Wizi wa mapato ya Serikali katika Bandari ya Dar es Salaam ndiyo sababu kubwa ya DP World kukabidhiwa

Wizi wa mapato ya Serikali katika Bandari ya Dar es Salaam ndiyo sababu kubwa ya DP World kukabidhiwa

Mr Why

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2019
Posts
2,235
Reaction score
4,252
Kumekuwa na malalamiko makubwa sana kwa bandari ya Dar es Salaam kukabidhiwa kwa DP World, lakini sababu kubwa zaidi ni wizi wa mapato ya Serikali uliokithiri pamoja na dhuluma kubwa kwa wateja wanaoagiza mizigo bandarini.

Mizigo inayopita bandarini ni mingi sana lakini Serikali imekuwa haipati mapato sahihi ya bandari hiyo kwani fedha hizo zimekuwa zikidhulumiwa tangu kipindi cha Mwl Nyerere na hata alipokuja Dr Magufuli wizi huu ulimkera sana na kujaribu kuchukua hatua ambazo hazikuzaa matunda.

Watanzania tujitoe boliti kwenye macho yetu ndipo tumnyooshee kidole raisi Samia Suluhu Hassan pamoja na Serikali kwa uamuzi waliochukua.

Watanzania tujiulize je tumekuwa tukipeleka mapato sahihi serikalini kama tulivyopaswa kufanya? Je hatukuwa tukidhulumu wateja wanaoagiza mizigo kupitia bandari hiyo? Lengo la Serikali kuleta wawekezaji DP World ni kupata mapato makubwa kwasababu ya uendeshaji wao mzuri wa bandari usiokuwa na hujuma.

Kama kusingekuwa na wizi na ubadhilifu unaofanyika bandarini basi Serikali isingewakumbuka wawekezaji wa nje ya nchi.

Watanzania tujifunze kuacha hujuma kupitia uamuzi huu wa DP World kwenye mali za Serikali kwasababu kadiri itakavyozidi kukosa mapato sahihi ndipo itazidi kualika wawekezaji kutoka nje ya nchi yetu ili wasimamie kwa haki.

Reference:
 
Kwanini wezi hawafikishwi mahakamani?
Kulea wezi, wazembe na wabadhirifu ni mfumo rasmi wa CCM ulioasisiwa tangu enzi za Nyerere. Haribu hapa, tukuhamishie kule
Tizama kwa kina Video iliyoambatanishwa
 
Haya ni matusi mengine tu kuja kutaka kuhalilisha Uwekezaji wa kinyonyaji na hatari wa Usalama wa Taifa.

Manake kama hoja ni kuwa akiwa mtu binafsi hawezi kuwa anakubali anaibiwa.

Kwanini wasibinafsishe na kuwagawia hawa mabilionea wetu hapa Nchini?
 
Haya ni matusi mengine tu kuja kutaka kuhalilisha Uwekezaji wa kinyonyaji na hatari wa Usalama wa Taifa...
Serikali inateseka sana mpaka inachukua huu uamuzi lengo ipate mapato makubwa lakini kila inapofumua utendaji wa pale bandarini basi wanakuja wafanyakazi wengine wenye tabia hiyo ya ubadhilifu.

Imani yetu kwa mali za uma imepotea kabisa, Serikali inatuogopa
 
Tupo pamoja ndugu yangu, tutazame video iliyoambatanishwa tuone jinsi gani Serikali inateseka na ubadhilifu😀

Watu wengi hawajui ukweli wao ni ushabiki tuu, na ndio maana hata Rostam Azizi, Godless Lema, General Ulimwengu, Sheikh Ponda, Padre Kitima na wengine wengi tuu, katika mkutano pale SERENA alitutahadharisha kuwa tujadili kwa hoja wala sio ushabiki kwani maendeleo hayachagui Chama, Dini wa Ukabila.
Mkuu "watake wasitake" hili la Bandari lazima DP World waje na walete ufanisi ili Serikali iweze kupata mapato hakuna haya ya kubembelezana kwenye issues zenye maslahi mapana kwa nchi.
 
Haya ni matusi mengine tu kuja kutaka kuhalilisha Uwekezaji wa kinyonyaji na hatari wa Usalama wa Taifa.


Manake kama hoja ni kuwa akiwa mtu binafsi hawezi kuwa anakubali anaibiwa....kwanini wasibinafsishe na kuwagawia hawa mabilionea wetu hapa Nchini?

Before ilikiwepo Ticts ya wazalendo nayo imeshindwa! Au unataka apewe nani!
 
Haswa,Wananchi wanaanza kukosa imani na Serikali yao pamoja na Chama kilichokuwa na Dola hiyo...

Mkuu una hoja nzuri sana ya uzalendo na ndio maana hata Rostam Aziz tycoon no 2 alihusishwa na ujio huu wa DP world na alijibu vizuri na kiungwana na kujidhihirisha uzalendo wake tena kwa kukemea ubaguzi uliokuwa unqtaka kupotoshwa na wengi waliojikita na hoja ya kipuuzi ya uzanzibar na ubara.
 
