William Miller: Kama Yesu hakujua Hisabati au kutafsiri mambo bora angalikaa Kimya. Mbona siku ya mwisho wa dunia inakokotoleka kirahisi?

William Miller: Kama Yesu hakujua Hisabati au kutafsiri mambo bora angalikaa Kimya. Mbona siku ya mwisho wa dunia inakokotoleka kirahisi?

Hatimaye, ndugu zangu, mambo yote yaliyo ya kweli, yoyote yaliyo na sifa njema, yoyote yaliyo ya haki, yoyote yaliyo safi, yoyote ya kupendeza, yoyote yenye staha, ukiwepo uzuri wowote, pakiwepo chochote kinachostahili kusifiwa, tafakarini mambo hayo.
Wafilipi 4:8 NEN
Wanazuoni:

Kichwa cha habari hapo juu sio kwamba ni cha uchochezi au kwamba kimelenga kupasukia watu kwa kashifa au kwamba ni kufuru kwa Mungu.La hasha, bali ni tafsiri ya kile alichomaanisha Mwanajeshi mmoja huko Marekani pale alipoibuka na Formula ya kukokotoa tarehe ya kurudi kwake Yesu duniani. Jamaa huyo anaitwa WILLIAM MILLER.


William Miller
alizaliwa tarehe 15 Februari1782, huko Jimboni Massachusetts, Marekani na kisha kulelewa katika familia ya Kikristu iliyokuwa na makazi yake Jimbo la New York ya Kaskazini.Familia ya William Miller ilikuwa ya Kibaptisti. Babu yake na wajomba zake wawili walikuwa ni wachungaji katika kanisa la Wabaptisti. Kanisa la Kibaptisti, ni mumeguko karne ya 17 BK kutoka Kanisa la England,yaani Kanisa la Serikali ya Uingereza (Anglikani) ambalo leo linaitwa Lutheran Church.



Miller, katika ujana wake alipata kujiunga na jeshi laMarekani na kufikiaCheo cha Kapteini, wakati wa vita kati ya Marekani na Uingereza (Great Britain) mnamo mwaka 1812.Na inasemekana alikuwa na akili sana na kwamba alikuwa na kipaji cha kufafanua mambo.Bwana Miller baada ya kumaliza utumishi wake Jeshini na kurudi toka vitani (kati ya Marekani na Uingereza mwaka 1812), alianzisha makazi katika Shamba lake huko Low Hampton, New York, ambamo alikuwa amejenga nyumba na akawa akiishi hapo na wakati fulani akawa akienda kusali kwenye kanisa la Baptist la karibu yake.



Bwana Miller kwa kujishughulisha na mambo ya kiimani alipata kuwa mwana-DEIST,yaani alipata kuamini katika Falsafa ya Deism.

Deism ni Falsafa inayokazia kwamba Mungu hajihusishi moja kwa moja na mambo ya ulimwengu huu; kwamba yeye ndiye muumba wa vyote na kwamba ni mkamilifu lakini mungu huyo, hajiingizi katika mambo ya ulimwengu unaonekana kwa njia ya miujiza na kuwa ufunuo sio chimbuko pekee la maarifa juu ya imani na kwamba kufikiri tu kwa mwanadamu na kufanya utafiti juu ya maumbile kunatosha kufahamu na kubainisha kwamba kuna Mungu mmoja.

Kwa hiyo, tafsiri ya imani hii ya Deism ni kwamba Mungu baada ya kuumba ulimwengu alijiondokea zake na kuacha vitu vyote tuvirithi na tokea wakati huo hana mpango navyo tena na wala hajali yanayoendelea huku duniani.

SASA katika mkururu huo wa kutaka kuchimbua mambo magumu ndio William Miller alijikuta akivamia suala ambalo ndio kiini cha mjadala huu wa leo.Ni suala la tarehe ya kurudi kwa YESU KRISTU.



