Kitu gani kinakuashiria kama Germany anamfunga Argentina?Kuifunga Brazil ya Benard na Fred au?Mbona walisumbuka sana kwa Ghana,Algeria,USA na France?
Messi anaimaliza mechi hii dakika ya 45
wajerumani walikuwa na hofu na ghana, algeria kwa hiyo hawakucheza kwa confidence walicheza kwa tahadhari zaidi kuepuka
kashfa ya kufungwa na timu ya africa..
Ghana hawaku-take advantage ya uoga wa german. Wachezaji wengi wa hii timu ya ghana walikuwemo kwenye vikosi vyao vya U21 ambavyo vilifanya vizuri sana kwenye WC ya U21, German wanatambua hilo.
Algeria waliwafunga German zamani, wakati huo German walikuwa na timu kali mno, kwa hiyo algeria walijua kuwafunga german inawezekana hivyo walikuwa na confidence na ile mechi algeria alicheza vuzuri kuliko mechi zote, na german walijua kwanba kufungwa na algeria inawezekana. Ukumbuke pia mpira ni psychological sometimes.
Kuhusu France: Defence ya France ukiangalia vizuri wanavyocheza sio rahisi hivyo kupenya, wanajipanga vizuri sana kwenye ku-defend, ingawa individually watu wanawadharau. Kama france wangekuwa na mfungaji mwingine wa kueleweka zaidi ya Benzema german wangeweza kutolewa.
Argentina ni wazuri isipokuwa wanaonekana nguvu zao kubwa zipo kwa messi , di maria na higuain. Wakati German nguvu zao zipo kwa wachezaji wao 11 wanaokuwepo uwanjani.
Nionavyo mimi, uchezaji wa argentina, brazil, colombia, chile, costarika unafanana. Sasa tusubiri tuone hiyo jumapili.
Messi hatokuwa na kazi rahisi kama unavyofikiria.