Wizi mkubwa unafanywa hivi manunuzi ya magari ya Serikali, pikipiki, ambulance nk, vifaa vya kielectronic vya umma, na manunuzi yote ya Serikali

Wizi mkubwa unafanywa hivi manunuzi ya magari ya Serikali, pikipiki, ambulance nk, vifaa vya kielectronic vya umma, na manunuzi yote ya Serikali

umezungumza ukweli sana, ingawa kumsaidia Mh. rais tungeainisha njia za ku mitigate hizi challenge, ingawa kwa sasa upo mfumo wa Nest ambao nadhani utatatua baadhi ya changamoto ulizozianisha.
Huo mfumo wa nest unafanyaje kazi?
 
Kwanini tunanunua TOYOTA TZ kwa bei kubwa wakati pesa ni yetu ns tunao uwezo wa kununua popote kwa toyota kwa bei nafuu,kenya hununua toyota japan kwa bei nafuu sisu TZ tunanunua jwa dealer kwa bei ya juu maradufu.
 
Nchi hii watu wanasema ukiwa serikalini hakuna hela,ila wangejua,hela zipo na zinapigwa vibaya sana.
Mama ashauriwe awakazie wapigaji,mbona mzee alithubutu?
 
Ni kweli Kabisa.....Magufuli alikuwa anawashughulikia...Watu wakalalamika. Sasa hivi hawashughulikiwi....watu wanalalamika tena. Sasa nyinyi Wa-Tanzania mnataka nini?
yeye mwenyewe alikuwa mwizi mkubwa sana kupitia kampuni za familia na marafiki zake, na zile zingine mjinga yule akaenda kuficha china
 
Huo mfumo wa nest unafanyaje kazi?
of coz utapunguza urasimu, ucheleweshaji na baadhi ya mambo machache ambayo hayahitaji mabadiliko ya sera. lkn kwa vitu vnahitaji mabadiliko ya sera bado mianya yake ya upigaji itakuwa wazi.... hata hivyo ukiukwaji wa sheria bado ni tatizo.. matahalani miradi ya Tanroad ambayo tender zimekuwa awarded mingi nimesikia malalamiko kuwa ni Kampuni za wakubwa ndizo zimepewa kazi which is contrarily na sheria ya manunuzi inayomtaka kampuni ya mtumishi wa umma, rafiki au ndugu ambaye ana influence kutopewa zabuni ili kuepuka conflict of interest... lakini hapo utakuana na kamouni za Kina Makamba, Riz one etc zikikiwa awarded tender bila haya! ndio mambo yanapaswa kuangaliwa, kutokuwa owner wa kampuni kisheria lkn unamiliki kampuni hiyo kwa mlango wa uani ni jambo la kulitazama sana kwa sasa kwenye sheria ya manunuzi!
 
Asilimia 90 ya watumishi wa Serikali ya Tanzania kwa kada zote na ngazi zote za utumishi, viongozi wakuu wakiwemo, wote wanawaza kutajirika kwa njia yoyote ile kwa kuhujumu mali ya umma.
Tabia ya wizi ubadhirifu na ubinafsi huko Serikalini ni itikadi iliyokubuhu kiasi kwamba hata wanaojiita walokole wakiisha kuajiriwa, hubadilika kuwa mafisadi kupita maelezo.
 
of coz utapunguza urasimu, ucheleweshaji na baadhi ya mambo machache ambayo hayahitaji mabadiliko ya sera. lkn kwa vitu vnahitaji mabadiliko ya sera bado mianya yake ya upigaji itakuwa wazi.... hata hivyo ukiukwaji wa sheria bado ni tatizo.. matahalani miradi ya Tanroad ambayo tender zimekuwa awarded mingi nimesikia malalamiko kuwa ni Kampuni za wakubwa ndizo zimepewa kazi which is contrarily na sheria ya manunuzi inayomtaka kampuni ya mtumishi wa umma, rafiki au ndugu ambaye ana influence kutopewa zabuni ili kuepuka conflict of interest... lakini hapo utakuana na kamouni za Kina Makamba, Riz one etc zikikiwa awarded tender bila haya! ndio mambo yanapaswa kuangaliwa, kutokuwa owner wa kampuni kisheria lkn unamiliki kampuni hiyo kwa mlango wa uani ni jambo la kulitazama sana kwa sasa kwenye sheria ya manunuzi!
Hujajibu swali langu mkuu..nimeuliza huo mfumo wa nest unafanyaje kazi?
 