Ni hivi, kwa muda miaka miwili William Miller alipata kujichimbia ndani kwake “akibundi” au akibukua Biblia na ndipo katika kukisoma Kitabu cha Nabii Daniel, sura 8:13-19 ambacho kiliandikwa kabla hata Yesu hajazaliwa akagundua fomula ya kukotoa tarehe ya kurudi kwa Yesu duniani ambako inasomeka hivi:

“13Ndipo nikamsikia mtakatifu mmoja akinena, na mtakatifu mwingine akamwuliza huyo aliyenena, Haya maono katika habari ya sadaka ya kuteketezwa ya daima, na lile kosa lifanyalo ukiwa, yataendelea hata lini, kukanyagisha patakatifu na jeshi? 14 Akamwambia, Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa. 15 Ikawa mimi, naam, mimi Danieli, nilipoyaona maono hayo, nalitafuta kuyafahamu, na tazama, alisimama mbele yangu mmoja mfano wa mwanadamu.16 Nikasikia sauti ya mwanadamu katikati ya mto Ulai, iliyoita na kusema, Gabrieli, mfahamishe mtu huyu maono haya.17 Basi alipakaribia mahali niliposimama; nami naliogopa alipokaribia, nikaanguka kifudifudi; lakini aliniambia, Fahamu, Ee mwanadamu, kwa maana maono haya ni ya wakati wa mwisho.18 Basi alipokuwa akisema nami, nalishikwa na usingizi mzito na uso wangu uliielekea nchi; lakini alinigusa, akanisimamisha wima.19 Akaniambia, Tazama, nitakujulisha yatakayokuwa wakati wa mwisho wa ghadhabu; maana, ni ya wakati wa mwisho ulioamriwa.”



Kanuni ya Miller inadai kwamba kinabii siku moja kwa Mungu ni sawa na mwaka mmoja wa Kalenda ya wakati huo na hata sasa. Kwa msingi hiyo, siku alizoziongelea Daniel kwa jicho la Miller ni sawa na miaka 2,300 kwa kutumia Kalenda ya wakati huo ambayo ilikuwa ni ya Gregori na ambayo inatumika hadi sasa. Kalenda ya Gregori ilianza kutumika nchini Marekani mwaka 1752. (Kalenda ya Gregori ilizinduliwa rasmimwaka 1582 na kuanza kutumiwa na nchi kama Ufaransa, Italia, Polandi, Ureno na Uhispania).

Katika Sadikifu(thesis) hiyo ya Miller, alikaza kudai kwamba wapo wasomi wengine kama yeye ambao tafiti zao zimeonyesha kuwa tarehe ya kurudi kwa Yesu INAKOKOTOLEKA KIRAHISI SANA. Miongoni mwa wanazuoni waliotajwa alikuwa ni Mwanasayansi Sir Issac Newton.Huyu kwa mjibu wa Miller anadai naye alipata kufanya hesabu kama zake (alipokuwa akitafiti juu ya Kanuni za asili zinazotawala mvutano kati ya Dunia na Jua, Laws of Gravity) na kupata majibu sawa na ya Miller juu ya unabii huo wa Biblia wa kurudi kwa Yesu, na kwamba Newton aliacha maandishi mengi sana juu ya jambo hilo!

Kwa maelezo ya Miller na kwa kadri ya “ufunuo wake” na kwa kanuni yake (ya Kitabu cha Daniel) na kwa kusoma historia, aliweza kwa hakika kwa madai yake kuona kuwa mwaka wa kuanza kuhesabika hizo siku 2,300 ambazo ni sawa na miaka 2,300 ilikuwa mwaka 457K.K. Kwa hiyo, kwa kutumia alichofanya ni kuchukua huo mwaka 457BK ns kutoa miaka 2,300 na hivi kupata jibu la 1843 kwamba ndiyo ingalikuwa ni muda wa kutakaswa “patakatifu pa patakatifu.” Hata hivyo baadaye tarehe ilisogezwa mbele hadi tarehe 22 Oktoba 1844.

Mathematically,Kanuni ya Miller ilikuwa ni hii:

2,300-457=1843 (siku ya kuingia Yesu duniani).


Vigezo alivyotumia Miller katika kuthibitisha Sadikifu yake

Kuna mambo mawili Miller aliyatumia katika kuthibitisha kwamba fomula yake ilikuwa sawa:

  • Miller alidai kuwa uelewa wa watu wa wakati wake ilikuwa kwamba patakatifu pa patakatifu kulimaanisha ulimwengu wetu tunamokaa.
  • Kutakaswaa kwa Ulimwengu tena kwa moto kulikuwa na maana ya kufikia mwisho na kufikia mwisho kwa dunia maana yake ni Yesu Kurudi?
Nini kilitokea baada ya Fomula ya kurudi Yesu kugunduliwa?

