Uchaguzi 2020 World Bank yapitisha Mkopo wa Zaidi ya Trillion 1 Uliopingwa na Wanasiasa pamoja na Wanaharakati

Uchaguzi 2020 World Bank yapitisha Mkopo wa Zaidi ya Trillion 1 Uliopingwa na Wanasiasa pamoja na Wanaharakati

Ilitegemewa kwani tulijua lazima serikali ibadili msimamo!Halafu huo ulikuwa msimamo binafsi wa JPM wala sio serikali nzima so tulijua itakuwa rahisi kubadili maamuzi yake!So its okay kwangu kwa hayo mambo mawili-
1.Fedha kutoka baada ya uchaguzi
2.Watoto wakaojifungua kupewa nafasi katika mfumo rasmi!
Kwa hayo,nimeridhika na moyo mweupee kabisaaa!😀
Upuuzi mtupu! Eti mzazi asome darasa hilohilo na mtoto! Haitawezekana abadani Tz! Wao walete hizo hela, after all ni mkopo tu! Mambo ya nyumbani na namna tunavyoendesha jamii yetu watuachie wenyewe! Otherwise waurudishe mkopo wao!
 
Kabudi kaenda kupiga magoti ndio mkopo ukatolewa.
 
Watoto 5500 kila mwaka wana drop out kutokana na kupigwa mimba,wewe unasema wanaogopa kutokana na kufukuzwa shule!Are you serious?Wengi wao wanapigwa mimba kutokana na mazingira ya kusomea kutokuwa rafiki kwao!
Over the past two years, about 300,000 children, half of them girls, have been unable to continue their lower secondary education due to insufficient space in public schools. In addition, an estimated 5,500 Tanzanian girls who are pregnant drop out every year. SEQUIP has been designed to enable more adolescent girls and boys to transition to upper secondary education. It gives pregnant girls, young mothers, and other vulnerable children who leave school early the possibility to return to the formal system and complete their education. The project tackles the issues facing pregnant girls with an approach informed by civil society organizations and NGOs, in Tanzania and around the world.



“SEQUIP’s design strives to give pregnant girls and young mothers a better chance to complete their education,” said Caren Grown, Senior Director of the Gender Group at the World Bank. “The Bank has stepped up its work to create a new generation of education programs that emphasize safe school environments for girls and boys, including measures that reduce gender-based violence, corporal punishment, bullying, and other forms of violence in and around schools. It gives girls better quality choices and opportunities for completing their secondary education.”
Yes, very serious! Ruhusu waendelee na shule rasmi wakiwa wazazi uone kama idadi hiyo kama haitakuwa ya wasiobeba mimba na kinyume chake ndio watakaokuwa wazazi waliopo shule rasmi! Sijui kama unaweza kuelewa kwa hii statement; ila kwa bahati mbaya sina muda kwa sasa!
 
Makamandaa!!! Fedha hii itasaidia watoto wote bila kuwasahau watoto wa makamanda wote popote walipo Tz au siyo!!!!?
 
ZITTO KABWE AUMBUKA.

Kampeni yake chafu dhidi ya Tanzania yakwama.
_
Benki ya Dunia yaidhinisha Mabilioni ya fedha za kusaidia Elimu alizotaka Tanzania inyimwe.

Saa chache zilizopita Benki ya Dunia kupitia Bodi ya Wakurugenzi Watendaji ya Chama cha Maendeleo ya Kimataifa (IDA) imefanya maamuzi ya kihistoria ya kuruhusu mkopo wa Dola za Marekani Milioni 500 utolewe kwa Tanzania kwa ajili ya kusaidia kuboresha elimu ya Sekondari baada ya mjadala mrefu uliochukua miezi zaidi ya mitatu.

Uamuzi wa Benki ya Dunia umezima kampeni ya kidhalimu iliyofanywa na Mwanasiasa mpuuzi Zitto Kabwe aliyeandika barua kwenda benki hiyo akitumia nembo za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutaka Tanzania inyimwe mkopo huo bila kujali athari zake kwa wananchi hasa wanyonge na maskini.

Zitto Kabwe akishirikiana na mabeberu wanaomfadhili alifanya uharamia kwa kuchochea uongo kuwa Tanzania inakandamiza wanafunzi wa kike kwa kuwanyima fursa ya kuendelea na masomo baada ya kupata ujauzito ilihali anajua kuwa sio kweli na kuna utaratibu ulio wazi wa watoto hao kupata elimu kupitia programu mbalimbali za Elimu ya Watu Wazima, Mpango wa Elimu kwa walioikosa na vyuo mbalimbali.

Hili ni pigo jingine baya sana kwa Zitto Kabwe na washirika wake ambao wamekuwa wakiichonganisha na kuichafua Serikali ya Tanzania na Mashirika ya Kitamaifa kwa kutafuta umaarufu wa kisiasa bila kujali athari ambazo wananchi wanazipata kutokana na kuinanga Tanzania ama kukwamisha miradi mikubwa na washirika wa maendeleo.

Katika safari ndefu ya mjadala ambao ulianza tangu Januari mwaka huu wa 2020, Benki ya Dunia imepiga chini msimamo wa mabeberu waliotaka Tanzania inyimwe fedha hizo baada ya kuingizwa mkenge na Zitto Kabwe.

Watu wengi wanaweza kujiuliza kwa nini Zitto Kabwe na wafadhili wake walikuwa wanashupalia Tanzania inyimwe fedha hizo? Ukweli ni kwamba Zitto na wadhalimu wenzake hawakuzuia fedha hizo kwa sababu ya kupigania wanafunzi wa kike wanaopata ujauzito wakiwa shule kama wanavyodai, bali walishupalia Tanzania isipewe fedha hizo baada ya msimamo wa Serikali ya Awamu ya Tano kukataa kukopeshwa fedha ambazo zingeingizwa nchi kupitia mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO) na miradi ambayo haina matokeo kwa wananchi ili baadaye zitumike kwa maslahi ya siasa za upinzani na sio wananchi.

Kwenye hili, Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Jemedali Rais Dk. John Pombe Joseph Magufuli inastahili pongezi za dhati kwa msimamo thabiti usiyoyumba na ushindi mkubwa dhidi ya kibaraka Zitto Kabwe na washirika wake ambao wamekuwa wakipiga tripu kwenda mabeberu hao kufanya kampeni ya kuiangamiza Tanzania eti wakitaka kuiondoa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani.

Kongole Rais Magufuli, hongera Watanzania wote kwa ushindi huu mkubwa. Zitto Kabwe na washirika wake washindwe na walegee.

Sasa Tanzania itapata Dola za Marekani Milioni 500 sawa na zaidi ya shilingi Trilioni 1 na Bilioni 135 kwa ajili ya kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopata elimu ya Sekondari, kuboresha mazingira ya elimu kwa wasichana na kuinua ubora wa elimu kwa wasichana na wavulana.

Mkopo huu ni wa gharama nafuu na sio fedha za bure. Watanzania watazilipa, lakini sasa watalipa fedha ambazo zinakopwa na kuelekezwa kuwasaidia mamilioni ya Watoto wa Tanzania na sio kwenda kwenye NGO na miradi ya kupitisha fedha zinazokwenda kwa wachumia tumbo akina Zitto Kabwe na washirika wake.

Tunaamini Serikali ya Tanzania itatoa mchanganuo wa fedha hizi zinakwenda wapi na zitawanufaishaje Wanzania.

