Wizara ya Elimu acheni kuwa madalali wa Scholarship za Ubalozi

Wizara ya Elimu acheni kuwa madalali wa Scholarship za Ubalozi

Genesis 9:25-27
3:17), (2) that Africans are cursed because they are portrayed as the descendants of Ham 's son, Canaan, who was cursed by his grandparent, Noah (Gen. 9:25-27),
 
Jana nilipata nafasi ya kukutana na Kiongozi mmoja wa Ubalozi wa New Zealand nchini Tanzania, tulipata wasaha wa kula chakula cha jioni yeye pamoja na familia yake. Tulikuwa kwenye hoteli moja maarufu sana haa Dar es Salaam, na baada ya kupata chakula tulizungumza mambo mengi na kupiga stori mbili tatu, na tukiwa kwenye stori nikapata mshawasha kuwa nimuulize kuhusu suala la scholarships haswa kwa wanafunzi wanaotoka Afrika hususani Tanzania.

View attachment 3058653

Nilimuuliza mengi kuhusu hili ila malengo yangu yalikuwa ni kwenye kufahamu haswa je mchakato wa kupata wanafunzi unakuwa ni mchakato wa namna gani? Lakini pia ushirikiano wao kama ubalozi na nchi husika unakuwaje linapokuja suala la ufadhili wa masomo (scholarship). Yule mzee alibaki kushangaa sana kuwa sifahamu namna mifumo ya Afrika ilivyokaa kihasarahasara tu.

Wanapokuwa na wazo la kutaka kuchukua wanafunzi waende nchi yao huwa wanalazimishwa maombi yapitie Wizara ya Elimu na sio njia nyingine, Wizara ya Elimu ndo inabeba dhamana ya kutafuta watu wenye vigezo ambavyo Ubalozi husika inakuwa inahitaji. Lakini ajabu ni kuwa Tangazo la scholarship la Ubalozi linabadilishwa mwanzo mwisho na kutengenezwa tangazo jingine kabsa ambalo linakuwa na upungufu wa taarifa au taarifa zisizo sahihi.

View attachment 3058654

Halmashauri huwa zina utaratibu wa kuweka matangazo kwenye mbao za matangazo ambazo mara kadhaa zinakuwa nje ya ofisini husika, lakini ukisoma matangazo ya scholarship mara kadhaa taarifa na maelekezo yake sio sahihi kwani zinaweka vigezo vingine visivyotakikana kwa ubalozi. Mfano, huweka kigezo cha muombaji awe mwajiriwa wa serikali ilihali tangazo halisi la ubalozi linadai waombaji wawe watanzania, unakutana na kigezo cha Mwaka wa kumaliza chuo au shule ya Sekondari.

Hizo pesa za kuwasomesha wanafunzi zinzotolewa na serikali husika za huko Ughaibuni sio pesa zenu, kwanini mnaweka ngumu hivyo watu kupata ambao mnataka nyie, sio sahihi. Pia alizunguzia suala la kujuana na kubebana sana. Binafsi nashangaa sana kuona nafasi ya kwenda kusoma nje kwa watanzania wanaoweka vikwazi ni watanzania, sijui tuna roho gani?

Kuna kiongozi mmoja mwaka fulani aliwahi kusema “Mnakwenda kusoma kwenye nchi za Ughaibuni ili iweje, Wakati tuna vyuo vingi bora hapa Tanzania? Kwanini uende Ughaibuni? Je ukipata matatizo? Na ajabu ni kuwa kiongozi huyu amesoma Shahada yake UDSM na viwango vingine vya elimu amesomea Japani pamoja na Uingereza. Ni wivu gani wa kijinga huu kiasi kwamba unaweka ngumu kwa Mtanzania mwenzako kwenda kuosha hata macho?

View attachment 3058655

Sikatai kuwa Tanzania kuna vyuo bora ila hivyo vyuo bora vipo vingapi? UDSM, Muhimbili, Sokoine, UDOM, Mzumbe na SAUT, NELSON MANDELA vilivyobaki sidhani kama vinaingia kwenye orodha ya kushindana na vyuo vikubwa vya nje. Lakini wapo wanaotamani kusoma nje ya nchi na kupata nafasi za kuzuru maeneo kadha duniani.

Kwa hakika nimeumia sana kuona watu walio na roho za ajabu sana kwenye maendeleo ya watanzania wenzao. Baadhi ya balozi wameanza kukataa kutumia mfumo ambao Wizara wameuweka kwani ni mfumo kandamizi sana na usiotoa nafasi kwa watu. Ni kawaida kukutana na majina ya walimu wa vyuo wakipelekwa kwenye usahili na kupewa endorsement za kila aina. Tanzania yangu tunarudishana nyuma mwenyewe.