Baada ya Miller kuwa amechoropoka na fomula yake alianza kupita huko na huko akiwahubiria watu ili wachukue tahadhari kwa kujiandaa kumpokea Yesu.Miongoni mwao alikuwa mwanamama anayedaiwa kuwa “Nabii mahiri” sana kuwahi kutokea hapa duniani(kwa sababu aliwahi kupewa maono zaidi ya 2000) kusimika usabato duniani na ambaye anatajwa kuwa ndiye amepewa “maono” juu ya jinsi ambavyo Papa atawafumusha wasabato waanze kusali Jumamosi siku zijazo.

Msimamo wa yesu juu ya mwisho wa dunia

Utakumbuka kuwa Kitabu cha Daniel kiliandikwa miaka mingi sana kabla Yesu hajazaliwa.Na utaona kwamba hata Kanuni ya Miller juu ya kurudi kwake ilianza kuhesabiwa mwaka 457BK. Kwa hiyo, wakati Yesu anazaliwa kitabu cha Daniel kilikuwepo tayari na hizo habari za kutakaswa Patakatifu pa Patakatifu Yesu alikuwa amezisoma.

Pamoja na ukweli huo wote kwamba Yesu alikuwa amekisoma kitabu hicho bado alipoulizwa juu ya mwisho wa dunia alisema hivi kwa kadri ya Injili ya Matayo 24:35-38:

“35 Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.36 Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.37 Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.38 Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina.”


Analysis ya Sadikifu ya “Mwanahisabati” Miller

Kwa kuisoma Sadikifu (thesis) ya Miller na msimamo wa Yesu juu ya mwisho wa dunia,yafuatayo yanajitokeza:

1. Miller na wenzie walikosea wapi katika fomula yao kiasi kwamba Yesu hajawahi kuonekana toka mwaka 1843?

2. Je, wanahisabati wanaweza kuendeleza pale Miller na wenzie walipoishia katika kukokotoa mwisho wa dunia kwa kuihakiki hiyo fomula ya Kisabato juu ya kurudi kwa Yesu?

3. Je, Miller na wenzie hawakuwa wamefanikiwa kulisoma Agano Jipya ambamo msimamo wa Yesu juu ya tarehe ya mwisho wa dunia unawekwa wazi wazi kuwa tarehe husika haijulikani?

4. Je,ikiwa Miller na wafuasi wake akiwemo Mama wa “maono”,Ellen White, walikuwa wamelisoma Agano Jipya ni kwa nini wao waliamua kuasisi Fomula ya jambo ambalo Yesu alikwisha kusema hana uwezo nalo?

5. Je,kwa Yesu kusema haijui tarehe halafu Miller na Ellen White wakaja wakasema wanaifahamu tarehe ina maana Wasabato hao na wa leo mbingu ni yao kiasi kwamba wanaingia na kutoka hata wameweza kushirikishwa yanayoendelea huko Mbinguni?

6. Je,kwa Miller na Ellen kukubaliana kwamba wao walikuwa wameipata fomula ya kurudi kwa Yesu walimaanisha kwamba wao walikuwa ni wasomi sana na kwamba Yesu kusema haijui tarehe kulimaanisha Yesu alikisoma Kitabu cha Daniel na kutokikielewa au kwamba Yesu alikuwa anasoma mambo kwa kurukaruka?

7. Je, hadi sasa tumsikilize nani kati ya Yesu na wasabato juu ya mwisho wa dunia kwa sababu Ellen White ameshapewa maono yanayoonyesha kwamba Yesu ameshaanza kushuka na kwamba kwa sasa yuko katika chumba cha patakatifu pa patakatifu sana ambako anapitia majina ya wasabato na akitoka hapo moja kwa moja anatia timu hapa duniani?


Kwa yote hayo,sasa KARIBUNI kwa mjadala.
 
Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamjia faraghani, wakamuuliza, “Tuambie, mambo haya yatatukia lini, nayo dalili ya kuja kwako na ya mwisho wa dunia ni gani?”

Yesu akawajibu, “Jihadharini, mtu yeyote asiwadanganye. Kwa maana wengi watakuja kwa Jina langu, wakidai, ‘Mimi ndiye Kristo,’ nao watawadanganya wengi.