Kila la kheri Watanzania na pole sana Zitto Kabwe kwa kuangukia pua katika mchazo huu mchafu. Tambua kuwa Mwenyezi Mungu husimama na wenye haki na katika hili amesimama na Watanzania wenye haki na Rais wao mpendwa Dk. John Pombe Joseph Magufuli.

Taarifa hii haina uhusiano na siku ya Wajinga Duniani. Ni ukweli mtupu na inapatikana katika tovuti mbalimbali za Kimataifa. Waweza kuisoma hapa kwenye tovuti ya Benki ya Dunia yenyewe

New Financing to Make Secondary Education Safer, Better, and More Accessible for Tanzanian Girls and Boys

Mwl. Damas Masele MPJ
Mkufunzi Mstaafu.
31 Machi, 2020.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe mjinga jaribu kutumia akili ndogo uliyonayo. Serikali imelazimishwa kukubali kutowabagua wanafunzi wa kike.Umesoma English yako wapi? Jina lako tu inaonekana una uelewa wa mashaka.
 
Upuuzi mtupu! Eti mzazi asome darasa hilohilo na mtoto! Haitawezekana abadani Tz! Wao walete hizo hela, after all ni mkopo tu! Mambo ya nyumbani na namna tunavyoendesha jamii yetu watuachie wenyewe! Otherwise waurudishe mkopo wao!
Ukiwa tegemezi au Omba Omba huwezi kuwa muweka masharti. Na huna jeuri ya kukataa msaada kwa vile wewe Tanzania bado ni nchi maskini.
 
Yes, very serious! Ruhusu waendelee na shule rasmi wakiwa wazazi uone kama idadi hiyo kama haitakuwa ya wasiobeba mimba na kinyume chake ndio watakaokuwa wazazi waliopo shule rasmi! Sijui kama unaweza kuelewa kwa hii statement; ila kwa bahati mbaya sina muda kwa sasa!
Hero , wewe mwenyewe ni zao la mwanamke aliyepata mimba akiwa shule, shika adabu yako. Mama yako aangekatizwa kuendelea kusoma na wewe usingesoma
 
Kiza hakiwezi shindani na Mwanga. Congole JPM
Jamani wengine kusoma document ya @WorldBank ni changamoto kubwa. Ni hivi: 96% ya fedha itatolewa tu pale Benki itakaporidhika na matokeo yatakayoidhinishwa na Agent anayejitegemea na Serikali ikiwa imetumia pesa zake zenyewe sawa na kiasi kinachoombwa Malipo yanaanza 2021

SOMENI NA KUELEWA
 
Lazima uwe na upeo wa hali ya juu kuelewa maana ya hela ya ndani. Baadhi ya mambo sio kwa ajili ya kila kichwa, basi tuu tunapenda kudandia kila kitu.

Kuna akili ipi ya kuelewa neno fedha za ndani we kiazi? Jiwe alikuwa anaropoka maneno ili aonekane kapandisha uchumi, bila kijua kwamba anaowaongopea walikuwa mjini kabla yake.
 
Afadhali zitatusaidia kwenye hii corona virus.
 
Mkopo lilikuwasiyo tatizo, tatizo ilikuwa ama tusomeshe wajawazito au waendelee na shule baada ya kujifungua.

Sasa tuambizane kuna sharti au hakuna kwenye mkopo?!

Mkuu nilichoona hakuna, world bank wamekubali masharti yaliowekwa na serekali ya CCM na tusubiri utekelezaji tu.
Moja ya sharti ambalo watu walipinga ni mtoto wakike akifeli aruhusiwi kurudi sekondari, bali atarudi kusoma alternative education yani vile vyuo vya CCM vikitwa (Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi - VMW (FCD’s)
 
Jambo jema ni kuwa wale waliokuwa wakitaka wanafunzi waliopata mimba wakiwa mashuleni, wapate nafasi nyingine tena ya kusoma, wameshinda.

Taarifa ya World Bank imesema wazi kuwa miongoni mwa watakaonufaika ni pamoja na wale walioondoka kwenye mfumo rasmi wa shule za serikali.

Kauli ya Rais kuwa aliyepata mimba akiwa shuleni hawezi kusoma tena, imefutwa. Sasa nao watapata elimu. Hatuungi mkono mimba zisizo na utaratibu, na hasa za wanafunzi. Lakini kwa sababu tumesema kuwa mwanafunzi ni mtoto, na anayefanya naye mapenzi, amembaka, huwezi kumwadhibu aliyebakwa bali unamwadhibu mbakaji.

Wasichana walioanguka na kupata mimba wakiwa mashuleni, watapata nafasi ya kusoma tena, na wabakaji wataendelea kuadhibiwa.

Haikuwa sahihi kusema binti mwanafunzi aliyepata mimba asisome. Huyu amekosewa. Afunzwe, arudishwe masomoni. Tunao watu wengi wanafanya makosa mbalimbali lakini baada ya makosa yao, hatuwaondolei fursa zao za kujiendeleza.

Hongera wote waliokuwa wanapigania haki ya mtoto wa kike. Wameshinda, Tanzania imeshinda, na sote tumeshinda. Cha muhimu ni kufuatilia ili kuhakikisha Serikali haikiuki ahadi yake kwa WB ua kuhakikisha mtoto wa kike anapata haki yake.
 
Mkuu nilichoona hakuna, world bank wamekubali masharti yaliowekwa na serekali ya CCM na tusubiri utekelezaji tu.
Moja ya sharti ambalo watu walipinga ni mtoto wakike akifeli aruhusiwi kurudi sekondari, bali atarudi kusoma alternative education yani vile vyuo vya CCM vikitwa (Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi - VMW (FCD’s)

Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi - VMW (FCD’s)



Historia fupi ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (VMW) ni “Taasisi za Kiserikali” ambazo zilianzishwa mwaka 1975 kutokana na wazo la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere, baada ya kutembelea nchi ya Sweden na kuona mfumo wa elimu isiyokuwa rasmi ulivyokuwa unaendeshwa na taasisi zinazojulikana kama Folk High Schools.
Vyuo ya Maendeleo ya Wananchi vilianzishwa kama sehemu ya awamu ya tatu ya Elimu ya Watu Wazima. Hatua ya kwanza ilihusu kuondoa ujinga wa kutojua kusoma, kuandika na kuhesabu. Hatua ya pili ilikuwa ya kuhakikisha kuwa mafanikio yaliyopatikana katika hatua ya kwanza yanakuwa endelevu na watu hawaurudii ujinga. Hatua ya tatu ilikuwa kuanzisha taasisi ambazo zingetoa maarifa na stadi kwa wananchi. Aidha, uamuzi wa kuanzishwa VMW ulitokana na Waraka wa Baraza la Mawaziri No. 96 wa mwaka 1974 ambapo vyuo 25 vilianzishwa mwaka 1975 na kuendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka kulingana na jinsi Wilaya mbalimbali zilivyo tambua umuhimu wa kuanzisha vyuo hivi. Hadi kufikia mwaka 1978, vyuo 53 vilikuwa vimeanzishwa.
Uanzishwaji wa VMW ulizingatiwa katika Sheria ya Elimu No. 25 ya mwaka 1978 chini ya Wizara ya Elimu. Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi vilipoanzishwa vilirithi majengo yaliyokuwa yakitumika kwa madhumuni tofauti tofauti vikiwemo Vituo vya Mafunzo ya Maendeleo Vijijini (Rural Training Centres) ambavyo vilianzishwa mwaka 1962, Vituo vya Mafunzo ya Wakulima (Farmers Training Centres) ambavyo vilianzishwa mwaka 1963, Shule za Kati (Middle Schools) ambazo zilianzishwa mwaka 1960 na Vituo vya Mafunzo ya Ushirika vilivyoanzishwa mwaka 1964. Vyuo pekee vilivyojengwa mahsusi kuitikia wazo la Baba wa Taifa la mwaka 1975 ni vinne, vyuo hivyo ni Sengerema, Ngara, Handeni na Bigwa, ambavyo vilijengwa mwaka 1975.

