Wizi wa kwenye mabasi wanaswa na kamera ya bus la ABC

Wizi wa kwenye mabasi wanaswa na kamera ya bus la ABC

Umenikumbusha kuna siku mshkaji aliibiwa Tablet kwenye Basi, Akagundua...

Yule Mwamba Nilimkubali, Daadeki alipiga biti mule ndani si la kitoko tunafika stend akasimama mlangoni, Hakuna mtu kushuka, Anagonga kabisa mlango "Hapa Sio wewe konda wala nani hamna kupitaa..., ukilazimisha wewe ndio Mwizi wangu, una haraka njoo tukaguane"

Utani utani ila kweli hakupita mtu mpk Police wakaja wakapekua wakamdaka mwizi wakaenda naye sijui walimalizia wapi.
 
Ticket ,zinaelekeza mzigo wandani jukumu lako ,bado hatuelewi

Na
Mwizi anaakili Sana huwaza begi zisizokumbatiwa ndizo zinamali (pesa au nyingine)
 
hii ndio hali ya hao wezi hivi sasa baada ya wao kuzidiwa mbinu na teknolojia.
 

Attachments

  • scared.gif
    scared.gif
    441.7 KB · Views: 5
Ngumu sana....Mimi mpaka Leo na RB ya dogo mmoja ni wanted aliiba 10M video na camera Kila kitu zilimuonyesha hatua zake zote.....................

Hii dar es salaam ni kubwa sana na ni ngumu kumpata otherwise wangekua na program kama za KGB au FBI au CIA au Mossad alama za mikono na picha zao zingeingizwa kwenye data base...
Kama walijiandikishaga

Mambo ni mengi muda mchache..😊
Wizi upo tu mkuu.
Niliwahi kupigwa matukio mara 2 kipindi fulani nikakoma.
Safari inaanza kwenda Mbeya.
Rungwe express.

Doc zoote ziko ndani ya begi kubwa na laptop nimejaza humo na camera mazaga kibao.
Fika Msamvu kuchimba dawa nilikua na kijana wangu.
Foleni chooni.
Tulikua tumekaa mbele pale na dereva nikamuaga kabisa kasema poa nawangoja.
Tunatoka kule Bus halipo

Nikapagawa
Wazo langu lile begi mle ndani wameenda nalo.
Boda wakanifata kaka rungwe imeenda ila tuifwate tu kabla haijashika njia kuu.
Sikuuliza
Tukapiga mshkaki mbio zikaanza.
Kweli tukalikuta mbele tu ndio linakamata barabara ya mikumi.
Piga mkono kasimama tukapanda.
Aisee ilibaki kidogo nimpe makofi yule dereva.
Bahati alikua mpole kaomba msamaha yakaisha.
Tukio la pili.
Mbeya pale 8×8.
Tumefika wale wapiga debe wanangangania begi kubwa.
Mmoja kalilamba.
Kapakia mzigo tulikua wanne.
Tumeingia ndani gari imejaa.
Ikabidi tushuke maana gari za kyela nyingi zipo.
Ile tunashuka yule konda msenge yule kumwambia dereva amsha.
Wakatimua kwa fujo zote.
Nikashikwa kiwewe tena.
Mle kwenye begi kubwa😁.
Toka mbio chukua taxi pale baloon nikajua ataiwai.
Kumbe gari mbovu kichizi na haina mafuta.
Tumetoka kidogo tu kufika pale relini likagima
Aisee nilichanganyikiwa.
Mungu alikuwepo.
Mara boda huyu anapita.
Piga mkono tukadandia.
Mbio tena.
Mpk Uyole mbele pale Uporoto ndio tukaikuta.
Huyo konda aliyepakiza begi anapiga debe.
Aisee sikuuliza kwanza nilipiga kichwa kadondoka kule.
anainuka aah brother ni wewe mawenge kibao.
Nikamwambia shusha begi.
Kashusha mwenyewe.
Sasa sijui alikua analipeleka wapi,
Ikabidi nimpigie mdingi aje na private car tutimke.
Niliapa sipandi tena mabus public
 
Hawa wezi walikuwa ni miongoni mwa abiria? Kama walikuwa sio miongoni mwa abiria basi ABC walikuwa wamezembea sana.

Ninavyojua ABC huwa hasimami ovyo kwenye vihotel uchwara(sijajua kwa route ya Iringa, Mbeya, Mafinga na Njombe) ila route ya Dom, Singida huwa wanasimama sehemu maalumu( Kwenye Hotel yao Moro, na Kituo chao Dom, area C) na wakisimama huwa wanafunga milango pindi abiria wakishuka wote.

Sasa sijui walikwama vipi kama ni wao ABC ndio wametokewa na hilo tukio...
Magufuli hapo nadhani ndo panakuaga na tafrani hizooo
 
Dah inawezekana Aisee Maana wamenipiga vitu Si chini ya 3M kulikuwa na Laptop,Tablet,Simu na Vitambulisho Vya kazi Na Vitu vyangu vingine ila me naamini Mungu Atawalipa Aisee walinirudisha sana Nyuma washenzi hawaaa
Pole sana inaumiza mnooo...
 
Ngumu sana....Mimi mpaka Leo na RB ya dogo mmoja ni wanted aliiba 10M video na camera Kila kitu zilimuonyesha hatua zake zote.....................

Hii dar es salaam ni kubwa sana na ni ngumu kumpata otherwise wangekua na program kama za KGB au FBI au CIA au Mossad alama za mikono na picha zao zingeingizwa kwenye data base...
Kama walijiandikishaga

Mambo ni mengi muda mchache..[emoji4]
Hukumtangaza Kwenye magroup ya wasap sasa hvi mtangaze halafu tangaza dau nono,mpeleke Kwa mange kimambi akutangazie au page za udaku udaku hizi wiki umemkamata
 
Magufuli hapo nadhani ndo panakuaga na tafrani hizooo
ABC inapakia Manzese, Magufuli inachukua wachache sana. sasa hapo inaonekana watu walishuka ndio hao wezi wakapata nafasi. Je Magufuli wangeshukaje?
 
Back
Top Bottom