Wizara ya Afya na Elimu: Kwanini Watoto wa shule ya msingi wamemezeshwa dawa pasipo mzazi kupewa taarifa?

Wizara ya Afya na Elimu: Kwanini Watoto wa shule ya msingi wamemezeshwa dawa pasipo mzazi kupewa taarifa?

IQup

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2018
Posts
1,166
Reaction score
1,808
Nimesikitishwa sana kuona leo watoto wa shule ya msingi "serikali" wakirudi kutoka shuleni wakiwa wamedhoofika sana, miili ikiwa dhaifu na macho mekundu kabisa.

Nilipowauliza, walisema wamepewa dawa shuleni na kumeza bila kula. Dawa hizo wamesema ni za kichocho na minyoo, na wamepewa pasipo wazazi kuarifiwa wala kuulizwa ridhaa yao.

Walimu nao wameeleza kuwa walipewa taarifa ghafla kwa njia ya simu kwamba waandae watoto kumeza dawa hizo.

Najiuliza, shuleni wana lengo la kuua watoto au kuna shida gani? Je, shule za msingi za serikali zimegeuzwa kuwa sehemu za majaribio ya dawa kwa watoto? Kila mzazi ana utaratibu wake wa kutibu watoto wake. Kwa nini watoto wanalazimishwa kumeza dawa bila taarifa kwa mzazi?

Mnawapa dawa za kichocho na minyoo, lakini mnajuaje kama tayari wazazi wao wamewapa dawa nyumbani?

Lengo la kupeleka mtoto shuleni ni kujifunza na kusoma, si kumeza dawa. Wanapata wapi ujasiri wa kuwamezesha watoto dawa kinyemela pasi na ridhaa ya wazazi? Serikali yangu inasikitisha sana kwa matendo haya.
 
Unalalamika hilo, hujui kama chanjo nyingi tu pia huwa zinatolewa shuleni?
Mwaka huu wamehawa hadi colgate na mswaki kwa wanafunzi aa s/msingi (sijui kama ni mikoa yote), dawa yenyewe ni ile saizi kama ya 600 sh kwa zile za whitedent.
wanalengo gani hasa? wameshindwa kuwapa elimu nzuri watoto...wameanza kuwanywesha dawa!!..tena kimya kimya?....wazazi wataamini vipi kama hizo dawa ni za minyoo na kichocho?, kwakuwa watoto hawana maamuzi basi wanawapa tu dawa bila mzazi kuhusishwa?
 
wanalengo gani hasa? wameshindwa kuwapa elimu nzuri watoto...wameanza kuwanywesha dawa!!..tena kimya kimya?....wazazi wataamini vipi kama hizo dawa ni za minyoo na kichocho?, kwakuwa watoto hawana maamuzi basi wanawapa tu dawa bila mzazi kuhusishwa?
Labda kupunguza idadi ya watoto watakaozaliwa na hao wanafunzi pindi akianza kupata watoto (ukiachana na family planning).
 
sasa hivi ni mwendo wa kimya kimya maana mkishapewa taarifa unaaza kuwa mjadala wa kitaifa ,wanaibuka wataalam uchwara kila mtu anaongelea lake kutia watu hofu, lakini wala sio jambo geni watoto kupewa chanjo mashuleni.

Maana huku mtaani kuna conspiracy nyingi sana kuhusu hizi dawa kwamba, ni ili kuwa fanya watoto kuwa mashoga ,kuwapunguza wa Africa wasiwe na uwezo wa kuongezeka ,lakini ukikaa ukijiuliza maswali una kosa majibu maana madawa yote ya hospital na vifaa mbalimbali wanaotengeneza ni wazungu kama kweli wana nia mbaya ya kuwa angamiza wa Africa mbona kuna njia nyingi tena nyepesi wanaweza timiza azma zao bila kutumia nguvu.
 
sasa hivi ni mwendo wa kimya kimya maana mkishapewa taarifa unaaza kuwa mjadala wa kitaifa ,wanaibuka wataalam uchwara kila mtu anaongelea lake kutia watu hofu, lakini wala sio jambo geni watoto kupewa chanjo mashuleni. Maana huku mtaani kuna conspiracy nyingi sana kuhusu hizi dawa kwamba, ni ili kuwa fanya watoto kuwa mashoga ,kuwapunguza wa Africa wasiwe na uwezo wa kuongezeka ,lakini ukikaa ukijiuliza maswali una kosa majibu maana madawa yote ya hospital na vifaa mbalimbali wanaotengeneza ni wazungu kama kweli wana nia mbaya ya kuwa angamiza wa Africa mbona kuna njia nyingi tena nyepesi wanaweza timiza azma zao bila kutumia nguvu.
sawa mkuu, ila sasa vipi kuhusu watoto kula mbona hawazingatii hilo. Kuwapa dawa pasipo kuwalisha kweli?
 