Lengo na madhumuni ya kuanzishwa kwa vyuo vya maendeleo ya wananchi (VMW)
Lengo Kuu

Lengo kuu la kuanzisha Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi lilikuwa ni kuimarisha maarifa na stadi kwa wananchi ili waondokane na ujinga, umaskini na maradhi na hatimaye kuleta maendeleo ya kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni.
Madhumuni mahsusi yakuanzisha VMW
Madhumuni mahsusi ya vyuo hivi yameelezwa katikaWaraka wa Serikali Na. 96 wa mwaka 1974 ambapo kipengele cha 5 kinaainisha madhumuni yafuatayo:
a) Kumtayarisha Mtanzania ambaye ni mtu mzima aweze kukuza utu wake na kumfanya awe kamili katika jumuiya ya Watu wake;
b) Kumtayarisha Mtanzania aweze kutumia akili zake vizuri na kuweza kuamua mambo yake au ya Umma kwa njia iliyo sahihi;
c) Kumsaidia Mtanzania aelewe siasa ya nchi yake na kumwezesha kushiriki kikamilifu bila woga au unafiki katika shughuli za siasa ya nchi yake;
d) Kujenga moyo wa Mtanzania wa kushirikiana na wenzake katika shughuli au kazi za nchi yake, na kuelewa umuhimu wa kuwa na uhusiano mwema na wenzake;
e) Kumwezesha Mtanzania aweze kufikia kiwango cha juu zaidi katika ufundi wa kazi anazozifanya;
f) Kumsaidia Mtanzania kukuza utamaduni wa Kitanzania; na
g) Kuwafanya Watanzania wawe raia wenye manufaa katika Tanzania na dunia nzima.

Lengo na madhumuni haya yaliendelea kutekelezwa hadi mwaka 1987 ilipoundwa Tume ya Nsekela iliyoazinsha majukumu ya Wizara na Idara mbalimbali za Serikali. Tume ya Nsekela ya Februari 1987 ilibaini kuwa madhumuni na majukumu ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi yanashabihiana sana na yale ya Maendeleo ya Jamii ya kuwajengea uwezo wananchi ili wamudu majukumu yao vyema na kuboresha utendaji na maisha yao. Tume hiyo iliishauri Serikali kuhamishia VMW katika Idara ya Maendeleo ya Jamii. Mwaka 1990, Serikali ilivihamishia VMW katika Idara ya Maendeleo ya Jamii chini ya iliyokuwa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto. Ingawa lengo kuu halikubadilika, madhumuni yaliboreshwa ili kukidhi mabadiliko ya wakati huo katika jamii kwa kuzingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025.

Madhumuni mahsusi yaliyoboreshwa
Madhumuni yaliyoboreshwa ni yafuatayo:
a) Kuwapatia wananchi stadi mbalimbali za ujuzi na maarifa ambayo yatawasaidia kujiajiri na kuajiriwa hivyo kuondoa umaskini katika jamii;

b) Kuwawezesha viongozi katika ngazi za Vijiji na Kata kuelewa majukumu yao na hivyo kusimamia kwa ufanisi utekelezaji wa sera mbalimbali za Serikali za kuondoa umaskini, kuwaletea wananchi maisha bora na kusimamia misingi ya utawala bora;

c) Kuwezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika maamuzi, kutambua masuala ya jinsia, kuimarisha na kudumisha utamaduni wa kupiga vita mila na desturi zinazomkandamiza mwanamke katika jamii;

d) Kuziwezesha jamii kuelewa umuhimu wa hifadhi, matumizi bora ya mazingira na kutumia rasilimali zilizopo kwa faida yao; na

e) Kuziwezesha jamii kuelewa na kujikinga na janga la UKIMWI.

Majukumu ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
Ili kufikia madhumuni tajwa hapo juu VMW vimepewa majukumu mbalimbali kupitia “Mwongozo wa Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi” wa mwaka 2002. Majukumu hayo ni pamoja na:
a) Kutoa mafunzo yenye kuongeza maarifa, stadi na mbinu mbalimbali za kutatua matatizo halisi ya wananchi, ili wajiletee maendeleo kwa kutumia rasilimali zilizopo;

b) Kutoa mafunzo yanayokidhi mahitaji halisi ya wananchi na soko;

c) Kubuni na kuendesha miradi ya uzalishaji mali na utoaji huduma vyuoni na kuvisaidia vijiji vinavyozunguka vyuo. Aidha, miradi hii ifanyiwe uchambuzi na upembuzi yakinifu ili miradi inayotekelezwa iwe na taathira chanya kwa jamii;

d) Kushirikiana na asasi na mashirika mbalimbali yanayotoa mafunzo, utaalam na rasilimali nyinginezo kuwaendeleza wananchi. Katika zoezi hili, vyuo vitapata fursa ya kubadilishana uzoefu na asasi hizo;

e) Kufanya utafiti wa mahitaji utakaotoa takwimu na taarifa sahihi zitakazotumiwa na vyuo, vijiji na mitaa, katika kubuni, kupanga na kutoa mafunzo ya ushirikishwaji, pamoja na kutekeleza miradi mbali mbali ya kujitegemea. Aidha taarifa na takwimu hizo zinaweza kutumiwa na Halmashauri za wilaya, Miji, Manispaa na Jiji katika kuandaa mipango ya uwiano ya maendeleo;

f) Kuwa vituo vya kufundishia, kutengeneza na kusambaza teknolojia na nyenzo za kurahisisha kazi wafanyazo wananchi;

g) Kubaini mila zisizo za maendeleo na vikwazo vingine vya maendeleo katika maeneo vilipo vyuo na kutoa mafunzo dhidi ya vikwazo na mila hizo;

h) Kubuni, kuandaa na kuendesha programu mbalimbali zitakazoinua kiwango cha fikra, maarifa na stadi za wananchi kuhusu mazingira yao na ulimwengu kwa jumla;

i) Kuendesha programu mbalimbali za hifadhi ya mazingira kwa wananchi zinazohusu matumizi bora ya ardhi kwa kuzingatia kanuni za kilimo na ufugaji bora, upandaji miti na maua na utunzaji wa vyanzo vya maji;

j) Kuwashirikisha wananchi katika mijadala inayohusu masuala ya jinsia;

k) Kubuni mikakati ya namna ya kuwafuatilia wahitimu kwa nia ya kupima kiwango cha taathira kilichofikiwa kutokana na mafunzo yanayotolewa vyuoni, matokeo ya upimaji huo yatatumika katika kurekebisha mitaala na mikakati ya utekelezaji; na

l) Kushirikiana na asasi nyingine za Serikali, madhehebu ya dini mbalimbali na Mashirika yasiyo ya Kiserikali na Wananchi kubuni na kutekeleza programu na miradi madhubuti ya kutokomeza janga la UKIMWI na umaskini na kupiga vita rushwa.
 
Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi - VMW (FCD’s)



Historia fupi ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (VMW) ni “Taasisi za Kiserikali” ambazo zilianzishwa mwaka 1975 kutokana na wazo la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere, baada ya kutembelea nchi ya Sweden na kuona mfumo wa elimu isiyokuwa rasmi ulivyokuwa unaendeshwa na taasisi zinazojulikana kama Folk High Schools.
Vyuo ya Maendeleo ya Wananchi vilianzishwa kama sehemu ya awamu ya tatu ya Elimu ya Watu Wazima. Hatua ya kwanza ilihusu kuondoa ujinga wa kutojua kusoma, kuandika na kuhesabu. Hatua ya pili ilikuwa ya kuhakikisha kuwa mafanikio yaliyopatikana katika hatua ya kwanza yanakuwa endelevu na watu hawaurudii ujinga. Hatua ya tatu ilikuwa kuanzisha taasisi ambazo zingetoa maarifa na stadi kwa wananchi. Aidha, uamuzi wa kuanzishwa VMW ulitokana na Waraka wa Baraza la Mawaziri No. 96 wa mwaka 1974 ambapo vyuo 25 vilianzishwa mwaka 1975 na kuendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka kulingana na jinsi Wilaya mbalimbali zilivyo tambua umuhimu wa kuanzisha vyuo hivi. Hadi kufikia mwaka 1978, vyuo 53 vilikuwa vimeanzishwa.
Uanzishwaji wa VMW ulizingatiwa katika Sheria ya Elimu No. 25 ya mwaka 1978 chini ya Wizara ya Elimu. Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi vilipoanzishwa vilirithi majengo yaliyokuwa yakitumika kwa madhumuni tofauti tofauti vikiwemo Vituo vya Mafunzo ya Maendeleo Vijijini (Rural Training Centres) ambavyo vilianzishwa mwaka 1962, Vituo vya Mafunzo ya Wakulima (Farmers Training Centres) ambavyo vilianzishwa mwaka 1963, Shule za Kati (Middle Schools) ambazo zilianzishwa mwaka 1960 na Vituo vya Mafunzo ya Ushirika vilivyoanzishwa mwaka 1964. Vyuo pekee vilivyojengwa mahsusi kuitikia wazo la Baba wa Taifa la mwaka 1975 ni vinne, vyuo hivyo ni Sengerema, Ngara, Handeni na Bigwa, ambavyo vilijengwa mwaka 1975.

Lengo na madhumuni ya kuanzishwa kwa vyuo vya maendeleo ya wananchi (VMW)
Lengo Kuu

Lengo kuu la kuanzisha Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi lilikuwa ni kuimarisha maarifa na stadi kwa wananchi ili waondokane na ujinga, umaskini na maradhi na hatimaye kuleta maendeleo ya kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni.
Madhumuni mahsusi yakuanzisha VMW
Madhumuni mahsusi ya vyuo hivi yameelezwa katikaWaraka wa Serikali Na. 96 wa mwaka 1974 ambapo kipengele cha 5 kinaainisha madhumuni yafuatayo:
a) Kumtayarisha Mtanzania ambaye ni mtu mzima aweze kukuza utu wake na kumfanya awe kamili katika jumuiya ya Watu wake;
b) Kumtayarisha Mtanzania aweze kutumia akili zake vizuri na kuweza kuamua mambo yake au ya Umma kwa njia iliyo sahihi;
c) Kumsaidia Mtanzania aelewe siasa ya nchi yake na kumwezesha kushiriki kikamilifu bila woga au unafiki katika shughuli za siasa ya nchi yake;
d) Kujenga moyo wa Mtanzania wa kushirikiana na wenzake katika shughuli au kazi za nchi yake, na kuelewa umuhimu wa kuwa na uhusiano mwema na wenzake;
e) Kumwezesha Mtanzania aweze kufikia kiwango cha juu zaidi katika ufundi wa kazi anazozifanya;
f) Kumsaidia Mtanzania kukuza utamaduni wa Kitanzania; na
g) Kuwafanya Watanzania wawe raia wenye manufaa katika Tanzania na dunia nzima.

Lengo na madhumuni haya yaliendelea kutekelezwa hadi mwaka 1987 ilipoundwa Tume ya Nsekela iliyoazinsha majukumu ya Wizara na Idara mbalimbali za Serikali. Tume ya Nsekela ya Februari 1987 ilibaini kuwa madhumuni na majukumu ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi yanashabihiana sana na yale ya Maendeleo ya Jamii ya kuwajengea uwezo wananchi ili wamudu majukumu yao vyema na kuboresha utendaji na maisha yao. Tume hiyo iliishauri Serikali kuhamishia VMW katika Idara ya Maendeleo ya Jamii. Mwaka 1990, Serikali ilivihamishia VMW katika Idara ya Maendeleo ya Jamii chini ya iliyokuwa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto. Ingawa lengo kuu halikubadilika, madhumuni yaliboreshwa ili kukidhi mabadiliko ya wakati huo katika jamii kwa kuzingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025.

Madhumuni mahsusi yaliyoboreshwa
Madhumuni yaliyoboreshwa ni yafuatayo:
a) Kuwapatia wananchi stadi mbalimbali za ujuzi na maarifa ambayo yatawasaidia kujiajiri na kuajiriwa hivyo kuondoa umaskini katika jamii;

b) Kuwawezesha viongozi katika ngazi za Vijiji na Kata kuelewa majukumu yao na hivyo kusimamia kwa ufanisi utekelezaji wa sera mbalimbali za Serikali za kuondoa umaskini, kuwaletea wananchi maisha bora na kusimamia misingi ya utawala bora;

c) Kuwezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika maamuzi, kutambua masuala ya jinsia, kuimarisha na kudumisha utamaduni wa kupiga vita mila na desturi zinazomkandamiza mwanamke katika jamii;

d) Kuziwezesha jamii kuelewa umuhimu wa hifadhi, matumizi bora ya mazingira na kutumia rasilimali zilizopo kwa faida yao; na

e) Kuziwezesha jamii kuelewa na kujikinga na janga la UKIMWI.

Majukumu ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
Ili kufikia madhumuni tajwa hapo juu VMW vimepewa majukumu mbalimbali kupitia “Mwongozo wa Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi” wa mwaka 2002. Majukumu hayo ni pamoja na:
a) Kutoa mafunzo yenye kuongeza maarifa, stadi na mbinu mbalimbali za kutatua matatizo halisi ya wananchi, ili wajiletee maendeleo kwa kutumia rasilimali zilizopo;

b) Kutoa mafunzo yanayokidhi mahitaji halisi ya wananchi na soko;

c) Kubuni na kuendesha miradi ya uzalishaji mali na utoaji huduma vyuoni na kuvisaidia vijiji vinavyozunguka vyuo. Aidha, miradi hii ifanyiwe uchambuzi na upembuzi yakinifu ili miradi inayotekelezwa iwe na taathira chanya kwa jamii;

d) Kushirikiana na asasi na mashirika mbalimbali yanayotoa mafunzo, utaalam na rasilimali nyinginezo kuwaendeleza wananchi. Katika zoezi hili, vyuo vitapata fursa ya kubadilishana uzoefu na asasi hizo;