VITA: Mtasikia habari za vita na matetesi ya vita. Angalieni msitishike, kwa maana haya hayana budi kutukia. Lakini ule mwisho bado. Taifa litainuka dhidi ya taifa, na ufalme dhidi ya ufalme.

NJAA& MATETEMEKO: Kutakuwa na njaa na mitetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali. “Ndipo mtasalitiwa, ili mteswe na kuuawa, nanyi mtachukiwa na mataifa yote kwa ajili yangu.

UPENDO KUPOA: Wakati huo, wengi wataacha imani yao, nao watasalitiana kila mmoja na mwenzake na kuchukiana.

ROHO YA UONGO: Watatokea manabii wengi wa uongo, nao watawadanganya watu wengi. Kwa sababu ya kuongezeka kwa uovu upendo wa watu wengi utapoa, lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.

Injili ya Ufalme itahubiriwa ulimwenguni kote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote. Ndipo mwisho utakapokuja. “Hivyo mtakapoona lile ‘chukizo la uharibifu’ lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu (asomaye na afahamu), basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani. Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke ili kuchukua chochote kutoka ndani ya nyumba. Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake. Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo! Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi au siku ya Sabato. Kwa maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa dunia mpaka sasa: wala haitakuwako tena kamwe. Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna hata mtu mmoja ambaye angeokoka. Lakini kwa ajili ya wateule, siku hizo zitafupizwa. Wakati huo kama mtu yeyote akiwaambia, ‘Tazama, Kristo huyu hapa!’ Au, ‘Kristo yuko kule,’ msisadiki. Kwa maana watatokea makristo wa uongo na manabii wa uongo, nao watafanya ishara kubwa na maajabu mengi ili kuwapotosha, ikiwezekana, hata wale wateule hasa. Angalieni, nimekwisha kuwaambia mapema. “Kwa hiyo mtu yeyote akiwaambia, ‘Yule kule nyikani,’ msiende huko. Au akisema, ‘Yuko kwenye chumba,’ msisadiki. Kwa maana kama vile umeme utokeavyo mashariki na kuonekana hata magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu. Kwa maana popote ulipo mzoga, huko ndiko wakusanyikapo tai. “Mara baada ya dhiki ya siku zile, “ ‘jua litatiwa giza, nao mwezi hautatoa nuru yake; nazo nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za anga zitatikisika.’


UJIO WA PILI WA KRISTO: “Ndipo itakapotokea ishara ya Mwana wa Adamu angani, na makabila yote ya dunia yataomboleza. Nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya angani, katika uwezo na utukufu mkuu. Naye atawatuma malaika zake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwisho mwingine.
Mathayo 24:3‭-‬7‭, ‬9‭-‬31 NEN
Wanazuoni:

Kichwa cha habari hapo juu sio kwamba ni cha uchochezi au kwamba kimelenga kupasukia watu kwa kashifa au kwamba ni kufuru kwa Mungu.La hasha, bali ni tafsiri ya kile alichomaanisha Mwanajeshi mmoja huko Marekani pale alipoibuka na Formula ya kukokotoa tarehe ya kurudi kwake Yesu duniani. Jamaa huyo anaitwa WILLIAM MILLER.


William Miller
alizaliwa tarehe 15 Februari1782, huko Jimboni Massachusetts, Marekani na kisha kulelewa katika familia ya Kikristu iliyokuwa na makazi yake Jimbo la New York ya Kaskazini.Familia ya William Miller ilikuwa ya Kibaptisti. Babu yake na wajomba zake wawili walikuwa ni wachungaji katika kanisa la Wabaptisti. Kanisa la Kibaptisti, ni mumeguko karne ya 17 BK kutoka Kanisa la England,yaani Kanisa la Serikali ya Uingereza (Anglikani) ambalo leo linaitwa Lutheran Church.



Miller, katika ujana wake alipata kujiunga na jeshi laMarekani na kufikiaCheo cha Kapteini, wakati wa vita kati ya Marekani na Uingereza (Great Britain) mnamo mwaka 1812.Na inasemekana alikuwa na akili sana na kwamba alikuwa na kipaji cha kufafanua mambo.Bwana Miller baada ya kumaliza utumishi wake Jeshini na kurudi toka vitani (kati ya Marekani na Uingereza mwaka 1812), alianzisha makazi katika Shamba lake huko Low Hampton, New York, ambamo alikuwa amejenga nyumba na akawa akiishi hapo na wakati fulani akawa akienda kusali kwenye kanisa la Baptist la karibu yake.



