World Cup 2010 SA: Match updates (From June 11)

I have given up, will not predict anymore... Oosh!
 

Wilting under presha!
 
Ndahani mbona wewe sio katika wachezaji pale, au hata hiyo timu ya nchi ya nchi yako haimo katika hizo?

Usidharau kazi za wenzio, kwani "mzigo wa mwenzako kwako kanda la usufi". Wanaotazama mpira huwa mahodari zaidi ya wale wachezaji waliopo uwanjani.
 
Siri ya Ushindi wa Ujermuani iko mikononi na puani mwa Joachim Loew!

 
Last edited by a moderator:
Chancellor wa Ujerumani naye hakuweza kujizuia kushangilia mabao pale uwanjani. Naona vijana wakichukua kombe watapata zawadi nono kutoka kwa serikali yao.
 
msiwakose spain mabingwa wa euro 2008 saa 3 na nusu kwa saa za tz wapo uwanjani,ndio mabingwa wapya,ujerumani anachapwa tu nusu na spain hilo wanalijua wazi.
 
Mimi aliyenikosesha usingizi ni Mensah na yule dogo, ambao walitoa pasi kwa kipa badala ya kupiga penalty. As for Asamoh, well yeye ndiye ameifikisha Ghana Q/final, literally. Amefunga magoli 3 kati ya 5 ya Ghana. Amepiga jumla ya penalty 4 kakosa 1. Hii ni record nzuri, anahitaji pongezi.
 

Tusibiri Blatter aiombe Ghana (na Africa) radhi. Najua ingekuwa ni England au Italy, hili lingezungumzwa sana sana
 
Kulingana na matokeo haya inaonyesha kuwa Ghana ilikuwa ni timu bora sana kuliko at least Argentina, England na Australia; Ghana iliwafunga Serbia ambao waliifunga Germany

Round 1 Group D:

Germany-Australia 4-0

Germany-Serbia 0-1

Germany-Ghana 1-0


Round 2
Germany - England 4-1

Quarter Finals

Germany - Argentina 4-0...

...
 
Najua companero na denovo hawataonekana, hao argentina wamefika hapa kwa kuunga unga tuu. Kundi lake lenyewe lilikuwa rahisi hehehe leo ni furaha tuu, hakuna mtu aliyekuwa anataka kumuona Maradona akikimbia bila nguo.
 
msiwakose spain mabingwa wa euro 2008 saa 3 na nusu kwa saa za tz wapo uwanjani,ndio mabingwa wapya,ujerumani anachapwa tu nusu na spain hilo wanalijua wazi.

Mkuu kwa mwaka huu Spain hawana timu tishio ya kuifunga Ujerumani, waishie tu huo mwaka 2008.
 
nilijua tu,sasa wengi wamehamia germany,sisi spain toka mwanzo mgumu mpaka mwisho kazi kwelikweli
 
Chancellor wa Ujerumani naye hakuweza kujizuia kushangilia mabao pale uwanjani. Naona vijana wakichukua kombe watapata zawadi nono kutoka kwa serikali yao.

Dah, sikujua kuwa hata huyu mama Anjela naye alikuwa pale uwanjani. Najua checkbob Klintoni alihudhuria mapambano karibu yote ya USA.
Kumbe ku-host world cup ni investment kubwa sana, kwa sabau watu heavyweight kama hawa wanakuja na ujumbe mzito sana ambao hutumia shilingi zao nyingi sana wakiwa nchini.

Inabidi Tanzania tuplani kufanya hivyo pia katika kipindi cha miaka 15 ijayo - tuandae world cup ya mwaka 2026.
 
KInachoshangaza ni kuona Messi anaungana na ''miungu watu'' akina Rooney & Drogba kwa kutofunga hata goli moja.
 
Hehehe kichuguu inabidi tuanze na AFCON kwanza kabla ya kupeleka maombi ya World Cup hivi tukiungana na nchi zote za great lakes tutashindwa kuandaa AFCON? Dah leo nina furaha sana kwa kutolewa Argentina.
 
semeni hivyohivyo spain sio tishio,mnababaika na germany kuwafunga england na argentina bao 4,4 tusiongelea mate,watatafuta mpira kwa tochi wajerumani wakicheza na spain,spain inafungwa na timu ndogondogo vigogo wote ulaya kafunga mechi 35 mfululizo hajafungwa,kapita kwenye group lake kuja bondeni kashinda mechi zote home and away,tusubiri tusiongee sana.
 
Kisa , mkasa na maana?
Ujiue sababu ya mpira? Huu ni ubinafsi na ujinga wa hali ya juu! Watamwambia Mungu wameharakisha kurudisha namba kwanini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…