e) Kufanya utafiti wa mahitaji utakaotoa takwimu na taarifa sahihi zitakazotumiwa na vyuo, vijiji na mitaa, katika kubuni, kupanga na kutoa mafunzo ya ushirikishwaji, pamoja na kutekeleza miradi mbali mbali ya kujitegemea. Aidha taarifa na takwimu hizo zinaweza kutumiwa na Halmashauri za wilaya, Miji, Manispaa na Jiji katika kuandaa mipango ya uwiano ya maendeleo;

f) Kuwa vituo vya kufundishia, kutengeneza na kusambaza teknolojia na nyenzo za kurahisisha kazi wafanyazo wananchi;

g) Kubaini mila zisizo za maendeleo na vikwazo vingine vya maendeleo katika maeneo vilipo vyuo na kutoa mafunzo dhidi ya vikwazo na mila hizo;

h) Kubuni, kuandaa na kuendesha programu mbalimbali zitakazoinua kiwango cha fikra, maarifa na stadi za wananchi kuhusu mazingira yao na ulimwengu kwa jumla;

i) Kuendesha programu mbalimbali za hifadhi ya mazingira kwa wananchi zinazohusu matumizi bora ya ardhi kwa kuzingatia kanuni za kilimo na ufugaji bora, upandaji miti na maua na utunzaji wa vyanzo vya maji;

j) Kuwashirikisha wananchi katika mijadala inayohusu masuala ya jinsia;

k) Kubuni mikakati ya namna ya kuwafuatilia wahitimu kwa nia ya kupima kiwango cha taathira kilichofikiwa kutokana na mafunzo yanayotolewa vyuoni, matokeo ya upimaji huo yatatumika katika kurekebisha mitaala na mikakati ya utekelezaji; na

l) Kushirikiana na asasi nyingine za Serikali, madhehebu ya dini mbalimbali na Mashirika yasiyo ya Kiserikali na Wananchi kubuni na kutekeleza programu na miradi madhubuti ya kutokomeza janga la UKIMWI na umaskini na kupiga vita rushwa.

Maeneo ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
Maeneo ya vyuo vya Maendeleo ya Jamii yamejumuisha mikoa yote 21 ya Tanzania Bara. Jedwali Na. 14 linaonesha Mikoa na Wilaya husika na idadi ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi na baadhi ya Vyuo vya Ufundi Stadi vilivyotembelewa.

Jedwali Na 1: Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
NaMkoaWilayaChuoIdadi yaWilayaIdadi ya Vyuo
1ArushaMonduliMonduli FDC11
2Dar es SalaamIlalaArnautoglu FDC22
TemekeChang’ombe
3DodomaMpwapwaChisalu FDC22
KondoaMunguri FDC
4KageraBiharamuloRubondo FDC44
Bukoba (M)Bukoba RVT&SC
Bukoba (V)Gera FDC
NgaraNgara FDC
5KilimanjaroMoshi (V)Msinga FDC44
Moshi (M)Moshi RVT&SC
RomboMamtukuna FDC
SameSame FDC
6KigomaKasuluKasulu FDC33
KibondoKibondo FDC
KigomaKihinga FDC
7IringaKiloloIlula FDC23
NjombeNjombe FDC
NjombeUlembwe FDC
8LindiLindi (V)Chilala FDC22
KilwaKilwa Masoko FDC
9ManyaraMbuluTango FDC11
10MaraMusomaMusoma FDC33
TarimeTarime FDC
BundaKisangwa FDC
11Mtwara

Masasi


Masasi FDC


3


4
Masasi VTC
MtwaraMtawanya FDC
NewalaNewala FDC
12MorogoroMorogoroBigwa FDC45
KilosaKilosa FDC
Mikumi VTC
IfakaraIfakara FDC
UlangaSofi FDC
13MwanzaMaswaMalya FDC55
MisungwiMisungwi CDTI
Mwanza (M)Mwanza RVT&SC
Mwanza (V)Karumo FDC
SengeremaSengerema FDC
14MbeyaRungweKatumba FDC22
Mbeya (M)Nzovwe FDC
15PwaniKibahaKibaha FDC33
KisaraweKisarawe FDC
IkwiririIkwiriri FDC
16TaboraSikongeSikonge FDC34
UramboUrambo FDC
NzegaNzega FDC
NzegaMwanhala FDC
17TangaHandeniHandeni FDC33
MuhezaKiwanda FDC
LushotoMabughai CDTI
18RukwaMpandaMsaginya FDC22
NkasiChalla FDC

19

Ruvuma

Mbinga

Mbinga FDC

3

3
Songea (V)Muhukuru FDC
TunduruNandembo FDC
20SingidaSingidaSingida FDC22
IrambaMsingi FDC
21ShinyangaShinyanga (M)Buhangija FDC44
GeitaMwanva FDC
MaswaMalampaka FDC
BariadiBariadi FDC
Jumla5662
 
Maeneo ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
Maeneo ya vyuo vya Maendeleo ya Jamii yamejumuisha mikoa yote 21 ya Tanzania Bara. Jedwali Na. 14 linaonesha Mikoa na Wilaya husika na idadi ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi na baadhi ya Vyuo vya Ufundi Stadi vilivyotembelewa.

Jedwali Na 1: Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi
NaMkoaWilayaChuoIdadi yaWilayaIdadi ya Vyuo
1ArushaMonduliMonduli FDC11
2Dar es SalaamIlalaArnautoglu FDC22
TemekeChang’ombe
3DodomaMpwapwaChisalu FDC22
KondoaMunguri FDC
4KageraBiharamuloRubondo FDC44
Bukoba (M)Bukoba RVT&SC
Bukoba (V)Gera FDC
NgaraNgara FDC
5KilimanjaroMoshi (V)Msinga FDC44
Moshi (M)Moshi RVT&SC
RomboMamtukuna FDC
SameSame FDC
6KigomaKasuluKasulu FDC33
KibondoKibondo FDC
KigomaKihinga FDC
7IringaKiloloIlula FDC23
NjombeNjombe FDC
NjombeUlembwe FDC
8LindiLindi (V)Chilala FDC22
KilwaKilwa Masoko FDC
9ManyaraMbuluTango FDC11
10MaraMusomaMusoma FDC33
TarimeTarime FDC
BundaKisangwa FDC
11Mtwara

Masasi


Masasi FDC


3


4
Masasi VTC
MtwaraMtawanya FDC
NewalaNewala FDC
12MorogoroMorogoroBigwa FDC45
KilosaKilosa FDC
Mikumi VTC
IfakaraIfakara FDC
UlangaSofi FDC
13MwanzaMaswaMalya FDC55
MisungwiMisungwi CDTI
Mwanza (M)Mwanza RVT&SC
Mwanza (V)Karumo FDC
SengeremaSengerema FDC
14MbeyaRungweKatumba FDC22
Mbeya (M)Nzovwe FDC
15PwaniKibahaKibaha FDC33
KisaraweKisarawe FDC
IkwiririIkwiriri FDC
16TaboraSikongeSikonge FDC34
UramboUrambo FDC
NzegaNzega FDC
NzegaMwanhala FDC
17TangaHandeniHandeni FDC33
MuhezaKiwanda FDC
LushotoMabughai CDTI
18RukwaMpandaMsaginya FDC22
NkasiChalla FDC

