Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 15,692
- 23,038
Wizara mbalimbali zimekuwa zikikabiliwa na matatizo kama ubadhilifu wa fedha, wizi wa kimtandao na wa kughushi na hata matishio ya kusambazwa kwa taharuki kutoka kwenye mitandao ya kijamii.
Kumekuwa na taarifa za vitendo vya udanganyifu katika Wizara ya Ardhi, nyumba na maendeleo mijini, wizi wa madawa katika mahospitali yalo chini ya Wizara ya Afya na utoaji wa taarifa za uzushi katika mitandao ya kijamii na wizi kwenye hamlashauri za manispaa au wilaya kadhaa hapa nchini.
Lakini ukiangalia sana utaona kwamba Mawaziri husika hutoa matamko kwamba watu walohusika na majanga hayo wanapaswa kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Pia taasisi ya kupambana na rushwa TAKUKURU imekuwa wima katika kipindi cha kuanzia mwaka 2016 hadi sasa ambapo mabilioni ya fedha za walipa kodi yameibwa au kupotea katika mazingira ya ubadhilifu, wizi wa kughushi na matumizi mabaya.
Kwa mfano wizara ya ardhi, nyumba na maendeleo mijini imekuwa ikikabiliwa na matatizo ya watumishi wasio waaminifu ambao wanajishughulisha na uuzaji wa viwanja katika maeneo mbalimbali nchini. Pia baadhi ya watumishi wa wizara hiyo wamekuwa wakifanya udanganyifu katika mifumo ya kanzidata ya wizara hiyo kwenye kuingiza taarifa zisizo za kweli.
Wizara ya Afya nayo imekuwa katika wakati mgumu ambapo taasisi yake ya ugavi dawa ya MSD imekuwa ikiingiliwa katika mfumo wake wa ambapo wizi wa madawa na vifaa vya kitabibu umekithiri ambapo juzijuzi madawa yenye thamani ya shilingi bilioni 1.2.
Katika taasisi ya MOI watumishi wapatao 23 ambao ni wafamasia walitumia mfumo wa kutunza taarifa kumbukumbu za madawa wa MEDPRO kuingiza taarifa za uongo kwa kuongeza idadi ya dawa kwenye cheti cha mgonjwa na pia kuongeza kiasi kikubwa cha gharama za dawa katika fomu ya daktari.
Halikadhalika wizi na matumizi mabaya ya fedha umekithiri katika wizaya ya TAMISEMI ambapo halmashauri kadhaa zimekumbwa na wizi na matumizi mabaya ya fedha. Halmashauri ya Biharamuro ilikumbwa na wizi wa shilingi milioni 400 ulofanywa na watumishi kumi na mmoja. Pia wilayani Makete watumishi tisa walifikishwa mahakamani kwa kuiba fedha za kodi milioni 39.
Wilayani Mbozi mkoani Songwe watumishi kadhaa walifikishwa mahakamani kwa wizi wa fedha za kodi kupoitia mfumo wa kielektroniki wa POS kiasi cha shilingi milioni 11.
Ntazungumzia kwa upana wizara ya teknolojia ambayo inaisimamia TCRA katika mikala ingine maalum kwa ajili hiyo.
Sasa basi tatizo ni nini kwa haya yote?
Unapata jibu kwamba wizara husika hazinayo tabia ya kufanya tathmini (Risk Assessment) katika wizara zao khasa katika maeneo husika.
Au inawezekana pia kwamba tathmini imefanywa lakini kuna mahali pana kasoro kwa kuzingatia kuwa tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani inapenda kufuatilia kila maagizo yake ambayo hutolewa.
Ni dhahiri kwamba TAKUKURU inazo taarifa zote tangu ianze kufanya kazi zake kikamilifu chini ya serikali ya awamu ya tano. Halikadhalika wizara ya ardhi nyumba, makazi na maendeleo mijini nayo imefanaya tathimini na pia hata wizara ya TAMISEMI nayo imefanya tathmini kabkla ya kuanza zoezi la kuorodhesha majengo na nyumba zote nchi nzima.
Tuangalie tathmini au Risk Assessment ni nini.
Kabla hujaanza kufikiria kufanya tathmini ni lazima uwe na mambo makuu matatu ya kuzingatia.