Bwana Miller kwa kujishughulisha na mambo ya kiimani alipata kuwa mwana-DEIST,yaani alipata kuamini katika Falsafa ya Deism.

Deism ni Falsafa inayokazia kwamba Mungu hajihusishi moja kwa moja na mambo ya ulimwengu huu; kwamba yeye ndiye muumba wa vyote na kwamba ni mkamilifu lakini mungu huyo, hajiingizi katika mambo ya ulimwengu unaonekana kwa njia ya miujiza na kuwa ufunuo sio chimbuko pekee la maarifa juu ya imani na kwamba kufikiri tu kwa mwanadamu na kufanya utafiti juu ya maumbile kunatosha kufahamu na kubainisha kwamba kuna Mungu mmoja.

Kwa hiyo, tafsiri ya imani hii ya Deism ni kwamba Mungu baada ya kuumba ulimwengu alijiondokea zake na kuacha vitu vyote tuvirithi na tokea wakati huo hana mpango navyo tena na wala hajali yanayoendelea huku duniani.

SASA katika mkururu huo wa kutaka kuchimbua mambo magumu ndio William Miller alijikuta akivamia suala ambalo ndio kiini cha mjadala huu wa leo.Ni suala la tarehe ya kurudi kwa YESU KRISTU.



Ni hivi, kwa muda miaka miwili William Miller alipata kujichimbia ndani kwake “akibundi” au akibukua Biblia na ndipo katika kukisoma Kitabu cha Nabii Daniel, sura 8:13-19 ambacho kiliandikwa kabla hata Yesu hajazaliwa akagundua fomula ya kukotoa tarehe ya kurudi kwa Yesu duniani ambako inasomeka hivi:

“13Ndipo nikamsikia mtakatifu mmoja akinena, na mtakatifu mwingine akamwuliza huyo aliyenena, Haya maono katika habari ya sadaka ya kuteketezwa ya daima, na lile kosa lifanyalo ukiwa, yataendelea hata lini, kukanyagisha patakatifu na jeshi? 14 Akamwambia, Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa. 15 Ikawa mimi, naam, mimi Danieli, nilipoyaona maono hayo, nalitafuta kuyafahamu, na tazama, alisimama mbele yangu mmoja mfano wa mwanadamu.16 Nikasikia sauti ya mwanadamu katikati ya mto Ulai, iliyoita na kusema, Gabrieli, mfahamishe mtu huyu maono haya.17 Basi alipakaribia mahali niliposimama; nami naliogopa alipokaribia, nikaanguka kifudifudi; lakini aliniambia, Fahamu, Ee mwanadamu, kwa maana maono haya ni ya wakati wa mwisho.18 Basi alipokuwa akisema nami, nalishikwa na usingizi mzito na uso wangu uliielekea nchi; lakini alinigusa, akanisimamisha wima.19 Akaniambia, Tazama, nitakujulisha yatakayokuwa wakati wa mwisho wa ghadhabu; maana, ni ya wakati wa mwisho ulioamriwa.”



Kanuni ya Miller inadai kwamba kinabii siku moja kwa Mungu ni sawa na mwaka mmoja wa Kalenda ya wakati huo na hata sasa. Kwa msingi hiyo, siku alizoziongelea Daniel kwa jicho la Miller ni sawa na miaka 2,300 kwa kutumia Kalenda ya wakati huo ambayo ilikuwa ni ya Gregori na ambayo inatumika hadi sasa. Kalenda ya Gregori ilianza kutumika nchini Marekani mwaka 1752. (Kalenda ya Gregori ilizinduliwa rasmimwaka 1582 na kuanza kutumiwa na nchi kama Ufaransa, Italia, Polandi, Ureno na Uhispania).

Katika Sadikifu(thesis) hiyo ya Miller, alikaza kudai kwamba wapo wasomi wengine kama yeye ambao tafiti zao zimeonyesha kuwa tarehe ya kurudi kwa Yesu INAKOKOTOLEKA KIRAHISI SANA. Miongoni mwa wanazuoni waliotajwa alikuwa ni Mwanasayansi Sir Issac Newton.Huyu kwa mjibu wa Miller anadai naye alipata kufanya hesabu kama zake (alipokuwa akitafiti juu ya Kanuni za asili zinazotawala mvutano kati ya Dunia na Jua, Laws of Gravity) na kupata majibu sawa na ya Miller juu ya unabii huo wa Biblia wa kurudi kwa Yesu, na kwamba Newton aliacha maandishi mengi sana juu ya jambo hilo!

