( by the way the whole thing is hokum, as much as I love reggae, this I have to say)

Mkuu anaongelea mitume wa Afrika as in walioandika mazingira ya Afrika.

Kama ulivyosema, tatizo tushakaririshwa kwamba tamaduni zetu ni ushenzi.
 
Naona historia imekupita kando kidogo. Waingereza (weupe) kwa Waingereza (weupe) wanabaguana, soma historia ya 'Belfast Unrest'. Hio ni kabla hata biashara ya utumwa haijaanza. Ukimaliza uje nikupe mfano mwingne.

Asante blaza.....historia yangu iliishia olevel na si msomaji...nawashukuru sana
cc Kiranga
 
Hao kina Joshua ni watoa fotokopi za hadithi za wayahudi.

Hata Selassie anasemwa ni mtume kama kijukuu cha Yesu wa Wayahudi, kwa hiyo si an authentic African prophet ( by the way the whole thing is hokum, as much as I love reggae, this I have to say)

Mkuu anaongelea mitume wa Afrika as in walioandika mazingira ya Afrika.

Kama ulivyosema, tatizo tushakaririshwa kwamba tamaduni zetu ni ushenzi.

Kiranga can i know you??are you historian or??nachoshangaa unaijua historia ambayo haijaandikwa kwenye Nyambari Nyangwine.....unayatoa wapi haya madini?
 
Back
Top Bottom