Kwanza uwe na hatari au kw akiingereza "risk" ambayo ni hali inaweza kusababisha hasara au hatari. Pili kuwepo kitu kinachoweza kusababisha hatari kwa kiingereza "Hazard" na mwisho kuwepo udhaifu au kwa kiingereza "Vulnerability" ambayo huitwa pia "weakness".
Nikitoa mfano ni kwamba mtu anaweza kuwa mdhaifu au ana udhaifu katika kukataa ushiwishi wa pombe na akanywa kisha kwa kutojali udhaifu wake akaamua kuendesha gari ambalo ni hatari (risk) kwa maana ya kitu kitakachosababisha ajali (hazard) na mwishi wake huwa ni majanga au kukamatwa na polisi ukiendesha gari ukiwa umelewa.
Lakini ukiomba mkopo benki CRDB wao watatumia tathmini iliyomo katika mfumo wa computer ili iwaeleze tathmini ya uloyaeleza katika fomu ya maombi ya mkopo. Hivyo kama una historia ya kutolipa mkopo kwa wakti, huna kazi ya kueleweka au permanent job wewe ni hatari kwa benki kwa maana ya (risk) na sio (hazard) hivyo neno neno risk limejigawa kwa maana ya "hali inayosababisha" na "kitu kinachosababisha" hasara, majanga, matukio mabaya kama ugaidi, kuharibiwa taswira kama nchi na majanga mengine mengi tu.
Halafu kuna mali au Assets yaani taasisi, shirika, kampuni, watu, mashine na vifaa mbalimbali na mali zingine zinazohamisha na zisizohamishika.
Ili uweze kufanya tathmini ni lazima uzingatie misingi mikuu mitano ambayo bila hiyo huwezi kupata majibu halisi ya tathmini yako.
Kugundua na kuainisha au "identification and analysing" ni lazima utambue matukio yaliyomo katika sehemu tatu nilozieleza hapo juu yaani hatari, udhaifu na udhoofu ambayo yanaweza kusababisha adhari kwa mali au asset uliyo nayo.
Pili, ni lazima uchambue udhaifu na kuupanga kulingana na uzito wake. hapa ndipo utaona ni yapi yanaweza kuleta athari au majanga zaidi na kwa kiasi gani.
Tatu, kufanyia tathmini madhaifu yote uloyagundua na kutengeneza taratibu za kudhibiti au "control measures". hapa ndipo unapoweza kulinda mali zako au assets zote kwa kuiondoa au kuidhibiti hatari.
Nne, kuweka kumbukumbu ya yale yote uloyagundua na kuanza kuyashughulikia. Hii ya kuweka kumbukumbu huitwa "risk register". Risk register hujazwa matukio na matishio yote na huwa ni kielelezo kizuri kwa mafunzo au hadidu za rejea.
Tano, ni kuipitia upya tathmini na kurekebisha au kuongeza zaidi madhaifu mengine na matukio ambayo yanajitokeza upya.
Tathmini ni endelevu na hupaswa kufanywa kila mwaka ili kuweza kutambua matukio mapya yanayoweza kusababisha athari.
Kwa mfano wizara ya afya inaweza kufanya tathmini ya kinachoendelea kuhusiana na vitendo vya wizi katika mahospitali yake nchini.
Inaonyesha dhahiri kwamba wizi na ubadhilifu hufanywa na wafamasia, wakishirikiana na madaktari na watumishi wengine waso waaminifu.
Baada ya kugundua matukio na hali zinazopolekea vitendo hivyo wizara inaweza kuweka udhibiti kwa kuhakikisha inaajiri maofisa watendaji wa hospitali nchi nzima.
Hivyo kila hospitali itakuwa yaongozwa na huu utawala ambao ni "Corporate" na uko juu ukishughulikia utawala, fedha, ugavi, usimamizi wa vyanzo vya mapato na rasilimali watu wakiwemo madaktari.
Kukiwepo ofisi ya mtendaji mkuu kutaleta nidhamu ya kazi na hawa wanaweza kuajiri watalaam wa kufanya tathmini ili kupata picha halisi ya taasisi zao kifedha na kiafya kuhusu hujuma dhidi yake.
Hivyo basi, napenda kutoa ushauri kwa serikali kupitia wizara zake kutambua kufanya tathmini ambazo zitasaidia kudhibiti wizi na ubadhilifu unoendelea kwa sasa.
Azimio la serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha kila Mtanzania anajikomboa kiuchumi na kuona maendeleo ya kweli.