Kwa maelezo ya Miller na kwa kadri ya “ufunuo wake” na kwa kanuni yake (ya Kitabu cha Daniel) na kwa kusoma historia, aliweza kwa hakika kwa madai yake kuona kuwa mwaka wa kuanza kuhesabika hizo siku 2,300 ambazo ni sawa na miaka 2,300 ilikuwa mwaka 457K.K. Kwa hiyo, kwa kutumia alichofanya ni kuchukua huo mwaka 457BK ns kutoa miaka 2,300 na hivi kupata jibu la 1843 kwamba ndiyo ingalikuwa ni muda wa kutakaswa “patakatifu pa patakatifu.” Hata hivyo baadaye tarehe ilisogezwa mbele hadi tarehe 22 Oktoba 1844.

Mathematically,Kanuni ya Miller ilikuwa ni hii:

2,300-457=1843 (siku ya kuingia Yesu duniani).


Vigezo alivyotumia Miller katika kuthibitisha Sadikifu yake

Kuna mambo mawili Miller aliyatumia katika kuthibitisha kwamba fomula yake ilikuwa sawa:

  • Miller alidai kuwa uelewa wa watu wa wakati wake ilikuwa kwamba patakatifu pa patakatifu kulimaanisha ulimwengu wetu tunamokaa.
  • Kutakaswaa kwa Ulimwengu tena kwa moto kulikuwa na maana ya kufikia mwisho na kufikia mwisho kwa dunia maana yake ni Yesu Kurudi?
Nini kilitokea baada ya Fomula ya kurudi Yesu kugunduliwa?

Baada ya Miller kuwa amechoropoka na fomula yake alianza kupita huko na huko akiwahubiria watu ili wachukue tahadhari kwa kujiandaa kumpokea Yesu.Miongoni mwao alikuwa mwanamama anayedaiwa kuwa “Nabii mahiri” sana kuwahi kutokea hapa duniani(kwa sababu aliwahi kupewa maono zaidi ya 2000) kusimika usabato duniani na ambaye anatajwa kuwa ndiye amepewa “maono” juu ya jinsi ambavyo Papa atawafumusha wasabato waanze kusali Jumamosi siku zijazo.

Msimamo wa yesu juu ya mwisho wa dunia

Utakumbuka kuwa Kitabu cha Daniel kiliandikwa miaka mingi sana kabla Yesu hajazaliwa.Na utaona kwamba hata Kanuni ya Miller juu ya kurudi kwake ilianza kuhesabiwa mwaka 457BK. Kwa hiyo, wakati Yesu anazaliwa kitabu cha Daniel kilikuwepo tayari na hizo habari za kutakaswa Patakatifu pa Patakatifu Yesu alikuwa amezisoma.

Pamoja na ukweli huo wote kwamba Yesu alikuwa amekisoma kitabu hicho bado alipoulizwa juu ya mwisho wa dunia alisema hivi kwa kadri ya Injili ya Matayo 24:35-38:

“35 Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.36 Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.37 Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.38 Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina.”


Analysis ya Sadikifu ya “Mwanahisabati” Miller

Kwa kuisoma Sadikifu (thesis) ya Miller na msimamo wa Yesu juu ya mwisho wa dunia,yafuatayo yanajitokeza:

1. Miller na wenzie walikosea wapi katika fomula yao kiasi kwamba Yesu hajawahi kuonekana toka mwaka 1843?

2. Je, wanahisabati wanaweza kuendeleza pale Miller na wenzie walipoishia katika kukokotoa mwisho wa dunia kwa kuihakiki hiyo fomula ya Kisabato juu ya kurudi kwa Yesu?

3. Je, Miller na wenzie hawakuwa wamefanikiwa kulisoma Agano Jipya ambamo msimamo wa Yesu juu ya tarehe ya mwisho wa dunia unawekwa wazi wazi kuwa tarehe husika haijulikani?