Tupite humo
 
Wamekosea kwa kutokutoa taarifa kwa wazazi ili watoto waje wamejiaanda kwa kula.

Ila dhumni/ lengo la kutoa dawa za minyoo hua Ni sera ya afya ya kupambana na magonjwa ya minyoo ambayo sansana uwapata watoto.

Ili kutimiza sera hio ndo maana dawa zinapelekwa mashuleni ambako kundi hilo lilio kwenye hatari ya magonjwa hayo yanayosababishwa na minyoo upatikana.
 
Watu mna gubu sana aisee, hizo dawa nakumbuka hata mimi nilikunywa nikiwa shule ya msingi. Dawa za kichocho na Minyoo ni utaratibu wa kawaida wa mass kampeni ya kuzuia hayo magonjwa husika, yemeonekana yanasumbua sana watoto wakati ni kitu kinazuilika.

Kuna watu wapo huko wizara ya afya kazi yao ni kuwaza wanapunguzaje haya magonjwa kwa watoto, njia wanazokuja nazo ndio kama hizi. Kama umempatia mtoto wako nyumbani hamna shida na wao wanajua hilo.
 
Watu mna gubu sana aisee, hizo dawa nakumbuka hata mimi nilikunywa nikiwa shule ya msingi. Dawa za kichocho na Minyoo ni utaratibu wa kawaida wa mass kampeni ya kuzuia hayo magonjwa husika, yemeonekana yanasumbua sana watoto wakati ni kitu kinazuilika.

Kuna watu wapo huko wizara ya afya kazi yao ni kuwaza wanapunguzaje haya magonjwa kwa watoto, njia wanazokuja nazo ndio kama hizi. Kama umempatia mtoto wako nyumbani hamna shida na wao wanajua hilo.
Huyu mzazi hajawahi kumeza??Auni ukorofi tu.
Je tunatambua madharq ya minyoo?
 
Ni program za kitaifa za magonjwa yasiyopewa kipaumbele, zinakuwa na phase ya upimaji na umezeshaji dawa. Kabla ya kumezeshwa dawa shule hupewa taarifa ya kuandaa chakula cha wanafunzi. Ni jambo la wengi hivyo wakujilegeza watajilegeza etc.

Kunatakiwa kuwe na ya elimu kwa jamii kabla ya yote, too bad bajeti zinakuwa tight.
 
sawa mkuu, ila sasa vipi kuhusu watoto kula mbona hawazingatii hilo. Kuwapa dawa pasipo kuwalisha kweli?
mimi huku nilipo ,hizo dawa walipewa juma moja lilipita , jambo moja muhimu watoto waliambiwa wabebe chakula na wale ambao hawakubeba walirudishwa nyumbani wakabebe chakula kabla ya kupewa dawa.
 
Nimesikitishwa sana kuona leo watoto wa shule ya msingi "serikali" wakirudi kutoka shuleni wakiwa wamedhoofika sana, miili ikiwa dhaifu na macho mekundu kabisa. Nilipowauliza, walisema wamepewa dawa shuleni na kumeza bila kula. Dawa hizo wamesema ni za kichocho na minyoo, na wamepewa pasipo wazazi kuarifiwa wala kuulizwa ridhaa yao. Walimu nao wameeleza kuwa walipewa taarifa ghafla kwa njia ya simu kwamba waandae watoto kumeza dawa hizo.

Najiuliza, shuleni wana lengo la kuua watoto au kuna shida gani? Je, shule za msingi za serikali zimegeuzwa kuwa sehemu za majaribio ya dawa kwa watoto? Kila mzazi ana utaratibu wake wa kutibu watoto wake. Kwa nini watoto wanalazimishwa kumeza dawa bila taarifa kwa mzazi?

Mnawapa dawa za kichocho na minyoo, lakini mnajuaje kama tayari wazazi wao wamewapa dawa nyumbani?

Lengo la kupeleka mtoto shuleni ni kujifunza na kusoma, si kumeza dawa. Wanapata wapi ujasiri wa kuwamezesha watoto dawa kinyemela pasi na ridhaa ya wazazi? Serikali yangu inasikitisha sana kwa matendo haya.
Taarifa nilipewa vizuri tu.
 
Back
Top Bottom