Willy Gamba, Hofu, Njama, na E MUSIBA, Mnakumbuka Enzi Hizo?

Willy Gamba, Hofu, Njama, na E MUSIBA, Mnakumbuka Enzi Hizo?

Kifo chake kilinihuzunisha na kunifanya nilie sana, tena nilishamjengea picha flan kichwani mwangu so alikuwa kama ana-exist katika upeo wangu


Na kifo chake kilianza hivI: "Bosi, twende haraka Veronika amenipigia simu anasema yuko katika matatizo, nimekuja sababu nilijua huna gari" Eddy alisema huku akitweta.

Halafu wanaume tulivyokuwa siyo, hapa jamaa alikuwa kwa mrembo Zabibu Abeid, Binti Mtanzania, akimwagia sifa kuwa hajaonapo mrembo kuliko yeye-ilisikitisha sana kwa kweli ukizingatia wakati fulani Willy Gamba aliokolewa na Veronika pale alipotekwa.

Hebu Mbuzi Mzee tumwagie mkuu, kitambo lakini tunakumbuka japo baadhi ya visa vilivyomo,
 
Mtoa mada umetukumbusha mbali sana,je kitabu chenye title ya "kikomo" kilifika sokoni,nani anacho?kwa bahati nzuri nilibahatika kuvisoma vyote mpaka hiki cha mwisho willy gamba alichoenda rwanda.
 
Niiegesha gari langu kwenye maegesho ya Hoteli ya New Afrika. Nikatelemka na kuzunguka ili nimfungulie Veronika. Tuliingia New Afrika Hoteli katika sehemu iitwayo duka la Kahawa tukatafuta meza tukaa.

"Ulishastafutahi?", nilimuuliza Veronika.

"Kawaida yangu huwa ninastafutahi kabla ya kufanya mazoezi kila siku, ili kujiweka katika hali nzuri".

"Ndio sababu umbo lako linapendeza namna hiyo".

"Asante".

Mtumishi wa hoteli alifika na kutuuliza mahitaji yetu.

"Mimi nitakunywa maji ya machungwa kama yapo".Veronika alisema.

"Mimi niletee maji ya ndimu". niliagiza.

Alipoondoka mtumishi huyo nilimweleza Veronika kuwa mimi nitakwenda mapokezi kumwita Sherriff, ambaye niliamini alikuwa bado chumbani.

"Habari za leo Tom?", nilimsalimia kijana wa mapokezi ambaye tunafahamiana vizuri sana.

"Aha mzee, shikamoo", alinisalimia.

"Marahaba", nilimjibu.

"Sijui nikusaidie nini mzee?".

"Kuna mgeni wangu hapa anaitwa Ahmed Sherriff, alifika usiku".

"Ndio ndio, yuko yuko namba 406, unahitaji kwenda huko au nimpigie simu".

"Mpigie simu nizungumze nae".

Alimpigia simu na alipompata akanipa.

"Hallo Sherriff habari za leo?".

"Ohoo, Willy salama?, nilikuwa ninakusubiri kwa hamu".

"Oke, telemka chini. Tuko hapa duka la kahawa pamoja na Veronika".

Oh, amekwisha wahi namna hii?".

"Sana tena".

"Oke nakuja sasa hivi".

"Haya tunakusubiri", nilimjibu na kukata simu.

"Oke Tom asante sana", nilimwambia kijana wa mapokezi.

"Asante mzee karibu", alijibu Tom.

"Asante niko hapa duka la kahawa".

Niliporudi nilikuta vinywaji tayari.

"Yupo?", aliuliza Veronika.

"Yupo, anakuja sasa hivi", nilimjibu.
 
Haukupita muda Sherriff alitokea na kuja moja kwa moja mezani kwetu. Tulisalimiana akavuta

kiti na kuketi. Mtumishi aliyekuwa anatuhudumia alipomuona alikuja mara moja.

"Mzee nikusaidie nini?," alimuuliza Sherriff.

"Kuna maji ya nanasi?".

"Ndio, yapo".

"Haya niletee hayo, lakini weka barafu nyingi, maana si joto hili".

"Bila ya wasiwasi mzee".

Mtumishi alipoondoka tulikaa kimya tunatazamana kwanza kila mtu anashindwa kuanza

mazungumzo. Veronika aipoona hivi akatabasamu kisha akasema. Sherriff wewe kidogo uko nyuma

ya habari, lakini nitakueleza kwa kifupi ili kukuweka pamoja nasi katika habari zinazotuhusu

wote".

"Nitakushukuru", alijibu Sherriff.

"Willy nimemweleza yote tunayojua juu yake, na jambo la kushangaza ni kwamba na yeye

anatufahamu sisi huenda kuliko tunavyojifahamu wenyewe".

"Usitie chumvi", nilimuasa.

"Ala!", Sherriff alitamka kwa mshangao mkubwa. "Kama ni hivyo basi ni vizuri sana. Kwani

wote sasa tunafahamiana misimamo yetu. Unajua mimi nilishangaa sana usiku pale uwanja wa

ndege. Waandishi wote wengine wa magazeti mbali mbali ulimwenguni tuliokuja nao wamekataliwa

kuingia hapa nchini, na tumewaacha uwanja wa ndege wakilalamika vibaya sana wakiomba kuonana

na mabalozi wao, lakini sisi tumeruhusiwa kwa urahisi sana, kitu hiki kilinishangaza sana

nikahisi lazima huu utakuwa mpango wa Willy. Sasa nimeamini kabisa. Uongo au kweli".

Sherriff aliuliza huku akiniangalia.

"Bila shaka niliwaahidi toka tukiwa Freetown kuwa mnakaribishwa kwa dhati Tanzania, sasa

nimetimiza ahadi yangu".

"Asante sasa", Sherriff alijibu.

"Mimi naamini unajua tumekuja kwa ajili gani, na vile vile naamini likizo yako imekatishwa

kwa ajili sababu hiyo hiyo tuliyoijia sisi", Veronika aieleza huku macho yake yaking'aa

kuonesha kuwa sasa tulikuwa tunazungumza kikazi.

"Sawa, endelea", nilimjibu.

"Mimi naonelea tungeliungana na wewe, kwani wewe ukiwa mwenyeji itakuwa kazi rahisi kwetu

kuweza kupata habari. Sijui wewe unaonaje?".

"Kwa taarifa yenu lazima niwaeleze kuwa tukio hili lililotokea si la kawaida. Mnaweza kuwa

mmeshiriki katika mambo ya hatari sana kama vile mambo ya vita, lakini lazima

niwatahadharishe kuwa kutafuta habari za aina yoyote zinazoweza kufichua kundi lililofanya

ujahiri wa hari ya juu ni hatari sana kwa maisha yenu kuliko hatari yoyote mliyokwisaha

kuikabiri. Nadhani mmenielewa. Ningewaomba ili kuponya maisha yenu muwe watoto wazuri,

muachane kabisa na kuuliza uliza habari za tukio hili".

"Kabla hatujatoka ofisini kwetu London, tumetahadharishwa kama unavyotutahadharisha sasa,

lakini tulikaa tukaamua kuwa tutaendelea; Lolote baya litakalotupata tutakuwa tumetoa damu

yetu kwa ajili ya ndugu zetu. Kwani sisi tunaamini watu waliofanya kitendo hiki si watu

wengine bali ni mabeberu wapinga ukomboni wa kusini mwa Afrika", alijibu Sherriff kwa nia

moja.

"Kama uamuzi wenu ni huo basi tutashirikiana kwa kadiri tutakavyoweza".

"Mlikuwa na nia ya kuanza kutafuta habari tokea lini?".

"Tokea sasa hivi kama unaweza kutupa fununu tuanzie wapi!", Sherriff alijibu.

Kwa vile katika mpango wangu wa upelelezi nilikuwa nimepanga kuwatumia ndugu hawa. niifurahi

sana kuona kuwa mambo yaikuwa yanakwenda kama nilivyopanga. Hivyo niliamua kuwaeleza kwa

kirefu maelezo aliyokuwa amenieleza Chifu.

"Ili kuwaweka sawasawa ninyi katika picha ya tukio hili mtakuwa wageni wa kampuni yangu. Kwa

hiyo mimi naona tangia sasa nitakuwa ni wakala wa gazeti lenu, kwa kufanya hivi nitapata

kisingizio cha kutembea na kupeleleza na nyinyi mkiwa kama wateja wangu; nafikiri

mmenielewa?".

Wote walitingisha vichwa kuonesha kuwa wamenielewa. Kutokana na mipango yangu ilivyokuwa

nilionelea tokea wakati huo tuanze kazi bila kupoteza muda.

Nilitoa onyo tena "Kukubali kwenu kushiriki na mimi katika upelelezi wa tukio hili mjue

kabisa mmejiwekea sahihi ya kifo. Natoa natoa muda wa mwisho kama kuna mtu anaona wasiwasi

katika moyo wake nampa nafasi aache shughuli hii", niliwaasa na kuwaangalia kwa makini sana.

Mwisho Veronika akasema

"Unajuwa Willy dakika ile mtu anapozaliwa pale pale anapewa huku ya kifo. Nina maana ya

kusema kuwa binadamu hata aishi vipi kufa lazima atakufa. Kule kuishi baada ya kuzaliwa ina

maana kuwa ile hukumu ya kifo inaahirishwa kutekelezwa. ..

ITAENDELEA
 
"Unajuwa Willy dakika ile mtu anapozaliwa pale pale anapewa huku ya kifo. Nina maana ya kusema

kuwa binadamu hata aishi vipi kufa lazima atakufa. Kule kuishi baada ya kuzaliwa ina maana

kuwa ile hukumu ya kifo inaahirishwa kutekelezwa.Wengine huahirishwa kwa mwezi mmoja. Hivyo

mtoto anazaliwa na baada ya mwezi mmoja anakufa. Hii si ajabu maana hukumu yake ya kifo

imetekelezwa baada ya mwezi mmoja. Wengine huishi hata miaka mia moja. Hii ina maana kuwa

hukumu yake aliyopewa dakika alipozaliwa imetekelezwa baada ya miaka mia.Hivyo kila mtu na

sehemu yake ya kuishi. Kwa hiyo kuogopa kufa ni ujinga."

"Mimi sina wasiwasi, maana kifo cha namna hii, nitakuwa nimekufa kifo cha heshima", alisema

Sherriff.

"Okke, sasa naamini nina watu. Tokea sasa nyinyi si ndugu tena ila ni makomredi", niliwaeleza.

"Kwani komredi ina maana kubwa zaidi ya ndugu?", Veronika aliuliza.

"Hasa, ina maana kali zaidi. Komredi ina maana mwenzi katika harakati".

"Asante komredi Willy, naona tunywe maji haya katika jina la komredi", Veronika aliomba. Wote

tukagonganisha glasi zetu.

"Sasa mimi naonelea itabidi tuanze upelelezi wetu bandarini. Itabidi tukamuone ofisa

aliyehusina ili na sisi tupate habari toka kwake ana kwa ana ingawaje atakuwa amekwisha

sumbuliwa sana na polisi na maafisa usalama kwa maswali. Huenda sisi tukapata jambo ambalo

huenda wao wameliruka. Halafu tukaendelea hivyo hivyo katika ofisi zote zilizohusika kabla

hatujachukua hatua kali zaidi", mnaonaje.

"Sawa", walijibu kwa pamoja.

Tulinyanyuka na kuelekea kwenye gari langu, nikawafungulia milango. Veronika alikaa mbele na

mimi. Sherriff akakaa nyuma. Nilipotaka kuwasha gari moto niliona kijikaratasi chini,

nikakiokota taratibu nikakisoma. Eddy alikuwa ameniandikia namba zote za magari aliyokodi.

Akionesha namba za magari aliyoacha kwenye maegesho ya New Afrika na Kilimanjaro Hoteli kama

nilivyokuwa nimeamru. Nilianza kusikia msisimko wa damu ikionyesha kuwa kazi imeanza. Nilipiga

gari moto tukaelekea bandarini.

MIWSHO WA SURA YA TATU


NJAMA
FUNUNU
SURA YA NNE
"Samahani binti tunaomba kumuona Meneja", nilimwambia mwandishi mahsusi wa Meneja wa Bandari.

"Sijui nyinyi ni akina nani?", aliuliza msichana huyu aliyeonekana amechoka choka.

"Mwambie ni Willy Gamba na wateja wake kutoka gazeti la Afrika".

Meneja wa Bandari tulikuwa tunafahamiana kikazi, hasa kutokana na shughuli zingine tulizokuwa

tunazifanya katika kampuni yetu ya Afrika Internation Agencies.

Yule msichana alizungumza na bosi wake kwa simu, alipomaliza alinyanyuka na kutufungulia

mlango tukaingia ndani. Tulimkuta Issack Mlingi ambaye ndiye Meneja wa Bandari aliyehusika na

tukio hili akionyesha hali ya kuchoka sana. Nafikiri hii ilitokana na bughudha alizopata toka

kwa polisi na watu wengine wanaohusika na upelelezi wa tukio hili. Macho yake yalikuwa mekundu

na yamevimba.

"Karibuni ndani", alisema huku akinyanyuka ili tusalimiane.

"Samahani ndugu Mlingi, naamini una shughuli nyingi sana", nilimuomba radhi.

"Si kitu Gamba, karibuni".

"Hawa ni wateja wangu Sherriff na Veronika kutoka gazeti la Afrika ambalo kampuni yangu ni

wakala wake, na jamani huyu ni Issack Mlingi, Meneja wa Bandari", walipeana mikono kisha wote

tukavuta viti tukakaa.

"Ndugu Mlingi ni imani yangu kuwa umeisha ulizwa maswali mengi juu ya tukio hili lililotokea

hapa bandarini. Lakini naamini hatutakuwa tumekuhangaisha kama tutakuuliza maswali. Kama

nilivyokwisha kwambia hawa waandishi wa gazeti la Afrika na ni waandishi pekee walioruhusiwa

kuingia hapa nchini kuandika juu ya tukio hili, naamini unajua msimamo wa gazeti la Afrika.

Hata hivyo tutakuuliza maswali kidogo tu kusudi tusikuchoshe sana".

"Hebu nipeni vitambulisho vyenu niviangalie", aliomba.

Sherriff na Veronika walimpa vitambulisho, akaviangalia na aliporidhika akavirudisha.

"Haya ulizeni maswali yenu, maana ikiendelea hivi naweza kupata wazimu", alisema huku akitoa

tabasamu la uchovu.

"Tumesoma maelezo yako uliyotoa polisi, ila tumekuja hapa kukuuliza maswali machache juu ya

mambo ambayo hatukuwa tumeyaelewa vizuri", alisema Sherriff.

"Ulieleza kuwa ulipata simu kutoka kwa Jones Mantare ambaye umezoea sana sauti yake, kiasi

kwamba huwezi kuikosea ukiisikia. Lakini jambo la kushangaza ni kwamba, Mantare anasema hakuwa

amekupigia simu kwani alikuwa na mkutano na Mwenyekiti wa Kamati na Mwenyekiti amethibitisha

kuwa ni kweli walikuwa wote toka saa tisa hadi saa kumi na moja. Baada ya kupata maelezo hayo

bado unaweza kusema kuwa sauti ile ni sawa kabisa na ya Mantare?".

"Kwa sababu wakati ule nilikuwa sina wasiwasi kuwa kuna jambo baya roho yangu iliridhika kuwa

ni Mantare. Lakini sasa kwa sababu Mantare anasema hakupiga simu, ndipo nakumbuka kuwa

nilimwuliza kama ana mafua, maana kwa mbali alikuwa akizungumzia puani, na yeye alijibu kweli

mafua yalikuwa yamemkaba sana. Lakini maelezo mengine, mathalani ambayo huwa tunataniana na

Jonas, yalikuwa yote sawa. Kusema kweli inawezekana kabisa alikuwa mtu mwingine anayemfahamu

sana, lazima niseme sana maana isingekuwa hili jambo la mafua bado ningeendelea kung'ang'ania

alikuwa Jones. Lakini Jones amekuja hapa hana mafua hata kidogo kwa siku nyingi".

"Hebu fikiria tena kidogo juu ya sura na sauti au umbile na tabia ya huyu mtu aliyekuwa

akijiita Meja Paul Liboi, unaweza kuwa na uhakika kabisa kuwa mtu huyu ni mzalendo wa

Tanzania?", Veronika aliuliza.

Ndugu Mlingi alisita kidogo kujibu swali hili na uso wake ukakunjamana kidogo. Baada ya

kufikiri sana akasema.

"Nafikiri anaweza asiwe mzalendo".

Wote tukamwangalia.

"Kwanini unafikiri hivyo?", mimi nilimuuliza.

"Wazo hili lilikuwa halijaingia kichwani mwangu, lakini sasa baada ya kuuliza swali hili

inawezekana mtu huyu asiwe mtanzania maana kwanza kiswahili chake hakikuwa kimenyooka na

alipenda sana kuchanganya na kiingereza. Mimi nilimfikiria kuwa huenda ni Mjaruo, lakini

alikuwa hajang'oa meno. Vile vile alikuwa na haraka haraka na maneno ya mkato mkato. Nikifiri

sana hakuna na ile hali ya kirafiki waliyonayo watanzania wengine wengi. Lakini kwa sababu

nilijuwa ni mwanajeshi nikafikiri ndio sababu aikuwa na tabia ya namna hiyo".

"Una jambo jingine ambalo huenda sasa unafikiri halikuwa lakawaida juu ya tukio lolote baada

ya kujuwa watu hawa walikuwa majahiri?".

"Nafikiri nimeshasema yote, ila tu huenda kitu kimoja, sijui kama kinahusika ama vipi".

"Ehe, kitu gani".

"Baada ya kuzungumza na huyo anayejiita Jones Mantare, simu za jengo hili hazikufanya kazi

tena. Tulipowaeleza Posta kesho yake, walikuja mafundi na kusema waya inayounganisha jengo

hili na waya zinazokwenda Posta ilikuwa imekatika kwa kuangukiwa na mti. Sasa nilianza kuona

picha kidogo ya tukio hili. Nilijua mara moja kuwa watu waliokuwa wameshughulikia tukio hili

ni watu wenye kujua ujasusi wa hali ya juu; kwani walihakikisha kuwa kila hatua wanayoichukua

na nyayo zake wanazifuta ili asiwepo mtu wa kuzifuatiia".

TUjikuta tumeridhishwa sana na safari yetu ya bandarini hivyo tukaona tuondoke.

"Asante sana ndugu Mlingi, kama tukihitaji mambo zaidi tutakuona tena, na kama utakumbuka kitu

cochote kinachoweza kutusaidia nipigie simu. Nafikiri simu yangu unayo?", nilimuuliza.

"Ndio ninayo", alijibu.

"Na tahadhali usizungumze ovyo juu ya tukio hili, maana si tukio zuri", nilimwonya.

"Bila shaka nitajitahidi".

Tuliagana nae, tukaondoka kuelekea mjini.

INAENDELEA...
 
SURA YA NNE
FUNUNU
"Samahani binti tunaomba kumuona Meneja", nilimwambia mwandishi mahsusi wa Meneja wa Bandari.

"Sijui nyinyi ni akina nani?", aliuliza msichana huyu aliyeonekana amechoka choka.

"Mwambie ni Willy Gamba na wateja wake kutoka gazeti la Afrika".

Meneja wa Bandari tulikuwa tunafahamiana kikazi, hasa kutokana na shughuli zingine tulizokuwa tunazifanya katika kampuni yetu ya Afrika Internation Agencies.

Yule msichana alizungumza na bosi wake kwa simu, alipomaliza alinyanyuka na kutufungulia mlango tukaingia ndani. Tulimkuta Issack Mlingi ambaye ndiye Meneja wa Bandari aliyehusika na tukio hili akionyesha hali ya kuchoka sana. Nafikiri hii ilitokana na bughudha alizopata toka kwa polisi na watu wengine wanaohusika na upelelezi wa tukio hili. Macho yake yalikuwa mekundu na yamevimba.

"Karibuni ndani", alisema huku akinyanyuka ili tusalimiane.

"Samahani ndugu Mlingi, naamini una shughuli nyingi sana", nilimuomba radhi.

"Si kitu Gamba, karibuni".

"Hawa ni wateja wangu Sherriff na Veronika kutoka gazeti la Afrika ambalo kampuni yangu ni wakala wake, na jamani huyu ni Issack Mlingi, Meneja wa Bandari", walipeana mikono kisha wote tukavuta viti tukakaa.

"Ndugu Mlingi ni imani yangu kuwa umeisha ulizwa maswali mengi juu ya tukio hili lililotokea hapa bandarini. Lakini naamini hatutakuwa tumekuhangaisha kama tutakuuliza maswali. Kama nilivyokwisha kwambia hawa waandishi wa gazeti la Afrika na ni waandishi pekee walioruhusiwa kuingia hapa nchini kuandika juu ya tukio hili, naamini unajua msimamo wa gazeti la Afrika. Hata hivyo tutakuuliza maswali kidogo tu kusudi tusikuchoshe sana".

"Hebu nipeni vitambulisho vyenu niviangalie", aliomba.

Sherriff na Veronika walimpa vitambulisho, akaviangalia na aliporidhika akavirudisha.

"Haya ulizeni maswali yenu, maana ikiendelea hivi naweza kupata wazimu", alisema huku akitoa tabasamu la uchovu.

"Tumesoma maelezo yako uliyotoa polisi, ila tumekuja hapa kukuuliza maswali machache juu ya mambo ambayo hatukuwa tumeyaelewa vizuri", alisema Sherriff.

"Ulieleza kuwa ulipata simu kutoka kwa Jones Mantare ambaye umezoea sana sauti yake, kiasi kwamba huwezi kuikosea ukiisikia. Lakini jambo la kushangaza ni kwamba, Mantare anasema hakuwa amekupigia simu kwani alikuwa na mkutano na Mwenyekiti wa Kamati na Mwenyekiti amethibitisha kuwa ni kweli walikuwa wote toka saa tisa hadi saa kumi na moja. Baada ya kupata maelezo hayo bado unaweza kusema kuwa sauti ile ni sawa kabisa na ya Mantare?".

"Kwa sababu wakati ule nilikuwa sina wasiwasi kuwa kuna jambo baya roho yangu iliridhika kuwa ni Mantare. Lakini sasa kwa sababu Mantare anasema hakupiga simu, ndipo nakumbuka kuwa nilimwuliza kama ana mafua, maana kwa mbali alikuwa akizungumzia puani, na yeye alijibu kweli mafua yalikuwa yamemkaba sana. Lakini maelezo mengine, mathalani ambayo huwa tunataniana na Jonas, yalikuwa yote sawa. Kusema kweli inawezekana kabisa alikuwa mtu mwingine anayemfahamu sana, lazima niseme sana maana isingekuwa hili jambo la mafua bado ningeendelea kung'ang'ania alikuwa Jones. Lakini Jones amekuja hapa hana mafua hata kidogo kwa siku nyingi".

"Hebu fikiria tena kidogo juu ya sura na sauti au umbile na tabia ya huyu mtu aliyekuwa akijiita Meja Paul Liboi, unaweza kuwa na uhakika kabisa kuwa mtu huyu ni mzalendo wa Tanzania?", Veronika aliuliza.

Ndugu Mlingi alisita kidogo kujibu swali hili na uso wake ukakunjamana kidogo. Baada ya kufikiri sana akasema.

"Nafikiri anaweza asiwe mzalendo".

Wote tukamwangalia.

"Kwanini unafikiri hivyo?", mimi nilimuuliza.

"Wazo hili lilikuwa halijaingia kichwani mwangu, lakini sasa baada ya kuuliza swali hili inawezekana mtu huyu asiwe mtanzania maana kwanza kiswahili chake hakikuwa kimenyooka na alipenda sana kuchanganya na kiingereza. Mimi nilimfikiria kuwa huenda ni Mjaruo, lakini alikuwa hajang'oa meno. Vile vile alikuwa na haraka haraka na maneno ya mkato mkato. Nikifiri sana hakuna na ile hali ya kirafiki waliyonayo watanzania wengine wengi. Lakini kwa sababu nilijuwa ni mwanajeshi nikafikiri ndio sababu aikuwa na tabia ya namna hiyo".

"Una jambo jingine ambalo huenda sasa unafikiri halikuwa lakawaida juu ya tukio lolote baada ya kujuwa watu hawa walikuwa majahiri?".

