World Cup 2014, Brazil: June 12 - July 13

World Cup 2014, Brazil: June 12 - July 13

We acha tu Mkuu mie leo siku yangu bomba sana nimefanya shughuli zangu chap chap ili kuhakikisha naona mpira huu kwa kituo, halafu kunakuwa na midabwada kama hii dakika 26 tu mechi imekwisha!!! Dah!!!

Nilikuwa na furaha leo siku nzima, mambo yalikuwa bumbum kheee, sikujua kama Brazil wataniharibia siku kirahisi hivi.
Tena ndani ya dakika chache, aaah hii ni historia mbaya wamejiwekea, tena home kwao.
Ndio itakuwa habari ya dunia hii.
 
Yaani kiukweli tusiwapende Wajerumani, sio watu wazuri kabisa hawana huruma hata kidogo haiwezekani wafanye hivi kwa magoli 2 waliyofungwa 2002

Mkuu unajua maana ya kisasi? Yaani kisasi kibaya we kisikie tu kwa jirani.
 
possession 56% kwa 44%
complete passes 234 kwa 173
shots 10 kwa 2
shots on target 7 kwa 0

ALL IN FAVOR OF GERMANS.....BADO TU UNAONA HAWAJAZIDIWA??? kama ingekuwa boxing hii ingekuwa TKO

Naah hawajazidiwa kivile bana....hilo nakataa kabisa.

Brasil wamechemka mno kwenye defense na kuwapat fursa hao Wajerumani na kufunga magoli tu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Halafu hata Ujerumani yenyewe si kali kivile....walipekekeshwa na Ghana....Algeria .....hata Ufaransa waliwafunga goli moja tu.

Nini hii leo? Khaaaaaa!!!

Heri hata Chile au Colombia wangeingia nusu fainali......

This is surreal......

Mpira,wa Brazil wa kukimbia sana,wa,kizamani...siku hizi ni technic na tactics
 
Breaking news...>>brazil wametangaza hawatarudi kipindi cha pili.
Source ni mimi mwenyewe.
 
mkuu kuna wakati mtu huwa anaomba baadhi ya matukio yawe ni ndoto tu au hadithi tu, unaomba uzinduke uone kilichotokea sio kweli ilikuwa ni haditi tu au ndoto. mfano ni match ya leo, yaani unaomba mpira uwe ni kama vile bado haujaanza na matokeo ni bila/bila.
cc Pasco

We have a God that can turn results
 
Pazi leo atakuwa na mshiko mkubwa hapo alipo anasubiri mechi iishe aende kupokea chake, DonDonald
 
Naah hawajazidiwa kivile bana....hilo nakataa kabisa.

Brasil wamechemka mno kwenye defense na kuwapat fursa hao Wajerumani na kufunga magoli tu.

Technics na tactics...unakumbuka Spain walifungwa 5 na uholanzi?
 
Back
Top Bottom