Hizi kesi ya wizi na ubadhilifu hata katika mashine za kielekroniki ni sehemu za hujuma ambazo serikali inapaswa kuzifanyia tathmini.
Richard JF.
Kumekuwa na taarifa za vitendo vya udanganyifu katika Wizara ya Ardhi, nyumba na maendeleo mijini, wizi wa madawa katika mahospitali yalo chini ya Wizara ya Afya na utoaji wa taarifa za uzushi katika mitandao ya kijamii na wizi kwenye hamlashauri za manispaa au wilaya kadhaa hapa nchini.
Lakini ukiangalia sana utaona kwamba Mawaziri husika hutoa matamko kwamba watu walohusika na majanga hayo wanapaswa kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Pia taasisi ya kupambana na rushwa TAKUKURU imekuwa wima katika kipindi cha kuanzia mwaka 2016 hadi sasa ambapo mabilioni ya fedha za walipa kodi yameibwa au kupotea katika mazingira ya ubadhilifu, wizi wa kughushi na matumizi mabaya.
Kwa mfano wizara ya ardhi, nyumba na maendeleo mijini imekuwa ikikabiliwa na matatizo ya watumishi wasio waaminifu ambao wanajishughulisha na uuzaji wa viwanja katika maeneo mbalimbali nchini. Pia baadhi ya watumishi wa wizara hiyo wamekuwa wakifanya udanganyifu katika mifumo ya kanzidata ya wizara hiyo kwenye kuingiza taarifa zisizo za kweli.
Wizara ya Afya nayo imekuwa katika wakati mgumu ambapo taasisi yake ya ugavi dawa ya MSD imekuwa ikiingiliwa katika mfumo wake wa ambapo wizi wa madawa na vifaa vya kitabibu umekithiri ambapo juzijuzi madawa yenye thamani ya shilingi bilioni 1.2.
Katika taasisi ya MOI watumishi wapatao 23 ambao ni wafamasia walitumia mfumo wa kutunza taarifa kumbukumbu za madawa wa MEDPRO kuingiza taarifa za uongo kwa kuongeza idadi ya dawa kwenye cheti cha mgonjwa na pia kuongeza kiasi kikubwa cha gharama za dawa katika fomu ya daktari.
Halikadhalika wizi na matumizi mabaya ya fedha umekithiri katika wizaya ya TAMISEMI ambapo halmashauri kadhaa zimekumbwa na wizi na matumizi mabaya ya fedha. Halmashauri ya Biharamuro ilikumbwa na wizi wa shilingi milioni 400 ulofanywa na watumishi kumi na mmoja. Pia wilayani Makete watumishi tisa walifikishwa mahakamani kwa kuiba fedha za kodi milioni 39.
Wilayani Mbozi mkoani Songwe watumishi kadhaa walifikishwa mahakamani kwa wizi wa fedha za kodi kupoitia mfumo wa kielektroniki wa POS kiasi cha shilingi milioni 11.
Ntazungumzia kwa upana wizara ya teknolojia ambayo inaisimamia TCRA katika mikala ingine maalum kwa ajili hiyo.
Sasa basi tatizo ni nini kwa haya yote?
Unapata jibu kwamba wizara husika hazinayo tabia ya kufanya tathmini (Risk Assessment) katika wizara zao khasa katika maeneo husika.
Au inawezekana pia kwamba tathmini imefanywa lakini kuna mahali pana kasoro kwa kuzingatia kuwa tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani inapenda kufuatilia kila maagizo yake ambayo hutolewa.
Ni dhahiri kwamba TAKUKURU inazo taarifa zote tangu ianze kufanya kazi zake kikamilifu chini ya serikali ya awamu ya tano. Halikadhalika wizara ya ardhi nyumba, makazi na maendeleo mijini nayo imefanaya tathimini na pia hata wizara ya TAMISEMI nayo imefanya tathmini kabkla ya kuanza zoezi la kuorodhesha majengo na nyumba zote nchi nzima.
Tuangalie tathmini au Risk Assessment ni nini.
Kabla hujaanza kufikiria kufanya tathmini ni lazima uwe na mambo makuu matatu ya kuzingatia.
Kwanza uwe na hatari au kw akiingereza "risk" ambayo ni hali inaweza kusababisha hasara au hatari. Pili kuwepo kitu kinachoweza kusababisha hatari kwa kiingereza "Hazard" na mwisho kuwepo udhaifu au kwa kiingereza "Vulnerability" ambayo huitwa pia "weakness".