"Nafikiri nimeshasema yote, ila tu huenda kitu kimoja, sijui kama kinahusika ama vipi".

"Ehe, kitu gani".

"Baada ya kuzungumza na huyo anayejiita Jones Mantare, simu za jengo hili hazikufanya kazi tena. Tulipowaeleza Posta kesho yake, walikuja mafundi na kusema waya inayounganisha jengo hili na waya zinazokwenda Posta ilikuwa imekatika kwa kuangukiwa na mti. Sasa nilianza kuona picha kidogo ya tukio hili. Nilijua mara moja kuwa watu waliokuwa wameshughulikia tukio hili ni watu wenye kujua ujasusi wa hali ya juu; kwani walihakikisha kuwa kila hatua wanayoichukua na nyayo zake wanazifuta ili asiwepo mtu wa kuzifuatiia".

TUjikuta tumeridhishwa sana na safari yetu ya bandarini hivyo tukaona tuondoke.

"Asante sana ndugu Mlingi, kama tukihitaji mambo zaidi tutakuona tena, na kama utakumbuka kitu cochote kinachoweza kutusaidia nipigie simu. Nafikiri simu yangu unayo?", nilimuuliza.

"Ndio ninayo", alijibu.

"Na tahadhali usizungumze ovyo juu ya tukio hili, maana si tukio zuri", nilimwonya.

"Bila shaka nitajitahidi".

Tuliagana nae, tukaondoka kuelekea mjini.

Nilijaribu nilivyoweza kuangalia kama naweza kumwona Eddy na mwenzake, lakini wapi hakika vijana walikuwa wanafanya kazi nzuri sana, maana kama mimi Willy sikuweza kuwatambua basi hakuna mtu mwingine tena, si kama najisifu ila huo ndio ukweli, mtu akitaka kunitafuta mimi basi ajiweke sawa, la sivyo shauri lake.

"Kamara kama ulivyomjua alikuwa mtu wa namna gani, unafiri anaweza kwa njia yoyote akawa kajiingiza katika jambo hili?", nilimuuliza Sherriff huku tukiwa tumesimama kungojea kuingia barabara ya site drive, tukutokea bandarini.

"Mimi nakuhakikishia komredi kuwa Kamara alikuwa hawezi kufanya jambo kama hilo, ni lazima tu iko namna ambayo alishambuliwa na kunyang'anywa karatasi hizo, alinihakikishia Sherriff.

"Oke, naona sasa twende kwenye ofisi ya kamati ya Ukombozi ya OAU", nilimweleza huku nageuza gari kuingia site drive na kuelekea kwenye ofisi ya kamati.

Tulipofika kwenye mapokezi ya ofisi hii ya kamati na kumkuta msichana mmoja akizungumza kwenye simu, ikatubidi tumsubiri kidogo amalize kuzungumza, niliangalia saa yangu ilikuwa yapata saa sita na dakika tano.

"Samani jamani, sijui niwasaidie nini", msichana alituuliza.

"Bila samahani binti, sisi tunaomba kumwona Jones Mantare", nilijibu.

"Mna ahadi naye?", binti aliuliza.

"Hapa, lakini nafikiri ukimwambia Willy Gamba wa AIA na wageni toka gazeti la Afrika, ambao wanataka kumwona, anaweza kutuona", nilimweleza.

"Msubiri basi", huyo msichana alijibu kisha akainua simu na kuanza kuzungumza na ofisi ya Mantare. Jones Mantare alikuwa ananifahamu, maana nilikuwa nimehakikisha kuwa nafahamiana karibu na kila mtu katika ofisi hii ya kamati, yeye alikuwa akinifahamu kama mfanyabiashara, maana ndivyo nilivyojulishwa kwake. Tokea hapo tulikuwa tunaonana mara kwa mara sehemu za starehe na kujenga uelewano wa kutosha, hivyo nilihisi kuwa asingeweza kunikatalia nisimuone, ingawa nilijuwa atakuwa katika hali isiyokuwa ya kawaida. Baada ya kuzungumza kwa muda kwenye simu msichana alitwambia.

"Mnaweza kwenda kumwona, ofisi yake ipo mwisho wa ujia mkono wa kulia".

"Asante sana binti", nilimjibu.

Tulimwacha tukaelekea alikotuelekeza. Tulibisha mlango pale tulipokuwa tumeelekezwa.

"Karibu", tulisikia sauti ya msichana ikitoka ndani. Nilifungua mlango tukaingia na tujikuta katika ofisi kubwa ya mwandishi mahsusi wa Mantare.

"Habari zako bibie", nilimsalimia kwa niaba ya mwenzangu.

"Nzuri, ni Gamba na wenzake nafikiri?", aliuliza.

"Hasa", nilijibu.

"Ingieni moja kwa moja anawasubiri", alisema huku akisimama na kutufungulia mlango wa bosi wake. Tulipoingia tu Mantare alisimama.

"Ahaa ndugu Willy, karibuni".

"Asante, asante Jones".

"Nafikiri niwajulishe, huyu ni ndugu Jones Mantare, ofisa katika kamati hii ya ukombozi, na hawa ni komredi Ahmedi Sherriff na komredi Veronika Amadu. Ni waandishi wa habari wa gazeti la "AFRIKA".

Walipeana mikono kwa mara nyingine.

"Ehe, mlitaka kuniona, sijui niwasaidie nini?", aliuliza.

"Hawa makomredi ni wateja wangu, kampuni yangu ndio wakala wa gazeti la Afrika hapa nchini. Hasa kitu kilichotueta hapa ni kutokana na tukio hili la juzi. Nafikiri unaelewa msimamo wa gazeti la Afrika katika ukombozi, na kutokana na msimamo huo wameiomba serikali kama wanaweza kuandika habari za kuaminika juu ya tukio hili. Ni wasiwasi wao kuwa magazeti mengi ya kibeberu yataandika habari za kupotosha, na wao wako hapa ili waweze kueleza jumuia ya ulimwengu ukweli mtupu. Kwa hiyo tutashukuru sana ukiweza kutusaidia katika kujibu maswali machache. Hatutataka kupoteza muda wako kutueleza mengi, maana nakala ya maelezo yako tumeipata toka polisi. Hivi ni nia yetu uweze kutufafanulia katika sehemu ambazo hazieleweki katika tukio hili".

Niliona kule kutaja nakala ya maelezo yake kutoka polisi kulimtoa wasiwasi aliokuwa ameuonyesha usoni mwake. Niliona macho ya Veronika yakiwaka kuonyesha kuwa nilivyoeleza nimeeleza vizuri sana na Sherriff alitingisha kichwa kuonyesha kuwa niliyoyasema ni sawa kabisa.

"Sawa ndugu Willy, nitakuwa tayari kuwajibu mwaswali yenu, kusema kweli kama ulivyosema, radio za kibeberu zimekwisha tangaza uongo ili kuridhisha maslahi yao. Kwa jinsi hii tutakuwa radhi kuona ukweli unaandikwa na gazeti hili. Haya sijui mna maswali gani?".

"Inasemekana kuwa hayati Kamara Franki ndiye alikuwa anashughulikia suala hili la silaha. Na amekutwa ameuawa. Nafikiria hizi karatasi zilitokatokaje mikononi mwa marehemu na kuingia mikononi mwa hawa majahiri?. Maana kutokana na maelezo ya Polisi ofisi yenu hii haikuvunjwa mahali popote", Sherriff aliuliza.

"Sawa kabisa?, kutokana na maelezo ya mwandishi mahsusi wa marehemu, anasema ya kwamba?, wakati marehemu anatoka ofisini alimweleza aweke zile karatasi za kuchukulia silaha ndani ya mkoba wake, kwa sababu alikuwa anategemea kwenda kwenye kikosi cha Jeshi kinachoshughulikia silaha za wapigania uhuru kesho yake, kabla hajaja ofisini. Kwa hiyo, jibu kwa swali lako ni kwamba watu hawa walimnyang'anya marehemu karatasi hizo na ndio sababu wamemuua."

"Watu hawa unafikiri walijuajuaje kuwa marehemu atakuwa na karatasi hizi ndani ya mkoba wake?", Veronika aliuliza.

"Hapo ndipo hata sisi tumekwama".

"Huyu mwandishi mahsusi wa marehemu yupo", nilimuuliza.

"Ndio yupo".

"Unaweza kumwita tukazungumza nae kidogo?".

"Hali yake si nzuri sana, bado ana mshituko kwa ajili ya marehemu. Unajua mnapofanya kazi kwa uhusiano ulio karibu na mtu mnakuwa na urafiki wa hali ya juu sana. Hata hivyo nitajaribu kuwaitieni".

Alishika simu na kuzungumza na mwandishi wake. Wakati tukimsubiri Veronika alimuuliza tena. "Ofisa wa kule bandarini Ndugu Mlingi anasema mtu aliyempigia simu alikuwa na sauti kama yako, mathalani mambo mnayotaniana yalikuwa vile vile, unaweza kufikiri mtu yeyote hapa ofisini au hata nje anayeweza kuigiza sauti yako kiasi hicho?".

"Ni imani yangu kuwa mtu kukuigiza kiasi hicho lazima awe mtu aliyekuzoea, na mtu aliyekusikia ukizungumza mara kwa mara, hasa na huyu ndugu Mlingi".

"Kuesema kweli, nimefikiria kweli juu ya mtu huyu mpaka nimechoka, nitazidi kumfikiria kama wazo likinijia nitakupigia simu."

Mara mlango ulifunguliwa akaingia msichana mrefu mwembamba mwenye nywele nyingi. Kama unapenda wasichana warefu na wembamba, basi hapa pana msichana wa namna hiyo, jina lake Margreth. Ni mzuri kiasi chake.

"Karibu Margreth", Mantare alimkaribisha, wote tukasimama akatujulisha kwake. Mwandishi mahsusi alileta kiti kingine na Margreth akaketi.

"Samahani Margreth", hawa ndugu wana maswali kidogo ya kukuuliza," Mantare alimwambia.

Margreth hakujibu kiti bali alituangalia tu.

"Samahani sana binti, sisi wote yunaelewa hali uliyonayo, ila imetubidi tukuone tuweze kuzungumza nawe huenda utatusaidia kutatua huu mkasa uliompata bosi wako", nilimwelezea.

"Niko tayari kuwaelezea chochote kama kitasidia kuwapata watu waliomuua bosi wangu." Magreth alijibu huku machozi yakimlengalenga.

"Jaribu kukumbuka, nilimwambia, "wakati marehemu anakueleza uweke zile karatasi za kuchukulia silaha kulikuwa na mtu mwingine yeyote?".

Alikaa kimya kwa muda kisha akajibu, "Hapana", harafu kama amegutuka akasema, "Ndio nakumbuka sasa, alikuwepo tarishi wetu wa hapa ofisini".

Nikasikia kengere ya tahadhari inalia kichwani mwangu. Wote tulitazamana.

"Tarishi huyu yuko hapa?", niliuliza.

"Hapana, ni mgonjwa anaumwa na ameandikiwa kulala siku tano', Margreth alijibu.

"Toka lini?".

"Toka tarehe nne".

"Yaani siku ambayo ilibainika kuwa silaha zimeibiwa na bosi wako ameuawa?".

"Ndio".

"Yaani atakuwa kazini tarehe tisa".

"Ndio".

"Una uhakika kabisa alikuwepo?".

"Ndio".

Habari kama hizi mimi ndizo huwa zinanitibua, maana wakati kifo kinatokea haafu kinatokea kitu kingine chenye uhusiano wa karibu namna hii, basi hapo ndipo huwa naanza kujumulisha moja kwa moja na kupata mbili.

Nilimgeukia Mantare na kumwuliza, "Huyu tarishi ndiye alikuwa tarishi wa ofisi nzima?".

"Ndio'.

"Anaitwa nani?".

"Anaitwa George Kiki".

"Mmekuwa naye muda gari?".

"Yapata miezi sita sasa".

"Ni MTANZANIA!".

"Hapana ni mkimbizi kutoka Afrika Kusini, aliletwa kwenye ofisi yetu na chama cha wapigania uhuru cha Afrika Kusini kilichopo hapa mjini cha SANP. Ili tumsaidie. Alipokuja hapa alitupa maelezo yake na kuonekana ni kati ya vijana walioanzisha maandamano ya kitongoji cha Soweto huko Afrika Kusini. Alieleza kuwa yeye alipata mwanya wa kutoroka gerezani ndipo akakimbia na kuweza kufika hapa baada ya safari ndefu ya taabu. Kwa vile alikuwa hana kisomo cha kutosha jinsi yeye alivyojieleza tuliamua kumpa kazi ya utarishi ili kumsaidia. Kusema kweli amekuwa kijana mwenye bidii sana, na anapendwa na kila mfanyakazi wa hapa, hasa kwa nidhamu yake, na utekelezaji wa kazi yake".

"Kwa hivi alikuwa na fursa ya kuingia ndani ya ofisi ya mtu yeyote wakati waowote ili kuchukua mafaili na mambo kama hayo?".

"Hasa ndivyo ilivyokuwa".

"Anaishi wapi?".

"Anaishi huko Kinondoni sehemu za Hananasifu Estate katika nyumba za shirika la nyumba".

"Nyumba yenyewe unaijuwa?".

"Mimi nimewahi kufika kwake; tumewahi kumpeleka na marehemu", alisema Margret huku tena machozi yakimlengalenga.

"Samahani Mantare, sijui unaweza kumruhusu Margret akatuelekeza kwa Ndugu Kiki?".

"Bila wasiwasi mnaweza kwenda nae".

Niliwaangalia wenzangu nikaona wameridhika na maswali na majibu ya hapa, hivyo kwa niaba yao nikamshukuru ndugu Mantare.

"Ikiwa tutahitaji jambo lolote tutarudi tena au tutapiga simu. Na wewe ukipata jambo lolote usisite kutufahamisha".

"Hamna tabu, nitafurahi kuwasaidia".

Tuliagana tukaondoka kuelekea Kinondoni.

ITAENDEEA....
 
FUNUNU III

"Mimi naona tukapate chakula cha mchana kwanza", Sherriff alishauri.

"Sawa", walijibu kwa pamoja. Sherriff alikaa nyuma pamoja na Margret na wakati huo mimi naendesha nikiwa katika mafikara mengi, Sherriff alichukua jukumu la kumtuliza Margret akimweleza mambo mengi juu ya matatizo ya binadamu na kumwambia kuwa asihuzunike sana maana ndiyo binadamu. Kadiri Sherriff alivyozidi kusema ndivyo Margret uso wake ulizidi kutokwa na huzuni kwani mimi nilikuwa nawaangalia katika kioo cha kuendeshea. Hata Sherriff alipofika kusema yeye huwa anaamini kuwa kwa kila linalotendeka linatendeka kwa ajili ya uzuri, nilimwona Margret anamwemwesa kwa mara ya kwanza, na ndipo sura yake ilionyesha uzuri aliokuwa nao. Niliona hata Sherriff aligundua uzuri huo, kwani uso wake ulibadilika kiasi cha kwamba moyo wake uliguswa.

Tulifika New Afrika Hoteli, nikaegesha gari wote tukatoka nje. Basi, moja kwa moja tulifuliza kwenda kwenye lifti ya kutupeleka orofa ya kwanza ambapo ndipo Bandari Grill ilipo. Mbele yangu nilimwona Eddy anavuka sehemu ya mapokezi, halafu akazungusha kichwa akaingia kwenye choo kilichopo hapa chini. Hii ilikuwa ishara kuwa alitaka kuniona.

"Samahani jamani nasikia nimebanwa haja ndogo, tangulieni nakuja sasa hivi. Margret, we ndiye mwenyeji washughulikie wagaeni".

"Bila wasiwasi", alijibu akiwa anaanza kupona kutoka katika mshituko alioupata.

Niliingia maliwatoni nikamkuta Eddy ananisubiri.

"Mpaka dakika hii hakuna chochote", aliniambia bila kuniangalia.

"Sawa, nendeni mkale halafu nenda ofisini nitakukuta huko kiasi cha saa kumi hivi".

"Oke", alisema huku akielekea kwenye mlango wa kutokea.

Mimi nilimaliZa haja yangu ya uongo na kweli nikaondoka kujiunga na wenzangu. Tulipata muro safi sana hapa Bandari Grill, na kwa sababu kila mtu alikuwa na njaa tulikula kimya kimya.

"Nasikia kichwa kinaniuma", Veronika alilalamika.

"Nafikiri kwa ajili ya hali ya hewa. Joto jingi sana kuliko ulilozoea", nilimjibu.

"Kama ni hivyo afadhali ukameze dawa upumzike, sisi tutakwenda kumwona Kiki halafu tutakuja kukuona", Sherriff alishauri.

"Naona hivyo ni sawa", alijibu.

Basi tulikubaliana Veronika apumzike sisi tuendelee na shughuli. Tuliondoka New Afrika na kumtelemsha Veronika Kilimanajaro.

"Vero mpenzi, kuna gari lile pale unaweza kulitumia wakati wowote. swichi iko chini ya zulia", nilimuonyesha gari ambalo Eddy alikuwa ameliacha hapo. Sisi tuliondoka na kuendelea na safari yetu ya Kinondoni.

"Twende kupitia barabara ya Upanga moja kwa moja, halafu tukivuka Salendar briji mbele kuna barabara ya Kinondoni hivyo tutaingia kushoto. Sehemu iko mbele ya makaburi. Baada ya makaburi kuna barabara la vumbi, linakatisha barabara hii. Tukiacha hilo na kuendelea mbele tukakuta barabara nyingine ya vumbi inaingia kushoto na kuna kibao kimeandikwa Bamboo Baa and Restauranti, basi hapo ndipo tutakapoingia", alieleza Margret kwa ufasaha kabisa.

Mimi hupenda maelezo ya namna hii, siyo mtu amefika mahali pa kukata kona ndipo anasema, kata hapa kushoto. Maelekezo hayo ni ya kihuni na ndiyo anayosababisha ajali nyingi.

Nilifuata maelezo ya Margret vizuri kabisa, nilipotaka kuingia kushoto pale kwenye bao la tangazo la Bamboo Baa and Restauranti, Margret alisema, 'Njia hapa si nzuri twende pole pole, halafu mbele kidogo utakata kushoto tena tuelekee kwenye nyumba hizo pale", alinielekeza na kuonyesha kwa kidole.

Niliendesha pole pole nikaikuta njia na kuifuata kuelekea kwenye nyumba hizi za shirika la nyumba.

"Baada ya nyumba hiyo yenye bendera ya CCM, ambayo ndiyo ya mjumbe, ya pili yake".

"Hapa?".

"Ndio, mlango huu huu".

Nyumba hizi zinakaa familia mbili mbili, lakini zimetengwa katikati kiasi kwamba kila familia ina sehemu yake kamili. Tulitoka ndani ya gari, Margret akatangulia na kibisha hodi. Lakini hatukupata jibu. Nilisikia moyo wangu unapiga haraka haraka, hii ni sirika niliyozaliwa nayo, na ilikuwa ni ishara kuwa kuna hatari.

"Hebu ngoja Margret", nilimwambia nikimrudisha nyuma.

Niliujaribu mlango ukafunguka nikamwita Sherriff na kumwambia hakuna mtu, tulifungua mlango mwingine uliokuwa unaelekea jikoni, bafuni na chumba cha kulala. Tukiwa wote na wasiwasi tukibisha hodi kwenye mlango wa chumba cha kulala. Lakini hatukupata jibu. Nilitoa Bastola yangu, na kusukuma mlango wazi.

Tulimkuta mtu ambaye tuliamini ni Kiki amechomwa kisu kifuani!, nilipomshika nikajua alikuwa amekwisha kufa saa nyingi sana. Kisu kilikuwa kimeachwa pale kifuani. Kilikuwa kisu kikubwa na mpini wake mwekundu. Tulimwita Margret aje atuhakikishie.

Akiwa anatetemeka kwa woga alikuja na kusema, "Ndiye yeye masikini", akaanza kulia tena tulimbembeleza na kumvuta na kuondoka haraka haraka ndani ya nyumba hiyo. Tuliingia katika gari langu na kuelekea mjini. Sasa nilianza kuongeza hesabu kwamba mbili na mbili na kupata nne. Na vile vile majahiri hawa walianza kunitisha kwani mbinu zao zilikuwa kubwa. Lakini hata hivyo mbinu za Willy ni kubwa zaidi.

"Mapambano yameanza Sherriff", nilisema kwa sauti ambayo sikuamini ilikuwa yangu.

"Na kweli yameanza", Sherriff alijibu.

Wakati huo tulikuwa tumesimama kwenye taa za usalama barabarani za salendar briji tukuelekea New Afrika. Saa yangu ilisema ni saa kumi na dakika mbili.

"Naona mimi mnifikishe nyumbani", Margret aliomba.

"Unakaa wapi".

"Ninakaa kwenye orofa pale nyuma ya Rex Hoteli".

"Nazijua orofa hizo, uko orofa ya ngapi, maana tunaweza kukuhitaji ama kikazi ama katika hali ya kustarehe, unasemaje?".

"Karibu mimi niko orofa ya pili chumba namba kumi na nane. Simu yangu ni 22221".

Basi wakati huo tulikuwa tumefika Posta ya Azikiwe, tulipofika kwenye sanamu ya Bisimini, tukaingia Independent Evenue.

"Unajua", Margret alitugutusha.

"Ehee", nilijibu na kumwangalia ndani ya kioo cha kuendeshea, maana yeye alikuwa amekaa nyuma.

"Sijui ni mafikara yangu, ila tu limekuja kama wazo la kunishangaza, maana baada ya kutokea mambo haya kila kitu nakiona si cha kawaida kinanigutusha".

"Nini kimekugutuusha?", Sherriff aliuliza akionesha msisimko.

"Unajua pale kwenye lango la kuingia ndani ya ofisi yetu kumekuwa na mwendawazimu ambaye amekaa pale zaidi ya mwezi mzima. Amekuwa amevaa matambalatambala tu na amebeba makopo mengi, sijui mmemuona?".

"Mimi nilimwona", Sherriff alijibu.

"Mimi sikumwona".

"Polisi walikuja kumchukua siku moja, na kumpeleka kunakohusika lakini hazikupita saa tatu akarudi. Alikuwa hatoki pale hata dakika moja, usiku na mchana kutokana na walinzi wa usiku wanavyosema. Leo mlipokuja alikuwepo maana mimi niliona gari lenu linaingia wakati natoka kunywa chai. Gari lenu lilipoingia na yeye alivuka lango akaingia ndani. Hii ni kawaida yake, kwani huwa anaombaomba kwa kila mgeni anayefika pale ofisini na ndio sababu aliitiwa polisi kwa sababu anawafadhaisha wageni wetu. Gari lenu mliliegesha mbele kabisa ya mlango wa kuingia mapokezi na kutoka ndani ya gari haraka hivyo hakuwahi. Mimi nilipoingia pale mapokezi nilikuta nyinyi mmekwisha kwenda ofisini kwa Mantare ila nilimkuta yule kichaa anamuuliza yule msichana wa mapokezi. Hawa watu wanasema wanatoka katika gazeti la Afrika. Yule msichana wa mapokezi alikasirika na kumfokea, Toka hapa! kama wanatoka gazeti la Afrika watakufaa nini wewe?, wana kazi ya maana kuliko kuonana na mwendawazimu kama wewe. Toka!".

"Kitu cha kushangaza ni kwamba wakati tunaondoka pale ofisini kwetu nakumbuka sikumuona wala makopo yake na kilago chake hakikuwepo, sijui jambo hili lina maana yoyote au mnaonaje nyinyi wenyewe?", alimalizia Margret.

"Unasema alikuja hajawahi kutoka pale hata dakika moja, ila tu siku ile aliyochukuliwa na polisi kwa muda wa masaa matatu?", nilimuuliza.

"Nina uhakika kabisa maana mimi damu yangu ilikuwa haipatani na yule mtu kabisa, na ni mimi niliyefanya kampeni ya kumuitia polisi lakini aliporudi alionekana kuwa maafisa wote walidharau kumchukulia hatua tena".

"Ukimwangalia alikuwa anaonekana kichaa au unafikiri anajifanya tu?", nilimuuliza.