Serikali inateseka sana mpaka inachukua huu uamuzi lengo ipate mapato makubwa lakini kila inapofumua utendaji wa pale bandarini basi wanakuja wafanyakazi wengine wenye tabia hiyo ya ubadhilifu. Imani yetu kwa mali za uma imepotea kabisa, Serikali inatuogopa
Sawa, Kwa hiyo tutegemee wafanyakazi Bandarini kukosa kazi, kwani wamesema asilimia 60 na ushee itakuwa ni wageni ambao wanategemea kuondolewa ushuru, tozo, sijui na vimbwanga gani ili waweze kufanya kazi kwa "Ufanisi" tunashindwa nini kuwafanyia wafanyakazi wetu....yaani kuwapatia motisha hizo hizo tunazokwenda kutunga sheria kwa ajili ya DP?

Serikali imesema mapato Asilimia karibia ya 40 yanatoka bandarini, tuliambiwa, Royal tour itaongeza mapato, tumesherehekea TRA kuongeza mapato, tumesherehekea Ugawiaji wa "gawio" za mashirika tena tumaambiwa hazina shuruti, tumeambiwa baada ya mikopo iliyokopwa kuwa itasaidia serikali kuboresha maeneo ya kuongezea vipato vya serikali... sasa hizi haraka za nini? Kwanini tusisubiri matunda ya uwekezaji wa kodi za Wananchi?
 
Sawa, Kwa hiyo tutegemee wafanyakazi Bandarini kukosa kazi, kwani wamesema asilimia 60 na ushee itakuwa ni wageni ambao wanategemea kuondolewa ushuru, tozo, sijui na vimbwanga gani ili waweze kufanya kazi kwa "Ufanisi" tunashindwa nini kuwafanyia wafanyakazi wetu....yaani kuwapatia motisha hizo hizo tunazokwenda kutunga sheria kwa ajili ya DP?

Serikali imesema mapato Asilimia karibia ya 40 yanatoka bandarini, tuliambiwa, Royal tour itaongeza mapato, tumesherehekea TRA kuongeza mapato...

Slylogist: ukweli ni kwamba hao wafanyakazi karibia wote wa bandari ya Dar es Salaam watapata kupunguzwa kazi na hawatakiwi kabisa hata kuonekana maeneo hayo kwani wao ndi chanzo KIKUU cha Tatizo.

Wajiandae tuu kufungasha virago nao wakalime au kufanya biashara kama wataweza walitutesa sana sisi wadau na wafanyabiashara.
 
Sawa, Kwa hiyo tutegemee wafanyakazi Bandarini kukosa kazi, kwani wamesema asilimia 60 na ushee itakuwa ni wageni ambao wanategemea kuondolewa ushuru, tozo, sijui na vimbwanga gani ili waweze kufanya kazi kwa "Ufanisi" tunashindwa nini kuwafanyia wafanyakazi wetu....yaani kuwapatia motisha hizo hizo tunazokwenda kutunga sheria kwa ajili ya DP?

Serikali imesema mapato Asilimia karibia ya 40 yanatoka bandarini, tuliambiwa, Royal tour itaongeza mapato, tumesherehekea TRA kuongeza mapato, tumesherehekea Ugawiaji wa "gawio" za mashirika tena tumaambiwa hazina shuruti, tumeambiwa baada ya mikopo iliyokopwa kuwa itasaidia serikali kuboresha maeneo ya kuongezea vipato vya serikali... sasa hizi haraka za nini? Kwanini tusisubiri matunda ya uwekezaji wa kodi za Wananchi?
Mkuu naomba kuuliza unapinga uwekezaji au Namna ya uwekezaji?

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
Tunawataka DP World ila sio kwa mkataba huu mbona hamsikii lakin achen kuruka ruka kama maharage jikon.

Kuna maslah gan kwako kutetea wao kupewa chini ya mkataba huu.
 
Acha waibe wazalendo, pesa itazunguka nchini,
Kuhamisha kabisa pesa yetu yaani sasa watanzania wakawatumikie waarabu kwa malipo kiduchu na mijeledi,

Hapana. Tunataka bandari.
Wewe mchaga kuiba ni dhambi, pia hakutakuwa na mijekedi. Kwani kipimo cha utendaji kwa kila mfanyakazi ni performance target. Sasa kuliko hizo pesa unazotegenea wafanyakazi wa bandari waibe ndio ziwe kwenye mzunguko huo ni uchumi yabisi.

Kwa kuwa serekali itapata mapato makuwa tutaweza kuboresha hudumu za jamii, miondombinu ili kukuza uchumi wa kila mtanzania kwa mapana yake.

Kwa hiyo nakutoa wasiwasi wewe mchaga usiwe na hofu na ndio maana baada ya Serikali kubinafshisha kiwanda cha Bia TBL ufanisi umeongezeka na faida kibao.

Mfano mzuri ni juzi Benki ya NMB zamani iliitwa Benki ya makabwela. Baada ya uwekejaji wa mholanzi wameweza kutoa gawio kwa Serikali Tsh 45.1 B.

Sasa pata picha je bandari watatoa ngapi!@@!!!!
"Mtake msitake Ni lazima DP world wachukue hizi Bandari"
 
Back
Top Bottom