Rai yangu:
1. Wapatie nafasi balozi wenyewe wafanye usahili na kuwafadhili watu kulingana na utaratibu wao, nyie kama Wizara ya Elimu mbakie kama washauri tu kwa wale ambao wamepata nafasi ya kwenda kusoma. Msiwe madalali wa kuonesha yupi ni bora na yupi sio bora kwa viongozi husika ndani ya balozi zilizopo ndani ya Tanzania.

2. Walimu na wakufunzi sio lazima wawe miongoni mwa watu watakaopewa ufadhili, kwa sababu moja, kila chuo kina mahusiano mazuri na vyuo vingine vya kimataifa duniani kote wanaweza kubadilishana watalaamu hivyo sio lazma wakabanane kuchukua nafasi za vijana ambao hutamani kwenda kusoma elimu nje ya nchi.

3. Waajiriwa ambao ni wazawa (watanzania) acheni chuki wajameni, kumkazia mtanzania mwenzako asipate nafasi sio faida kwako bali ni uchoyo wa kipuuzi sana. Kuna dada yupo Ubalozi wa Uswisi, aisee mbinguni sidhani kama utaingia. Dada ana roho mbaya utadhani anaishi Uswisi. Sio kitu kizuri kabsa.
SIO KWA UBAYA! SIO KWA UBAYA!
Nimeshtushwa sana khaaa
 
Jana nilipata nafasi ya kukutana na Kiongozi mmoja wa Ubalozi wa New Zealand nchini Tanzania, tulipata wasaha wa kula chakula cha jioni yeye pamoja na familia yake. Tulikuwa kwenye hoteli moja maarufu sana haa Dar es Salaam, na baada ya kupata chakula tulizungumza mambo mengi na kupiga stori mbili tatu, na tukiwa kwenye stori nikapata mshawasha kuwa nimuulize kuhusu suala la scholarships haswa kwa wanafunzi wanaotoka Afrika hususani Tanzania.

View attachment 3058653

Nilimuuliza mengi kuhusu hili ila malengo yangu yalikuwa ni kwenye kufahamu haswa je mchakato wa kupata wanafunzi unakuwa ni mchakato wa namna gani? Lakini pia ushirikiano wao kama ubalozi na nchi husika unakuwaje linapokuja suala la ufadhili wa masomo (scholarship). Yule mzee alibaki kushangaa sana kuwa sifahamu namna mifumo ya Afrika ilivyokaa kihasarahasara tu.

Wanapokuwa na wazo la kutaka kuchukua wanafunzi waende nchi yao huwa wanalazimishwa maombi yapitie Wizara ya Elimu na sio njia nyingine, Wizara ya Elimu ndo inabeba dhamana ya kutafuta watu wenye vigezo ambavyo Ubalozi husika inakuwa inahitaji. Lakini ajabu ni kuwa Tangazo la scholarship la Ubalozi linabadilishwa mwanzo mwisho na kutengenezwa tangazo jingine kabsa ambalo linakuwa na upungufu wa taarifa au taarifa zisizo sahihi.

View attachment 3058654

Halmashauri huwa zina utaratibu wa kuweka matangazo kwenye mbao za matangazo ambazo mara kadhaa zinakuwa nje ya ofisini husika, lakini ukisoma matangazo ya scholarship mara kadhaa taarifa na maelekezo yake sio sahihi kwani zinaweka vigezo vingine visivyotakikana kwa ubalozi. Mfano, huweka kigezo cha muombaji awe mwajiriwa wa serikali ilihali tangazo halisi la ubalozi linadai waombaji wawe watanzania, unakutana na kigezo cha Mwaka wa kumaliza chuo au shule ya Sekondari.

Hizo pesa za kuwasomesha wanafunzi zinzotolewa na serikali husika za huko Ughaibuni sio pesa zenu, kwanini mnaweka ngumu hivyo watu kupata ambao mnataka nyie, sio sahihi. Pia alizunguzia suala la kujuana na kubebana sana. Binafsi nashangaa sana kuona nafasi ya kwenda kusoma nje kwa watanzania wanaoweka vikwazi ni watanzania, sijui tuna roho gani?