"Kitu kilichonikosanisha naye ni kwa sababu siku moja aliniambia yeye si kichaa ila anajifanya tu ili kujipatia pesa bila jasho. maana ilikuwa ukimwangalia sana wakati yeye hana habari anakuwa kama si mtu kichaa, ila huwa anapoona watu anakuwa kichaa kabisa".

"Asante sana, kumbuka jambo hili linaweza likawa na msingi tutaliangalia".

"Asante".

Niliegesha gari mbele ya Rex Hoteli.

"Wakati wowote tutegemee", nilimweleza huku akitelemka.

"Mnakaribishwa", akiwa zaidi anamwangalia Sherriff. Sherriff alitoa mkono wake wakapeana mikono. Tayari kulikuwa na kitu kinapita kati yao, maana nyuso zilikuwa wakati wanapeana mikono, mimi ndiye najua, maana hata mimi hali hii inanitokea. Walikuwa wameanguka katika penzi.

"Mimi naona turudi pale ofisi ya kamati tukahakikishe kama kweli hayupo pale yule kichaa", nikimwambia Sherriff.

"Sawa".

Tulikwenda kimya kimya kila mtu akichambua mambo, tuliyokuwa tumeyapata na kuyaona, tulipofika pale ofisini tulimkuta mlinzi wa jioni anayeingia kazini saa tisa wanapofunga kazi mpaka saa kumi na mbili asubuhi, ilionekana alikuwa anafanyakazi masaa mengi sana, lakini yeye alipenda kazi yake na kuridhika na kipato alichokuwa anakipata, baada ya kutusalimia na kutueleza hizo saa zake za kazi, nilimuuliza.

"Unajua kulikuwa na mzee mmoja kichaa hapa sijui amehamia wapi?'.

"Hata mimi nashangaa, kichaa huyu alikuwa hatoki hapa hata dakika moja. Hata haja zake alikuwa akiifanya hapa hapa karibu. Polisi walimchukua hapa akawachenga akarudi mwishowe wakamwachia akae tu. sasa leo nafika nakuta kiisha ondoka na wala harufu yake hakuna. Nimeshangaa sana. Amekaa karibu mwezi mzima".

"Ulikuwa unapata fursa ya kuzungumza nae?".

"Si mara nyingi, ila tu siku moja nilikuja na ..........akasita kusema.

"Sema tu usiogope, hata kama ni siri, sisi tutakufichia".

"Lakini nyinyi ni akina nani?".

"Sisi tunashughulikia wagonjwa wa akili, tumepata habari toka polisi kuwa kuna mwendawazimu hapa, hivyo unaweza kutueleza tabia yake ili tuweze kumtafuta. Kwa hiyo usisite kutueleza", nilidanganya.

Baada ya kutafakari mambo haya aliendelea, "Siku moja kulikuwa na tafrija hapa ofisini jioni. Mimi niliweza kwa mbinu zangu kujipatia mzinga mzima wa whiski aina ya 'Dimple' nikauficha wagaeni wote walipoondoka, nilitoka nje ya lango na kuanza kunywa huu mzinga wa whiski. yeye alipoona ninakunywa hii whiski alikuja na kopo lake akaniomba kwa vile nilikuwa najuwa siwezi kumaliza chupa nzima nilimgawia nusu basi alikunywa ile pombe kama maji. Basi ilipomkolea akaanza kuzungumza Kiingereza ila mara kwa mara alisema neno sijui 'Sazafrika' neno hili alilirudia mara nyingi. Na nyinyi mnajua vichaa mimi niliachana nae nikaendelea na shughuli zangu. Sasa sielewi kama kilikuwa Kiingereza sawa sawa. Lakini kitu kilichonivutia ni kule kutamka hicho Kiingereza chake kama mzungu. Lakini husema kichaa ana mashetani saba, anaweza kuzungumza lugha saba tofauti."

"Asante sana, na samahani sana kwa kukubugudhi", Sherriff alitoa mfukoni shilingi arobaini akampa. Yule Mzee alifurahi sana.

"Mungu awaongezee wanangu".

Tuliingia ndani ya gari tukaondoka zetu.

"Unaona mambo yalivyo Sherriff?, hii inaonyesha wazi kuwa George Kiki alikuwa ni jasusi aliyepachikwa hapa na mabeberu na wakafanikiwa. Mimi simulaumu mtu yeyote, hata mimi huenda ningemsaidia kupata kazi. Baada ya mabeberu kujua mkataba wa silaha kati ya PLF na Urusi miezi sita iliyopita walichukua hatua ya kuhakikisha hizo silaha haziwafikii wapigania uhuru wa PLF maana inasemekana ni silaha za kisasa kabisa. Tutakapoonana na kiongozi wa PLF atatueleza zaidi, kuajiliwa kwa kiki miezi sita iliyopita kunaoana kabisa na nyakati za mkataba huo. Inaonekana kazi ya jasusi huyo ni kujua mambo yote yanayotendeka juu ya huo ili mwishowe aweze kuiba hizo karatasi za kuchukulia silaha, jambo hili amefanikiwa", nilinyamazi kidogo.

"Kwanini wamwue?", Sherriff aliuliza.

"Kwa sababu hawakuwa na haja nae tena, asije akashikwa na kutoa siri. Hii inanionyesha jinsi watu hawa walivyo wajuzi katika kazi yao, hawataki kufanya makosa".

Wakati huu tukizungumza tulikuwa tukielekea mjini.

"Juu ya huyu kichaa unasemaje?".

"Huyu kichaa nae ni jasusi. Ninavyoona mimi huyu aliwekwa pale ofisini kusudi aweze kuona nini kitatokea hapo ofisini baada ya silaha kuibwa. Aliwekwa mwezi mmoja ili kuondoa mashaka. Hivyo alikuwa anangoja kuona baada ya polisi na maofisa wa usalama ni nani mwingine aliyekuwa na dukuduku juu ya jambo hili. Aliposikia waandishi wa habari wa gazeti la Afrika nao wamejiingiza akawa amemaliza kazi, akaondoka kwenda kupeleka ujumbe, ni wazi kabisa wao walijuwa polisi na maofisa wa usalama watalishughulikia jambo hili na ninafikiri walishapima uzito na kuona wanaweza kukabiliana nao. Hivyo walingoja wajue kama kuna kundi jingine litakalojiingiza katika katika upelelezi wa tukio hili. Sasa wamejua; kwa hivyo waandishi wa gazeti lazima muwe macho. Tokea sasa kaeni katika tahadhari; lolote linaweza kutokea. Unaonaje maoni yangu?'.

"Lo Willy, ndio maana wewe ni mpelelezi maarufu katika Afrika. Maelezo yako yanaeleza hali halisi kabisa. Na swali ulilomuuliza Margret kama kuna mtu mwingine aliyeweza kuona akiweka karatasi ndani ya mkoba, mimi nilikuwa silifikilii kabisa na ndilo swali lililotupa mwanga. Kweli kila mtu na kazi yake", alisifu Sherriff.

"Lakini maswali mliyouliza ninyi vile vile ni ya maana sana, nafikiri kuliko waliyoulizwa na Polisi. Sidhani Polisi wameishafikia hii tuliyofikia kwa muda huu mfupi".

Mara wazo likanijia.

"Lile jambo lililokuwa linakutatanisha nimepata jibu lake. Swali la nani aliyepiga simu kwa Mlingi akiiga sauti ya Mantare na maneno ya Mantare aliyozoea kuzungumza na Mlingi".

"George kiki", alijibu Sharriff.

"Kabisa, unajuwa Kiki alikuwa anaingia ndani ya kila ofisi ya ofisa akiwa kama tarishi. Swali hili nilimuuliza Mantare akakubali. Hivyo Kiki akiwa jasusi aliyefundishwa, ninavyofikilia, haikuwa kazi kumsiliza Mantare katika simu zake nyingi na ninafikiri alifanya kila njia kusikiliza simu kati ya Mantare na Mlingi. Hii inaonekana wazi kabisa".

"Lo tunaanza kuona mwanga sasa", Sherriff alisema.

"Kweli tumeona mwanga, lakini ni mwanga unaotufikisha kwenye giza nene. Maana Kiki ambaye angetupa fununu ya watu hawa amekufa, yule kichaa lazima ameshapotea hewani, gtumerudi pale pale".

"Watu hawa ni akina nani na silaha hizi ziko wapi?", niliuliza swali hili wakati naegesha gari New Afrika.

"Hilo ndio swali gumu lakini afadhali tunajua Afrika Kusini inahusika, maana Kiki katokea huko. Na yule kichaa alipolewa alizungumzia Sozafrika ambayo nasadiki ni South Afrika".

"Sawa kabisa, lazima tujuwe tunapambana na South Afrika na haikosi shirika lao la ujasusi 'BOSS', linasaidiwa na mashirika mengine ya ujasusi ya nchi za kibeberu. Hivyo tutakuwa na kazi ngumu maana watu hawa nimewahi kupambana nao ni watu hatari kabisa".

"Tumwombe Mungu atasaidia".

"Na wewe ukijisaidia", nilijibu.

Wote tukacheka na kutoka ndani ya gari. Ilikuwa saa kumi na moja. Hivyo kabla hatujavuka barabara nilionelea nifike ofisini kidogo halafu niende nyumbani.

"Sherriff mimi nafika nyumbani kidogo, nitakuona saa kumi na mbili kamili".

"Sawa nitakusubiri hapa duka la kahawa".

oke basi saa kumi na mbili".

Niliingia ndani ya gari na kuondoka. Nilipofika ofisini nilimkuta Eddy na vijana wengine. Linda alikuwa ameshaondoka.

"Eddy kuna mtu mmoja anaitwa George Kiki, alikuwa akifanyakazi kwenye ofisi ya Kamati ya ukombozi kama tarishi?, hapa aliingia kama mkimbizi baada ya kutoroka Afrika Kusini. Alifika ofisi za chama cha SANP, ambao walimpeleka kwenye Kamati ya Ukombozi waweze kumsaidia angalau kazi yoyote. Inawezekana hana kisomo cha kutosha. Nataka ukague habari hii kwa kutumia njia zetu za kawaida. Unaweza kuwajulisha makomredi wetu kule Soweto, nadhani watakuwa na maelezo kamili. Habari hizi nazitaka haraka. Kila kitu, aliingiaje hapa alikwendaje kwenye ofisi za SANP alikuwa anaishi namna gani, nani walikuwa rafiki zake nk. wewe unajua".

Eddy aliyekuwa anachuku maelezo haya alijibu.

"Atashughulikiwa bosi, usiwe na wasiwasi".

"Chifu yuko?".

"Kaondoka".

"Haya asante, usitoke mpaka nitakapokujulisha tena".

"Mimi nipo".

Ndio sababu nilimpenda mtoto huyu. Nidhamu yake kwangu ilizidi ya mdogo wangu ambaye tumetoka ndani ya tumbo la Mama Willy. Niliingia ndani ya gari nikaelekea zangu Upanga.

Niliposimamisha gari mbele ya mlango, moja kwa moja macho yangu macho yangu yakaangukia kwenye kitu kilichokuwa kwenye ubao wa juu ya mlango mkubwa wa kutokea nje. Nilitoka nje ya gari haraka haraka nikiwa tayari kwa mapambano.

Nilikuta ni kisu chenye mpini mwekundu kama kile tulichokikuta kwenye kifua cha maiti Kiki; ncha yake ilitumiwa kama kipini cha kubandika kipande cha karatasi pale mlangoni.
Niliking'oa nikachukua karatasi na kusoma yaliyobandikwa hapo yalisema.

Willy Gamba, kama unathamini maisha yako achana na hao watu wa gazeti la Afrika. na kama ni rafiki zako waambie waondoke hapa mjini tunawapa mpaka saa kumi na mbili jioni wawe uwanja wa ndege. Vinginevyo yaliyompata Kamara Frank yatawapata na nyinyi. Hili ni onyo kali na si mchezo. Shughulika na mambo yako usishughulike na mambo ya watu wengine. Wapo wenyewe wanaohusika waachie. Nasema tena saa kumi na mbili jioni leo wawe uwanja wa ndege na wewe baada ya kuwafikishia habari hizi tusikuone unashughulika zaidi ya kazi yako ya kawaida ya AIA Subiani.

Kwanza nilicheka maana niliona kazi sasa inaanza. Hii inaonyesha upelelezi wetu ulikuwa umewashitua kuliko wa Polisi. Nilijua yule kichaa alifanya kazi yake vizuri sana, maana ni yeye tu aliyetufahamisha kwa majahiri wenzake. Hiki kisu chenye mpini mwekundu ilimaanisha damu. Nami niljua damu imeanza kunuka.

Nilifungua mlango nikaingia ndani, nikakoga haraka haraka kisha nikabadilisha nguo nilifungua sanduku langu la silaha na kuchukua bastola zingine mbili kwa madhumuni ya kuwapa Sharriff na Verokika kwani hakukuwa na mchezo tena, maana upatapo onyo toka kwa watu kama hawa huwa hawatanii. Kisha niliinua simu na kupiga kituo cha Polisi cha Salendar Bridge.

"Hallo kituo cha Polisi hapa".

"Sikiliza, nenda Kinondoni Hananasifu, Estate kwenye nyumba ndogo ndogo za shirika la Nyumba nambari IIC utakuta kuna maiti ambayo ina zaidi ya masaa ishirini na nne", kabla hajatamka neno nilikata simu. Niliangalia saa yangu muda ulikuwa umekimbia na ilikuwa saa kumi na mbili kamili. Niliingia ndani ya gari nikakimbilia New Afrika.

Nilipoingia duka la kahawa sikumwona Sherriff nikapata wasiwasi. Nikaenda mapokezi kuuliza wakaniambia aliacha habari kuwa amekwenda dukani mara moja nimsubiri. Nilirudi nikasimama nje pale magari yanapoleta watu New Afrika yanapozungukia. Niliangaza huku na huku na mara nikamwona Sharriff anakuja akiwa anavuka tawi la Benki ya nyumba. ghafla alipokuwa anataka kuvuka barabara ilitokea gari sijui wapi ikapiga breki, wakatoka watu wawili haraka kama umeme, wakamvuta Sharriff ndani ya kiti cha nyuma cha gari, na gari hilo likaondoka tena kama umeme. Kitendo hiki hakikuchukua hata nukta tano.

Watu wote waliduwaa wasijue cha kufanya, lakini mimi Willy nilijua la kufanya. Nilikimbia kwenye gari Eddy alilokuwa amekodi na kuliacha New Afrika. Kwa vile alikuwa ameliegesha vizuri niliingia na kuondoka kama umeme. Nilikuwa nimeona lile gari linakata kulia kutoka barabara ya Azikiwe kuingia Azania Front. Nilipoingia Azania Front niliona gari lao linafika kwenye ofisi za NASACO nikacheka.

ITAENDELEA
 
SURA YA TANO
TWATOANA JASHO

Niliongeza gari moto ili wasije kunipotea. walikata kulia wakaingia mtaa wa Railway, nilipoingia mimi mtaa huu wao walikuwa wamefika kwenye mzunguko wa 'Clock Tower' na kuingia mtaa wa Nkurumah.

Kwenye mtaa huu wa Nkurumah niliwakaribia kabisa, nikiwa nimeacha gari mbili tu kati yangu na wao. Niliona mmoja katika gari lao akitoa kichwa nje na kuangalia nyuma, nadhani wanadhani nitawafuata na gari langu ambalo wanalijua sana. Lakini hawajui Willy ni mtu wa namna gani. Wakati huo nilikuwa naendesha gari aina ya Fiat 132 GLS, na si Colt Gallant Sports kama ambavyo walikuwa wanafikiria.

Walikwenda moja kwa moja na kushika barabara ya Pugu. Walipofika kwenye njia panda ya barabara ya chang'ombe na Pugu, walikata kushoto na kuingia barabara ya Chang'ombe. Saa hizi magari hayakuwa mengi hivyo kila gari lilikwenda kasi. Nilikuwa na bahati kuwa magari yale mawili yaliyokuwa kati yangu na wao nayo yalikata na kuingia barabara hiyo hiyo kuzidi kunificha.

Walipofika kwenye sehemu ambayo barabara ya Mbozi inagongana na Chang'ombe walikata kulia na kufuata barabara hiyo. hizi gari mbili mbele yangu zilionyesha kuwa zilikuwa zinaendelea na barabara ya Chang'ombe. Nilipunguza mwendo ili wasije wajanitambua. Mara nilisikia wanapiga honi ya namna ya pekee kabla ya kufika kwenye jengo la Kampuni ya rangi ya Sadolins.

Ghafla lango la uwa la bohari moja lilifunguliwa na bila hata kupunguza mwendo, gari hii ilikata kushoto na kuingia ndani na hapo lango likafungwa. Mimi nilipitiliza kama kwamba sina habari na watu hawa. Ilikuwa inakaribia saa moja za jioni, hivyo giza lilikuwa limeanza kuingia. Nilisimamisha gari langu kama mita mia mbili hivi, nikaanza kurudi haraka kwa miguu.

Bohari hili ambalo lilikuwa limezungukwa na ukuta wa matofali ya saruji, lilikuwa limeandikwa 'Mamlaka ya Pamba'. Mimi nilishangaa sana kwani sikujua hii ni maana gani. Ukuta wa uwa huu ulikuwa na urefu usiozidi futi kumi na mbili, hivyo kwangu ukuta kama huu kuupanda ni kazi ndogo. Nilikwenda kwenye upande wa lango kubwa, nikazunguka pembe ya kushoto ya uwa huu. Ukuta huu ulikuwa unapakana na ukuta wa bohari nyingine la namna hiyo hiyo kwa upande huu wa kushoto.

Nilikwenda kama hatua tatu hivi kwenye nafasi hii ya kati ya mabohari haya, nikavua viatu, nikarudi nyuma kidogo halafu nikaurukia huu ukuta na kuukwea huku mikono yangu ikikamata juu yake. nilivuta mwili wangu wote kimya kimya kama paka nikachungulia ndani ya uwa.

Pale karibu na mlango nilimwona mtu amevaa koti refu la khaki rangi nyekundu lililokuwa linavuka magoti yake kidogo huku ameshikilia bunduki ya aina ya 'SMG' na akiangalia mlangoni. Bila kufanya hata chembe ya kelele nilivuta mwili wangu wote na kutambaa kama nyoka juuya ukuta huu uliokuwa na upana wa futi moja. Nilitambaa mpaka nikawa karibu kabisa na mtu huyu kwa juu yake bila yeye kufahamu. Nilijirusha chini na kufanya kishindo kidogo nae akageuka. Mimi nilikuwa tayari nikamkata karate ya shingo kabla hajajua nini kinamjia. Akazilai. Nikamshikilia na kumlaza chini taratibu. Muda kitambo aloikufa.

Nilimvua lile koti lake nikalivaa mimi, halafu nikamnyanyua tena nikamlalisha chini na kumwegemeza kwenye ukuta. Nilichukua bunduki yake ambayo ilikuwa imejazwa risasi, nikafurahi sana kishika silaha namna ile. Mimi nikiwa na silaha namna ile hata likija jeshi la watu mia hawaniwezi. Nilijidhatiti tayari kwa mapambano zaidi nikanyata kwenda nyuma ya jengo la bohari ambako niliamini kuna mlango mwingine. Nilipofika kwenye pembe ya ukuta wa kushoto nilichungulia. Niliona kuna mlango wa mbele wa mlango alisimama mlinzi mwingine akiwa amevaa sawasawa na yule wa kwanza; koti refu jekundu.

Alikuwa nae ameshika bunduki ina ya 'SMG', niliona anafungua mlango anasema kwa sauti kali "Fanhyeni haraka bwana, kama hataki kueleza si niambieni mimi akaonane na babu zake huko ahera". Alirudisha mlango akaangaza huku na huku. Kutokana na maelezo yake ni kwamba Sherriff alikuwa anaswalishwa na majahiri na bila shaka alikuwa akipata kipigo kikubwa.

Nilitumbukiza mkono ndani ya mifuko ya koti nililovaa nikakuta mna sigara na hamna kiberiti. Wazo likanijua nikamfanyia yule mlinzi 'sss' aligeuka akaniona akidhani ni mwenzake, nilimuonyesha sigara na kuwa nataka moto. Bila kusita akaja akatoa kiberiti na kwa ajili ya giza sasa hakuweza kunitambua sababu ya lile koti. Aliponyoosha mkono kunipa kiberiti. Kama radi nilimrukia na kumpiga karate ya mikono miwili shingoni. Sikuwa na haja ya kumwangalia maana nilijua kwa kipigo hicho hawezi kuishi. Nilimvutia upande huu wa kushoto na kumwegemeza kwenye gari lao. Nilichukua bunduki yake iliyokuwa na ukanda mrefu nikaingika begani na kuiweka mgongoni.

Sasa njia ilikuwa wazi kwenda mpaka mlangoni, kwa kutokana na ujuzi wangu wa kuiga sauti ya yule mlinzi wa nje kwa maneno yake aliyosema mimi nilisema. 'Vipi hajasema lolote?," nikiwa nimefungua mlango kidogo na kuchungulia ndani. Bohari lilikuwa limejaa robo tu ya marobota ya pamba. Sherriff alikuwa ameshikwa na watu wawili na mmoja alikuwa amebeba bao akimtandika tumboni kwa nguvu sana.

"Sema nyie si waandishi wa magazeti ila ni wapelelezi, ndio".

"Yote ya kweli nimeshaeleza ".

Kabla hajaanza kumpigab tena nilisema. "Mmoja wenu aje hapa, mimi mnanijua hivyo hatachukua dakika kabla hajasema uweli wake".

Shomvi alikuja akikimbia, nikamfungulia mlango na kurudisha mara moja. Alipoangalia ba kutambua mimi si Luis akataka kupiga kelele lakini nilimwahi karate ya katikati ya kichwa akafa bila kelele. Watu wa mle ndani waliokuwa wamemshikilia Sherriff walikuwa hawana bastola mikononi ila zilionekana kwenye mapaja. Nilifungua mlango ghafla SMG mkononi nikamwahi mmoja wao kabla hata hawajaelewa nini kinatokea.

"Ukijaribu chochote umekufa", nilisema kwa sauti ya kutetemesha.

Sherriff alishangaa kuniona akaruka ile maiti akasimama upande mwingine. Niliona ile SMG ya pili nikampa, akatabasamu. Jinsi alivyoijaribu mkononi nilikua huyu mtu anajua kuitumia.

"Chukua hizo silaha zake", Sherriff alimkagua akatoa bastola mbili zenye sailensa na visu viwili vyenye mpini mwekundu.

"Ah, ni wakati wako sasa kujibu maswali yetu, nyinyi ni nani", nilimwuliza.

"Mimi sijui, mimi niliajiriwa tu leo hii asubuhi na Kimkondo, huyu uliyemwua hapo chini, kuwa kuna kazi ya kumkamata mtu mwenye habari ambazo wakubwa wake wanataka. Pesa tulizolipwa zilikuwa nyingi, shilingi elfu kumi kwa kila mtu kwa kazi ya masaa machache tu nami nikakubali, kusema ukweli sijui lolote".

"Yeye Kimkondo anafanya kazi gani?".

"Yeye ni jambazi tu anayepewa kazi ya ujambazi hapa na pale".

Kutokana na maelezo ya huyu mtu nikajua anasema kweli. Nilijilaumu kumwua Kimkondo maana yeye huenda angetupa mwanga zaidi. Lakini hii yote inaonyesha jinsi majahiri hawa yalivyokuwa yamepanga ujahili wao kwa ufundi.

"Lo Willy asante sana".

"Sahau", nilimjibu kwa mkato.

Ile sura ya kikatili ilikuwa tayari imekuja usoni mwangu. Katika hali kama hii sura yangu hubadilika na kuwa mtu tofauti kabisa. Hivyo nilipomwambia Sherriff sahau niliona anashituka kidogo.

"Twende zetu tutoke hapa Sherriff, huyu nitajua mahali ya kumpeleka".

Tulimtangulia, tukafungua mlango wa bohari tayari kurudi mjini. Tulipokuwa tumefika kwenye kona niliyotokea, tukasikia honi ya gari ya namna ile ile waliokuwa wamepiga hawa majahili wa kwanza.

"Sherriff na wewe mtu mjifiche nyuma ya hili gari, kwa vile mimi nimevalia koti lao ambalo naona ndicho kitambulisho chao nitakwenda kufungua lango, unayo ile bastola uliyochukua kwake?".

"Ndio".