4. Je,ikiwa Miller na wafuasi wake akiwemo Mama wa “maono”,Ellen White, walikuwa wamelisoma Agano Jipya ni kwa nini wao waliamua kuasisi Fomula ya jambo ambalo Yesu alikwisha kusema hana uwezo nalo?

5. Je,kwa Yesu kusema haijui tarehe halafu Miller na Ellen White wakaja wakasema wanaifahamu tarehe ina maana Wasabato hao na wa leo mbingu ni yao kiasi kwamba wanaingia na kutoka hata wameweza kushirikishwa yanayoendelea huko Mbinguni?

6. Je,kwa Miller na Ellen kukubaliana kwamba wao walikuwa wameipata fomula ya kurudi kwa Yesu walimaanisha kwamba wao walikuwa ni wasomi sana na kwamba Yesu kusema haijui tarehe kulimaanisha Yesu alikisoma Kitabu cha Daniel na kutokikielewa au kwamba Yesu alikuwa anasoma mambo kwa kurukaruka?

7. Je, hadi sasa tumsikilize nani kati ya Yesu na wasabato juu ya mwisho wa dunia kwa sababu Ellen White ameshapewa maono yanayoonyesha kwamba Yesu ameshaanza kushuka na kwamba kwa sasa yuko katika chumba cha patakatifu pa patakatifu sana ambako anapitia majina ya wasabato na akitoka hapo moja kwa moja anatia timu hapa duniani?


Kwa yote hayo,sasa KARIBUNI kwa mjadala.
 
Mnajadili "fix" tupu!
Kwa maana Lutheran haikutokea Anglican bali Roman Catholic.
Sasa kama hili lililo wazi kabisa machoni petu linadanganywa itakuwaje hayo ya miaka maelfu kadhaa iliyopita?
 
Huu mjadala mtamu sana ngoja nikitafute kitabu cha Daniel nikipitie alafu nirudi.

Ni kweli mjadala ni mzuri sana kwa sababu yawezekana tumepuuza jambo ambalo linaweza kutusaidia binadamu kujiandaa dakika za mwisho mwisho kabla Yesu hajaanza kutoka katika chumba cha "patakatifu pa patakatifu" na hivi nasi watenda dhambi kuingia pamoja na wasabato wateule.
 
Umeandika kiushabiki sana. Lengo lako ni kuwaattack wasabato na wala si vinginevyo.

Mambo mengi uliyoeleza hapa si ya kweli, kama ifuatavyo.

1. Miller haukuwa msabato na hata kipindi akiwa anahubiri kurudi kwa Yesu, hapakuwa na dhehebu la kisabato.

2. Mama White pia hakuwa msabato kipindi hicho maana hapakuwa na hilo dhehebu, na wala hakuwa mwanzilishi wa hiyo kanuni ya kurudi Yesu unayoisema, isipokuwa alikuwa mfuasi wa Miller.

3. Papa hatawafumusha wasabato kusali jumamosi kama ulivyodai, badala yake atawalazimisha watu wote kusali siku ya kwanza ya juma (yaani Jumapili) badala ya siku ya saba ya juma (yaani Jumamosi).

4. Yesu yuko katika chumba cha patakatifu pa patakatifu mbinguni akifanya huduma ya uombezi, na si kwamba ameshaanza kushuka kuja duniani kama unavyodai. Maana patakatifu pa patakatifu ni mbinguni.

5. Wasabato hawaja set siku yoyote ya kuja kwa Yesu kama unavyotaka kuwaaminisha watu, badala yake wamaamini kwamba Yesu amekaribia sana maana dalili karibia zote zimeshatimia.

6. Pamoja na kukosoa mahesabu ya Miller kuhusiana na unabii wa Daniel wa siku 2,300, hujatoa tafsiri mbadala wa unabii huo kana k
kwamba unabii huo hauna maana yoyote kwa wanadamu wa leo.

7. Ukweli ni kwamba, mahesabu ya Miller yalikuwa sahihi, kwamba mwaka 1844 kulikuwa na tukio kubwa lilikuwa linaenda kutokea. Kosa la Miller ni kwamba, alitafasri vibaya kuwa hekalu ni dunia na kutakaswa kwa Hekalu ni dunia kusafishwa kwa moto (kama ulivyoelezea vizuri kabisa).

Ukitaka kujua tafasri ya huo unabii wa siku 2,300 unakaribishwa kuuliza.

