Ukisikia upumbavu basi huu ni wa kiwango cha ajabu!
Wenye kumiliki Vitz tena vya mkopo kabisaaa!, ni Rahisi sana kuwajua, wana mihasira hao!!! hee! hawataki kuviachia, na hela ya kununua Midude km ya nyarusare hawana!! na Kirkuu haikamatiki siku hizi!! wanadharaulika sana Barabarani Bongo! huko mikoani sijui ...
Yaani Mara wachomekewe Maksudi na madereva wa Daladala, kisingizio sijakuona mkuu!! kigari kiko chini!! sasa wewe simamisha hicho kidude chako barabarani eti una subiri trafik aje kupima utoporo,
Uone utakavyo koga mitusi na kashfa kwa wenye ndinga kali! !! kama siyo kusukumwa na wapiga debe ili upishe wapate hela! utasikia ''hoyaaa!! kapike kwanza ndo uje" wa mkoa ni ngumu kujua matusi ya hivi!
Kama mimi muongo test! nenda nako kanisani siku moja! kama utapewa seat ya mbele na wahudumu wa kanisa!! uje unambie, lkn wenye mindinga mikali wanapokelewa na wahudumu wanaonyeshwa viti vya mbele kabisa wanakuwa wa kwanza kubarikiwa na Padre!
Kama ni mkate wa Bwana wenye ndinga kali na familia zao! wanapewa wa aina ya pekee! ili wabarikiwe zaidi!! halafu wanakuwaga wa mwisho mwisho wakitoka na Mapadre,
Sasa wewe mzee wa heli 79 na kadude kako hako kamebanwa katikati humo! hutokimo mpaka waje! tena kwa muda wao! na madoi ido! bwena bwena! utasikia ''Oooh! sorry! sorry!'' halafu hawakuangalii usoni! ukirudi kanisa hilo.....heee!!
Kama naongopa jaribu paleee SDA Magomeni uone!! KKT, RC city centre!! Arusha Usaliver, nk utazimia. ni bora ukiache home! na watu wanao ishi jirani na makanisa wanauzio mkali hapo lazima ukomae na Parking ya kanisa tuuu! je hujawekwa mtu kati?
labda ubaki humohumo kwenye ki gari kila wakija unakarudisha nyuma! waongoza park watakubananisha tu humo kati!
Pole sana Mkuu ila kwa Dar! utaumia sana! kwa kuendesha hivi vidude!! kuna vitu ni mateso unaweza kujinyonga hivihivi! najua sana madhila mnayopitia ujue hakauziki kirahisi!! ni rahisi dereva wa Lori la mchanga kukwepa mpita njia ili agonge vitz!! sasa huoni kuwa wewe ni target?
Ni vizuri ukaendeshee nje ya Mji km Chalinze hukooo! kwa kina kikwete lkn pia baba uwe makini Mabasi ya Mkoa ndo zao! tatizo ni kwamba hawaoni tabu kukuletea! sababu ni vilaini mno! Gari lake litabaki zimaaa! hasa ukikosea tu ukawa wrong site! heeeee!!! sijui......