"Basi akifanya ushenzi unajua la kufanya; maiti hazisemi'.

Niliwaacha nikakimbia mpaka kwenye lango nikafungua. Gari aina ya VW Kombi iliingia imejaa watu wamevalia makoti kama langu, Gari hili lilisimama nyuma ya lile gari la kwanza. Milango ikafunguliwa wakaanza kutoka. Mimi nilikuwa tayari na SMG yangu.

"Rudini ndani......." niliona yule mtu tuliyekuwa tumemshika ameruka juu ya gari na kutoa onyo, lakini kabla hajamaliza Sherriff alimlamba risasi ya kichwa akaanguka juu ya gari, mimi nikajua tayari mambo yametibuka, hivyo sasa ni kazi.

Dereva wa gari hii na watu wengine waliokuwa bado ndani ya gari walifunga mlango ili waondoke. Wale waliotoka nje walianguka chini na kutoa bastola tayari kwa mapambano. Mimi nilikuwa nimeishavua koti nimerukia ukutani na tayari SMG mkononi. Nilikuwa nimelalia tumbo juu kabisa ya ukuta. Lile gari lilipopiga moto, nililenga mlango wa dereva na kuachia risasi mfululizo kama mchezo.

Sherriff alikuwa bado kimya hajaanza shughuli. Wale watu watano waliokuwa wametoka ndani ya gari nao walikuwa wametambaa upande mwingine wa kombi. Kumbe mmoja wao aliniona kule juu baada ya kuona risasi zilizoua wenzake zikitokea juu. Mimi nilikuwa bado sijamwona hivyo akainuka kunimaliza. Lakini kumbe Sherriff alimwona kabla hajafyatua risasi, akamwahi. Nilipomwona Sherriff akanionyesha ishara. Alikunja kiganja halafu akainua kidole kimoja kuonyesha kuwa ni watano na mmoja tayari kafa.

Mimi nilijirusha chini toka ukutani na kujiviringisha huku nakoswa koswa risasi za maadui. Niliposimama huku nikikimbia zigizaga na wakati huo nikipiga risasi ovyo kuwazuia wasipige. Nilifika mlango na kufungua kama ninakimbia nje. Wale kwa woga wao walipoona hivi nao walianza kukimbia kuwahi mlangoni.

Kumbe ndipo walikuwa wanampa fursa Sherriff kuwachukua mmoja mmoja vizuri sana. Na mimi ghafla nilijitokeza tena na kumimina risasi kwa wawili waliokuwa mbele. Bahati nzuri Sherriff alijitupa chini la sivyo ingetokea ajali kwani yeye alifikiri nitawasubiri nje hivyo naye alikuwa anawafuata nyuma.

"Kazi nzuri Sherriff, la sivyo ningekuua, pole sana", nilimpa mkono.

"Hali kama hizi nimezizoea sana hivyo huwa niko tayari katika tahadhari kila mara kwani lazima kama huna uhakika mwenzako atafanya nini baadaye tegemea lolote", Sherriff alijibu.

Tulikimbia kutoka pale mpaka kwenye gari langu. Tuliingia na kuwasha gari moto na kuelekea zetu mjini.

"Mimi nilijua ndio mwisho wangu", Sherriff aliniambia.

"Kwa nini?".

"Maana walivyonivamia hata nilishindwa la kufanya halafu nilijua wewe utakuwa unanisubiri New Afrika na kumbe mimi nimeshauawa. Na kweli wangeniua".

Alitoa shati lake kuonyesha uvimbe mbaya sana kwenye tumbo lake.

"Nasikia maumivu ya ajabu. Watu hawa ni katili sana".

"Pole sana. Jambo la kusikitisha ni kwamba imebidi tuwaue wote. Hivyo bado tumerudi pale pale; hatujui lolote, isipokuwa tu kwamba watu hawa ni majahili wa hatari sana wanaovaa makoti mekundu na bunduki wanazotumia ni SMG za kichina, bastola za kirusi zenye sailensa. Zaidi ya hapo bado tuko mbali sana na ukweli wa mambo. Ila kinachonifurahisha ni kwamba sasa watashtuka baada ya mapambano haya ambamo tumeua watu wao karibu kumi na tano. Kule kushtuka ndiko kutatusaidia maana lazima watahaha na kufanya makosa".

"Sawa kabisa. Lakini mimi nataka kujua jinsi ulivyojua nimekamatwa na namna ya gari umeweza kuniokoa. Maana mimi sikuamini nilipokuona, nilidhani huenda ni malaika kashuka toka mbinguni katika sura yako".

Tukiwa bado tunaelekea mjini nilimweleza jinsi nilivyofanya.

"Lo ndio sababu wewe ni mpelelezi namba moja katika Afrika; mimi sasa nadhani hata katika dunia. Tukirudi London salama nitailisha komputa maelezo zaidi juu yako tuone itakuonyesha katika nafasi gani katika wapelelezi wa ulimwengu".

Mimi nilicheka tu sikujibu kitu.

"Na kule kubadili gari kulisaidia sana maana walipochungulia na kulikosa gari lako walinidhihaki kwa kusema kuwa sasa nitakufa peke yangu hata rafiki zangu hawatathubutu kuja hata kama wangeniona wakati ninakamatwa".

"Mimi ni mjuzi zaidi yao; lazima tuzidiane maarifa".

Tuliingia barabara ya Independece Avenue.

"Nitakupeleka kwa daktari wangu hapa Zanaki Street, na utalala hapo. Nafikiri kesho utakuwa katika hali nzuri, kwa leo lala hapo usirudi New Afrika ili daktari aweze kukupa matibabu kwanza. Nitakuja kukupitia asubuhi".

"Sawa wewe ndiye bosi", Sherriff alijibu.

Nilimpeleka kwenye zahati ya rafiki yangu Dk. Kiluwa na kumweleza amtibu na malipo yatalipwa na AIA. Nilimwacha nikawaahidi kuwaona asubuhi yake.

ITAENDELEA
 
SURA YA TANO
TWATOANA JASHO
III
"Eddy nafikiri unaweza kwenda kupumzika. Acha vijana wa zamu waendelee, maana kesho tunaweza kuwa na kazi nyingi sana".

"Asante tutaonana asubuhi", alijibu huku akikusanya kusanya karatasi zake.

Mimi niilimuaga nikaondoka zangu kuelekea New Afrika tayari kuonana na Veronika. Nilipofika New Afrika nilikuta duka la kahawa limejaa watu na ile sehemu ya Patio Baa ndio usiseme, maana vijana walikuwa wamejazana wakifurahia saa zao za baada ya kazi.

Nilishikashika mfukoni, nikachukua funguo za gari mkononi nikaelekea kwenye gari langu, niliona Vero alikuwa bado hajafika kwani hamkuwa na mtu ndani ya gari. Nilifungua mlango wa upande wa dereva ili nikae nimsubiri, maana nilijua asingechukua muda mwingi.

Nilipoingia na kukaa kitini na kuanza kutelemsha kioo, nilisikia kama kuna kitu kwenye viti vya nyuma vya gari langu. Nilipotaka kugeuka kuangalia nilisikia sauti ikisema. "Usigeuke la sivyo utakuwa ndio mwisho wako. Washa gari ondoka, na ufuate maelezo yangu".

Nilisikia mdomo baridi wa bastola ukigusa shingo yangu.

"Sawa mzee", nilijibu huku nikijifanya kama sijali.

"Siyo mzee, sema wazee. Tuko wawili na wote tuna bastola na tunajua kuzitumia hivyo usijaribu kitu chochote cha kuleta matatizo".

"Mimi sina wasiwasi, maana sijui kwanini natekwa nyara, kama nia yenu ni gari niambieni niwaachie. Mimi ni mfanyabiashara nitapata gari nyingine, kwangu pesa si tatizo".

"Funga domo lako, sisi hatuna haja na gari lako wala pesa yako, sisi tuna pesa kuliko wewe".

Kabla sijasema lolote aliniambia. "Kata kushoto ingia Independence Avenue, halafu ukifika 'Clock Tower' ingia mtaa wa Railway halafu shika barabara inayopita kwenye kituo cha polisi wa usalama barabarani, halafu ukifika kwenye mzunguko ingia kushoto, fuata barabara ya Kilwa mpaka nitakapo kueleza tena. Nasema tena ujanja wowote utakutokea puani".

"Usiwe na wasiwasi", nilijibu kiume.

"Nyamaza", alijibu kwa sauti ya ukali.

Nilijilaumu sana kwa kutochukua tahadhari zaidi kwa watu hawa.

Nilifikiria kama naweza kufanya lolote sasa nitakuwa kwenye upande wa hasara hivyo nikakata shauri la kufuata maelekezo mpaka mwisho ndipo nione la kufanya. Maana nafikiri kama nia yao ilikuwa ni kuniua wasingesita, walikuwa na mwanya mzuri sana nilipoingia bila tahadhari ndani ya gari. Nilijua nia yao si kuniua ila kuna habari walizozitaka. Nilimfikilia Veronika nikajua atahangaika sana kwani hatanikuta halafu hatajua Sherriff aliko.

Tulipokaribia uwanja wa Sabasaba aliniamuru nikate kushoto kwenye njia inayoelekea kwenye ofisi mojawapo za reli ya Tazara ya Kurasini. Tulipotelemka kidogo aliniamuru nikate kulia na kuingia kwenye mlango wa pembeni wa uwanja wa Monyesho ya Sabasaba.

Tulipofika kwenye mlango huu aliniamuru nipige honi. Nilipopiga honi mlango ulifunguliwa. Taa zangu zikamwulika mlinzi aliyevaa joho jekundu, nikajua mara moja ni nani nimepambana nae tena. Tena huyu mtu aliongeza na kofia nyekundu juu.

Nilishangazwa sana na mbinu za watu hawa, maana sehemu zo walizokuwa wanazitumia kama kambi zao za kufanyia uovu zilikuwa sehemu za kiserikali. Hii ilionyesha jinsi mbinu za watu hawa zilivyozidi kiwango.

"Ingia ndani moja kwa moja, fuata barabara mpaka nitakapokuabia simama", niliamriwa.

Uwanja ulikuwa kimya kabisa. Giza lilitanda kote ila taa za gari langu peke yake. Tulikwenda mpaka katikati ya vibanda.

"Simama hapa, zima taa na telemka taratibu. Ukifanya makosa usinilaumu", alinieleza. Nilipozima taa tu niliona vivuli vya watu vikinyata polepole kuja kwenye gari. Nilipokanyaga nje tu gari likawa limezungukwa na watu watatu. Wale waliokuwa ndani ya gari walitelemka.

"Mmemleta?", mmoja wa wale waliozunguka gari aliuliza.

"Ndio", alijibu yule mtu aliyekuwa ananipa amri".

"Kazi nzuri, haya twendeni".

Yule mtu aliyezungumza alitangulia mbele mimi nikaambiwa nimfuate huku nimezingirwa na watu wanne. Yaani wale wawili walioniteka, na wengine wawili waliokuwa wamebeba bunduki aina ile ile ya SMG, ilionekana hawa watu walitumia sana aina hii ya bunduki.

Niliongozwa moja kwa moja mpaka kwenye kibanda kimoja katikati kabisa ya uwanja wa maonyesho wa Sabasaba. Nilikumbuka kuwa kibanda hiki kilikuwa kinatumiwa na nchi za Zambia katika maonyesho ya Kimataifa. Mlango ulifunguliwa tukaingia. Ndani tulimkuta mtu mwingine anavuta mtemba amekaa kwenye kiti huku akitabasamu. Watu hawa wote walivalia majoho mekundu. Na hawa wanne niliowakuta huku kiwanjani walivaa kofia nyekundu isipokuwa wale walioniteka ndio hawakuwa na kofia.

"Karibu Willy Gamba, keti chini kwenye kiti", aliniambia yule mtu tuliyemkuta ndani.

"Asante, mimi ningependa kusimama", nilijibu.

"Mimi sitaki kukukarisha kwa nguvu, lakini kama unaona ni lazima nifanye hivyo ninao uwezo, Willy", aliniambia taratibu huku wale watu wengine wakinisogelea. Niliona hakuna haja kuchachamaa hapa hivyo niliketi kwenye kiti.

Chumba hiki kilikuwa kimewekwa fenicha nzuri sana, hata nikashangaa saa ngapi watu hawa waliweza kuaandaa chumba hiki kama ofisi na huku uwanja huu siku zote unalindwa.

"Romano na Charles mnaweza kwenda nje kusudi muwe tayari kukabiri jambo lolote linaloweza kutokea hapo nje wakati nikiwa na mazungumzo mafupi na Willy hapa", alitoa amri polepole kiasi kwamba ungeweza kuamini kuwa ni mtu mzuri sana, lakini macho yake yalionyesha uovu usio kifani.

NIlifurahi sana kwani nilijua kuwa sasa ninaonana na mtu wa maana katika kundi hili la majahili. Macho yetu yalipokutana ana kwa ana mara moja tukatambuana, maana huyu alikuwa jasusi wa hali ya juu. Sisi tuko kama mbwa tunajuana kwa harufu. Wale watu wawili wenye SMG walitoka nje tukabaki na wale watu walioniteka nyara, yule mtu aliyetupokea na huyu mtu tuliyemkuta humu ndani. Walipotoka nje waliufunga mlango.

"Bwana Gamba, mimi ni mtu nisiyependa kuumiza kwa sababu mimi huwa sijisikii vizuri nikiona mtu anaumizwa. Lakini nikilazimika kufanya hivyo, basi mimi hufumba macho. Nisingependa nifumbe macho kwako kwa hiyo naomba sana uwe mtu mwungwana katika kujibu maswa yangu".

"Nadhani ungependa kujua sisi ambao tuko hapa ni nani, sisi ni WANAMAPINDUZI WAPINGA MAPINDUZI".

"Wanamapinduzi wapinga mapinduzi maana yake nini?. Sikuelewi.

"Ni kwamba sisi tunapinga watu wanaojiita Wana mapinduzi, wanaofikiri wataleta uhuru Afrika Kusini kwa njia ya vita. Sisi ni wanamapinduzi ambao tuna imani kuwa tutaleta uhuru Afrika Kusini kwa mazungumzo bila kuua mtu hata mmoja. Sasa swali langu ni hili; Wewe na rafiki zako mna nia gani katika kupeleleza upoteaji wa silaha?, Kwanini msiwaachie watu wanaohusika?".

"Mimi si mwana siasa hivyo unayonieleza juu ya namna gani uhuru utakavyopatikana huko Afrika Kusini sina haja ya kujua. Lakini wageni wangu ni waandishi wa habari na kumetokea hapa mjini Dar es Salaam wizi wa silaha uliotingisha ulimwengu.Hivyo wakiwa waandishi lazima wapeleleze wapate kueleza ulimwengu mambo haya yametokeaje. Sidhani kama kitu hocho ni dhambi. Ni kitu cha kawaida". Nilimjibu taratibu nikijaribu kupima hali ndani ya chumba hiki.

"Imeonekana hawa waandishi wa habari wamekwenda zaidi ya kiwango cha upelelezi wa kigazeti, kiasi cha sisi kuamini kuwa si waandishi wa gazeti ila wapelelezi. Jioni hii kama huna habari rafiki yako Sherriff ameua vijana wangu zaidi ya kumi. Mtu mmoja, Willy, mtu mmoja?, siamini kabisa kuwa yeye ni mwandishi".

"Swali langu la pili nataka nujue yeye ni nani na sasa hivi yuko wapi?. Ukijibu maswali haya nitakuachia, usipojibu jua ya kwamba kesho huioni".

"Mimi ninavyojua ni kwamba yeye ni mwandishi wa habari, kama ni mpelelezi haya ni maneno yako, Kampuni yangu ni wakala, hivyo nilivyofanya mkataba na gazeti la Afrika na watu hawa walipokuja nilijuwa ni waandishi. Pili sijui aliko sasa hivi, tuliachana saa nyingi na tulipanga tuonane saa kumi na mbili New Afrika Hoteli lakini sikumkuta.

Baada ya kufikiri kidogo akasema, "La hasa, unajua".

"Sijui".

"Au unataka mpaka nifumbe macho".

"Hata kama ukifumba macho, sijui".

"Lucas na Moshi hebu mmwonyesheni huyu namna ya kujibu", alisema tena pole pole.

"Simama", alisema Lucas.

Sikusimama. Basi walinijia wote pale kitini kama faru, na mimi Willy tayari nilikuwa nawashwa kumwonyesha huyu mkubwa wa kuwa Willy hasukumwi ovyo.

Kama umeme nilisimama upesi na kukwepa ngumi ya Lucas na kwa sababu alikuwa ameitupa kwa nguvu sana alipepesuka mimi nikampiga teke kwenye mapumbu akalia kama nguruwe na wkati huo shoto langu lilimfikia Moshi singoni nae akapepesuka mpaka chini. Yule mtu mwingine aliyetuongoza toka mwenye gari alitoa bastola yake lakini mimi niliona hatua hiyo nikaruka upande mwingine wa chumba na risasi zikanikosa, na wakati huo mlango nao ulifunguliwa na mtu aliyevaa joho jekundu na kofia nyekundu akiwa na SMG mkononi akampiga risasi ya mgongo kabla hajanimaliza pale niliporukia, na yule mtu akafa pale pale. Huyu mtu wa SMG alimimina risasi kwa wale wengine waliokuwa wanajaribu kutoa silaha zao na kuwamaliza hapo hapo. Mimi katika harakati za kujiokoa niona yule mkubwa wao anaruka nyuma ya kiti, nikatoa bastola yangu, lakini nikawa nimechelewa, kwani nyuma ya kiti chake kulikuwa na mlango mdogo kimo cha urefu wa kochi. Hivyo alijitumbukiza.

"Anaondoka huyo Willy", nilisikia sauti nya Veronika akimimina risasi pale kwenye mlango lakini yule mtu alikuwa anajua nini anachofanya, hazikumpata akakimbia nje.

Mimi nilishangaa sana kumwona Veronika katika joho jekundu na kofia nyekundu na SMG mkononi amefika wakati kabisa uliohitajika kuniokoa.

"Oh Vero mkombozi wangu, umetokea kama malaika vile".

Alitupa bunduki akavua kofia na joho, haraka hara akaja akanirukia shingoni na kuanza kunibusu, kisha akaniachia.

"Tutoke hapa mpenzi, nitakueleza baadae", alininong'oneza.

Tulitoka ndani ya banda hilo na kusikia gari linaondoka.

"Mshenzi amepona", Veronika alisema.

"Iko siku yake", nilijibu.

Niliokota bunduki mbili pale nje. tukaenda kwenye gari letu tukaziweka ndani. Tukawasha gari na kuelekea mjini. Tulipofika Kilwa Road Veronika alianza kunisimulia,

ITAENDELEA...
 
SURA YA SITA
CHIMALAMO

"Baada ya kuzungumza na wewe kwenye simu, niliondoka kwenda New Afrika kama tulivyoagana. Niliona hakuna sababu ya kuchukua gari, hivyo niliondoka kwa miguu kwani nilijua dakika kumi ningenitosha. Nilikuja moja kwa moja na barabara ya Azania Front nikakatisha pale kwenye kanisa la Kilutheri na kutokea barabara ya City Drive. Kama unavyojua New Afrika inajengwa kwa mbele kwa hivyo nilijipenyeza kwenye mwanya wa jengo la Benki ya Taifa ya Biashara tawi la City Drive na Azikiwe, nikawa nimetokea karibu kabisa na pale ulipoegesha gari lako".

Ghafla nikaona watu wawili, mmoja wao akifungua mlango wa gari lako. Mimi nikasimama na kujibanza kwenye moja ya nguzo za jengo hili la Benki huku giza likinisaidia. Yule wa mbele aliingia na nyuma akaangalia huku na huko hakuona kitu nafikiri, maana alitoa bastola mwenye joho lake nae akaingia. Kama unavyojua gari hili lina milango miwili tu, hivi waliinamisha kiti na kuingia nyuma ya gari.

Mara moja nikajua nia yao; nilijua wanakusubiri wewe ama kukuua ama kukuteka nyara. Nilipofikiri sana niliona nia yao kukuteka nyara kwani kama ni kukuua wasingeingia ndani ya gari, hasa nyuma, na mahali penyewe pakiwa karibu sana na New Afrika. Huwa naamini sana akili zangu zinavyonituma hivyo nikaona kuwa nia yao ni kukuteka nyara. nilifikiri nikufuate lakini sikuwa najua ofisi yako ilipo. Hivyo nikaamua kitu kimoja, kuingia ndani ya buti la gari kama iwazi. Kwa kuwa gari yako ina nyavu kioo cha nyuma, nilijua watu hawa hawataniona wala kunisikia, kwani nilijua na wao watakuwa wamelala chini ili usije ukawaona wakati unaingia".

Alinyamza kidogo ili kulegeza koo kwa mate, akaniangalia akanikuta mimi naendesha taratibu huku nikimsiliza kwa makini sana. Kisha akaendelea, "Nikisaidia na giza la ukuta wa mabati uliozungushiwa jengo hili la mbele la New Afrika huku nikinyata nimeinama kimo cha buti la gari. Kama bahati ilivyokuwa na mimi nilikuta buti lako halikufungwa na funguo. Jihadhari sana siku nyingine utabeba adui ndani ya gari lako".

"Nimekuwa sina aduin Tanzania, hivyo nimekuwa nikiamini kuwa hakuna mtu wa kunifanyia ubaya, maana hata sijawahi kugombana na mtu hapa Dar es Salaam".

"Haya sasa lazima utambue kuwa umepata maadui; lazima ujihadhari".

"Sawa nitajihadhari lakini vile vile kama ningekuwa nimefunga usingeweza kuniokoa, hivyo kujiachia mambo mara nyingine ni vizuri".

"Haya nimekubari kushindwa, lakini hata hivyo ningepata njia nyingine. Basi taratibu nilifungua buti la gari na kuingia ndani, kimya kimya kabisa bila kelele yoyote. Niliwahi kusafiri ndani ya buti wakati ninakaa na majeshi ya POLISALIO, hivyo najua sana hali ilivyo ndani ya buti la gari kiasi kuwa kwangu hewa ya mle ninaweza kuistahamili ingawa ni kidogo. Unajua gari linapoanza kutembea hewa inajaa kabisa. Basi baada ya kuingia na kulifunga kinamna, kiasi ambacho lisingeweza kunishinda kufungua, baada ya kuliangalia kufuli lenyewe.

"Muda si mrefu nilisikia mlango unafunguliwa; unajua hili gari lako lilivyoundwa ukiwa ndani ya buti unasikia maneno yanayozungumzwa ndani ya gari. Basi niliwasikia wakikuamrisha kuendesha gari ndipo nikajua nilivyohisi ni sawa. Ulipopiga honi na kusimama kama ulivyoamrishwa, nilijua tunaingia mahali na nikajua kuna mtu anayefungua na kufunga mlango ni wa kundi lao hivyo atakuwa ni mlinzi mwenye silaha.

"Tulipoanza kuondoka niliinua mlango wa buti kidogo sana na nikamuona mtu huyu nusu amebeba bunduki. Niliendelea kuchungulia hivi hivi nikaona njia tuliyotokea kutoka kwenye lango mpaka gari liliposimama nikabana tena mlango. Nikasikia wanakuamru toka kisha nikasikia sauti zingine hapo nje halafu pakawa kimya, ndipo nikafungua taratibu mlango na kutoka nje. nikakata shauri lazima nipate silaha ili niweze kukuokoa.

"Hapo ndipo nilipoanza kurudi mbio kwenye lango ili nikamnyanganye silaha yule mlinzi. Nilipokaribia lango nilimuona yule mlinzi amesimama anavuta sigara huku anaangalia upande wangu. Nililala chini na kusubiri. Alipogeuka na kuangalia upande mwingine nilianza kutambaa chini kimya kimya. Nilikuwa nimefundishwa na wanajeshi wa Polisalio namna ya kumnyemelea mtu kwenye giza bila yeye kushituka. Nilipokuwa karibu nae kabisa, nilisimama na kupiga kelele, "Yeeeeee".