Kuna kiongozi mmoja mwaka fulani aliwahi kusema “Mnakwenda kusoma kwenye nchi za Ughaibuni ili iweje, Wakati tuna vyuo vingi bora hapa Tanzania? Kwanini uende Ughaibuni? Je ukipata matatizo? Na ajabu ni kuwa kiongozi huyu amesoma Shahada yake UDSM na viwango vingine vya elimu amesomea Japani pamoja na Uingereza. Ni wivu gani wa kijinga huu kiasi kwamba unaweka ngumu kwa Mtanzania mwenzako kwenda kuosha hata macho?

View attachment 3058655

Sikatai kuwa Tanzania kuna vyuo bora ila hivyo vyuo bora vipo vingapi? UDSM, Muhimbili, Sokoine, UDOM, Mzumbe na SAUT, NELSON MANDELA vilivyobaki sidhani kama vinaingia kwenye orodha ya kushindana na vyuo vikubwa vya nje. Lakini wapo wanaotamani kusoma nje ya nchi na kupata nafasi za kuzuru maeneo kadha duniani.

Kwa hakika nimeumia sana kuona watu walio na roho za ajabu sana kwenye maendeleo ya watanzania wenzao. Baadhi ya balozi wameanza kukataa kutumia mfumo ambao Wizara wameuweka kwani ni mfumo kandamizi sana na usiotoa nafasi kwa watu. Ni kawaida kukutana na majina ya walimu wa vyuo wakipelekwa kwenye usahili na kupewa endorsement za kila aina. Tanzania yangu tunarudishana nyuma mwenyewe.

Rai yangu:
1. Wapatie nafasi balozi wenyewe wafanye usahili na kuwafadhili watu kulingana na utaratibu wao, nyie kama Wizara ya Elimu mbakie kama washauri tu kwa wale ambao wamepata nafasi ya kwenda kusoma. Msiwe madalali wa kuonesha yupi ni bora na yupi sio bora kwa viongozi husika ndani ya balozi zilizopo ndani ya Tanzania.

2. Walimu na wakufunzi sio lazima wawe miongoni mwa watu watakaopewa ufadhili, kwa sababu moja, kila chuo kina mahusiano mazuri na vyuo vingine vya kimataifa duniani kote wanaweza kubadilishana watalaamu hivyo sio lazma wakabanane kuchukua nafasi za vijana ambao hutamani kwenda kusoma elimu nje ya nchi.

3. Waajiriwa ambao ni wazawa (watanzania) acheni chuki wajameni, kumkazia mtanzania mwenzako asipate nafasi sio faida kwako bali ni uchoyo wa kipuuzi sana. Kuna dada yupo Ubalozi wa Uswisi, aisee mbinguni sidhani kama utaingia. Dada ana roho mbaya utadhani anaishi Uswisi. Sio kitu kizuri kabsa.
SIO KWA UBAYA! SIO KWA UBAYA!
Nchi ngumu sana hii,
Kuna sista mmoja kitaa alinipa story yake jinsi alivyopata nafasi ya Masomo uingereza kimagumashi, kwa sasa ni meneja mkubwa tu makampuni ya simu.
Alinipa ramani niende wzarani ili nijiongeze, nlipofika nlipata somo kubwa sana tangia hapo nikajua watoto wa mafukala tuna njia ngumu sana kufikia mafanikio...
 
Ubinafsi asili yetu labda kama we ni mgeni lengo ni kucontrol watu,hata nguvu kazi tele zinatakiwa nje ya nchi lakini serikali inaweka ngumu watu kwenda kufanya kazi nchi wabakie nchini
Kwanza kitendo tu cha wao kuweka mlolongo mrefu kwenye kupata pasi ya kusafiria kunaonesha ni jinsi gani hii nchi viongozi wake walivyokuwa wabinafsi to the core na wanafurahia watu kukosa exposure, wakati huo wenyewe watoto wao hadi wenye umri wa miaka 2 tayari wamewakatia passport
 
Ni kama hizi scholarship zinazotelewa na TAEC kwa jina la Samia scholarship extended program, hadi nimeapply chuo huko UK na kwa bahati nzuri nikapata ndani ya wakati. Kuja kufungua link sasa ni apply link haifunguki na website Yao mzima haifunguki. Nikachukua iniative ya kuwasialana na wahusika wao, sababu Yao ni kwamba fibre Yao ya Arusha umepata hitilafu (kwa zaidi ya siku 10 sasa) na deadline ni Tarehe 16 mwezi huu. Kuna namna nahisi wanacheza mchezo ila I still believe things will workout in my favour.
 
Kama kuna mtu ana mdogo wake yupo sekondari basi wasiliana na Ofisi za Iqra Fm Mwanza kuna nafasi ya Scholarship. Nimepata kuambiwa kuwa fomu ni 10,000/= tu. Ni kwa ajili ya wanafunzi wa sekondari.
 
Nchi ngumu sana hii,
Kuna sista mmoja kitaa alinipa story yake jinsi alivyopata nafasi ya Masomo uingereza kimagumashi, kwa sasa ni meneja mkubwa tu makampuni ya simu.
Alinipa ramani niende wzarani ili nijiongeze, nlipofika nlipata somo kubwa sana tangia hapo nikajua watoto wa mafukala tuna njia ngumu sana kufikia mafanikio...
Mchakato tu wa Mandela Washington Fellowship ni kipengele kikubwa ajabu sana
 
Kwanza kitendo tu cha wao kuweka mlolongo mrefu kwenye kupata pasi ya kusafiria kunaonesha ni jinsi gani hii nchi viongozi wake walivyokuwa wabinafsi to the core na wanafurahia watu kukosa exposure, wakati huo wenyewe watoto wao hadi wenye umri wa miaka 2 tayari wamewakatia passport
Ukifanya process za kupata passport wakikuuliza mbona una haraka usiwaambie kuwa unataka kwenda kusoma na upo kwenye deadline! Hapo ndo umefungua njia ya rushwa na kuzungushwa kama mpira wa kona
 
Ni kama hizi scholarship zinazotelewa na TAEC kwa jina la Samia scholarship extended program, hadi nimeapply chuo huko UK na kwa bahati nzuri nikapata ndani ya wakati. Kuja kufungua link sasa ni apply link haifunguki na website Yao mzima haifunguki. Nikachukua iniative ya kuwasialana na wahusika wao, sababu Yao ni kwamba fibre Yao ya Arusha umepata hitilafu (kwa zaidi ya siku 10 sasa) na deadline ni Tarehe 16 mwezi huu. Kuna namna nahisi wanacheza mchezo ila I still believe things will workout in my favour.
Wanafanya makusudi! Ila Mungu akutangulie upate haja ya moyo wako Mkuu
 
Jana nilipata nafasi ya kukutana na Kiongozi mmoja wa Ubalozi wa New Zealand nchini Tanzania, tulipata wasaha wa kula chakula cha jioni yeye pamoja na familia yake. Tulikuwa kwenye hoteli moja maarufu sana haa Dar es Salaam, na baada ya kupata chakula tulizungumza mambo mengi na kupiga stori mbili tatu, na tukiwa kwenye stori nikapata mshawasha kuwa nimuulize kuhusu suala la scholarships haswa kwa wanafunzi wanaotoka Afrika hususani Tanzania.

View attachment 3058653

Nilimuuliza mengi kuhusu hili ila malengo yangu yalikuwa ni kwenye kufahamu haswa je mchakato wa kupata wanafunzi unakuwa ni mchakato wa namna gani? Lakini pia ushirikiano wao kama ubalozi na nchi husika unakuwaje linapokuja suala la ufadhili wa masomo (scholarship). Yule mzee alibaki kushangaa sana kuwa sifahamu namna mifumo ya Afrika ilivyokaa kihasarahasara tu.

Wanapokuwa na wazo la kutaka kuchukua wanafunzi waende nchi yao huwa wanalazimishwa maombi yapitie Wizara ya Elimu na sio njia nyingine, Wizara ya Elimu ndo inabeba dhamana ya kutafuta watu wenye vigezo ambavyo Ubalozi husika inakuwa inahitaji. Lakini ajabu ni kuwa Tangazo la scholarship la Ubalozi linabadilishwa mwanzo mwisho na kutengenezwa tangazo jingine kabsa ambalo linakuwa na upungufu wa taarifa au taarifa zisizo sahihi.

View attachment 3058654

Halmashauri huwa zina utaratibu wa kuweka matangazo kwenye mbao za matangazo ambazo mara kadhaa zinakuwa nje ya ofisini husika, lakini ukisoma matangazo ya scholarship mara kadhaa taarifa na maelekezo yake sio sahihi kwani zinaweka vigezo vingine visivyotakikana kwa ubalozi. Mfano, huweka kigezo cha muombaji awe mwajiriwa wa serikali ilihali tangazo halisi la ubalozi linadai waombaji wawe watanzania, unakutana na kigezo cha Mwaka wa kumaliza chuo au shule ya Sekondari.

Hizo pesa za kuwasomesha wanafunzi zinzotolewa na serikali husika za huko Ughaibuni sio pesa zenu, kwanini mnaweka ngumu hivyo watu kupata ambao mnataka nyie, sio sahihi. Pia alizunguzia suala la kujuana na kubebana sana. Binafsi nashangaa sana kuona nafasi ya kwenda kusoma nje kwa watanzania wanaoweka vikwazi ni watanzania, sijui tuna roho gani?

Kuna kiongozi mmoja mwaka fulani aliwahi kusema “Mnakwenda kusoma kwenye nchi za Ughaibuni ili iweje, Wakati tuna vyuo vingi bora hapa Tanzania? Kwanini uende Ughaibuni? Je ukipata matatizo? Na ajabu ni kuwa kiongozi huyu amesoma Shahada yake UDSM na viwango vingine vya elimu amesomea Japani pamoja na Uingereza. Ni wivu gani wa kijinga huu kiasi kwamba unaweka ngumu kwa Mtanzania mwenzako kwenda kuosha hata macho?

View attachment 3058655

Sikatai kuwa Tanzania kuna vyuo bora ila hivyo vyuo bora vipo vingapi? UDSM, Muhimbili, Sokoine, UDOM, Mzumbe na SAUT, NELSON MANDELA vilivyobaki sidhani kama vinaingia kwenye orodha ya kushindana na vyuo vikubwa vya nje. Lakini wapo wanaotamani kusoma nje ya nchi na kupata nafasi za kuzuru maeneo kadha duniani.

Kwa hakika nimeumia sana kuona watu walio na roho za ajabu sana kwenye maendeleo ya watanzania wenzao. Baadhi ya balozi wameanza kukataa kutumia mfumo ambao Wizara wameuweka kwani ni mfumo kandamizi sana na usiotoa nafasi kwa watu. Ni kawaida kukutana na majina ya walimu wa vyuo wakipelekwa kwenye usahili na kupewa endorsement za kila aina. Tanzania yangu tunarudishana nyuma mwenyewe.

Rai yangu:
1. Wapatie nafasi balozi wenyewe wafanye usahili na kuwafadhili watu kulingana na utaratibu wao, nyie kama Wizara ya Elimu mbakie kama washauri tu kwa wale ambao wamepata nafasi ya kwenda kusoma. Msiwe madalali wa kuonesha yupi ni bora na yupi sio bora kwa viongozi husika ndani ya balozi zilizopo ndani ya Tanzania.

2. Walimu na wakufunzi sio lazima wawe miongoni mwa watu watakaopewa ufadhili, kwa sababu moja, kila chuo kina mahusiano mazuri na vyuo vingine vya kimataifa duniani kote wanaweza kubadilishana watalaamu hivyo sio lazma wakabanane kuchukua nafasi za vijana ambao hutamani kwenda kusoma elimu nje ya nchi.

3. Waajiriwa ambao ni wazawa (watanzania) acheni chuki wajameni, kumkazia mtanzania mwenzako asipate nafasi sio faida kwako bali ni uchoyo wa kipuuzi sana. Kuna dada yupo Ubalozi wa Uswisi, aisee mbinguni sidhani kama utaingia. Dada ana roho mbaya utadhani anaishi Uswisi. Sio kitu kizuri kabsa.
SIO KWA UBAYA! SIO KWA UBAYA!
Ni kwa Ubaya Ubwela
 
Vigezo vilikuwa nini mkuu?
Mwanzoni wakati Hungary wanadahili wenyewe moja kwa moja mambo yalikuwa mepesi tu na washkaji nawajua wanne walisepa hadi leo wapo huko changamoto ilianza baada ya wazara kuingilia kati scholarship zipitie kwao kwanza wao ndo wachuje hatua za awali halafu baadae ndo wapeleke majina huko Hungary hapo ndo kizaazaa kilipoanzia ni mwendo wa kuweka watoto wao tuu na ndugu kujuana kwingiii
 
Ninaposema kuwa hawa jamaa ni wahuni sidhani kama mnanielewa?! Wameweka tangazo tarehe 2 Agosti na deadline ni tarehe 8 Agosti aisee ni majanga.
Naombeni maadmin waweke hii:
Sambazeni kwa wadogo zenu wapate nafasi.
Site gani au njia gani rahisi ambayo mtu anaweza kuona fursa za Scholarship na nyinginezo nje ya nchi ? maana mimi namalizia Bachelor Degree hapa Tz na natamani sana fursa hizo.
 
Back
Top Bottom