Ni lazima ifike hatua tukubali kuwa hii nchi na nyingi za Africa bado hazijawa tayari kutawaliwa kidemokrasia, hii nchi inataka sheria kandamizi kusha wawepo watu wa kuzisimamia haswa, ndani ya miaka 3 tu hela ya umma itaogopeka vibaya.

Katiba irekebishwe ili kusiwepo na kiongozi yoyote aliye na kinga, mihimili ipewe nguvu halisi ya kujitegemea.

Akigundulika yoyote kufanya ufisadi, kwanza anyang'angwe mali zake ZOTE, kisha kesi za ufisadi zisiwe na dhamana, ziendeshwe harakaharaka na kifungo kiwe miaka 30 au kunyongwa bila huruma.

Ukionyesha mfano kwa chambo kama watatu hivi, hakuna raia watakaokuwa wanakimbilia teuzi tena.

Bila kudhibiti rushwa tusitarajie maendeleo yoyote yale, hela zinapotea nyingi sana huko.
Ukifanya yote haya kwa ufanisi na uaminifu mkubwa utajijengea maadui nje na ndani ya nchi....

Rejea yaliyomkuta JPM au mahojiano ya waziri Tax na BBC hivi karibuni, utaona jinsi nchi za nje zinavyo shabikia Serikali dharimu na fisadi kwa mwavuli wa utawala bora na haki za binadamu.
 
Sijui ni kwanini Serikali kwenye suala la manunuzi ya mali zake huwa haipo makini kila manunuzi ya Serikali yanapofanyika kuna pesa ya wizi inapita huko na kuna njia mbalimbali zinazotumika hapa ili kuiibia Serikali

1. Kuagiza vitu kwa idadi kubwa tofauti na mahitaji halisi ya Serikali sasa hapa kuna mambo, kwanza vinaagizwa vitu vingi na ndani yake inaingizwa order yao binafsi (Mafisadi) kwa hiyo mfano mahitaji ni 200,000 basi vitaombwa 250,000, hivyo elfu hamsini watajua wao watakavyoupeleka mchakato kati ya wanunuzi na watu wa store na record za ledger book ila Serikali itatoa hela ya 250,000 maana yake hapo kuna vitakavyoingizwa kwenye ledger na kuonekana vimetoka au visiingizwe kabisa kwenye ledger book.

2. Kuongeza gharama za manunuzi mara mbili au zaid ya bei halisi kama kitu kinauzwa Tsh.200,000/ basi serikali itauziwa kati ya Tsh.300,000 hadi Tsh. 350,000/- au zaid

3. Kununua vitu ambavyo ni low quality wakati vinavyohitajika na pesa iliyotoka serikalini ni ya vifaa vyenye high quality ( hili lilijitokeza kwenye vishkwambi, mashine za kusajili wapiga kura, mifumo ya kimtandao ya serikali , servers nk ndio maana mifumo mingi ya Derikali haiishi kusumbua kila mara)

4. Kuchanganya bidhaa original na feki zake, hasa zile zinazohitajika kwa wingi mf. Vifaa vya afya , vifaa vya kielectronic ,vifaa vya miradi ,vifaa vya kazi maalumu nk.

Yaani hapa iko hivi mfano vinahitajika vifaa 200,000 ambavyo bei yake ni Tsh.600,000/- kila kimoja ambacho ni original na high quality, kitakachofanyika ni kununua vifaa 100,000 original kabisa ambavyo navyo unaweza kukuta bei iliongezwa , halafu hivyo 100,000 vilivyo baki vinatafutwa feki yake vifananavyo na vinavyoweza kufanya kazi ile ile ila sio kwa ubora lakini kwa bei ya chini labda Tsh 250,000/- na hapa huwa order inatolewa China maana ndio kuna local industries zenye ubingwa wa kutoa copy za vitu kwa bei ndogo ili pesa ya juu watu waibe

5. Kuleta vitu vilivyoagizwa kwa mafungu mafungu yani kama vilihitajika vifaa labda 200,000 vinaletwa kwanza 130,000 halafu wanasikilizia kwanza kama kutakuwa na kelele wakiona kimya ndio imetoka hiyo vilivyobaki haviji tena pamoja na kwamba Serikali inakuwa ilishatoa hela ya vyote 200,000 na baada ya hapo wanacheza na watu wa record kwenye ledger book idadi inajazwa lakini vitu havipo.