"Alishituka na kuingiwa na hofu na kabla hajatokwa na hofu nilipiga teke mikono yake bunduki ikaanguka chini. Alipoona hivi akaanza kukimbia. Niliruka na kumpiga teke mgongoni akaanguka chini. Bila kuchelewa nilimrukia shingoni, ndivyo ikawa kwaheri. Nilimvua joho nikalivaa halafu nikatafuta kofia. Nilipoipata nikaivaa halafu nikachukua bunduki nikakuta ni aina ambayo wanaitumia wana mapinduzi wa Polisalio, yaani SMG ya kichina, hii bunduki niliitumia sana wakati nimekaa na hawa mashujaa wa Polisalio.

"Nilipoipata silaha hii, nilikimbia kurudi kwenye kibanda mlichoingia nipokaribia nikaona watu wawili wenye bunduki nikononi wakizunguza. Mimi nilizunguka nyuma ya kibanda cha karibu, halafu nikakohoa kisha nikazunguka haraka kutoka pale nilipokoholea. Nilisikia mmoja wao akisema; "Umesikia hicho".

"Ndio", alijibu mwenzake.

"Wewe zunguka huku na mimi nitapita huku".

"Hii ilinipa nafasi kujitayarisha, sikuwa nahitaji kutumia bunduki maana mrio ungewashitua watu waliokuwa ndani ya kibanda. Kwa vile nilikuwa nimevaa nguo kama wao na kofia, nilizunguka na kukutana na mmoja wao, yeye alinichukulia ni mwenzake shauri ya mavazi na giza. Tulikaribiana sana akabweteka; "Umeona nini?". Mimi niliinua mkono kumuonyesha nyuma yake na alipogeuka tu nikamkata karate ya shingo iitwayo ua na bila shaka alikufa pale pale. Nilimdaka haraka haraka na kumlaza chini bila kishindo. Kisha nikageuka upesi upesi ili nikutane na yule aliyepita upande mwingie sikuchukua hata hatua tatu tukawa tumekumbana hata yeye mavazi yalimdanganya na kufikiri mimi ni mwenzake.

"Huku hakuna kitu", aliniambia kwa sauti ya chini chini. Nilimdanganya kwa kumuonyesha kwa ishara aangalie nyuma yake na yeye akadanganyika. Hapo ndipo nilipomrukia nikamtia kabali ya hali ya juu mpaka niliposikia shingo linakatika nikamwachia. Sina mkanda mweusi wa judo na karate bure Willy, najua jinsi ya kuutumia".

"Zaidi ya ambavyo ningetegemea mrembo kama wewe kuutumia", nilimjibu huku nikitoa tabasamu.

"Asante. Baada ya hapo ndipo nilikimbia na kupiga teke mlango kwani nilisikia mlio wa bastola kabla sijapiga teke mlango. nilipoingia nilikuona chini hivyo nikafanya kama ulivyoona. Lo! Willy mpenzi niliogopa niliposikia mlio wa bastola nikafikiri wamekuua!".

"Si lahisi kuniua".

Nia yao ilikuwa nini?".

Nilimweleza yote waliyoniuliza.

Wakati namaliza kumweleza nilikuwa nataka kutoka barabara ya Upanga na kuingia nyumbani kwangu na kupeleka gari moja kwa moja gereji. Tukashuka nikafunga mlango wa gereji.

Karibu ndani vero.Hapa ndipo nyumbani kwangu".

Nilifungua mlango na kuwasha taa ya sebuleni halafu nikamkaribisha ndani akaketi kwenye
kochi.

"Asante lakini sitakaa sana, maana nasikia uchovu, nataka kurudi hotelini nikalale".

"Hakuna haja Vero nina mengi sana ya kukusimulia, maana hata sijakueleza yaliyotupata na Sherriff. Halafu....... nikasita kidogo".

"Halafu nini?", aliuliza kwa shauku.

"Halafu uliniahidi tulipokuwa Siera Leone kuwa tutafahamiana vizuri zaidi Dar es Saalaam, lazima ujuwe kwamba ahadi ni deni".

"Haya baba umeshinda".

"Asante".

Nilichukua vinywaji ndani ya barafu, halafu nikamkaribisha katika chumba cha kulala. Nilizima taa sebuleni nikafunga mlango wa mbele, nikakagua vyumba vyote vya nyumba pamoja na madirisha na milango. Nilipoona kila kitu ni salama nilirudi chumbani nikafungua mlango wa maliwatoni, nikajaza maji kwenye karai la kuogea. Nilimwita Veronika aje tuoge. Tulioga pamoja na mtoto huyu mara moja nikasahau matatizo yangu yote na uchovu wote wa jioni ile. Baada ya kutoka maliwatoni tulikuwa tayari kulala.

"Haya nieleze sasa wakati tukipumzika", Veronika alisema huku amelala karibu yangu.

Nilizima taa yenye mwanga mweupe, nikawasha yenye mwanga wa bluu. Nikaleta chupa yenye whiski kwenye meza ya kitanda nikammiminia Vero ndani ya glasi nikaweka mawe ya barafu na mimi nikatengeneza yangu.

"Na tunywe kwa usalama wa maisha yetu wote".

Tulianza kunywa huku nikimweleza yote yaliyotupata. Baadae tukaelezana mambo yetu binafisi ambayo yalitufanya tujishitukie tumekumbatiana na kubusiana.
 
SURA YA SITA
CHIMALAMO

II

"Amka", Vero alinishitua, "ni saa mbili sasa.

Nilimwangalia Vero ambae alionekana kuwa alikuwa ameamka kitambo kwani alikuwa na sahani ya mayai ya kukaanga na vikombe viwili vya kahawa. Alikuwa amevaa pajama zangu; alitoa sura ya kuchekesha, hivyo nilimcheka, maana zilimpwaya sana.

"Unapendeza katika pajama hizo", nilimtania.

"Kwenda huko".

Mimi nikaangua kicheko, nikatoka kitandani na kukaa.

"Mwenzangu umelala fofofo leo. Mimi nimeamka nikafanya mazoezi kisha nimekwenda jikoni nikatayarisha chochote. Haya tunywe kahawa utoe usingizi", alisema huku akikaa karibu nami.

"Mimi naona nikaoge kwanza".

"Hapana. Tunywe kahawa kwanza halafu tutafanya mazoezi ya judo na karate ili niwe katika hali nzuri, halafu ndipo tutakwenda kuoga".

Basi tulikunywa kahawa na mayai ya kukaanga, halafu tukatoka nje uani kufanya mazoezi. Nyumbaq yangu ilikuwa imezungukwa na ua mzuri wa michongoma iliyokatwa vizuri na yenye urefu wa futi saba. Hivi ukiwa uwani kwangu mtu anayepita nje ya ua hawezi kuona kitu chochote kinachofanyika ndani. Basi tulifanya mazoezi ya karate na judo ya hali ya juu sana. Hii ilinihakikishia kuwa Veronika alikuwan na ujuzi wa kutosha. Ilibidi tu kumwonyesha kuwa mimi najua zaidi nilipomwingizia staili nyingine za pekee ambazo hutumiwa na wajuzi wa hali nya juu katika karate na kung-fu kama mimi, ambazo zilimshinda kuzifuata.

"Ujuzi wako unatosha kabisa Veronika. Naamini unaweza kupambana na mtu yeyote, na nina imani ni watu wachache sana wanaweza kukushinda katika karate na judo".

"Asante kwa pongezi laki. Lo, lakini wewe mwenzangu ni zaidi. Mitindo mingine unayotumia sikuwahi kuiona hata kwa walimu wetu huko Japan. Ndio sababu wanasema ulipambana na Inoki na kutoka nae sare. Nilivyani walikuwa wanaongeza chumvi lakini sasa ninaamini ni kweli. Kokote nitakapotembea na wewe hata pakiwa ni pa hatari namna gani sitaogopa kabisa maana nina imani kubwa katika uwezo wako kwa jambo lolote sasa".

"Asante".

Baada ya mazoezi tuliingia pamoja maliwatoni tukakoga.

"Mimi itabidi unipeleke hotelini nikabadili nguo. Angalia hizi zilivgyochafuka kwa ajili ya matatizo ya jana usiku!".

"Usiwe na taabu, lolote utakalosema".

Mimi nilibadilisha nguo, nikavaa vizuri kabisa kama mfanyabiashara. Nilichukua silaha tulizokuwa tumeziteka nikaziweka sehemu yangu ya siri ambako huweka silaha zangu na ni mimi peke yangu ninayepajua mahali hapo. Na hata ukiwa mtu wa namna gani huwezi kupagundua. Nilichukua silaha nyepesi kwa ajili ya siku hiyo kama litatokea jambo lolote. Nilimpatia Veronika bastola yenya sailensa. Nilipoona mipango yote nimekamilisha tuliondoka kuelekea Kilimanjaro hoteli. Ilikuwa saa tatu na robo tulipofika Kilimanjaro.

"Nenda kajitayarishe, kabla ya saa nne mimi nitakuwa hapa".

"Utanikuta tayari", Veronika alijibu.

Niliondoka na kuelekea ofisini. Nilimkuta Eddy nae anaingia. Alipoona gari langu akasimama mlangoni kunisubiri.

"Habari za leo bosi?".

"Nzuri Eddy, umelala salama kijana?".

"Ndio, bila taabu".

"Twende ofisini kwangu". Tulielekea ofisini kwangu. Tulimkuta Linda anazungumza kwenye simu. Alipotuona akasema, "Huyu ameingia", Akanipa simu huku akisema "Maselina huyo.

"Halo mrembo, habari za asubuhi?".

"Nzuri tu, wasiwasi kwako ambaye unalala mpaka saa tatu na waandishi wa habari ".

"Mwongo, nani kakuambia huyo mwandishi kalala kwangu ?".

"Nani hakujui, danganya wengine lakini miye baba unajua kabisa kuwa nakujua kama nyuma ya kiganja changu".

"Haya umeshinda wewe".

"Njoo Chifu anakuhitaji, anataka kujua umefikia wapi mpaka sasa".

"Haya nakuja, nitamweleza mpaka yeye atachoka".

"Haraka basi", alisema Maselina na kukata simu.

"Eddy jambo lolote juu ya Kiki?".

"Si nilikwambia nitakuwa na habari zote saa nne, na saa nne bado". Eddy alijibu.

"Oke, je juu ya bohari la Mamlaka ya Pamba umepata nini?".

"Walinzi wote wa bohari hilo wamekutwa leo asubuhi wameuawa huko Temeke. Inaonekana walilichukua bohari hilo kwa nguvu ili wafanyie kazi zao kwa muda tu. Kila kitu kingine ni salama. Polisi wanashughulikia hayo ya jana na kujaribu kutambua maiti walizozikuta hapo. Wao wanafikilia ni wezi. Gari walilotumia nalo lilikuwa limeibiwa".

Kisha nikamweleza yaliyokuwa yametupata na Veronika, baada ya kuachana nae jioni ile.

"Sasa fanya uchunguzi ujuwe watu hawa wamejiingizaje huko uwanja ya maonyesho ya Saba Saba, maana uwanja huo unalindwa na polisi masaa ishirini na nne!.

"Nafikiri mtindo wao ni ule ule. Wanaua walinzi na kufanya makao ya muda. Wakimaliza shughuli zao wanakwenda kuteka mahali pengine lakini hata hivyo vijana watachunguza".

"Oke, ngoja mimi nikamwone Chifu halafu tutaanza upelelezi wetu, kama kawaida utatufuata toka New Afrika kama jana, sawa>".

"Bila wasiwasi bosi, kiijana ninayefuatana nae ni mzuri sana nafikiri hata nyinyi mlitupoteza".

"Ndio, kazi yenu ya jana ilikuwa nzuri sana, nilimpongeza.

"Bossi unapendeza sana leo".

"Asante sana kwa pongezi lako. Ngoja nikamwone Chifu".

Nilimwacha akiwa anataka kuzungumza mengi na mimi. Nilipanda ngazi na kuingia ofisini kwa chifu.

"Anatusubiri, amesema nichukue ripoti yako", Maselina alisema.

Basi tulifungua mlango na kuingia ofisini kwa Chifu. Chifu alikuwa amekaa kitini mwake akivuta mtemba kama kawaida yake.

"Shikamoo Chifu".

"Marahaba, ketini chini".

"Asante...

Maselina alichukua kitabu chake cha hatimkato na kukaa tayari kuandika mazungumzo yetu".

"Ehee, nieleze kwa kirefu mambo ambayo umeishafanya. Maana huko makamo makuu ya Polisi kuna kelele, mauaji ya ajabu yanatokea mjini hapa kwa mara ya kwanza mpaka wameshindwa mahali pa kuanzia upelelezi. Nilipopata ripoti yao juu ya mauaji haya, nilihisi hii ni kazi ya Namba Moja. Kwa hiyo naomba maelezo kamili ili nami niweze kuieleza serikali maendeleo yoyote juu ya jambo hili maana kuna wasiwasi mkubwa. Jumuia ya Ulimwengu inaikera serikali kwa kutaka kujua ukweli wa jambo hili, na wakati huo huo maadui zetu wanaendelea kutupaka matope bila kupata ukweli wa jambo hili".

Nilichukua muda huu kumweleza yote tangu nilipotoka ofisini mwake; kwenda kwetu bandarini na ofisi ya Kamati ya Ukombozi, barua niliyoikuta mlangoni kwangu; mapambano dhidi ya waliomteka nyara Sherriff na mwisho walioniteka nyara. Nilimweleza kila kitu kwa ufasaha bila kuacha tukio hata moja. Huenda jambo nililoacha ni juu ya tuliyofanya nyumbani kwangu na Veronika ambayo ni siri yetu hata nyinyi sitaki mjue.


"Kwa kutokana na maelezo ya mtu wa kikundi hiki kinachojiita 'Wanamapinnduzi wapinga mapinduzi' mimi naamini hawa watu ni VIBARAKA wa serikali ya makaburu ambao wanataka kupiga vita harakati za ukombozi dhidi ya serikali hizi dhalimu. Na mtu huyu niliyezungumza nae nina imani ni mtanzania kutokana na sura yake na sauti yake ingawaje alijitahidi sana kunidanganya kwa sauti.

Mimi ninavyofikiri kuna chama kimojawapo katika vyama vinavyopigania uhuru, ambacho makaburu wamekidanganya kuwa kikiweza kupiga vita harakati za mapambano ya silaha dhidi ya serikali ya Afrika Kusini itakipa mwanya chama hicho katika serikali ya makubaliano.

"Kwa hiyo chama hiki kimekubali kuwa kibaraka wa Afrika Kusini na kuanza vita dhidi ya vyama vingine vinavyoendeleza mapambano ya silaha. Kwa vile isingekuwa rahisi chama hiki kufanya mapambano bila msaada. Serikali ya makaburu lazima inakipa misaada ya kila hali, yaani wagtu, silaha na fedha. Kwa hiyo Chifu, ni imani yangu kuwa silaha hizi hazikibwa na watu wengine ila majasusi wa makaburu ili kutimiza lengo lao hilo'.

Chifu alikuwa ananiangalia kwa makini sana kisha akatingisha kichwa.

"Nimekuelewa vizuri sana Namba Moja. Hata unavyofikiri mimi naona ni sawa. Lakini tatizo letu liko pale pale; watu hawa wamejipenyezaje nchini humu na sasa silaha hizo ziko wapi?. Maana silaha hizo ni za kisasa kabisa. Hatua uliyofikia kwa siku moja inaridhisha, tafadhali kazana zaidi katika masaa ishirini na manne yajayo tuwe na fununu zaidi.

"Hapa tuna vyama viwili, PLF na SANP na vyama hivi ndivyo vinaendesha mapambano ya silaha huko Afrika Kusini. Kwa hiyo tuna chama kimoja ambacho kiko nje ya nchi hii; ama kiko Afrika ya Kusini ama katika nchi jirani na ndicho kimejipenyeza kuvipiga vita hivi vyama viwili".

"Hata mimi nafiri hivyo. Kwani kuna vyama vingapi vinavyopigana na serikali ya Afrika Kusini?".

"Viko vingi, kati ya hivyo vitatu viko Afrika Kusini na vitano viko nchi ya nje, kwa hiyo jumla ni vinane".

"Hili ndilo tatizo la vyama vingi. kingekuwa chama kimoja yote haya yasingetokea", nilisema kwa huzuni.

"Siasa kijana, wanasiasa ndio wanaleta taabu ulimwenguni; ndio wanayumbisha vichwa vyetu. Kila mtu na siasa yake na imani yake, na kuna wengine hawana cha siasa wala cha nini; nia yao kutaka ukubwa ili wale", alijibu Chifu kwa uchungu mkubwa.

"Sawa, sisi tunaendelea na upelelezi wetu na ushauri wako nitauweka manani".

"Asante sana Namba Moja".

"Polisi wamefikia wapi?".

"Polisi hawajafika popote. Sasa ndio wamechanganyikiwa zaidi baada ya mauaji haya ya usiku. Hivyo mimi nakutegemea wewe, maana umefanya maendeleo mazuri".

Nilisimama nikampigia kope Maselina nae akaminya midomo kuzuia tabasamu alilotaka kunipa. Chifu alinifungulia mlango na kuniambia. "Nakutakia mafanikio katika kazi hii kijana".

"Asante Chifu", nilijibu kisha akafungua mlango.

"Kavae upesi twende zetu Komredi", nilimwambia Sherriff aliyetaka kubadilisha nguo.

"Dakika tano tu", alijibu kisha akaenda haraka haraka.

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA SITA

CHIMALAMO

III

Ilikuwa saa tano tulipofika New Afrika baada ya kumchukua Sherriff kutoka kwa daktari akiwa anajisikia vizuri kabisa. Veronika ndiye nilikuwa nimewahi kumchukua kabla ya Sherriff.

"Kavae upesi, twende zetu Komredi", nilimwambia Sherriff aliyetaka.

"Dakika tano tu", alijibu kisha akaenda haraka haraka.

Ilikuwa saa tano na dakika kumi na tano tulipoondoka kuelekea Ofisi za PLF. Njiani tulimweleza yote yaliyokuwa yametupata jioni ile tukibakiza tu ile habari ya kwenda kwetu pamoja kulala nyumbani kwangu.

Ofisi za PLF zilikuwa mtaa wa Makunganya karibu na Achells Limited hivyo haikutuchukua muda kufika pale kutokea New Afrika.Tulitokea barabara ya Azikiwe, tukaingia mtaa wa Independence pale kwenye mzunguko wa sanamu ya Askari halafu tukakata kulia pale kwenye taa za usalama barabarani za mtaa wa Independence na Postway, na kuingia Postway. Tukatelemka kidogo mpaka kwenye mtaa wa makunganya moja kwa moja kwenye ofisi za PLF. Tuliegesha gari pale pale mbele ya ofisi tukatelemka na kuingia mapokezi. tulimkuta kijana mmoja akiwa mapokezi.

"Habari zako ndugu", nilimsalimu.

"Salama, sijui niwasaidie nini?".

"Tunaomba kumwona ndugu Cecil Chimalamo".

"Mna miadi naye?'.

"Hapana, lakini ukimweleza kuwa kuna waandishi wa habari toka gazeti la Afrika natumaini anaweza kutuona".

"Subirini hapa kwenye viti".

Tulikaa kwenye makochi mazuri sana. Cecil Chimalamo nilikuwa ninamfahamu kwa sura na vile vile mambo yake kwani nilikuwa nimeshasoma faili lake mara nyingi ofisini. Kwa kifupi wanasiasa wengi walimpenda kwa sababu ya imani zake za kisiasa ambazo mara nyingi zilikuwa na msimamo. Alitambulikana kama kiongozi mmojawapo mashuhuri mpinga ubaguzi na mpenda serikali ya wengi katika Afrika ya Kusini, makaburu walimchukia sana.

Punde yule kijana alirudi akayakatisha mawazo yangu juu ya Chimalamo.

"Mnaweza kumwona chumba namba tatu".

"Asante', nilishukuru kwa niaba ya wenzangu.

Tulikwenda moja kwa moja mpaka chumba namba tatu tukabisha hodi.

"Karibu".

Nilifungua mlango tukaingia ndani tukajikuta katika ofisi.

"Karibuni", alitukaribisha huku akisimama.

"Asante".

"Nyinyi ndio mmetoka kwenye ofisi za gazeti la Afrika".

"Ndio".

"Twendeni mzee anawasubiri".

Alifungua mlango, tukaingia ndani na kumkuta ndugu Chimalamo amekaa anavuta sigara. Alipotuona alisimama.

"Karibuni, ketini chini".

Kabla hatujakaa nilichukua mwanya huu kujijulisha mimi pamoja na wenzangu kwake.

"Mimi naitwa Willy Gamba na ni Meneja Mkuu wa Kampuni iitwayo Afrika Internation Agencies (AIA), na hawa ni waandishi wa gazeti la Afrika. Huyu anaitwa Veronika Amadu na huyu ni Ahmed Sherriff. Wote ni wananchi wa Sierra Leone", tulishikana mikono na kusabahiana halafu tukaketi chini.

"Imekuwaje wewe uwe pamoja nao?", aliuliza.

"Kampuni yangu ndiyo wakala wa gazeti la Afrika hapa Tanzania kwa hivyo haja zao zote naziwakilisha mimi.

"Aisii, nafikiri tumeshaonana mara nyingi. Wewe si mgeni kabisa kwangu ", aliniambia na kuniangalia kwa macho ya kudadisi.

"Bila shaka tumeonana mara nyingi hasa katika tafrija za vyama hivi ingawaje hatujawahi kujulishwa moja kwa moja".

"Ehe gazeti la Afrika linataka nini?", Nilishangaa sana maana hata hakuuliza vitambulisho. Mara moja nikajua mtu huyu aliweza kuwasoma watu na kujua ni watu wa namna gani. Alikuwa mtu mwenye busara nami nikaondokea kumpenda.

"Sisi tumekuja hapa mjini baada ya kupata habari za tukio lililokikabiri chama chako na serikali ya Tanzania kwa ujumla. Jumuia ya Ulimwengu mpaka sasa imegawanyika katika pande mbili. Moja inalaumu Serikali ya Tanzania kuwa ndiyo inahusika na wizi wa silaha hizi ambazo ni za kisasa kabisa, upande wa pili unaamini kuwa hizi ni njama za mabeberu zinazopiga vita harakati za ukombozi wa Afrika Kusini. Kwa hiyo gazeti la Afrika likiwa kila siku linafuatilia kwa makini harakati za ukombozi Kusini mwa Afrika na kuweza kusaidia inapowezekana, linahitaji hasa ukweli wa tukio hili. Hii ndio sababu tuko hapa. Tumeshawaona wakuu wengine katika OAU na katika Serikali ya Tanzania na tumeona hatuwezi kufika mbali bila kujua mawazo yako wewe ambaye ndiye hasa uliyehusika na mali iliyopotea", Sherriff alieleza kwa kinagaubaga.

"Kwa hiyo mnataka kujua mimi niko upande gani katika mawazo hayo mawili ya Jumuia ya Ulimwengu?".

"Hilo ndilo swali letu la kwanza", Sherriff alijibu.

"Mimi nawaunga mkono wanaoamini kuwa hizi ni njama za mabeberu. Wale wanaosema Tanzania inahusika wanajaribu kuongeza petrol kwenye moto huku wakijua kuwa Tanzania ni nchi pekee katika Afrika ambayo haiwezi kufanya jambo hili. Nakuhakikishia kwamba tangu nikae hapa nina miaka sita na sijaona Serikali ya kimapinduzi kama hii. La hasha, Tanzania haiwezi kabisa kufanya jambo hilo ila hizo ni mbinu za mabeberu za kutugonganisha sisi na wenyeji wetu ili mambo yaharibike kabisa. Mimi sitakubali washenzi hao watugonganishe. nafikiri umenielewa.

"Nimekuelewa sana. Sasa unafikiri silaha hizi zimepotea poteaje?. Hapa nataka mawazo yako binafsi".

"Hata mimi sijui. Ni njama ya hali ya juu iliyofanyika, hivyo nimeachia shauri hilo Serikali ya Tanzania ambayo imeniahidi itafanya juu chini kufichua njama hizi".

"Na isipowezekana?", Veronika aliuliza.

"Tutajua la kufanya wakati huo.

"Ilibainikaje kama wewe umekwenda Urusi kutafuta silaha za kisasa na hali naamini jambo hili lilifanywa kwa siri?", Sherriff aliuliza.