Nikitoa mfano ni kwamba mtu anaweza kuwa mdhaifu au ana udhaifu katika kukataa ushiwishi wa pombe na akanywa kisha kwa kutojali udhaifu wake akaamua kuendesha gari ambalo ni hatari (risk) kwa maana ya kitu kitakachosababisha ajali (hazard) na mwishi wake huwa ni majanga au kukamatwa na polisi ukiendesha gari ukiwa umelewa.
Lakini ukiomba mkopo benki CRDB wao watatumia tathmini iliyomo katika mfumo wa computer ili iwaeleze tathmini ya uloyaeleza katika fomu ya maombi ya mkopo. Hivyo kama una historia ya kutolipa mkopo kwa wakti, huna kazi ya kueleweka au permanent job wewe ni hatari kwa benki kwa maana ya (risk) na sio (hazard) hivyo neno neno risk limejigawa kwa maana ya "hali inayosababisha" na "kitu kinachosababisha" hasara, majanga, matukio mabaya kama ugaidi, kuharibiwa taswira kama nchi na majanga mengine mengi tu.
Halafu kuna mali au Assets yaani taasisi, shirika, kampuni, watu, mashine na vifaa mbalimbali na mali zingine zinazohamisha na zisizohamishika.
Ili uweze kufanya tathmini ni lazima uzingatie misingi mikuu mitano ambayo bila hiyo huwezi kupata majibu halisi ya tathmini yako.
Kugundua na kuainisha au "identification and analysing" ni lazima utambue matukio yaliyomo katika sehemu tatu nilozieleza hapo juu yaani hatari, udhaifu na udhoofu ambayo yanaweza kusababisha adhari kwa mali au asset uliyo nayo.
Pili, ni lazima uchambue udhaifu na kuupanga kulingana na uzito wake. hapa ndipo utaona ni yapi yanaweza kuleta athari au majanga zaidi na kwa kiasi gani.
Tatu, kufanyia tathmini madhaifu yote uloyagundua na kutengeneza taratibu za kudhibiti au "control measures". hapa ndipo unapoweza kulinda mali zako au assets zote kwa kuiondoa au kuidhibiti hatari.
Nne, kuweka kumbukumbu ya yale yote uloyagundua na kuanza kuyashughulikia. Hii ya kuweka kumbukumbu huitwa "risk register". Risk register hujazwa matukio na matishio yote na huwa ni kielelezo kizuri kwa mafunzo au hadidu za rejea.
Tano, ni kuipitia upya tathmini na kurekebisha au kuongeza zaidi madhaifu mengine na matukio ambayo yanajitokeza upya.
Tathmini ni endelevu na hupaswa kufanywa kila mwaka ili kuweza kutambua matukio mapya yanayoweza kusababisha athari.
Kwa mfano wizara ya afya inaweza kufanya tathmini ya kinachoendelea kuhusiana na vitendo vya wizi katika mahospitali yake nchini.
Inaonyesha dhahiri kwamba wizi na ubadhilifu hufanywa na wafamasia, wakishirikiana na madaktari na watumishi wengine waso waaminifu.
Baada ya kugundua matukio na hali zinazopolekea vitendo hivyo wizara inaweza kuweka udhibiti kwa kuhakikisha inaajiri maofisa watendaji wa hospitali nchi nzima.
Hivyo kila hospitali itakuwa yaongozwa na huu utawala ambao ni "Corporate" na uko juu ukishughulikia utawala, fedha, ugavi, usimamizi wa vyanzo vya mapato na rasilimali watu wakiwemo madaktari.
Kukiwepo ofisi ya mtendaji mkuu kutaleta nidhamu ya kazi na hawa wanaweza kuajiri watalaam wa kufanya tathmini ili kupata picha halisi ya taasisi zao kifedha na kiafya kuhusu hujuma dhidi yake.
Hivyo basi, napenda kutoa ushauri kwa serikali kupitia wizara zake kutambua kufanya tathmini ambazo zitasaidia kudhibiti wizi na ubadhilifu unoendelea kwa sasa.
Azimio la serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha kila Mtanzania anajikomboa kiuchumi na kuona maendeleo ya kweli.
Hizi kesi ya wizi na ubadhilifu hata katika mashine za kielekroniki ni sehemu za hujuma ambazo serikali inapaswa kuzifanyia tathmini.
Richard JF.