WW1, WW2 na kinachoendelea sasa Middle east vilipangwa mwaka 1871 kama barua hii ni kweli

Mseza mkulu na eiyer,mie naomba ufafanuzi kuhusu pembe kumi katika kichwa cha mnyama na kung'oka tatu na kuibuka pembe moja ndogo yenye kunena,je hayo mataifa kumi ni yepi na hayo saba yaliyobaki katika dunia ya leo ni akina nani?
Na pia naomba kueleweshwa kwa nini marekani inahusishwa na unabii wa siku za mwisho ilhali wakati wa mipango hiyo haikuwa superpower?
Ndugu mseza mkulu,huwa napata hisia chanya kuhusu existence ya hawa machotara ya shetani na binadamu kutokana na hoja za eiyer kwa sababu kuu moja. Ukiangalia mtiririko wa huo mpango wao wa kuitawala dunia haionyeshi unufaikaji wa hawa viongozi wa dunia (katika hali ya kiuanadamu) kutokana na end point ya huu mpango,lakini kwanini wanashiriki kama sio kweli nao ni sehemu ya hiyo jamii inayopingana na Mungu? Hii inanipa wasiwasi kama wao ni sehemu ya hawa machotara ndio maana mwanzo 6 Mungu anasema hatawaangamiza hadi pale watakapouona uharibifu waliouleta duniani.
 
Mkuu Eiyer, za siku tele nakuona bado unakomaa na mada hahahaah....
 
It's all true and is about new world order, religion unification for sake of fake peace and unity!! And roman catholism under papacy are match maker and the master mind! But the Bible warns about this,through the Revelation,,!!
 
Binafsi ninaamini vita vinavyoendelea vinamahusiano makubwa sana maisha ya kiroho ya wakazi wadunia na hatima ya dunia,,kweli vs truth , uovu(dhambi) vs mema!
 
Nimewafuatilia vya kutosha kwa masaa kadhaa nimeishia page ya 10, nitarudi kumalizia hiki kiporo.
 
Mimi kuna kitabu Fulani nilisoma kinasema ni vita kati ya binadamu wafuasi wa mpinga kristo ambao ni malaika wa kuzimu na malaika wa mbinguni na vitapigana muda wa siku moja tu katika bonde la Megiddo sasa sikuelewa uwezo wa binadamu kupigana na viumbe wa ajabu utakuwaje na huyu mpinga kristo ni binadamu au? Na atakuwepo lini
 
Sawa mkubwa, naomba nikuhoji wewe. Tofauti na Plato,umeshamsoma mwana falsafa mwingine mkubwa yupi?
Unafahamu Aristotle alikua mwanafunzi wa Plato lakini anapingana nae kwa zaidi ya 90%?
Ukisoma post yangu ya kwanza utapata jibu la hili swali lako....

Pia,ungekuwa unawafuatilia hawa "watu" ungeelewa hicho unachokiita "kupingana" kwa Aristotle na mwalimu wake kuwa ni danganya toto tu,ni kama vile unavyoamini kuwa kuna vita na kutokuelewana kati ya Urusi na Marekani....
Unafahamu watu wawili pekee waliopewa cheo cha "Father of knowledge" katika historia ya dunia?
Sijui,lakini pia sioni umuhimu wa kujua hili kwasababu najua sana hii mipango na lengo lake....

Ni sawa na unioulize kama nawajua matajir watano wa dunia wakati nijuavyo mimi huo ni uongo tu....
Unafahamu Plato alikua hapendi kujihusisha na siasa (mathalani hapa tuongelea siasa za anga tofauti ambayo jamii zetu hazitambui)?
Hata kama nikijua,hili sijaona lina umuhimu gani kwangu kwasababu ambazo nimeshakueleza hapo juu....

This world is full of lies mkuu....
Wewe una amini nini kuhusu vita, United Nations(na vitengo vyake), IFM na World Bank?
Soma mada utapata jibu la hili swali lako mkuu....
 