"Siku hizi hakuna kitu cha siri. Nafikiri hata kabla sijaondoka hapa Dar es Salaam kwenda Moscow ilikuwa imeshajulikana nini nafuata. Ulimwengu huu wa teknolojia hakuna kitu cha siri. Hata mkutano uliofanyika huko camp Davis Marekani, kati ya Marais wa Israel, Misri na Marekani na kuweka hali ya uficho wa hali ya juu, bado watu walijua kabla mazungumzo hayo ya kisiri ya hali ya pekee hayajatangazwa rasmi. ili kujibu swali lako hata sisi hatukutegemea tutajulikana.

"Watu wanafikiri kuwa, silaha hizo zimefanyiwa njama za kuibiwa kwa sababu ni silaha za kisasa kabisa na za hali ya juu. Ndio sababu watu wanasema Tanzania isingeweza kuziona zinakwenda hivi hivi. Sasa swali langu ni kwamba kwa nini uliamua kuomba silaha za kisasa za jinsi hii wakati vita havijafikia hali ya juu sana kuhitaji silaha za namna hiyo.

"Ahaa, swali lako zuri sana. Ili mwelewe kwa nini nilichukua hatua hiyo ni lazima niwape maelezo kamili, juu ya hali ya silaha alizonazo adui tunayepigana naye", alinyamaza kidogo akaegemeza mikono yake mezani.

"Maana mtu hawezi kupigana kwa rungu dhidi ya mtu mwenye bunduki. Kwa hiyo hamtajali naona nikiwaeleza kwa kirefu jinsi wapinzani wetu walivyojidhatiti kijeshi na ndipo tu mnaweza kuona kwa nini niliagiza silaha za kisasa".

"Sisi tutafurahi sana kupata fursa ya kusikia maelezo hayo", nilijibu kwa niaba ya wenzangu.

"Katika miaka 15 iliyopita", alieleza Chimalamo. "Makampuni ya kimataifa yamezidisha rasilimali zao ili kuimalisha uchumi wa Afrika Kusini. Makampuni makubwa ya Marekani na Ujerumani Magharibi yamepanua rasilimali zao katika sehemu muhimu za utawala wa Makaburu. Na makampuni haya yana ushirikiano mzuri sana na utawala wa Makaburu.

"Miaka michache iliyopita mabenki ya kigeni yameikopesha afrika Kusini mamilioni ya fedha ili kuwezesha kukabili migogoro ya kiuchumi iliyosababishwa na kulegalega kwa uchumi wa nchi za magharibi na kuendelea kukua kwa mapambano ya wazalendo wanaokandamizwa na utawala wa Makaburu.

"Mabenki ya kigeni yametoa mtaji mkubwa kwa utawala wa Makaburu kwa mahitaji ya fedha kwa ajili ya mambo ya kijeshi na kiuchumi, katika miaka michache iliyopita deni la kigeni la Afrika Kusini limeongezeka haraka kufidia gharama za mafuta yake, kupanua ununuzi wa silaha na gharama za mipango ya kuuwezesha utawala huo dhalimu ujitegemee. Kwa taarifa yenu mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 1976 utawala wa Makaburu ulikuwa na deni lipatalo Shs.72 bilion, lakini idadi inaweza kuwa kubwa kuzidi hapo maana mikopo kwa Afrika Kusini ni siri. Sijui mnanielewa?".

"Tunakuelewa sana", tulijibu kwa pamoja, huku Veronika akiwa anaandika maelezo hayo.

"Kuna ukweli unaoonysha jinsi biashara ya makampuni ya kigeni na rasilimali zao zilivyosaidia kuimarisha viwanda vya kijeshi vya Afrika Kusini hata kuuwezesha utawala wa Makaburu kuwa na kiburi na kupuuza maoni ya dunia na kuendelea kudumisha udhalimu wake na kuwakandamiza wananchi walio wengi wa Afrika Kusini.

Makampuni ya kigeni yamejihusisha moja kwa moja katika kuimarisha kijeshi Afrika Kusini. Kumbukumbu za kampuni moja inayoshughulika na utengenezaji wa silaha katika nchi zinazoendelea zinaonyesha kuwa makampuni ya kigeni yametoa liseni kwa makampuni ya Afrika Kusini kutengeneza zana za kijeshi za aina mbali mbali, pamoja na ndege za kijeshi, mabomu, risasi na bunduki. Vile vile kuna makampuni yanayotengeneza vipuri na vifaa vingine kwa madhumuni ya kijeshi. Shirika la Baruti na madawa la Afrika Kusini 'AECI' linatajwa kuwa linamiliki viwanda vitatu vinavyotengeneza silaha na linashirikiana na kampuni moja ya viwanda vya madawa ya Uingereza. "Imperial Chemical Industries", Kampuni hiyo ya Uingereza., imetoa utaalamu na vifaa vinavyotumiwa na Shirika la AECI la Afrika Kusini. Na wakati huo huo kampuni ya Darman Long ya Afrika Kusini iliyounda manowari moja yenye uzito wa tani 220 inashirikiana na Shirika la vyuma linalomilikiwa na serikali ya Uingereza katika shughuli za utengenezaji silaha".

Alinyamaza kidogo, akachukua sigara akaiwasha kisha akavuta mara tatu hivi halafu akaendelea.

"Kutokana na misaada hii toka nchi za Magharibi, Afrika Kusini imejiimarisha sana kijeshi. Utaona kuwa miaka ya sitini, matumizi ya kijeshi ya Afrika Kusini yameongezeka mara sita kutoka Shg 520 milioni hadi mwaka 1977/78 matumizi ya kijeshi yalikuwa yameongezeka tena na kufikia kiasi cha Shg 16,450/- milioni kwa mwaka. Nimetoa maelezo hayo pamoja na tarakimu ili kuwaonyesha kimsingi kuwa Afrika Kusini ina uwezo kifedha kutengeneza au kununua silaha za kisasa kabisa.

Alitua tena ili kuvuta sigara yake kisha akaendelea huku sisi tukimsikiliza kwa makini kama wanafunzi wanavyomsikiliza mwalimu katika somo wanalolipenda.

"Vijana lazima mtu ujue nguvu za adui yako kabla hujamkabili, la sivyo, utakuwa unafanya mapambano yasiyo ya kimsingi. Ili kuwapa ukweli hasa uliopo, jeshi la Afrika Kusini limekuwa likitumia zana za kisasa zilizoko duniani tangu mwaka 1970. Matumizi ya kijeshi kwa ajili ya kununulia silaha na vifaa maalumu vya kisasa vya kijeshi badala ya vya zamani yaliongezeka kwa asilimia 32 mwaka 1971 kufikia asilimia 53 mwaka 1973. Kati ya mwaka 1970 na 1979 Shg 2,240 milioni zilitumika kwa mambo ya ndege za kijeshi, shs 1,000/- milioni kwa ajili ya kununua radio, mitambo ya kutazama ndege angani (radar) na vifaa vingine vya kisasa. Kama nilivyokwisha kuwaeleza hapo awali, wakati huo huo utawala wa Afrika Kusini umekuwa ukichukua hatua kuimarisha utengenezaji wa zana humo humo nchini kadiri vipuli na vifaa vya mahitaji yake ya kijeshi yanavyozidi kuongenzeka.

"Kwa mjibu wa toleo moja la kijeshi la Marekani, tangu tangu mapema mwaka 1971 makaburu walikuwa wanaweza kutengeneza mabumu na baruti kiasi cha kujitosheleza na wanaweza kuuza nchi za nje. Juu ya risasi Afrika Kusini inatengeneza aina 100 za risasi. Kwa bunduki inajitosheleza kabisa. Kwa silaha za jeshi la nchi kavu, ama imejitosheleza ama imefikia hatua za utoaji, na itajitosheleza hivi karibuni kwa zana za jeshi la maji na sasa inatoa zana zote za moto inazohitaji. Bunduki za kisasa kama vile Rifle na Machine-gun vile vile zinatengenezwa. Hivi utengenezaji wa mizinga unaanza, na kuna huduma ya kuweza kutengeneza karibu kila aina ya magari ya kijeshi. Radio za ndege, vifaa vya kutegulia mabomu na vifaa vingine vya kisasa vya kijeshi vinabuniwa na kutengenezwa huko huko Afrika Kusini.

Alinyamaza na kuwasha sigara nyingine na kwa nguvu zile zile akaendelea kueleza.

"Hivi karibuni ilidokezwa kuwa Afrika Kusini inaunda aina fulani za bunduki, mabomu ya kudondoshwa na ndege yenye uzito wa kufikia ratili 1,000 kila moja na inaendelea na utengenezaji wa makombora ya kuangusha ndege. Mabomu hayo inasemekana yalifanyiwa majaribio mwezi Septemba 1977 kwa kutumia ndege za aina ya 'Mirage'. ndege hizi za mirage zilianza kuundwa huko Afrika Kusini chini ya liseni ya kampuni ya ufaransa ya Sessoult mnamo mwaka 1974. Kama hatua ya mwanzo. Afrika Kusini ilinunua vipande 50 vya ndege za aina hiyo na kuunda yenyewe ndege za mirage".

"Wakati huo vile vile ilikuwa tayari imeanza kuunda ndege za kijeshi aina ya Impala za muundo wa Italia-Armachi MB-326, magari ya kijeshi aina nyingi ya silaha ndogo ndogo pamoja na bunduki za aina ya rifle muundo wa Ubelgiji. Na kwa mjibu wa Waziri wa Uliniz wa Makaburu. Afrika Kusini ilitegemewa ianze kutengeneza vifaru vyake. Vile vile Afrika Kusini inasemekana imeanza kuendeleza utengenezaji wa mizinga ya kutungulia ndege aina ya CAC-TUS, ikisaidiwa na kampuni moja ya Ufaransa".

Alipofika hapa aliinua simu na kumwamru mwandishi wake mahsusi atuletee vinywaji baridi na sambusa kisha akaendelea.

"Naona nitawachosha lakini kwa sababu nyie wenyewe mmeuliza mimi nitawapa hali halisi ilivyo na mkiwa kama waandishi wa habari ni vizuri kujua hali ya kijeshi ya huyu adui wetu mkubwa katika Afrika. Kwa kutumia gazeti lenu mnaweza kujulisha jumuia ya ulimwengu ukweli wa nguvu za adui yetu huyu zilivyo, hivyo msitahimili karibu nitamaliza.

Mwandishi wake alileta vinywaji barudi na sambusa.

"Habari unazotueleza ni za kusisimua mno kwani kwetu sisi wengine ni habari mpya, hivyo hata ukiendelea mpaka usiku tutakuwa tayari kabisa kukusikiliza", nilimhakikishia.

"Kama hivyo basi nitaendelea. Magari ni muhimu sana katika mambo ya kijeshi. Kuna makampuni kadha wa kadha ya kigeni ambayo yamekuwa yakiisaidia Afrika Kusini kijeshi katika mambo ya magari. Makampuni hayo ni pamoja na kampuni ya Marekani ya General MOtors (GM), kampuni kubwa duniani inayotoa magari kwa wingi baada ya Vita Kuu ya kwanza. Hivi sasa ina mtambo wa kuunganisha na kuunda magari huko Port Elizabeth, na mtambo wa kutengeneza injini za magari nje kidogo ya mji huo.

"Kampuni nyingine ya magari ni ile ya Ujerumani inayotengeneza magari ya aina ya 'Benz'. Magari ya kijeshi ya aina hii ndiyo yanatumiwa sana na majeshi ya Afrika Kusini. Msemaji mmoja wa kampuni ya magari ya Benz na BMW, alijigamba hivi karibuni kwamba kampuni yake inatengeneza magari hayo Ujerumani kwenyewe na Afrika Kusini na inakusudia kutumia Afrika Kusini kama kituo cha kuuzia magari hayo kwa nchi za nje zilizoko Kusini kwa Ikweta. Hii inaonyesha dhahiri kuwa Afrika Kusini inayo magari haya zaidi ya mahitaji yake ya kijeshi".

Alinyamaza tena akachukua glasi yake iliyojaa Coca-cola akainywa kwa mara moja kisha akainua macho yake na sura yake ikageuka kuwa nzito kisha akaendelea.

"Na mwisho napenda kuwaeleza jambo la mwisho lakini muhimu si kwa sisi wapigania uhuru tu bali kwa Afrika nzima. Katika mwaka 1974 Shirika la Nyuklia la Marekani lililoko Oak Ridge lilipeleka kilo 45 za madini ya 'Uranium' kwa mtambo wa utafiti wa nyuklia uliopo Palandaba huko Afrika Kusini baada ya Tume ya Nyuklia, chombo pekee cha Marekani kinachotoa liseni za usafirishaji nje vifaa vya nyuklia kukubaliana na Afrika Kusini kwamba haitaruhusu madini hayo yapelekwe pengine au kutumiwa vinginevyo. Marekani vile vile mwaka 1975 na 1976 iliipa Afrika Kusini madini hayo yanayotumiwa kutengeneza zana za nyuklia na kuahidi kuuza zaidi madini hayo kwa mtambo wa pamoja na nguvu za nyuklia wa Marekani na Ufarasa unaotazamiwa kujengwa Afrika Kusini mwaka 1984. Kwa jumla Marekani imeiuzia au imeahidi kuiuzia Afrika Kusini ratili 300 za madini hayo kwa ajili ya mtambo wa utafiti wa nyuklia uliopo Palandaba. Kwa taarifa yenu ratili 300 za Uranium zinawza kutengeneza mabomu 15 ya Atomiki".

Kila mmoja alipiga mluzi wa mshangao.

"Nafikiri ndugu Willy nimejibu swali lako kwa kirefu, kwa hiyo utaona sisi wapigania uhuru hatuna budi kuomba silaha za kisasa zinazoweza kukabili nguvu hizi kubwa ya kijeshi za adui yetu. Kwa hiyo tukio hili lililotokea linaonyesha dhahiri kuwa hawa makaburu wameona hatari inayowajia hivyo kuiba silaha hizi ni mbinu moja ya kujihami. Na mimi nimeapa sitarudi nyuma nitaondoka tena karibuni kwenda kutafuta silaha za kisasa na kali toka nchi rafiki ambazo naamini zitaamini kuwa tukio hili ni njama za mabeberu. Hivyo njama zao zinazidisha tu moto katika wapigania uhuru na ndugu zao wanaowasaidia. Huu si mwisho wa mapambano. Ila ni matayarisho tu ya mapambano - historia itanihukumu. Mna swali zaidi?".

Tuliangalia na kukawa hakuna mtu mwenye swali kwani risala yake ilituchoma mioyoni kama miali ya moto wa umeme.

"Asante, tumetosheka", nilijibu kwa niaba ya wenzangu.

"Oke mnakaribishwa tena siku yoyote kwani katika kuzungumza nanyi ndipo tunapoweza kujua hali halisi ya Kusini mwa Afrika. Asante sana vijana wa Afrika kuja kunitembelea". Alitupa mkono wa kuagana.

"Asante sana", tulijibu na kuondoka ofisini mwake kimya kimya.

Tulipofika kwenye gari langu niliona ni saa saba u-nusu, kweli tulikuwa tumekaa sana ndani. Tuliingia ndani ya gari.

"Sasa twende tukaonane na Ray Sikazwe. Rais wa Chama za SANP

ITAENDELEA
 
SURA YA SITA

CHIMALAMO

IV

Ofisi za SANP zilikuwa barabara ya Umoja wa Mataifa baada ya kuvuka barabara inayoingia Hospitali ya Muhimbili. Hivyo niliendesha moja kwa moja na kuingia barabara ya Morogoro kutokea mtaa wa Makunganya. Tulipofika kwenye taa za usalama barabara za Jangwani, nilikata kulia na kuingia barabara ya Umoja wa Mataifa. Nilisimamisha gari karibu na mlango wa ofisi kwani kwa upande mwingine wa barabara kuna gereji na magari yalikuwa yamejaa kibao.

Tuliingia mapokezi na kumkuta binti mmoja anajipaka poda usoni. Alipotuona akaweka mkebe wa poda kando, alijifuta vizuri usoni halafu akatutolea tabasamu.

"Karibuni".

"Asante. Hujambo Binti?".

"Mimi sijambo, sijui niwasaidie nini?".

"Tunaomba kuonana na Ndugu Sikazwe.

"Mna miadi naye?".

"Hapana".

"Basi hawezi kuwaona, ana kazi nyingi sana. Huenda mnaweza kumwona ndugu Amos Shumka ambaye naye ni ofisa katika ofisi hii".

"Wewe ni Mtanzania?".

"Ndio".

"Basi dada sisi hatutaki kumwona mtu mwingine ila ndugu Sikazwe".

"Basi kaka yangu, ndio huwezi kumwona leo. Amesema hawezi kumwona mtu yeyote hata awe nani kama hana miadi naye. Mimi ninatii amri ya wakubwa wangu kwa hiyo siwezi kufanya vinginevyo".

"Jaribu kumpigia simu umwambie sisi tunataka kumwona tunatoka gazeti la Afrika, mwache yeye aamue".

"Hata kama mnatoka katika gazeti la dunia, siwezi", alichukua rangi ya midomo na kuanza kujipaka.

"Naona tumenoa", alisema Veronika.

"Basi, tutajipeleka wenyewe, twendeni", niliwaambia wenzangu.

Yule msichana alisimama na kututangulia haraka haraka na kuelekea kwenye ofisi moja huku uso wake umejaa hasira. Na sisi tukamfuata mbio mbio nyuma. Alipofungua mlango wa ofisi hiyo tu na sisi tukaingia.

Hawa watu nimewakatalia kumwona mzee lakini wamekuja kwa mabavu", alimweleza msichana mwingine aliyekuwa anapiga taipu. Kabla yule msichana hajajibu mimi nilipita mbele na kufungua mlango wa ofisi ya ndugu Sikazwe kwani bila huyu msichana kujua alikuwa ametuelekeza mwenyewe. Wasichana wote wawili walibaki wameshikwa na butwaa na kushika midomo yao. Mimi nilifungua mlango na wote watatu tukaingia ndani. Tulimkuta Ndugu Sikazwe anazungumza kwenye simu, na alipotuona tunaingia mara moja alikata simu na sura yake ikawa na hasira.

"Nani amewaruhusu kuingia ofisini mwangu kwa kikuku namna hii?".

"Samahani ndugu Sikazwe. Sisi tunatoka kwenye ofisi za gazeti la Afrika na tumekuja kukuona kwa jambo la maana sana kuhusu wewe na Afrika nzima. Sasa tulipofika hapa ofisini kwako mzee, msichana wa mapokezi akatukatalia tusikuone. Kwa sababu sisi tuna uhakika kuwa ungeturuhusu tuonane nawe, tumeona hatuna budi kufanya jambo lililo la busara, ambalo ni kujileta sisi wenyewe tukiwa na imani kubwa kuwa utatuona. Naamini umeelewa kwa nini tumechukua hatua hii, na ukiwa kiongozi mmojawapo mwenye busara kati ya viongozi wa vyama vya wapigania uhuru wa Afrika Kusini tuna imani utatupokea kwa mikono miwili. Jambo lililotuleta si jambo la kitoto", nilimweleza kwa utaratibu sana.

Ghafla uso wake ukabadilika. Tabasamu kubwa likaonekana usoni mwake naye akasimama.

"Samahani sana ndugu zangu katika jina la Afrika huru. naamini mtawasamehe hao wasichana pamoja na mimi, kwani ilibidi kutoa amri hiyo kwa sababu sasa hivi nashughulikia tukio ambalo limetokea hivi karibuni ambalo limevuruga vichwa vyetu. Msiwe na wasiwasi jioneni kama halikutokea jambo la kuwaudhi. Karibuni tuendelee na shughuli zilizowaleta".

Baada ya maelezo haya tulipeana mikono tukajulishana kisha tukaketi chini tayari kwa mazungumzo.

"Nafikiri ndugu Gamba tumewahi kuonana?", aliuliza.

"Ndio tumewahi kuonana kwenye tafrija nyingi".

"Umesema kampuni yako ndio wakala wa gazeti la Afrika hapa Tanzania?".

"Ndio".

"Aisee, haya mimi niko tayari tuendelee na mazungumzo yaliyowaleta".

Veronika alikohoa kuliweka koo lake vizuri kabla hajaanza kusema. Alipokuwa tayari alichukua uwanja.

"Gazeti la Afrika ni gazeti ambalo limekuwa na litazidi kutetea mapambano ya Kusini mwa Afrika. Hivi majuzi tumesikia tukio lililotokea hapa mjini, ambalo sisi tumelichukua kama pigo kubwa sana kwenye harakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika. Ndio sababu tuko hapa ili tuweze kuzungumza na viongozi wa Serikali ya Tanzania na Maraisi wa vyama vya wapigania Uhuru walioko hapa nchini hivyo tuweze kupata mwanga wa jambo hili. Kumekuwa na uvumi wa kutatanisha ulimwengu mzima juu ya tukio hili.

"Kuna mambo mawili yanazungumziwa. Jambo la kwanza ni kwamba tukio hili limetokana na njama za mabeberu za kutaka kuzima harakati za ukomboni Afrika Kusini na ndiyo sababu silaha hizi zimeibiwa. Wengine wanalaumu serikali ya Tanzania kuwa ndiyo iliyofanya njama hizi kwani silaha zilizokuwa zimekuja. Serikali yoyote hata iwe ya kimapinduzi namna gani ingeweza kupata kishawishi cha kuchukua silaha hizi kwa manufaa yake. Sijui wewe una mawazo gani juu ya jambo hili", Veronika aliuliza baada ya kutoa maelezo haya marefu.

"Kusema kweli mimi bado nimechanganyikiwa juu ya tukio hili. Mambo yote haya mawili nimeyasikia lakini bado mimi sijasikia uamuzi jambo lipi ni sawa. Kama mlivyonikuta hata mimi najaribu kuzungumza na maofisa mbali mbali wa serikali ya Tanzania na Ofisi ya ukombozi ya OAU ili na mimi nipate msimamo wangu. Tukio hili si la kukimbilia kuamua".

"Kwa hiyo tuseme una wasiwasi kuwa huenda ikawa kweli Serikali ya Tanzania ikawa inahusika?", aliuliza Veronika huku macho yake yakimwuliza Sikazwe.

"Sikazwe alisita kidogo akajaribu kukwepa macho ya Veronika.

"Sina wasiwasi na Serikali ya Tanzania kuhusika na tukio hili, lakini ili niwe na uhakika vile vile ni lazima nichunguze upande huo vile vile. Msinielewe vibaya, mimi ni mtu ambaye mara kwa mara hupenda kuchunguza mambo na nipatapo ukweli nang'ang'ania kwenye ukweli. Sijui mumenielewa?".

"Mimi nimekuelewa kuwa utakuwa na uhakika tu kuwa Tanzania haijahusika utakapopata ukweli wa jambo lilivyo", Veronika alijibu.

Sikazwe alisita tena.

"Kitu kama hicho. Mnajua sisi wapigania Uhuru tuko katika hali ya kutatanisha sana. Kwa sababu serikali za nchi huru za Kiafrika unakuta moja inapendelea chama hiki nyingine chama kile maana sisi tuko vyama vingi. Hivyo ili kuamua jambo hili ni lazima uangalie mambo mengi", alijibu.

"Kama nimekuelewa vizuri unatupa tena hali ya tatu kuwa huenda si Tanzania wala mabeberu waliohusika katika njama hizi ila inaweza kuwa nchi mojawapo katika nchi huru za Kiafrika", nilisema.

"Nafikiri sasa umenipata".

Sisi tuliangaliana kwa mshangao kwani fikra hii ilikuwa haijaingia vichwani mwetu.

"Vizuri tumejua msimamo wako", nilijibu.

"Kwa hiyo ili niweze kuwapa msimamo wangu kamili mnipe muda ili niweze kutuliza mawazo yangu baada ya kuzungumza na watu fulani".

"Unamjua kijana mmmoja aitwae George Kiki", Sherriff aliuliza.

Sura ya Sikazwe ilionyesha mshituko ambao ni mtu kama mimi tu ambaye angeweza kuona.

"Ndio ninamkumbuka aliwahi kuja hapa ofisini kwangu akiwa mkimbizi kutoka Afrika Kusini baada ya matatizo ya Soweto. Na sisi huwa ni wajibu wetu kama chama cha wapigania uhuru kuwasaidia. Tokea siku hiyo mpaka leo sijapata kumwona tena. Je ana nini?".

"Amekutwa ameuawa nyumbani kwake", Sherriff alimjibu.