Hayo maombezi,Yesu anawaombea akina nani hapo "chumbani patakatifu pa patakatifu'?
 
Ilishaandikwa "Hakuna ajuaye siku wala saa ya kurudi kwa mwana wa Adam" ikimaanisha kurudi kwa Yesu Kristo ni siri ya Mungu mwenyewe, kwahiyo huyo Miller na wapuuzi wenzie waondolee huko upuuzi wao
Na ndivyo wazee wa kanisa walinifundisha, mpaka watakapobadilisha mafunzo hayo sibadili msimamo huo, wazee wa kanisa wakisema jambo sibadili msimamo wao hadi waseme tena vingjnevyo, halafu period!
 
Kanisa la anglikana ndio Lutherani ya leo???

Kuna tofauti kubwa mkuu.Kanisa la Anglikana ni lile ambalo muanzilishi wake ni Mfalme Henrio wa VII wa Uingereza.Huyu alijiondoa kutoka Kanisa Katoliki baada ya kukataliwa na Papa kumtaliki mke wake wa ndoa ili aweze kuvuta kimada.

Na Kanisa la Lutheran ni lile linaloitwa KKKT au wana matengenezo.Hili lilichomoka kutoka Kanisa Katoliki baada ya Padri anayeitwa Martin Luther kutengwa na kanisa katoliki kwa kudai alikuwa na mambo yake yaliyokuwa yanahitaji kufanyiwa kazi.
 
Kuna tofauti kubwa mkuu.Kanisa la Anglikana ni lile ambalo muanzilishi wake ni Mfalme Henrio wa VII wa Uingereza.Huyu alijiondoa kutoka Kanisa Katoliki baada ya kukataliwa na Papa kumtaliki mke wake wa ndoa ili aweze kuvuta kimada.

Na Kanisa la Lutheran ni lile linaloitwa KKKT au wana matengenezo.Hili lilichomoka kutoka Kanisa Katoliki baada ya Padri anayeitwa Martin Luther kutengwa na kanisa katoliki kwa kudai alikuwa na mambo yake yaliyokuwa yanahitaji kufanyiwa kazi.
Na lilianza Lutheran ,kisha wakafuata Anglican si ndio Mkuu ?
 
Kuna tofauti kubwa mkuu.Kanisa la Anglikana ni lile ambalo muanzilishi wake ni Mfalme Henrio wa VII wa Uingereza.Huyu alijiondoa kutoka Kanisa Katoliki baada ya kukataliwa na Papa kumtaliki mke wake wa ndoa ili aweze kuvuta kimada.

Na Kanisa la Lutheran ni lile linaloitwa KKKT au wana matengenezo.Hili lilichomoka kutoka Kanisa Katoliki baada ya Padri anayeitwa Martin Luther kutengwa na kanisa katoliki kwa kudai alikuwa na mambo yake yaliyokuwa yanahitaji kufanyiwa kazi.
Nimekuelewa, rekebisha kwenye mada umeandika Lutherani ya leo asili yake ni anglikana.
 
Kuna tofauti kubwa mkuu.Kanisa la Anglikana ni lile ambalo muanzilishi wake ni Mfalme Henrio wa VII wa Uingereza.Huyu alijiondoa kutoka Kanisa Katoliki baada ya kukataliwa na Papa kumtaliki mke wake wa ndoa ili aweze kuvuta kimada.

Na Kanisa la Lutheran ni lile linaloitwa KKKT au wana matengenezo.Hili lilichomoka kutoka Kanisa Katoliki baada ya Padri anayeitwa Martin Luther kutengwa na kanisa katoliki kwa kudai alikuwa na mambo yake yaliyokuwa yanahitaji kufanyiwa kazi.
Mkuu kwenye maada ukaedit kule ili kutowachanganya watu kwani kuna sehemu umeandika lutherani ilitokana na kanisa la Anglican
 
Ume-panic sana mpaka inafikia hatua umeamua kujitungia mambo....Hebu kaa chini usome mada ueleww.....mbona mada ina mlenga nwana hisabati nguli wa kukokotoa tarehe Bw William Miller....

Mada haimuongelei Ellen G White.....Kwanini unalazimisha kumuweka Ellen G White....?
Soma yale maswali yake ndo utaona alikuwa analenga nini?
 
Back
Top Bottom