19

Ruvuma

Mbinga

Mbinga FDC

3

3
Songea (V)Muhukuru FDC
TunduruNandembo FDC
20SingidaSingidaSingida FDC22
IrambaMsingi FDC
21ShinyangaShinyanga (M)Buhangija FDC44
GeitaMwanva FDC
MaswaMalampaka FDC
BariadiBariadi FDC
Jumla5662


Stadi zinazotolewa katika VMW
Katika VMW ilibainika kuwa stadi zinazotolewa ni pamoja na hizi zifuatazo:

a) Upishi;

b) Kilimo na Ufugaji;

c) Ufundi umeme wa majumbani;

d) Ufugaji samaki na nyuki;

e) Ususi na ufumaji;

f) Usindikaji wa vyakula na matunda;

g) Ushonaji;

h) Uchomeleaji vyuma;

i) Umekanika;

j) Kompyuta;

k) Useremala;

l) Uashi;

m) Utengenezaji mapambo;

n) Ujasiriamali;

o) Uendeshaji hoteli; na

p) Umeme wa magari
 
Stadi zinazotolewa katika VMW
Katika VMW ilibainika kuwa stadi zinazotolewa ni pamoja na hizi zifuatazo:

a) Upishi;

b) Kilimo na Ufugaji;

c) Ufundi umeme wa majumbani;

d) Ufugaji samaki na nyuki;

e) Ususi na ufumaji;

f) Usindikaji wa vyakula na matunda;

g) Ushonaji;

h) Uchomeleaji vyuma;

i) Umekanika;

j) Kompyuta;

k) Useremala;

l) Uashi;

m) Utengenezaji mapambo;

n) Ujasiriamali;

o) Uendeshaji hoteli; na

p) Umeme wa magari

Jedwali Na. 18: Mafunzo/Stadi katika kila Chuo
Na​
Mikoa​
Wilaya​
Chuo​
Stadi Zilizopo​
Stadi za Ziada​
1​
ArushaMonduliMonduli FDCUseremala, Uashi, Ushoni, Udereva, Kompyuta, Kilimo, Ufugaji, Upishi na Lishe na Ufundi ChumaUfundi Chuma, Ufundi Magari, Udereva, Ujasiriamali, Ushonaji, Useremala, Uashi, Umeme, Uungaji Vyuma, Ufundi Bomba, Umeme wa Magari, Kilimo na Ususi.
2​
Dar es SalaamIlalaArnautogluFDCBiashara, Umeme na Ufundi wa MagariUfundi Viatu, Kompyuta, Udereva, Ufundi Magari, Ufundi Bomba, Uchomeleaji na Ufundi Rangi
3​
DodomaMpwapwaChisalu FDCUseremala, Maarifa ya Nyumbani na Kilimo Kompyuta, Udereva, Ufugaji,Ufundi Magari, Secretatarial, Ufundi Bomba, Uchomeleaji na Ufundi Rangi
KondoaMunguri FDCUseremala, Uashi,ushonaji, Upishi na lisheUfundi Magari, uchomeleaji, Umeme wa Majumbani, Umeme Jua, Udereva, Kompyuta, Uhazili, Ufundi Bomba, Uchomeleaji na Ufundi rangi
4​
KageraBiharamuloRbondo FDCUshonaji (Sayansi Kimu), Uashi, Useremala na Ufundi Chuma.Kilimo, Ufugaji, Ujasiliamali, Kompyuta, Electronics, Umeme wa Majumbani, Uungaji Vyuma, MV Mechanics, Udereva, Ujenzi Barabara, Kompyuta na Upishi.
Bukoba (M)Bukoba RVT&SC--
Bukoba (V)GeraFDCS/Kimu, Useremala, Uashi, Mafunzo ya muda mfupi – UKIMWI, Kilimo na Uchaguzi.Umeme wa Majumbani, Uchomeleaji, Kompyuta, Electronics, Usindikaji, Umeme wa Magari, Mv Mechanics, Udereva, Kupiga Chapa, Kilimo na Catering.
NgaraNgara FEDCUshonaji, Uashi, Useremala, Ufundi magari, Udereva, Bidhaa za ngozi, mafunzo ya UelewaUshonaji, Uashi, Uchomeleaji vyuma, Umeme wa Magari, Umeme wa Majumbani, Electonics, Usindikaji Mazao, Ushonaji Bidhaa za Ngozi, Useremala, Kompyuta, Ufundi Bomba, Upishi, Ufundi Rangi, Kilimo na Ufugaji.
5​
KilimanjaroMoshi (V)Msinga FDCUseremala, Uashi,ufundi magari, Ushonaji, Upishi na Lishe, Umeme wa Majumbani, Udereva, Ufundi Bomba, Kompyuta, Kilimo na UfugajiUmeme, Ufundi Magari, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Ufundi Rangi, Electronics na Uchimbaji Madini, Userermala, Uashi, Umakenika, Udereva, Kilimo na Ufugaji
RomboMamtukuna FDCUseremala, Uashi, Ufundi Magari, Kilimo, Ufugaji, Upishi na Lishe, Ushonaji na KompyutaUfundi Magari, Ufundi Bomba, Upambaji, Kompyuta, Ujasiriamali, Useremala, Uashi, Udereva, Uafundi wa Friji, Ufundi Umeme wa Majumbani, Upishi na Lishe, Kilimo na Ufugaji
SameSame FDCKompyuta, Udereva, Ufundi Magari, Kilimo, Ufugaji, Useremala, Ushonaji.Umeme, Ufundi Magari, Ufundi Bomba, Upambaji, Kompyuta, Ujasiriamali, Useremala, Uchomeleaji, Udereva, Umakenika wa Kilimo, Electronics, Ufundi Friji na Usanii
6​
KigomaKasuluKasulu FDCKilimo, Ufugaji, Usremala, Uashi, Ushonaji (S/Kimu), Umakenika.Computer Maintenance, ICT, Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Kilimo cha Mitambo na Matengezo yake, Ushonaji, Uashi, Kilimo cha Matunda, Ufundi Bomba, Ufundi Magari, Uashi, Useremala, Uungaji Vyuma, Upishi na Uhazili.
KibondoKibondo FDCUashi, Umakanika, Upishi, Kilimo na Ushonaji.Useremala, Uashi, Umakenika, Kilimo, Kompyuta, Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Utengenezaji wa Majokofu, Utengezaji wa Barabara, Uhazili, Ufundi Magari, Uungaji Vyuma, Ufundi Bomba, Ufundi Rangi na Uchoraji, Udereva na Ufundi Viatu.
KigomaKihinga FDCUshonaji, Uashi, Umakanika, Upishi, na Kilimo.Useremala, Uashi, Umakenika, Kilimo, Kompyuta, Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Utengenezaji wa Majikofu, Utengezaji wa Bara bara, Mafunzo ya Uelewa, Ufundi Magari, Uungaji Vyuma, Umeme, Kompyuta, Lishe na Upishi, Ufundi Bomba na Udereva.
7​
IringaKiloloIlula FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Ufumaji, Kilimo cha mboga, Ufugaji wa ng’ombe na ComputerUfundi magari, Mafunzo ya Computer, Udereva, Useremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Udereva, Kilimo, Ufugaji, Ufundi Bomba na Uungaji Vyuma.
NjombeNjombe FDCUseremala, Uashi, Umeme, Ufundi magari Ushonaji,Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Udereva, Upishi, Hotel Management, Userermala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Udereva, Kilimo, Ufugaji, Uungaji Vyuma na Kompyuta.
NjombeUlembwe FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Umeme majumbani.Umeme wa Majumbani, Ufundi wa Magari, Uungaji Vyuma, Udereva, Useremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Ufugaji, Ufundi Bomba, Kompyuta na stadi zilizopo sasa ziendelee,
8​
LindiLindi (V)Chilala FDCUseremala, Ufumaji, Kilimo, Mifugo, Mafunzo nje ya Chuo na Mafunzo ya Muda Mfupi.Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Udereva, Upishi, Hotel Management, Useremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Ufugaji na Kompyuta.
KilwaKilwa Masoko FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Ufumaji, Kilimo, Mifugo, Mafunzo nje ya Chuo na Mafunzo ya Muda Mfupi.Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Kompyuta, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Udereva, Upishi, Hotel Management, Useremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Ufugaji, Uungaji Vyuma na Ujasiriamali,
9​
ManyaraMbuluTango FDCUseremala na UshonajiUserermala, Uashi, Umakenika, Kilimo, Ufugaji, Umeme, Ufundi Umeme mbadala, Ufundi Magari, Udereva na Ujasiriamali
10​
MaraMusomaMusoma FDCUashi, Kilimo, Upishi, Ushoni na UseremalaKilimo; Udereva; Uvuvi; Utengenezaji wa Maboti/Mashua; Useremara; Uashi/Ujenzi; Ushonaji; Umeme; Ufundi Magari, Upishi, Uendeshaji Canteen, Hotel Management, Umeme wa Magari, Udereva na Kompyuta
TarimeTarime FDCUshonaji, Useremala, Umeme na Uashi.Computer, Udereva, Kilimo, Mechanics, Ujasiliamali, Useremala, Umeme, Udereva, Kompyuta na Uchomeaji Vyuma.
BundaKisangwa FDCUseremala, Ushonaji, Upishi na Uashi.Umeme, Mechanics, Udereva, Ufundi Bomba, Kilimo, Useremala, Welding, Ufugaji, MV Mechanics na Hotel Management.
11​
MtwaraMasasiMasasi FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Umeme wa majumbani, Upishi na Elimu ya Sekondari.Usindikaji, Ujasiliamali, Udereva, Uchomeleaji, Hotel Management. Useremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Ufugaji, Ufundi Bomba, Uungaji Vyuma na Kompyuta.
MtwaraMtawanya FDCUseremala, Ujenzi, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Uraia na UderevaUmeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Uchomeleaji, Udereva, Upishi, Hotel Management, Useremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Udereva, Kilimo, Ufugaji, Ufundi Bomba na Kompyuta.
NewalaNewala FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Ufumaji, Magari, Kilimo, Umeme wa majumbani, UchomeleajiUdereva, Kompuyta, ICT, Hotelia, Userermala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Ufugaji, Ufundi Bomba, Uungaji Vyuma, Electronics na stadi zote zilizopo sasa ziendelee.
12​
MorogoroMorogoroBigwa FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Upishi na Lishe, Umeme wa Majumbani, Ufundi Magari na Elimu ya Chekechea.Uchomeleaji, Ujasiliamali, Usindikaji wa Vyakula, Udereva, Upishi, Upambaji, Uhifadhi wa Vyakula, Ufundi Magari, Uashi, Kompyuta, Kilimo na Ufugaji
KilosaKilosa FDCUseremala, Ushonaji, Kilimo na UsusiKilimo cha Matunda, Uashi, Uchomeleaji, Electronics, Umakenika, Udereva, Kilimo, Ufugaji na Umeme.
IfakaraIfakara FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Kilimo, Mifugo na Sanyansi KimuUmeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Kompyuta, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Udereva, Upishi, Hotel Management, Useremala, Uashi, Kilimo, Umeme na stadi za sasa na elimu ya sekondari ziendelee.
UlangaSofi FDCUashi, Useremala, Ushonaji, Kilimo, Ufugaji, Sayansi Kimu na Upishi.Useremala, Ushonaji, S/Kimu, Kilimo, Ushonaji, Umeme, Uungaji Vyuma, Ufundi Bomba, Umeme wa Magri, Ususi na Ujasiriamali.
13​
MwanzaMaswaMalya FDCKilimo, Ufugaji, Useremala, Ushonaji, Uashi na Welding.Mechanics, Computer, Udereva, Upishi, Umeme, Uungaji Vyuma, Kilimo, Ufugaji, Kompyuta na Catering.
MisungwiMisungwi CDTI--
Mwanza (M)Mwanza RVT&SC--
Mwanza (V)Karumo FDCKilimo, Useremala, Ushonaji na UashiUmeme, Udereva, Uvuvi, Ushonaji, Uashi, Useremala, Uungaji Vyuma, Umeme, Ufundi Magari, Utengenezaji bidhaa za Ngozi na stadi za sasa ziendelee.
SengeremaSengerema FDCWelding, Hifadhi za Mazao, Mazingira, UKIMWI, Kilimo na Udereva.Ujasiliamali, Usindikaji mazao ya Kilimo, Kompyuta, Uashi, Uvuvi, Umeme, Kuunga Vyuma, Uashi, Useremala, Ushonaji, Udereva, Makenika, Mama Lishe, Kilimo na Ufugaji.
14​
MbeyaRungweKatumba FDCUseremala, Umeme, Uashi, Ushonaji, Hotel Management, Biashara, UKIMWI, KilimoUmeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Kompyuta, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Udereva, Upishi, Hotel Management, Uashi, Umakenika, Kilimo, Ufugaji, Electronics na stadi za sasa ziendelee.
Mbeya (M)Nzovwe FDCUashi, Useremala, Ushonaji na Kilimo.Kompyuta,Elctronics,Umakenika, Umeme wa Magari, Umeme wa Majumbani, Udereva, Upishi na Hotel Managaement, Uashi, Uungaji Vyuma, Ufundi Bomba, Kilimo, Ususi, S/Kimu na Ujasiriamali
15​
PwaniKibahaKibaha FDCUseremala, Uashi, Umeme Majumbani, Ufundi Chuma, Ufundi Magari, Udereva, Upishi, Menejimenti ya Hotel, Ushonaji, Kilimo, mifugo na Ufundi BombaUfundi Viatu, Ufundi Magari, Kompyuta, Secretarial, Uchomeleaji na Ufundi Rangi na stadi za sasa ziendelee
KisaraweKisarawe FDCKompyuta, Udereva, Ufundi Magari, Kilimo, Ufugaji, Useremala na UshonajiUmeme, Ufundi Bomba, Upambaji, Kompyuta, Ujasiriamali, Useremala, Udereva, Ufundi Magari, Uhazili, Uchomeleaji na Ufundi Rangi
IkwiririIkwiriri FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Ufumaji, Kilimo, Mifugo, Mafunzo nje ya Chuo na Mafunzo ya Muda Mfupi.Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Kompyuta, Uchomeleaji, Udereva, Upishi, Hotel Management, Kilimo, Ufugaji, Ufundi Bomba, Uungaji Vyuma, Electronics na Umeme Jua na stadi za sasa ziendelee.
16​
TaboraSikongeSikonge FDCUashi, Useremala, Ushonaji na Kilimo.Kompyuta, Elctronics, Umakenika, Umeme wa Magari, Umeme wa Majumbani, Udereva, Upishi na Hotel Managaement, Uashi, Umeme, Uungaji Vyuma, Ufundi Bomba, Umeme wa Magri, Kilimo na Ususi.
UramboUrambo FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Ufumaji, Kilimo, Mifugo, Mafunzo nje ya Chuo na Mafunzo ya Muda Mfupi.Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Udereva, Upishi, Hotel Management, Udereva, Kilimo, Ufugaji, Kompyuta na stadi za sasa ziendelee.
NzegaNzega FDCUseremala, Uashi, Ushoni, Udereva, Kompyuta, Ufugaji na KilimoUmeme, Ufundi Magari, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Ufundi Rangi, Electronics, Uchimbaji Madini, Uashi, Umakenika, Ufugaji na Umeme
NzegaMwanahala FDCUseremala, Uashi, Ufundi Magari, Kilimo, Ufugaji, Ushonaji, Upishi na Lishe.Uumeme, Ufundi Magari, Ufundi Bomba, Upambaji, Kompyuta, Ujasiriamali, Useremala, Uashi, Udereva, Ufundi wa Friji, Upishi na Uendeshaji wa Migahawa
17​
TangaHandeniHandeni FDCUshonaji, Useremala, Upishi na Lishe, Uashi, Menejimenti ya Hotel, Umeme wa Majumbani, Ufundi Magari na KompyutaUjasiriamali, Kompyuta, Uchomeleaji, Udereva, Uhandisi wa Kilimo, Electronic, Ufundi Friji na Usanii
MuhezaKiwanda FDCUseremala, Uashi, Upishi na Lishe, Ushonaji na Kilimo, Ufugaji na UjasiriamaliUdereva, Ufundi Magari, Uashi, Ufundi wa Friji, Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Upishi na Uendeshaji wa Migahawa.
LushotoMabughai CDTI--
18​
RukwaMpandaMsaginya FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Mifugo, Ujasiliamali.Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Kompyuta, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Udereva, Upishi, na Hotel Management, Userermala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Ufugaji, Electronics na zilizopo ziendelee.
NkasiChalla FDCUashi, Useremala, Ushonaji na Kilimo.Useremala, Uashi, Ushonaji, Kilimo, Umeme na Computer, Ushonaji, Useremala, Uashi, Umeme, Uungaji Vyuma, Ufundi Bomba, Umeme wa Magri, Kilimo, Ususi S/Kimu na Ujasiriamali.
19​
RuvumaMbingaMbinga FDCUseremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Ufumaji, Kilimo, Mifugo, Mafunzo nje ya Chuo na Mafunzo ya Muda MfupiUmeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Kompyuta, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Udereva, Upishi, Hotel Management, Useremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Ufugaji, Electronics na zilizopo sasa ziendelee.
Songea (V)Muhukuru FDCUashi, Useremala, Ushonaji Kilimo, Ufundi Magari, Umeme na MifugoKompyuta, Elctronics, Umakenika, Umeme wa Magari, Umeme wa Majumbani, Udereva, Upishi, Hotel Managaement, Ushonaji, Uselemala, Ufugaji, Uashi, Uungaji Vyuma, Ufundi Bomba, Kilimo, Ususi, S/Kimu na Ujasiriamali.
TunduruNandembo FDCUseremala, Uashi na UshonajiKilimo, Ufugaji, Kompyuta, Uchomeleaji, Ufundi Bomba, Udereva, Upishi, Hotel Management, Useremala, Uashi, Ushonaji, Umakenika, Kilimo, Ufugaji na stadi zilizopo ziendelee.
20​
SingidaSingidaSingida FDCUseremala,Uashi, umeme wa nyumbani,ushoni, na upishi na lisheUfundi Magari, Udereva, Kompyuta, Menejimenti ya Hoteli na Utalii, Userermala, Uashi, Umakenika, Kilimo, Ufugaji na Umeme
IrambaMsingi FDCUseremala, Upishi, Ushonaji, Uchomeleaji Chuma.Kilimo, Ushirika, Ufugaji wa nyuki na Urinaji wa asali, Upishi na Lishe, Udereva, Ufundi Magari, Uashi, Udereva, Ufundi wa Friji, Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Upishi na Uendeshaji wa migahawa.
21​
ShinyangaShinyaga (M)Buhangija FDCUshonaji, Upishi, Ujasiliamali, Useremala, Umeme Majumbani, Uchomeleaji, Stadi za Maisha na Masomo ya Jioni.Mitambo na Magari, Ufundi Bomba, Udereva, Uashi, Kompyuta, Upambaji, Usindikaji Mazao, Umeme wa Magari, Umeme, Useremala, Ushonaji, Upishi, Uungaji Vyuma, Uashi, Kilimo, Ufugaji na Hotel Management na stadi za sasa ziendelee.
GeitaMwanva FDCUmeme wa Majumbani, Uashi, Useremala, Umakenika, Kompyuta, Udereva, Kilimo, Ushonaji na Welding.Ufundi Bomba, Ujasiliamali, Umeme wa Mgari, Electronics, Fitter Mechanics, IT, Ushonaji, Useremala, Uashi, Uhazili, Kompyuta, Ufundi Magari, Uungaji Vyuma, Umeme Majumbani, Ufundi Rangi, Uchoraji, Kilimo, Udereva na Ufundi Viatu.
MalampakaMalampaka FDCKilimo, Ufugaji, Useremala, Uashi, Ujasiriamali.Udereva; Kilimo; Ufugaji; Welding; Fitter Mechanics na Mv Mechanics, Ushonaji, Useremala, Uashi, Umeme, Mv Mechanics, Udereva, Catering & Hotel Management na Computer Applications
BariadiBaradi FDCUseremala, Kilimo, Uashi, Ushonaji, Udereva, Ujasiliamali, Elimu ya Biashara, Elimu ya Jinsia, Elimu ya UKIMWI na Uraia.Kompyuta, Umakenika, Ufundi Chuma, Uchmeleaji, Umeme wa Majumbani, Umeme wa Magari, Electronics, Udereva, Ufundi Magari, Useremala, Ushonaji, Upishi, Kilimo, Uungaji Vyuma, Uchongaji Vyuma, Ufundi Bomba, Uchoraji na Ufundi Rangi.


Ambatisho Na. 1: Mafunzo yanayotolewa katika Vyuo vya Ufundi Stadi nchini

S/NTraining AreaOccupations
1Building Construction1.1 Masonary & Bricklaying
1.2 Capentry & Joimery
1.3 Plumbing & Pipe Fitting
1.4 Painting and Decoration
2Metal Work2.1 Welding and Fabnrication
2.2 Blacksmithing
2.3 Fitter Mechanics Work
3General Maintenance and Mechanics3.1 Motor Vehicle Mechanics
3.2 Agro – Mechanics
3.3 Motor Cycle/Bicycle Maintenance
4Electrical Installation4.1 Domestic Electrical Inatallation
4.2 Telecommunications
5Clothing and Textile5.1 Tailoring
5.2 Tie and Dye
5.3 Batik
5.4 Handloom Weaving
6Agriculture and Food Processing6.1 Crop Production
6.2 Horticulture
6.3 Floriculture
6.4 Meat Processing Technology
6.5 Mushroom Production
6.6 Dairy Production
6.7 Wine Making
6.8 Poultry Production
6.9 Vegetable Production
6.10 Vegetable Processing
6.11 Animal Husbandry
7Hotel & Services7.1 Food Production
7.2 Food & Beverage Services
7.3 House Keeping
7.4 Front Office
 
Back
Top Bottom