Sikazwe alionyesha hali ya mshangao.

"Nimesikitishwa sana; alionekana kijana mzuri".

Simu ililia Sikazwe akaichukua.

"Sikazwe hapa".

Akaisikiliza kwa muda halafu akajibu. "Sawa, nakuja sasa hivi".

Akakata simu.

"Sijui mna maswali zaidi maana nahitajiwa ofisi za Ubalozi wa Botswana kwani kesho kutwa nina safari ya kwenda huko kuonana na wanachama na wanajeshi wangu walioko huko".

Tulitazamana tukaona hakuna zaidi.

"Nafikiri inatosha, tukikuhitaji naamini utakuwa tayari kutuona kabla hujaondoka".

"Bila shaka".

Tulisimama, tukapeana mikono na tukaagana. Tulitoka na kuingia ndani ya ofisi ya mwandishi wake.

"Hujambo mrembo, maana hatukusalimiana wakati tunaingia kwani tulikuwa katika haraka", nilimsalimu.

"Mimi sijambo", alijibu huku bado anatuangalia kwa macho ya kushangaa.

Tulimwacha ashangae tukatoka nje ya ofisi na kuelekea mapokezi. Hapo tulimkuta yule msichana.

"Siku nyingine ukitukatalia utafukuzwa kazi. Angalia vizuri sana sura hizi maana sidhani utapata kazi mahali pengine wanakochukua muda kujirembua wakati wa kazi. Hivyo chunga kazi yako", nilimshauri.

"Si nikikosa kazi kwa sababu yako nitakutafuta".

"Nani atataka msichana wa kujirembua huku chungu jikoni kinaungua nyumbani kwake?".

Msichana yule alivimba, tukaona tuondoke kabla hajapasuka. Tulipotoka nje tulielekea moja kwa moja kwenye gari letu tayari kwa safari ya mjini. Ghafla nikasikia sauti.

"Bosi, rukeni ua".

Kama umeme tuliruka na kuanguka chini upande mwingine wa ua wakati ambapo risasi zilimiminika pale pale tulipokuwa tumesimama.

"Nenda ofisini", tulisikia sauti ya Eddy ikiamru.

Kama umeme tuliruka na kuangukia mapokezi wakati tuliposikia mlipuko mkubwa wa bomu uliotingisha hata ofisi za SANP.

Baada ya dakika-mbili hivi Eddy alisimamisha gari lake mbele ya mlango na kuamru twende. Kama risasi tuliingia ndani ya gari na kuondoka kasi na kuacha gari langu likiwa limesambazwa vipande vipande.

ITAENDEEEEEEEEEEENJAMA
CHIMALAMO
IV

Ofisi za SANP zilikuwa barabara ya Umoja wa Mataifa baada ya kuvuka barabara inayoingia hospitali ya Muhimbili. Hivyo niliendesha moja kwa moja na kuingia barabara ya Morogoro kutokea mtaa wa Makunganya. Tulipofika kwenye taa za usalama barabara ya Jangwani, nilikata kulia na kuingia barabara ya Umoja wa Mataifa. Nilisimamisha gari karibu na mlango wa ofisi kwani kwa upande mwingine wa barabara kuna gereji na magari yalikuwa yamejaa kibao.

Tuliingia mapokezi na kumkuta binti mmoja anajipaka poda usoni. Alipotuona akaweka mkebe wa poda kando, alijifuta vizuri usoni halafu akatutolea tabasamu.

"Karibuni".

"Asante. Hujambo Binti?".

"Mimi sijambo, sijui niwasaidie nini?".

"Tunaomba kuonana na Ndugu Sikazwe.

"Mna miadi naye?".

"Hapana".

"Basi hawezi kuwaona, ana kazi nyingi sana. Huenda mnaweza kumwona ndugu Amos Shumka ambaye naye ni ofisa katika ofisi hii".

"Wewe ni Mtanzania?".

"Ndio".

"Basi dada sisi hatutaki kumwona mtu mwingine ila ndugu Sikazwe".

"Basi kaka yangu, ndio huwezi kumwona leo. Amesema hawezi kumwona mtu yeyote hata awe nani kama hana miadi naye. Mimi ninatii amri ya wakubwa wangu kwa hiyo siwezi kufanya vinginevyo".

"Jaribu kumpigia simu umwambie sisi tunataka kumwona tunatoka gazeti la Afrika, mwache yeye aamue".

"Hata kama mnatoka katika gazeti la dunia, siwezi", alichukua rangi ya midomo na kuanza kujipaka.

"Naona tumenoa", alisema Veronika.

"Basi, tutajipeleka wenyewe, twendeni", niliwaambia wenzangu.

Yule msichana alisimama na kututangulia haraka haraka na kuelekea kwenye ofisi moja huku uso wake umejaa hasira. Na sisi tukamfuata mbio mbio nyuma. Alipofungua mlango wa ofisi hiyo tu na sisi tukaingia.

Hawa watu nimewakatalia kumwona mzee lakini wamekuja kwa mabavu", alimweleza msichana mwingine aliyekuwa anapiga taipu. Kabla yule msichana hajajibu mimi nilipita mbele na kufungua mlango wa ofisi ya ndugu Sikazwe kwani bila huyu msichana kujua alikuwa ametuelekeza mwenyewe. Wasichana wote wawili walibaki wameshikwa na butwaa na kushika midomo yao. Mimi nilifungua mlango na wote watatu tukaingia ndani. Tulimkuta Ndugu Sikazwe anazungumza kwenye simu, na alipotuona tunaingia mara moja alikata simu na sura yake ikawa na hasira.

"Nani amewaruhusu kuingia ofisini mwangu kwa kikuku namna hii?".

"Samahani ndugu Sikazwe. Sisi tunatoka kwenye ofisi za gazeti la Afrika na tumekuja kukuona kwa jambo la maana sana kuhusu wewe na Afrika nzima. Sasa tulipofika hapa ofisini kwako mzee, msichana wa mapokezi akatukatalia tusikuone. Kwa sababu sisi tuna uhakika kuwa ungeturuhusu tuonane nawe, tumeona hatuna budi kufanya jambo lililo la busara, ambalo ni kujileta sisi wenyewe tukiwa na imani kubwa kuwa utatuona. Naamini umeelewa kwa nini tumechukua hatua hii, na ukiwa kiongozi mmojawapo mwenye busara kati ya viongozi wa vyama vya wapigania uhuru wa Afrika Kusini tuna imani utatupokea kwa mikono miwili. Jambo lililotuleta si jambo la kitoto", nilimweleza kwa utaratibu sana.

Ghafla uso wake ukabadilika. Tabasamu kubwa likaonekana usoni mwake naye akasimama.

"Samahani sana ndugu zangu katika jina la Afrika huru. naamini mtawasamehe hao wasichana pamoja na mimi, kwani ilibidi kutoa amri hiyo kwa sababu sasa hivi nashughulikia tukio ambalo limetokea hivi karibuni ambalo limevuruga vichwa vyetu. Msiwe na wasiwasi jioneni kama halikutokea jambo la kuwaudhi. Karibuni tuendelee na shughuli zilizowaleta".

Baada ya maelezo haya tulipeana mikono tukajulishana kisha tukaketi chini tayari kwa mazungumzo.

"Nafikiri ndugu Gamba tumewahi kuonana?", aliuliza.

"Ndio tumewahi kuonana kwenye tafrija nyingi".

"Umesema kampuni yako ndio wakala wa gazeti la Afrika hapa Tanzania?".

"Ndio".

"Aisee, haya mimi niko tayari tuendelee na mazungumzo yaliyowaleta".

Veronika alikohoa kuliweka koo lake vizuri kabla hajaanza kusema. Alipokuwa tayari alichukua uwanja.

"Gazeti la Afrika ni gazeti ambalo limekuwa na litazidi kutetea mapambano ya Kusini mwa Afrika. Hivi majuzi tumesikia tukio lililotokea hapa mjini, ambalo sisi tumelichukua kama pigo kubwa sana kwenye harakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika. Ndio sababu tuko hapa ili tuweze kuzungumza na viongozi wa Serikali ya Tanzania na Maraisi wa vyama vya wapigania Uhuru walioko hapa nchini hivyo tuweze kupata mwanga wa jambo hili. Kumekuwa na uvumi wa kutatanisha ulimwengu mzima juu ya tukio hili.

"Kuna mambo mawili yanazungumziwa. Jambo la kwanza ni kwamba tukio hili limetokana na njama za mabeberu za kutaka kuzima harakati za ukomboni Afrika Kusini na ndiyo sababu silaha hizi zimeibiwa. Wengine wanalaumu serikali ya Tanzania kuwa ndiyo iliyofanya njama hizi kwani silaha zilizokuwa zimekuja. Serikali yoyote hata iwe ya kimapinduzi namna gani ingeweza kupata kishawishi cha kuchukua silaha hizi kwa manufaa yake. Sijui wewe una mawazo gani juu ya jambo hili", Veronika aliuliza baada ya kutoa maelezo haya marefu.

"Kusema kweli mimi bado nimechanganyikiwa juu ya tukio hili. Mambo yote haya mawili nimeyasikia lakini bado mimi sijasikia uamuzi jambo lipi ni sawa. Kama mlivyonikuta hata mimi najaribu kuzungumza na maofisa mbali mbali wa serikali ya Tanzania na Ofisi ya ukombozi ya OAU ili na mimi nipate msimamo wangu. Tukio hili si la kukimbilia kuamua".

"Kwa hiyo tuseme una wasiwasi kuwa huenda ikawa kweli Serikali ya Tanzania ikawa inahusika?", aliuliza Veronika huku macho yake yakimwuliza Sikazwe.

"Sikazwe alisita kidogo akajaribu kukwepa macho ya Veronika.

"Sina wasiwasi na Serikali ya Tanzania kuhusika na tukio hili, lakini ili niwe na uhakika vile vile ni lazima nichunguze upande huo vile vile. Msinielewe vibaya, mimi ni mtu ambaye mara kwa mara hupenda kuchunguza mambo na nipatapo ukweli nang'ang'ania kwenye ukweli. Sijui mumenielewa?".

"Mimi nimekuelewa kuwa utakuwa na uhakika tu kuwa Tanzania haijahusika utakapopata ukweli wa jambo lilivyo", Veronika alijibu.

Sikazwe alisita tena.

"Kitu kama hicho. Mnajua sisi wapigania Uhuru tuko katika hali ya kutatanisha sana. Kwa sababu serikali za nchi huru za Kiafrika unakuta moja inapendelea chama hiki nyingine chama kile maana sisi tuko vyama vingi. Hivyo ili kuamua jambo hili ni lazima uangalie mambo mengi", alijibu.

"Kama nimekuelewa vizuri unatupa tena hali ya tatu kuwa huenda si Tanzania wala mabeberu waliohusika katika njama hizi ila inaweza kuwa nchi mojawapo katika nchi huru za Kiafrika", nilisema.

"Nafikiri sasa umenipata".

Sisi tuliangaliana kwa mshangao kwani fikra hii ilikuwa haijaingia vichwani mwetu.

"Vizuri tumejua msimamo wako", nilijibu.

"Kwa hiyo ili niweze kuwapa msimamo wangu kamili mnipe muda ili niweze kutuliza mawazo yangu baada ya kuzungumza na watu fulani".

"Unamjua kijana mmmoja aitwae George Kiki", Sherriff aliuliza.

Sura ya Sikazwe ilionyesha mshituko ambao ni mtu kama mimi tu ambaye angeweza kuona.

"Ndio ninamkumbuka aliwahi kuja hapa ofisini kwangu akiwa mkimbizi kutoka Afrika Kusini baada ya matatizo ya Soweto. Na sisi huwa ni wajibu wetu kama chama cha wapigania uhuru kuwasaidia. Tokea siku hiyo mpaka leo sijapata kumwona tena. Je ana nini?".

"Amekutwa ameuawa nyumbani kwake", Sherriff alimjibu.

Sikazwe alionyesha hali ya mshangao.

"Nimesikitishwa sana; alionekana kijana mzuri".

Simu ililia Sikazwe akaichukua.

"Sikazwe hapa".

Akaisikiliza kwa muda halafu akajibu. "Sawa, nakuja sasa hivi".

Akakata simu.

"Sijui mna maswali zaidi maana nahitajiwa ofisi za Ubalozi wa Botswana kwani kesho kutwa nina safari ya kwenda huko kuonana na wanachama na wanajeshi wangu walioko huko".

Tulitazamana tukaona hakuna zaidi.

"Nafikiri inatosha, tukikuhitaji naamini utakuwa tayari kutuona kabla hujaondoka".

"Bila shaka".

Tulisimama, tukapeana mikono na tukaagana. Tulitoka na kuingia ndani ya ofisi ya mwandishi wake.

"Hujambo mrembo, maana hatukusalimiana wakati tunaingia kwani tulikuwa katika haraka", nilimsalimu.

"Mimi sijambo", alijibu huku bado anatuangalia kwa macho ya kushangaa.

Tulimwacha ashangae tukatoka nje ya ofisi na kuelekea mapokezi. Hapo tulimkuta yule msichana.

"Siku nyingine ukitukatalia utafukuzwa kazi. Angalia vizuri sana sura hizi maana sidhani utapata kazi mahali pengine wanakochukua muda kujirembua wakati wa kazi. Hivyo chunga kazi yako", nilimshauri.

"Si nikikosa kazi kwa sababu yako nitakutafuta".

"Nani atataka msichana wa kujirembua huku chungu jikoni kinaungua nyumbani kwake?".

Msichana yule alivimba, tukaona tuondoke kabla hajapasuka. Tulipotoka nje tulielekea moja kwa moja kwenye gari letu tayari kwa safari ya mjini. Ghafla nikasikia sauti.

"Bosi, rukeni ua".

Kama umeme tuliruka na kuanguka chini upande mwingine wa ua wakati ambapo risasi zilimiminika pale pale tulipokuwa tumesimama.

"Nenda ofisini", tulisikia sauti ya Eddy ikiamru.

Kama umeme tuliruka na kuangukia mapokezi wakati tuliposikia mlipuko mkubwa wa bomu uliotingisha hata ofisi za SANP.

Baada ya dakika-mbili hivi Eddy alisimamisha gari lake mbele ya mlango na kuamru twende. Kama risasi tuliingia ndani ya gari na kuondoka kasi na kuacha gari langu likiwa limesambazwa vipande vipande.

ITAENDELEA
 
SURA YA SABA

BINTI TANZANIA

"Lo, hiyo ilkuwa alimanusura", veronika alisema huku jasho likimtoka na akihema.

"Nakuambia", Sherriff naye huku akihema.

"Eddy, moja kwa moja nyumbani kwangu, akili yangu imevurugika", nilimwambia Eddy aliyekuwa akiendesha kwa kasi sana.

"Huyu Eddy ni nani na katokea wapi?, maana bila yeye sasa hivi sote tungekuwa maiti", aliuliza Sherriff.

"Katika kazi hizi Komred Sherriff lazima uwe na plani bila plani huenda mimi ningekuwa nimeuawa siku nyingi. Huyu kijana ni mfanyakazi mwenzetu, na toka asubuhi yuko pamoja nasi lakini kazi yake ilikuwa ni kutulinda sisi. Na kwa jumla ndivyo hivyo tunavyofanya kazi".

Eddy alisimamisha gari mbele ya nyumba yangu. Tulitelemka ndani ya gari, nikafungua mlango tukaingia sebuleni wote na kuketi. Nilikwenda katika barafu na kutoa chupa ya whiski na chupa za soda kali. Nilitenga glasi, wote wanne tukaanza kunywa. Nilipoangalia saa ilikuwa saa tisa kasoro robo.

"Eddy nafikiri hatuna muda wa kupika hapa nyumbani, hivyo nenda Palm Beach Hoteli wakakufungie chakula cha watu wanne", nilimwambia Eddy".

"Sawa".

Eddy aliondoka kwenda kutafuta chakula.

"Willy, watu hawa wamepania sana", Sherriff alisema kwa sauti nzito.

"Mimi nilijua watapania, ndio sababu nikaweka tahadhari yote hii. Ngoja Eddy arudi atueleze ilikuwaje mpaka wakaweza kutufuata mpaka pale walipotushambulia. Ni bahati nzuri sana kwamba wote mna mafunzo ya kijeshi hivi mlitii amri za Eddy bila hata kufikiri. Jambo hili limenifurahisha sana maana kama mtu angesita, sasa hivi tungekuwa tunamuombolezea".

"Naona wote tumejenga silika ya hali ya juu kwa wakati wa namna hii", Sherriff alijibu.

"Tukimsubiri Eddy, sijui mmewaonaje hawa Maraisi wa vyama hivi vile vile", Veronika aliuliza.

"Mimi moja kwa moja nimempenda Chimalamo maana ni mtu aliye wazi. Nafikiri ni kiongozi mwenye busara. Kutokana na maelezo aliyotupa nafikiri anajua anafanya nini, na mtu kama huyu anaweza kabisa kuendesha harakati za ukombozi dhidi ya Makaburu maana anawajua nje na ndani. Ukikumbuka mazungumzo yetu siku ile huko Freetown juu ya Afrika Kusini sasa ukiongeza haya aliyotupasha ndugu Chimalamo hata wewe unazidi kupata mwanga mkubwa juu ya Afrika Kusini. Kwa ujumla nafikiri Chimalamo ni kiongozi mzuri na halisi. Juu ya Sikazwe nina dukuduku nae moyoni, maana sikumwelewa sawasawa sababu si mtu wazi. Hata nidhamu ya ofisi yake ilivyo kabla hujaonana naye, inaonyesha kasoro fulani. Nafikiri bila Willy kuwa mtu anayejua mbinu nyingi tusingemwona maana mbinu aliyotumia mimi mwenyewe mkufu. Halafu kuna kitu fulani ndani ya Ndugu Sikazwe ambacho sijui ni nini lakini kinanidundadunda sijui wenzangu mmemuonaje?", Sherriff alieleza.

"Nafikiri mawazo yako na ya kwangu hayako mbali. Nakubaliana na wewe kuwa Ndugu Chimalamo ni kiongozi mzuri. Na vile vile kuhusu Sikazwe hata mimi kuna kitu fulani ambacho sikukielewa ni nini kilicho ndani yake, lakini huenda nitakijua nikipata muda mrefu kufikiri. Lakini huenda ni mtu wa tabia ya namna hiyo, na kwa namna yake hiyo anaweza kuwa ni kiongozi mzuri zaidi kuliko hata Chimalamo. Huenda kila kitu kilicho ndani yake ni uongozi bora", nilieleza.

"Mimi sina la kuongeza, naona mawazo yetu yameoana", Veronika alijibu.

"Kusema kweli jamani sijastuka kama leo, kweli tumeponea chupu chupu, asante sana Willy kwa kuweka tahadhari".

"Bila asante Vero, maana ni kazi yangu kuhakikisha usalama wenu na wangu, hivyo uwe na amani kuwa nitafanya kila jitihada kuhakikisha usalama wetu, kama nikishindwa itakuwa nje tu ya uwezo wangu".

"Naomba sigara", Sherriff aliniambia.

"Hapa mimi nina aina ya sigara iitwayo Tropicana, sijui kama itakufaa".

"Wewe nipe tu, sigara zangu ziko hotelini. Baada ya kashikashi nahitaji sigara kama kufa".

"Nilitoa pakiti ya Tropicana nikaiweka mezani tukaanza kuivuta.

"Lo, mbona sigara safi kabisa, ni sawa sawa tu na 555, zinatengenezwa wapi?", Sherriff aliuliza.

"Hapa hapa nchini kwetu".

"Lo, mmeendelea sana, mnaziuza na nje?", aliuliza Veronika ambaye naye alichukua moja akavuta ingawaje hakuwa mvutaji sana.

"Sijui maana wameanza kuzitengeneza hivi karibuni, lakini naamini watafanya hivyo".

Mara Eddy akawa amerudi tukapata chakula ambacho tulikishambulia vizuri sana maana njaa zilituuma vibaya.

ITAENDELEA.....
 
SURA YA SABA
BINTI TANZANIA
II

Baada ya kula chakula cha mchana tulikaa kitako kumsikiliza Eddy, akitusimulia jinsi mambo yalivyotokea pale SANP.

"Baada ya nyinyi kuondoka kwenye ofisi za PLF, nilingoja hadi nikaona gari Peogeot 504 namba TZ 311251 likijitokeza kwa upande mwingine na dereva wake akichungulia kwenye kioo cha kuendeshea baada nafikiri ya kuona hakuna gari zaidi lililokuwa nyuma yake; liliongoza kufuata njia mliyofuata. Mimi nililitilia mashaka nikalifuata nyuma baada ya magari kama mawili hivi kuwa kati yangu na gari hilo. Gari hilo pia lilikuwa limeacha magari matatu kati yake na gari lenu. Tulifuatana hivyo hivyo mpaka kwenye taa za usalama barabarani za Jangwani.

"Hapo ndipo nilihakikisha kuwa huenda gari hili lilikuwa na jambo. Mlipoingia barabara ya Umoja wa Mataifa gari hili lilisita kidogo mpaka gari zingine zikalipigia honi kwani taa zingebadili kabla hatujapita. Inaonekana kulikuwa na ubishi. Baada ya hapo gari hili liliingia barabara ya Umoja wa Mataifa nami nikalifuata. Niliona nyinyi mnasimamisha gari kwenye ofisi za SANP. Nilitelemka na kufungua boneti ya gari langu kwamba limeharibika, huku nikifikilia kuwa lile gari litarudi.

"Nilichukua spana na kuanza kujifanya ninalishughulikia gari langu. Gari lile halikurudi. Mimi niliendelea kujishughulisha hivi kiasi cha nusu saa, wakati nyinyi bado mko ndani ya ofisi. Mara nilistukia gari moja linaingia pale gereji, kwa bahati lilisimama karibu tu na mimi. Ndani ya lile gari mlikuwa na watu wanne. Dereva wa gari hili alitoka na kuingia ndani ya ofisi ya gereji hii. Alikuwa amevalia vizuri sana. Nilimwangalia kwani alikwenda akazungumza na mfanyakazi aliyekuwa amekaa mezani akiandika risti na simu iko upande wake. Alizungumza na mtu huyu wakabishana kidogo kisha nikaona anatoa kitu kama shilingi moja akampa yule mfanyakazi. Halafu yule mfanyakazi akachukua funguo na kufungua kufuli la kwenye simu. Yule mtu akapewa simu akaanza kupiga. Mambo yote haya niliyaangalia kwa chati huku nikiendelea kujishughulisha na gari langu".

Eddy alitua akachukua sigara nikamwashia, akavuta kidogo kisha akaendelea.

"Sura za wale watu wengine ndani ya gari hazikuwa za kawaidana vile vile walikuwa na wasiwasi. Kila mara walikuwa wakigeuka kuangalia upande wa SANP. Yule mwingine alipomaliza kuzungumza na simu alikuja moja kwa moja akaingia ndani ya gari na kulizungusha. Mimi pale pale nikafunga boneti ya gari langu, maana tayari akili yangu ilikuwa imeshakuwa katika hali ya tahadhari nami nikageuza gari langu kuangalia barabarani. Hapo ndipo niliona mnatoka nje ya ofisi. Nikaona mmoja wa watu wale katika gari anainua "machine gun" kutoka chini na kabla hajaweka sawa nyinyi mlikuwa mmefika kwenye gari. Niliruka toka ndani langu na kuwapigia kelele. Nashukru kuwa mlinitii mara moja, kwani wakati ule ule mliporuka alimimina risasi pale pale mliposimama nikajua alikuwa mtu mwenye shabaha ya hali ya juu kwani gari lilikuwa likienda polepole.

"Mliporuka tu niliona mtu mwingine anatoa bomu la mkono na kuuma kifungo chake. Hapo ndipo nilipopiga kelele ya pili kisha nikarukia ndani ya gari wakati yule mtu anatupa hilo bomu na gari lao linaondoka kwa kasi. Ndipo na mimi nikaja na kusimamisha gari langu pale mlangoni baada ya ule mlipuko wa lile bomu. Pole sana bosi gari lako zuri sana limeteketea".

"Siku Eddy, nitapata jingine aina hiyo hiyo, nimetokea kupenda sana aina hiyo ya magari.

"Lo, inaonekana watu hawa wamejitayarisha vizuri sana", Veronika alisema kwa mshangao.

