Wizara ya elimu yakana kuwapima mimba watoto wa kike kwa lazima, yasema wataendelea na masomo baada ya kujifungua

Wizara ya elimu yakana kuwapima mimba watoto wa kike kwa lazima, yasema wataendelea na masomo baada ya kujifungua

Yule mtu anaitwa sijui Pascal Mayalla yuko wapi hapa atufafanulie kuhusu "Sovereignty" yetu kama bado ipo.

Hichi kibano tunataka kiendelezwe hadi kwenye uchaguzi ili watu wakome kufanya uhuni kwenye maswala nyeti.
 
Madhara ya hii njaa tutayaona miaka michache baade.
Siasa zimechangia serikali kuingia huu mkenge.

Bado la tume huru ya uchaguzi, wazungu shikilieni hapo mpaka wazee wa siasa chafu wanyooke. Inatakiwa wapinzani wasusie uchaguzi mpaka ipatikane tume huru ya uchaguzi ipatikane. Na isipopatikana tuwekewe vikwazo vya kiuchumi.
 
Angalau wewe umesema ukweli.

Ukipata mimba serekali inakufukuza kwenye mfumo wake wa elimu.

Ina maana ni mzazi kwenda private au Veta, ambayo huwezi kusema ni government opportunity.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni Government opportunity kwani private na veta vyote vipo chini ya mfumo wa elimu ya serikali. Hata mitihani inaandaliwa na kupitishwa na serikali. Chakuzingatia ni kuwa, maadili yetu hayaruhusu Mzazi kukaa darasa moja na watoto.
 
Anaposema ataendelea na masomo baada ya kujifungua na kulea mtoto sio kwenye secondary! Bali vyuo au VETA au QT!
 
Kama ni kweli shukrani zimfikie mhe. Zitto Kabwe hata kama alikwiaha uawa kwa maamuzi ya bunge.
Hizo siasa tu kijana! Ukipata mimba mpaka unazaa ni mwaka mmoja (yaani miezi 10). Ongeza miaka 2 ya kunyonyesha miaka 3 imeishapotea. Sasa atarudi asome secondary hipi? Hapa ni kwenda veta tu, wala sio secondary zetu! Weeee kalaghabao!
 
Tangu enzi za nyerere wanafunzi hupimwa mimba kwa kushitukiza,Tena enzi hizo wanapima kwa kutomasa,kabla ya hivi vipimo sikuhiz ni unapima mkojo tu,
Iwapo mwanafunzi akipatikana na mimba,ilikua no discussion,,unafukuzwa shule,
Nini kimebadirika?.
Wanafunzi ruksa kufanya mapenzi?
 
Katika kile kinachoonekana kama kupiga hatua kwenye uelekeo sahihi, wizara ya elimu kupitia katibu mkuu wake Dr. Leonard Akwilapo imekanusha madai ya kuwa watoto wa kike waliopo mashuleni watapimwa mimba kwa lazima.

Taarifa hiyo iliyotolewa tarehe 06-03-2020 imefafanua kuwa kauli ya kuwapima mimba wanafunzi haikutoka wizara ya elimu, na pia hakuna sera wala sheria yoyote inayowaelekeza wakuu wa shule au mamlaka nyingine yeyote kuwapima mimba kwa lazima wanafunzi wa kike.

Pia kwenye taarifa hiyo, wizara imesema mwanafunzi atakaye bainika kuwa na ujauzito, atapewa muda wa kutosha kumttunza mtoto wake mchanga na baadaye katika muda sahihi ataruhusiwa kuendelea na masomo.
View attachment 1381582
haya mzee wa pingamizi awaambie jamaa watupe mkopo basi walichokitaka tayari
 
Katika kile kinachoonekana kama kupiga hatua kwenye uelekeo sahihi, wizara ya elimu kupitia katibu mkuu wake Dr. Leonard Akwilapo imekanusha madai ya kuwa watoto wa kike waliopo mashuleni watapimwa mimba kwa lazima.

Taarifa hiyo iliyotolewa tarehe 06-03-2020 imefafanua kuwa kauli ya kuwapima mimba wanafunzi haikutoka wizara ya elimu, na pia hakuna sera wala sheria yoyote inayowaelekeza wakuu wa shule au mamlaka nyingine yeyote kuwapima mimba kwa lazima wanafunzi wa kike.

Pia kwenye taarifa hiyo, wizara imesema mwanafunzi atakaye bainika kuwa na ujauzito, atapewa muda wa kutosha kumttunza mtoto wake mchanga na baadaye katika muda sahihi ataruhusiwa kuendelea na masomo.
View attachment 1381582
Kiingereza bado nitatizo kwa baadhi yawatu hum jf. Tatizo hapa ni neno opportunity siyo shall! Wangetumia neno shall! Hapo mgesema serikari imesalim amri.
RUDINI SHULE MKASOME WOTE MLIOSHANGILIA ETI SERIKARI IMESALIM AMRI BADO FURUSA ZIPO.
 
Hamuelewi nyie, hawajawahi kukatazwa masomo shida wataendea na masomo wapi ndiyo big case.
Kiingereza kinalitesa sana taifa hili. Mtu hajaelewa maana halisi anaanza kumshangilia Zito na kuiponda serikali. Technically hakuna chochote kilichobadirika, hayo aliyoandika katibu ndo sela iliyopo inasema hivo. Watanzania wengi wajinga ndo wanajiona wanajua zaidi. Tunaliangamiza taifa
 
Adjustments.JPG
 
Kiingereza bado nitatizo kwa baadhi yawatu hum jf. Tatizo hapa ni neno opportunity siyo shall! Wangetumia neno shall! Hapo mgesema serikari imesalim amri.
RUDINI SHULE MKASOME WOTE MLIOSHANGILIA ETI SERIKARI IMESALIM AMRI BADO FURUSA ZIPO.
Acha ujuaji, hiyo ni taarifa tu. Ukitaka hizo 'shall' nenda kasome sera ya elimu.
 
Hii tunaita kufanyia siasa maisha ya watu. Future ya msichana maskini wa kijijini inaenda kutokomezwa. Future engineers, doctors, teachers, business women wanalazimishwa kuishia kuwa mama ntilie anayeuza nusu ndoo ya wali ili kutunza familia.

Nchi inaangamizwa na wanasiasa
 
Back
Top Bottom