Ukiisha iita historia fake maana yake uiite bibilia pia fake.
Kabla hujaniambia niseme hiki unachonitaka niseme unachopaswa ni kuunganisha ukisemacho na biblical prophecies ndipo uniambie haya.lakini unapodai tu haya madai yako bila kufanya ninachokutaka ufanye ni kupoteza tu muda....
Unatoa madai bila hata kusema ni kivipi unasema hivyo....

Huo mtiririko wa unabii wa Biblia kwenye Danieli 2 unahusiana nini na unachokisema hapa?
Katikati ya Roman Empire Alizaliwa yesu. Evidence Luke 2:1 Kaisali Agustus alipotoa agizo sensa ifanyike kote duniani enzi hizo palipokuwa chini ya Roma ikiwepo na Middle east.
Hii sensa ilifanyika dunia nzima mkuu?

Mbona unaongeza chumvi sana?

Pia,haya nayo yanahusiana nini na unachokisema?
Ukisema Ni uongo itabidi useme pia Kama baada ya Babylon, Akaja Medo-persia, Akaja Greece chini ya alexander ni Ufalme gani uliofuata kama Mungu alitabiri kupitia daniel na falme zilikuwa sequential?
Hakuna mahali ambapo Mungu alisema kutakuwa na tofauti ipi ya miaka baina ya ufalme mmoja na mwingine...

Kama kutakuwa na tofauti ya wiki moja au hakutakuwa na tofauti hata ya siku moja baina ya ufalme A na ufalme B hii haimaanishi pia itakuwa hivyo baina ya ufalme B na C au C na D,hili ndilo tatizo kubwa sana kwa ninyi ambao mnauhusisha unabii huu na Rumi....
Moja:Unapaswa uwe makini sana kwenye maswali ninayokuuliza kwasababu sikuulizi kwasababu sijui bali nakuuliza ili nipate ufafanuzi kwako kuhusu suala husika ili nione kama unatumia mantiki au sivyo hivyo usidhani kwamba nauliza kitu nisichokijua...

Mbili:Ishu ya kuhusishwa kwa ufalme wa nne kwenye sanamu ya Danieli 2 na miguu miwili ni assumtion tu na jambo hilo halipo kwenye maandiko.Mungu anapotaka kukitolea kitu maelezo huwa anakuwa wazi,tazama Danieli 2:42,hivyo kwasababu Mungu hakutaja suala la miguu kuhusiana na ufalme ule wa nne basi hili suala la wewe na wenzako mnaokubaliana na hiyo fasiri yenu ya unabii siyo sahihi ni asumption yenu tu na tunawaachia ninyi wenyewe....

Tatu:Kosa kubwa kabisa ambalo huwa mnalifanya wewe na hao wanaokubaliana na hii fasiri ya unabii wenu wa Danieli 7 na 2 ni kudai kwamba Rumi ilianguka mwaka 476 wakati ufalme ulioanguka mwaka huo ni Rumi ya Magharibi tu.Rumi ya mashariki haikuanguka mwaka huo na iliendelea hadi karne ya 13 huko ikaja kuangushwa na Ottoman Empire kule Istanbul Constantinople] hivyo madai yenu hayapo sahihi...

Rumi ya mashariki ilianguka mwaka 1453 soma hapa Byzantine Empire - Wikipedia

Nne:Unabii wa Danieli 7 kuhusu mnyama wa nne na pembe zake unazungumza kinyume na usemacho.Malaika alipokuwa akimpa ufafanuzi Danieli juu ya pembe za mnyama wa nne alisema "hao ni wafalme watakaoinuka kwenye ufalme huo" hakusema "hizo ni falme" zitakazoinuka katika ufalme huo kwa sababu unaposema pembe zile ni nchi unakuwa unamaanisha hizo ni mamlaka ambazo kiunabii ni falme na hazihusiano kabisa na ufalme husika wakati siyo kweli kama unabii unavyosema....

Danieli 7:24

24 Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.


Kwa context ya ufafanuzi huo wa unabii kutoka kwa malaika ni kwamba hao wafalme kumi ndiyo watakuwa wanaongoza ufalme huo wa nne na mmoja ataibuka ambaye atakuwa tofauti na wengine ambapo atawaangusha wafalme watatu na siyo kuobndoa falme tatu kama tafsiri yako inavyosema,kwa maana hii ni kwamba haupo sahihi kabisa mkuu....
 
Hii vita ya tatu unachoongea ni uongo mtupu unaoutaja katika barua yako
 
mkuu nitakitafuta hicho kitabu kwa kuwa leo umeni jibia swali langu la muda mrefu mi mwenyewe nilikuwa najiuliza maswali kuhusiana na uongozi wa marekani kwanini kila siku ni democratic,republican kila siku vyama hivi vinajirudia nahakuna siku hata moja kilichowahi kuongoza mara mbili kati ya vyama vyote hivi leo kidogo nimeelewa.ubarikiwe
 
Sikukupa mstari kutoka kwenye kitabu kitakatifu cha Biblia kukuonesha hili na ukashindwa vibaya sana kutetea hoja yako?
Aliyesema kuwa ukubwa wa Goliati ndiyo sababu ya mimi kusema ni Mnephil ni nani?
Phil Sneider: Kaona yeye,kasimulia yeye, mazingira yote ni uzushi,Sio usahisi ule ndio maana hata wewe unatilia shaka baadhi ya sentesi zake na umegome kuziendorse.
Hadi sasa Hujatoa ushahidi wowote mkuu.
Moja:Sikumleta hapa Phill Schneider kwaajili ya kuthibitisha Wanefili,hii inaonesha ni namna gani hauko makini na ninachoandika hapa mkuu...

Pili:Nilisema ni kwenye maelezo yapi sikubaliani naye na kwaanini na siyo kwasababu unayoileta hapa,acha kuzusha mkuu,sema tu ukweli hata kama hutaki...

Tatu:Ni uongo mkubwa kusema mazingira yote ni uzishi wakati hujafanikiwa hata kuonesha angalau jambo moja tu ambalo ni uongo,tangu umeanza kumjadili huyu jamaa umekuwa ukirusha shutuma kuwa ni uzushi na uongo bila hata kujenga hoja ya unachosema,hii ni mbaya sana mkuu...
Ujue wakati mwingine hadi napata uvivu kuandika na kujibu maana ni kama sijui husomi ninachoandika au inakuwaje...

Nilikuonesha kwa kujenga hoja namna ambayo binadamu wa kwanza na huyu wa sasa wana tofauti kubwa sana ya kiuwezo,lengo na kukuonesha hili ni kutaka uone vile ambavyo umekubali uongo wa kwamba dunia sasa ina maendeleo makubwa na maendeleo haya yameletwa na mwanadamu tu.Nikakuuliza kwamba,kama Adamu,kwa namna nilivyokuonesha,alikuwa bora mara millioni zaidi ya mimi na wewe,alishindwaje kufikia haya maendeleo halafu wewe ambaye ni dhaifu zaidi uyafikie? Hili nilikuwa nataka tu uone uongo uliopo ili uanze kufikiri zaidi...

Hapo sijazungumzia mambo mengine ambayo nayo nilikuonesha kukufabnya uelewe ninachokuambia....

Pia,pamoja na kusema yote hayo sikuwa na maana kwamba binadamu amekuwa kama kondoo asiyeweza kitu,jambo hili nimekuambia huko nyuma lakini sijui ni kwanini huelewi na unakuja kusema hapa kwamba naweza hata kumsema @Maxence Mello kuwa ni hybrid kwasababu tu amebuni hii forum.Hii niseme kabisa kutoka ndani ya moyo wangu kwamba imenisikitisha sana maana kama maelezo yote yale ndiyo unaelewa hiki siyo siri napata wasiwasi kama hata kuna ambacho unacho gain hapa...

Ninachotaka uelewe na wengine wakielewe ni kwamba,binadamu ana akili lakini siyo ya namna hii na haya maendeleo yote,kuna msaada kutoka nje ya mwanadamu huyu....
Mkuu,sasa hakuna Mpinga Kristo bali kuna roho ya Mpinga Kristo ambayo inafanya kazi ndani ya watu.Mpinga Kristo kama kiongozi mkuu wa dunia hayupo kwa sasa...

Hujanielewa kuhusu waaminifu wa Mungu na kuwepo kwao wakati wa Mpinga Kristo,hili tuliache kwanza,lakini ninachotaka kukueleza ni kwamba ulichodhania kuhusu ninachoamini juu ya hili siyo sahihi....
 
Karibu sana mkuu.....

Tuendelee kujiuliza tu maswali tutapata majibu mengi sana mkuu.....
 
Hii vita ya tatu unachoongea ni uongo mtupu unaoutaja katika barua yako
Uongo ni kusema jambo fulani ni uongo bila kusema ni uongo kwa namna gani....

By the way,mtoa mada hajaandika barua yoyote ile,kusema "barua yako" ni kumzushia uongo tu na hili linakufanya uendelee kuonekana muongo na mzushi....
 
Niliwahi kusema kwamba hizi silaha ambazo zinaundwa kwa sayansi ya kutisha kabisa siyo kwaajili ya mwanadamu,yaani siyo kwaajili ya kumdhibiti mwanadamu maana hata sasa anadhibitiwa tu.....

Kwa namna ninavyoona huyu Mpinga Kristo hatakuwa mwanadamu kamili kama mimi na wewe,hili naendelea kulifanyia utafiti mkuu....

Kipindi ambacho atakuwepo kimeelezwa kwenye biblia,ni wewe na mimi kusoma unabii huo na kufuatilia matukio ya duniani tuitajua....
 
Hapo nimepata picha, lakini vip kuhusu hii ya Gog and Magog nayo ipo katka mlolongo wa hawa jamaa?
Kwa namna ninavyoona ipo kwenye mlolongo wa hawa jamaa mkuu....
 
Mkuu,kwa mujibu wa ninavyojua mimi zile pembe kumi siyo mataifa kumi maana hiyo iko kinyume na unabii wenyewe,hili nimelielezea kwenye post moja hapo juu....

Sina uhakika kama Marekani ipo kwenye unabii wa siku za mwisho japokuwa wapo wanaoihusisha na unabii wa nabii wa uongo,kuna rafiki yangu mmoja anamsimamo kama huu na kila siku tukipata muda huwa tunalijadili lakini kadiri siku zinavyoenda anaonekana kuanza kuuona uongo wa jambo hilo....

Marekani haiwezi kuwa nabii wa uongo maana masuala ya kinabii yana uhusiano na masuala ya kiroho na Marekani ni nchi na hivyo inahusiana na masuala ya kisiasa...

Kwenye suala hili,watakuwepo binadamu lakini hawa hawatakuwa wanajua chochote juu ya uhalisi wa end game ya hili suala,ni sawa na ukutane na Mason wa degree ya tatu halafu ajue Mason ni nini na ipo kwaajili ya nini,haipo hiyo,sanasana atakueleza juu ya sababu chanya alizoambiwa kuhusu Freemason ambazo siyo lengo halisi la Freemason...
Hii inanipa wasiwasi kama wao ni sehemu ya hawa machotara ndio maana mwanzo 6 Mungu anasema hatawaangamiza hadi pale watakapouona uharibifu waliouleta duniani.
Shukrabnn kwa kunikumbusha hili nan nitaliangalia lipo kwenye mstari wa ngapi maana hapa ndipo tunakuja kuona "creation" ya majini.....
 
Dahh kaka pole, kama umeshindwa kutambua kwamba Solomon alikua na maarifa na hekima zaidi ya Adam basi bado unaamini huyo Adam alituzidi akili pia!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…