"Toka niliposikia jinsi walivyoiba zile silaha sikuwa na hamu nao tena. Nilijua ni watu wanaojua wanafanya nini. Ndio sababu niliwaasa hatari zitakazotokea toka mwanzo. Nafikiri sasa mnaamini mawazo yangu", hakuna aliyejibu; wote walinyamaza tu. Nafikiri walikuwa wakijutia kwa nini wamejiingiza katika janga hili.

"Vipi Eddy umepata habari zozote juu ya Kiki?", nilimwuliza.

"Kama nilivyokuahidi nimepata habari za kutosha".

Sisi wote tukawa tena tayari kumsikiliza huyu kijana na kusahau yote yaliyopita.

"Ehee hebu lete habari", nilimwambia.

"Nitaanzia toka ripoti nilizopata toka kwa makomredi wetu wa Soweto. Makomredi wetu huko wanakataa katakata kuwa hakukuwa na mtu mwenye jina au wa sura kama nilivyowaeleza huko Soweto. Wanasema mtu aliyetoroka gerezani kati ya wale waliokamatwa na kutiwa ndani, yuko huko huko Soweto na wanaye sasa hivi. Hivyo ni uongo mkubwa kuwa huyu mtu alihusika na matatizo ya Soweto. Inasemekana kuwa mara ya kwanza mtu huyu kuonekana Tanzania ni wakati alipofika Mbeya akiwa na hiyo hadithi yake kuwa ametoroka gerezani huko Afrika Kusini baada ya kutiwa ndani kutokana na machafuko ya Soweto. Habari hii aliitoa kwa ofisi ya Chama huko Mbeya na ofisi hiyo ndiyo iliyomleta Dar es Salaam baada ya kusema kuwa yeye ni mwanachama wa SANP. Hivyo alipofikishwa hapa alipelekwa kwenye ofisi za SANP ambako inasemekana aliwaonyesha kadi yake, hivyo katika hali ya kumsaidia wakampeleka kwenye Kamati ya Ukombozi ya OAU.

"Je umepata habari zozote kuhusu maisha yake hapa mjini".

"Ndiyo, vijana wetu wamefanya kazi nzuri sana. Wameweza kupata habari kuwa Kiki alikuwa mtu asiye na rafiki. Ila alikuwa na rafiki mmoja wa kike Mtanzania anayeitwa Zabibu Abeid. Wanasema msichana huyu aliingia hapa mjini toka Tanga miezi minne iliyopita kwani alikuwa amepatiwa kazi na Meneja wa Kampuni iitwayo Twiga Safari ambayo inashughulikia mambo ya watalii. Msichana huyu amesoma mpaka kidato cha Nne alichomaliza mwaka jana. Anasemekana kuwa na uuzuri wa pekee. Katika ripoti yao wanasema kuwa kama hujamwona msichana huyo basi hujamwona binti Tanzania. Hivyo baada ya Kiki kufanya urafiki na msichana huyu mrembo, muda wake na maisha yake aliyatoa kwa msichana huyu.

"Zababu anakaa mtaa wa Jamhuri, kwenye orofa karibu ya mzunguko wa mtaa wa Zanaki na Jamhuri. Yuko mwenye nyumba ya orofa ya Msajili wa Majumba. Jengo Nambari K orofa ya tatu, nyumba nambari 7a. Nyumba hii amepewa na waajiri wake. Inasemekana kuwa fanicha yote ya mle ndani imenunuliwa na Kiki pamoja na gari moja zuri aina ya Ford Mustang"

"Na huku Kiki alikuwa tarishi tu... nilimkata kauli Eddy.

"Ofisini alikuwa tarishi, lakini nje alikuwa na fedha nyingi za kutosha. Hivyo kwa nje alikuwa ofisa wa mkubwa katika Kamati ya Ukombozi ya OAU".

"Na ndio sababu aliweza kumpata msichana mrembo kiasi hicho?", Sherriff aliuliza.

"Bila shaka maana sura ya Kiki ilikuwa ya kupendeza sana hivyo sioni ajabu kumpata msichana mrembo kiasi hicho".

"Kwa hivyo zaidi ya msichana huyu maisha ya Kiki hapa mjini hayaeleweki".

"Ndiyo, Kiki hakuwa na rafiki mwingine zaidi ya Zabaibu, lakini muda mwingi alikuwa kwa Zabibu. Tumejaribu sana kupata habari nyingine zozote juu yake lakini tunashindwa. Huenda Zabibu anaweza kujua".

"Okejamani nafikiri nyinyi mnaweza kurudi matotelini kwenu. Ila mjihadhari sana maana hali ya sasa ni ya hatari, nitakuja kuwaona baadaye msitoke mpaka nimekuja. Eddy atawapeleka mkapumzike. Mimi nitakwenda kumwona Zabibu sasa hivi, nafikiri atakuwa ametoka kazini", niliwaeleza.

"Nafikiri atakuwa amerudi maana anatoka kazini saa kumi kamili", Eddy alinieleza.

"Twende wote", Veronika alinieleza huku akiniangalia kwa macho ya wizi.

"Hapana wewe nenda ukapumzike, kazi uliyofanya mpaka sasa inatosha. Usiwe na wasiwasi nitajiangalia".

Veronika alikuwa haamini kwenda kuonana na msichana mrembo namna hiyo peke yangu. Hiyo ndiyo ya kazi na dawa.

Waliondoka wakaniacha mimi nikienda maliwatoni. Baada ya kukoga na kubadili nguo, niliangalia saa yangu nikaona ni saa kumi na moja na nusu. Nilichukua bastola yangu nikaiweka ndani ya jaketi nililovaa, nikajiona nilikuwa tayari kupita kiasi kuonana na Binti Tanzania. Nilitoka nje nikafungua mlango, nikaenda mpaka Palm Beach ambako nilichukua teksi kunipeleka kwa Binti Tanzania.






ITAENDELEA
 
SURA YA SABA

BINTI TANZANIA

III

Ilikuwa yapata saa kumi na mbili wakati dereva wa teksi aliponishusha hatua chache kabla ya kufika kwenye mzunguko wa Mtaa wa Jamhuri na Zanaki.

"Hapo hapo pananitosha", nilimweleza huku nikimpa shilingi ishirini kisha nikatelemka. Niliangalia kwenye maegesho ya mtaa huu wa Jamhuri nikaiona gari ya Zabibu. Ilikuwa gari ya rangi ya kijani ambayo haikuiva sana, na ilikuwa ni aina ya Ford Mustang muundo wa kisasa. Kama umeshaiona Ford Mustang zilizoundwa vizuri basi hii ilikuwa mojawapo. Hata mimi niliipenda kwa umbo lake maana ilikuwa na milango miwili. Yaani 'Ford Mustang Sports Car', kama wanavyoiita wenyewe walioitengeneza.

Kule kuona gari hii kulinihakikishia kuwa Zabibu alikuwepo nyumbani, niliangalia jengo, nikaangaza huku na huku kuona kama kuna mtu ananifuata, nikaona hakuna. Kila mtu alionekana kuwa na hamsini zake. Basi mimi Willy nilijipenyeza kwenye lango linaloelekea kwenye ngazi za jengo hili. Nilipofikia ngazi nilianza kupanda taratibu kama mtu anayejua anapokwenda. Nilipanda mpaka orofa ya tatu, na nyumba iliyokuwa inatazamana na ngazi hizi ilikuwa namba 1a na nikajua 7a itakuwa mkono wa kulia hivyo nikafuatia taratibu.

Kwa sababu giza lilikuwa linaingia nyumba zingine zilikuwa zimewasha taa na zingine zikiwa giza kuonyesha wenye nyumba walikuwa bado hawajafika. Nyumba namba 5a na 6a zilikuwa giza ila 7a ilikuwa inawaka taa sebuleni. Nilitembea taratibu bila kupiga kelele mpaka kwenye mwisho wa namba 6a, niliposikia sauti ya msichana inapiga kelele ndani ya namba 7a. Harafu nikasikia sauti ya mwanaume.

"Mimi nisingependa kukuua Zabibu maana mimi nafurahia uumbaji wa Mungu mzuri aliokuumba lakini mimi nimeamriwa nikuue hivyo sina njia. Nisipokuua wewe, mimi nitauawa. Hivyo huna haja ya kupiga kelele, kufa hakika utakufa".

"Kwani mimi nimekosa nini masikini?", msichana aliuliza.

"Hata mimi sijui, haya kwa...".

Mimi nilikuwa nimejivuta na kuwa sawasawa na mlango wa hii nyumba, hivyo nilisikia mazungumzo haya. Niliona nikichelewa msichana huyu anaweza kuuawa. Basi nilitudi nyuma, bastola mkononi, niliurukia ule mlango na kuupiga teke ukafunguka. Hapo hapo mimi nikatumbukia ndani nikitanguliza kichwa chini lakini nikafyatua bastola na kumpata yule kijana niliyemuona ameshika kisu chenye mpini mwekundu. Ile risasi ilikuwa haikumpata vizuri hivi alisimama wakati na mimi nimeshasimama yakaanza masumbwi. Alitupa konde moja likanikosa mimi nikampa shoto langu lililompata shingoni akaenda chini na hakusimama tena.

Mambo haya yalitokea kwa muda mfupi sana. Zabibu alikuwa amepigwa na butwaa kiasi cha kwamba yule mtu alipoanguka chini na yeye akaanguka juu ya kochi na kuzirai. Nilienda kumwangalia yule mtu pale chini, sikuwa na haja hata ya kumgusa ili nijue kama amekufa. Niliona kulikuwa na barafu pale sebuleni, nikaifungua nikatoa chupa ya maji baridi nikammiminia Zabibu naye akashituka.

"Kweli huyu Zazibu alikuwa ndiye Binti Tanzania. Mimi nimeona warembo katika nchi hii, lakini huyu alikuwa ni zaidi. Ukiwa unaamini kuwa kuna binadamu wengine hushushwa moja kwa moja toka mbinguni, basi Zabibu alikuwa mmoja wao, kwani mpaka sasa siamini kama msichana huyu alizaliwa na binadamu. Ingawaje haiwezekani kuamini kuwa mtu anaweza kutelemshwa toka mbinguni, lakini ukimwona Zabibu wewe mwenyewe utaona uwezekano. Maana hata mimi niliona inawezekana kwa huyu kiumbe wa binadamu alikuwa ameumbwa bila kasoro. Palipo ukweli lazima tuseme; mwenzetu alikuwa na uzuri sio kifani. Mcho yake manene ya mviringo yaliyozungukwa na nyusi zenye rutuba yalifunguka na kuniangalia mimi.

"Umetoka wapi?", aliuliza kwa sauti nyororo iliyotoboa rohoni mwangu kama miali ya moto.

"Nimekuja kukuokoa".

"Kama wewe si mmoja wao umejuaje kuwa amekuja kuniua?".

"Kama mimi ni mmoja wao kwa nini nimwue wakati anataka kukuua?".

"Ndicho kinachonishangaza".

"Basi mimi si mmoja wao, mimi ni rafiki yako. Kama una akili timamu tuondoke hapa chumbani kwako maana kinanuka mauti".

"Sijui kwa nini naona kama ninakuamini".

"Kwa sababu ndio jambo la busara".

"Haya nichukue, nitoe hapa, yule mtu kweli angeniua. Huenda lazima nikushukuru, asante sana?".

"Bila asante, msichana kama wewe una haki ya kuokolewa, huna haja ya kushukuru, hiyo ni haki yako".

"Na huyu mtu tutamwacha humu?".

"Nitafanya mipango aondolewe, simu iko wapi?".

"Chumbani".

Aliniongoza chumbani, nikapigaa simu ofisini nikamkuta Eddy nikamweleza kwa kifupi, kisha nikamwambia afanye mpango mtu huyu aondolewe hapa. Eddy akasema atatekeleza.

"Wewe ni polisi?", Zabibu aliuliza.

"Hapana".

'Sasa wewe ni nani?".

"Mimi ni mtu ninayesaidia warembo kama wewe".

Nilimjengea tabasamu babu kubwa kisha nilimshika mkono tukazima taa, nakurudisha mlango, halafu tukaondoka. Nilipata teksi pale chini, tukapanda na kumwelekeza dereva nyumbani kwangu.

"Tunakwenda wapi?", Zabibu aliuliza.

"Nyumbani kwangu, unaonaje?".

"Nakuona wewe ni mtu wa ajabu ajabu tu, usingekuwa umeniokoa nisingekuamini hata chembe!.

Nilikuwa nimeingia na mashaka makubwa kwenda moja kwa moja nyumbani kwangu. Nilikuwa sijui kwa nini, hivyo nikabadili mawazo na kumwelekeza teksi dereva twende Ocean Road ambako ndiko Eddy alikuwa akikaa. Nilikuwa nina ufunguo mmoja wa nyumba yake kwa ajili ya nyakati kama hizi.

Tulikwenda moja kwa moja mpaka nyumbani kwa Eddy baada ya kumwelekeza dereva nyumba. Nilimlipa dereva teksi pesa zake, halafu tukatelemka. Nilifungua mlango kisha nikawasha taa.

"Karibu ndani bibie".

Asante sana".

Nilikwenda kwenye barafu nikaifungua.

"Sijui utakunywa nini?".

"Baada ya vituko vilivyotokea nafikiri whiski na soda kali vitanifaa".

Nilichukua chupa ya whiski na soda kali halafu nikaendea glasi na kumimina kwenye glasi mbili ya Zabibu na ya kwangu halafu tukainua glasi zetu.

"Na tunywe kwa maisha yako marefu mrembo", nilisema.

"Na tunywe", alijibu kisha akanywa whiski ile haraka haraka.

Mimi nilikwenda kwenye simu nikapiga tena ofisini nikampata Eddy. Nilimpasha habari kuwa mimi na huyu mrembo Zabibu tulikuwa nyumbani kwake. Na yeye vile vile akanieleza juu ya kazi niliyokuwa nimemuagiza; vijana walikuwa wamempigia simu kuwa tayari walikuwa wameshaifanya. Nilimpongeza kwa jinsi kazi yake alivyokuwa anaifanya haraka kwa juhudi na maarifa.

"Nafikiri kwanza itabidi tufahamiane", nilimweleza Zabibu.

"Hasa ndilo litakuwa jambo la maana", alijibu.

"Mimi naitwa Willya Gamba, sijui wewe mwenzangu unaitwa nani?".

"Mimi naitwa Zabibu Abeid".

"Lo kweli aliyekuwa jina la Zabibu alijua kweli, kwani mimi naamini umtamu kama Zabibu".

"Ndio unataka kusemaje?".

"Nataka kusema wewe ni msichana mrembo ambaye sijawahi kumwona, na bila shaka aliyekuwa jina la Zabibu alijua utakuwa mtamu kama Zabibu".

"Usinivike kilemba cha ukoka. Kijana nadhifu mwenye sura nzuri na vituko vingi namna hii, haiwezekani kuwa haujamwona msichana mrembo kunizidi".

"Amini usiamini".

"Asante, lakini hata mimi leo nimemwona mvulana wa kipimo changu, sijui ulikuwa umejificha wapi mji huu hata nisikuone?".

"Mimi nilikuwepo nimejaa tele hapa mjini, lakini najua ingekuwa vigumu kuniona maana George Kiki alikuwa amekuganda kama kupe".

Pale pale sura yake iligeuka akainua macho yake marembo kunitazama machoni. Mimi nikamjengea tabasamu la sheria yake, Zabibu alionekana alikuwa amechanganyikiwa mawazo.

"Unajua nini juu ya George?".

"Hakuna haja ya kuzungushana sana, nafikiri inabidi sasa tuelezane ukweli. Na kabla hatujaendelea mbali ningependa kukuuliza lini umeonana na Kiki kwa mara ya mwisho".

Kwa kutokana na uzito wa sura yangu, Zabibu alilegeza sura yake kisha akajibu kwa sauti nyororo.

"Siku nne zilizopita, alisema atakwenda safari Botswana na atarudi baada ya wiki tatu".

"Na hauna habari nyingine yoyote kuhusu yeye?".

"Sina, kwani kumetokea nini?".

"Kwani yule mtu aliyetaka kukuua alikuwa amekueleza nini?".

"Hata, alinieleza tu kuwa alikuwa ametumwa kuja kuniua ingawaje yeye hakutaka lakini alikuwa amelazimishwa. Hakunieleza kabisa sababu.

"Nakuomba uwe na roho ngumu, rafiki yako George Kiki ameuawa jana. Maiti yake ilikutwa chumbani mwake ikiwa imechomwa kisu chenye mpini mwekundu".

Nilitoa kisu nilichokuwa nimekiokota nyumbani kwa Zabibu kabla hatujaondoka.

"Na watu wale wale waliomwua ndio walikuwa wanakuja kukumalizia wewe".

Zabibu alibubujikwa machozi na kidogo azirai tena.

"Lazima ujitulize kwa sababu mimi niko hapa kupeleleza mauaji ya mpenzi wako".

"Mimi nilijua tu wewe ni Polisi. Sura yako na namna ulivyoingia chumbani kwangu sijapata kuona kwa macho ila ndani ya sinema tu. Zile sinema za kijasusi".

"Mimi si polisi bali ni mpelelezi. Huenda polisi nao wakaja kufanya upelelezi wao, lakini mimi bahati nimewahi na kukuokoa huenda wao wangefika wakati wewe umekwisha kuwa maiti".

"Una maana gani kusema wewe ni mpelelezi wala si polisi?".

"Mimi ni mpelelezi wa siri kama umewahi kusikia watu kama hao".

Macho ya Zabibu yakapanuka.

"Usije ukawa wewe ndiye mtu ambaye huwa tunasoma habari zake kwenye magazeti akipambana na majasusi mbali mbali wanaofanya maovu dhidi ya Afrika".

"Ndio mimi".

Zabibu aliruka pale alipokaa akaja katibu na mimi.

"Ooh! Mungu ni bahati gani kuonana na mtu kama wewe maana mimi nilikuwa nafikiri ni maneno ya uzushi tu ya magazeti maana walikuwa hata hawatoi jina. Kila mara ukisoma unaona tu vijana wa Afrika wakiongozwa na mpelelezi mashuhuri kutoka Tanzania wamefaulu katika kuwateketeza majasusi ya mabeberu yaliyokuwa yanatenda mambo maovu dhidi ya Afrika. Nitawaeleza rafiki zangu kuwa ni kweli huyu mtu yupo na mimi nimeonana naye".

"Halitakuwa jambo la busara, tafadhali fanya hii iwe siri kati yangu na wewe, nimekueleza tu kwa sababu unaweza kunisaidia katika upelelezi wangu juu ya tukio la kutisha lililotokea hapa mjini siku chache zilizopita".

"Ahaa nimeelewa tumesikia kwenye maredio ya nchi za nje, kuwa silaha kali za wapigania uhuru zimeibiwa kwenye bandari ya Dar es Salaam".

"Basi umebashiri sawa".

"Sasa George ana uhusiano gani na tukio hili?".

"Ndio sababu tumekuja kukuona, huenda ukajibu maswali yangu nitaweza kuambulia jambo lolote linalomwunganisha Kiki na tukio hili".

"Niko tayari kukusadia, kwanza kwa sababu umeniokoa, pili kwa sababu unapeleleza kifo cha mpenzi wangu na tatu nafikiri wewe ni kijana mwenye kupendeka".

"Asante, swali langu la kwanza nilitaka kujua kama ulikuwa unajua Kiki ni mtu wa Afrika Kusini?".

"Nilikuwa najua".

"Alikwambia alikuwa akifanya kazi gani?".

"Alisema yeye ni mwakilishi wa chama cha SANP katika Kamati ya Ukombozi ya OAU".

Nilishangazwa na jibu hili lakini sikuonyesha.

"Kwa hiyo mara nyingi alipokuwa anakuja kwako alikuwa akiandamana na wanachama wenzake wa SANP?".

"Hapana, George alikuwa mtu wa pekee, huenda ndio sababu nilimpenda. Alikuwa kila siku ananiambia kama ninataka kuepukana na matatizo nisizoeane na watu wengi. Na yeye kweli alikuwa hakuzoeana na watu. ila alikuwa na marafiki wawili tu. Ndugu Ray Sikazwe, rais wa SANP na Patlako Shuta ambaye ni ofisa mkubwa katika SANP. Sikumwona na mtu mwingine. Oh, kidogo nisahau, vile vile walikuwa na rafikio yao mwingine Mzungu ambaye George alifahamishwa kwake na Sembuche na mwenzake Shuta. Na hata gari nililo nalo, George aliuziwa na Mzungu huyu. Kwa vile yeye alikuwa hapendelei gari kwani alikuwa anatumia gari la ofisini alinipa mimi".

Kwa mara ya kwanza niliona mwanga kwa mbali, na nikajua kwa nini msichana huyu alitakiwa auawe. Nilijivunia bahati yangu kuwahi kabla hajauawa.

"Unaweza kujua Mzungu huyu anafanya kazi gani?".

"Lo! hawa ndio wenye lile kampuni kubwa lililo na makampuni kadha wa kadha katika nchi nyingi za kiafrika yaani EUROAFRO Limited. Na huyu Mzungu ndiye mwakilishi wa kampuni hilo hapa akiangalia akiangalia makampuni yake madogomadogo yaliyoko hapa".

Kapuni hili EUROAFRO Limited lilikuwa kampuni kubwa la kibepari lililokuwa na hisa nyingi katika makampuni katika nchi nyingi za Afrika. Kirefu chake kilikuwa EUROPE - AFRIKA COMPANY. Uhusiano huu kati ya wanachama wa chahama cha wapigania uhuru na kampuni ya kibepari ulinishinda kuelewa.

"Kwa hiyo unasema huyu Sikazwe na Shuta walikuwa marafiki wa karibu sana wa Kiki

"Ndiyo, hao ndio alikuwa anatembea nao mara kwa mara na vile vile walikuwa wanajuja kumwona au kumchukua pale kwangu mara kwa mara. Lakini zaidi ya watu hawa wawili na yule Mzungu, George hakuwa na rafiki mwingine".

"Huyu Mzungu unaweza kumkumbuka jina?".

"Ndiyo anaitwa Tony Harrison".

"Hawa marafiki wa Kiki uliweza kuzoeana nao?".

"Kusema kweli, Shuta na yule Mzungu walikuwa wananiheshimu kiasi cha kutosha lakini Sikazwe alikuwa wa ovyo sana. Amewahi kunitongoza mara nyingi na kunitaka nimwache George. Kwanza alikuwa anajivuna kuwa yeye ni Rais wa Chama na George alikuwa mtu mdogo tu, na kwamba msichana kama mimi sikufaa kutembea na George ila mtu kama yeye. Mimi nilimponda na kumwambia cheo na pesa havileti mapenzi, ila mtu anampenda mtu kwa vile alivyo, maana mtu na mtu ndio wanapendana".

Lakini nakwambia uso wa msichana huyu unapoonyesha sura ya haya ndipo uzuri wake unapozidi. Ingekuwa wewe usingevumilia lakini mie nilipiga moyo konde na kuendelea na kazi. Nilifikiria swali jingine nikaona nimepata maelezo ya kutosha ila nikaamua nimweke zabibu chini ya ulinzi wangu mpaka hapo baadaye.

Nilikuwa bado nafikiri hivi wakati tuliposikia gari linapiga breki mbele ya nyumba. Nilitoa bastola yangu tayari. Mlango ulipofunguliwa na Eddy akakingia.

"Bosi, twende haraka Veronika amenipigia simu anasema yuko katika matatizo. Nimekuja sababu nilijua huna gari", Eddy alisema huku akitweta.

"Oke Zabibu, subiri hapa tutarudi sasa hivi".

Nilifungua mlango kabla Zabibu hajasema neno lolote.

ITAENDELEA
 
Mkuu Mbuzi, baraka zikufikie popote ulipo! endelea kutupa uhondo! nasubiri kwa hamu!
 
wengine tunaweza kusoma papillon (560 pages) kwa siku moja sasa hii ya kushusha hiki kitabu kama Doz ya panadol inaumiza kichwa wewe unashusha kwa wiki nzima wakati watu wanasoma kwa lisaa limoja..

Fanya hima Mbuzi Mzee nadhani watu wamesubiri vya kutosha (shusha hii kitu for educational purpose kabla w/end haijaisha)
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom