Wito: Watu Wenye Uwezo, Tujitokeze Tujitolee Kumsaidia TAL na Kuisaidia Chadema to Play Real Politics, No Reforms No Election ni Utopian Politics!.

Ni nani anayeweza kuongelea vyote ulivyotaja.
 
Mkuu Ben, Benny Haraba , naomba unielimishe kidogo hii kastigatingi kwenye siasa ni nini, sisi wengine vingeleza vyetu ni tulisoma enzi za waalimu wa UPE!.
P
Ni kumuongelea mpinzani wako wa kisiasa mbele ya kadamnasi kuhusu mambo yake mabaya hata kama niyakweli ili jamii imchukie tena kwa dhihaka

Mara nyingi wanasiasa wana maamuzi chanya na hasi ambayo yanaweza kuijenga jamii ama kuibomoa jamii mengi tunayajua hatuna fursa ya kuyaongelea

Kumbe viongozi wa kitaifa wanatakiwa watunze kauli zao

Public figures have to keep their words

TAL has to change, he is leading a political party not a pressure group
 
Kwa mazingira ya sasa Lissu hafai anaenda kuiua chadema. Situational Leadership kwa muktadha wa kisiasa walau uzingatie mambo manne, mosi nguvu ya chama chako kipindi hicho (hali ndani na nje ya chama). pili, nguvu ya chama tawala (ndani na nje ya chama). Tatu, hali ya ushawishi wenu kwa watendaji wa serikali (vyombo vya ulinzi na usalama na watumishi wa umma). Nne, ushawishi wenu kwenye jamii (mf viongozi wa dini, michezo, sanaa). Kwa maoni yangu chadema vitus hivyo kwa sasa hawana na Lissu hana. Uongozi mpya wa chadema ungejikita kwanza katika kazi za ndani ya chama i.e. kuunganisha chama na kisha kitafute kuwa na ushawishi na makundi tajwa hapo juu. Kitu ambacho Mwenyekiti Lissu hakiwezi, kwa kuwa hajawahi kufanya siasa na upatanishi na ushawishi. Mtu sahihi kwa kazi hiyo walau angeweza kuwa Mwenyekiti John Heche.
 
Anafaa sana kwasababu anaongea ukweli ili jamii iamke tunaishi kwenye jamii ya kanyaga twende yaani jamii ya bora liende jamii ambayo haiwezi kuchakata fikra chanya na hasi, jamii unayoweza kuisafisha ubongo ikafikiri unavyotaka taka wewe

Kwasasa inatumika tabia ya unyumbu wa kisiasa kuendesha nchi, unyumbu wa kisiasa ni tabia ya wanaopewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza ama kulitumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi na uoga wa kuigiza kwa viongozi wao, (unafiki)

Upumbavu ni kipaji, mpumbavu ni mtu aliyebobea kwenye jambo fulani lakini ana mapuuza hatekelezi majukumu yake kwa weledi anajizima data tuseme kuahirisha kufikiri kizalendo kwasasa uchawa

Kuhusu chaguzi zetu ni chaguzi za mauaji, uporaji haki za mpiga kura kuwaweka madarakani watu ambao hawakuchagulia kihalali

Silent society -jamii iliyo nyamaza ama nyamazishwa swali je jamii Itaendelea kunyamaza hadi lini

Silence surrenders public responsibilities -ukimya ni sawa na kusalimu amri, (nyoosha mikono juu), kuhusu maswala ya kijamii

Huwezi kuendesha shughuri za kiuchumi kwenye jamii mfu tuseme jamii iliyo nyamaza kwavile huwezi kufanikiwa
 
Wewe Pascal na mwenzio Ansbert Ngurumo ni watu hatari sana kwa maendeleo ya Chadema!! Nyie wawili ni mapandikizi/ Askari kipenzi!! Viongozi wa Chadema ya sasa hawana budi kuwaweka mbali .
 
Nilipoanza kusoma nikaona umeanza kwa kumpa maujiko na vyeo kibao, nikajua tu mwisho utamsagia kunguni mazee....😜
Ila TAL anapaswa kupunguza uanaharakati ili ajikite kwenye siasa na hoja pasipo na jazba..😊
Lissu chama kimeshamshinda jana nilikua na leaders wa chadema wanasema hana pesa hajakamilisha wajumbe wa kamati kuu so msajilmyika kaondoshwa kimya kimya ofisini akienda anasoma vmsajiki a batambua kamati ya mboe anatambua watu wa mboe
 

Huu ushauri ningeuelewa kama Uchaguzi wetu ungekuwa ni fair game. Sasa CCM wanavuruga uchaguzi na kuuiba wote halafu badala ya watu kuwanyoshea vidole CCM na Mama Abdul, mnawanyoshea wale wanaojaribu kutafuta solution.

Hivi kweli kwa akili ya kawaida kabisa, kuna sababu yoyote ya Wapinzani kushiriki chaguxi za design ya 2020 au 2024 wa MWENYE KIFUA KIPANA?
 
Siyo chaguzi bali uchafuzi
 
Mwenye kale ka video clip cha Sugu cha ..Maneno meengi,unamaliza miti tu.Angekiweka hapa kangefupisha vya kuandika.
 
Toa summarize tunataka mzee wa vipindi vya sabasaba 😁😂🔥 jaah ni mengi kusoma yanachosha
 
Yah, Bora kupumzika till 2030, hopefully REFORM zitakuwa done
 
Zamani nilikuovarate, labda kwakuwa ulikuwa bado kijana, ila unavyozidi kuzeeka naona unakuwa utopolo zaidi. Cdm wajipange na uchaguzi wakati unaona chaguzi zinazidi kuwa za kipuuzi. Upuuzi uliojitokeza juzi uchaguzi wa SM za mitaa ulikuwa wazi, ni kipi kinachokufanya uone huo mkuu utakuwa na tofauti hadi utake wafanye siasa za mikakati?

Huu ushauri wako ndio Zito Kabwe anafuata, si huyo anajiliza kila uchaguzi kwa kufanyiwa uhuni? Unataka watu wafanye siasa huku chama chako kinanajisi demokrasia!
 
Mkuu umeanza tena, no reforms no election ndo mpango mzima, wewe si unakumbuka kwenye kura za maoni ,pangekuepo na haki ndani ya chama chenu wafikri ungeweza pata izo kura ulizopata mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…