Zipo njia nyingi zaidi na sitaki kuamini kwamba serikali haijui
Duh!
 
Ukifanya yote haya kwa ufanisi na uaminifu mkubwa utajijengea maadui nje na ndani ya nchi....

Rejea yaliyomkuta JPM au mahojiano ya waziri Tax na BBC hivi karibuni, utaona jinsi nchi za nje zinavyo shabikia Serikali dharimu na fisadi kwa mwavuli wa utawala bora na haki za binadamu.

Hii nchi inahitaji kuongozwa kwa mkono wa chuma, Watz hawahitaji demokrasia.
 
Sijui ni kwanini Serikali kwenye suala la manunuzi ya mali zake huwa haipo makini kila manunuzi ya Serikali yanapofanyika kuna pesa ya wizi inapita huko na kuna njia mbalimbali zinazotumika hapa ili kuiibia Serikali

1. Kuagiza vitu kwa idadi kubwa tofauti na mahitaji halisi ya Serikali sasa hapa kuna mambo, kwanza vinaagizwa vitu vingi na ndani yake inaingizwa order yao binafsi (Mafisadi) kwa hiyo mfano mahitaji ni 200,000 basi vitaombwa 250,000, hivyo elfu hamsini watajua wao watakavyoupeleka mchakato kati ya wanunuzi na watu wa store na record za ledger book ila Serikali itatoa hela ya 250,000 maana yake hapo kuna vitakavyoingizwa kwenye ledger na kuonekana vimetoka au visiingizwe kabisa kwenye ledger book.

2. Kuongeza gharama za manunuzi mara mbili au zaid ya bei halisi kama kitu kinauzwa Tsh.200,000/ basi serikali itauziwa kati ya Tsh.300,000 hadi Tsh. 350,000/- au zaid

3. Kununua vitu ambavyo ni low quality wakati vinavyohitajika na pesa iliyotoka serikalini ni ya vifaa vyenye high quality ( hili lilijitokeza kwenye vishkwambi, mashine za kusajili wapiga kura, mifumo ya kimtandao ya serikali , servers nk ndio maana mifumo mingi ya Derikali haiishi kusumbua kila mara)

4. Kuchanganya bidhaa original na feki zake, hasa zile zinazohitajika kwa wingi mf. Vifaa vya afya , vifaa vya kielectronic ,vifaa vya miradi ,vifaa vya kazi maalumu nk.

Yaani hapa iko hivi mfano vinahitajika vifaa 200,000 ambavyo bei yake ni Tsh.600,000/- kila kimoja ambacho ni original na high quality, kitakachofanyika ni kununua vifaa 100,000 original kabisa ambavyo navyo unaweza kukuta bei iliongezwa , halafu hivyo 100,000 vilivyo baki vinatafutwa feki yake vifananavyo na vinavyoweza kufanya kazi ile ile ila sio kwa ubora lakini kwa bei ya chini labda Tsh 250,000/- na hapa huwa order inatolewa China maana ndio kuna local industries zenye ubingwa wa kutoa copy za vitu kwa bei ndogo ili pesa ya juu watu waibe

5. Kuleta vitu vilivyoagizwa kwa mafungu mafungu yani kama vilihitajika vifaa labda 200,000 vinaletwa kwanza 130,000 halafu wanasikilizia kwanza kama kutakuwa na kelele wakiona kimya ndio imetoka hiyo vilivyobaki haviji tena pamoja na kwamba Serikali inakuwa ilishatoa hela ya vyote 200,000 na baada ya hapo wanacheza na watu wa record kwenye ledger book idadi inajazwa lakini vitu havipo.

Zipo njia nyingi zaidi na sitaki kuamini kwamba serikali haijui
Mfumo wa manunuzi ukweli ni kuwa sirikali imeshindwa ama kwa makusudi au kwa bahati mbaya, na hicho ni chanzo cha umaskini wetu na umaskini wa taifa letu.Yafaa tujifunze kwa wenzetu wao wameweza je na sisi tumeshindwa je🤔
 
Back
Top Bottom