WW1, WW2 na kinachoendelea sasa Middle east vilipangwa mwaka 1871 kama barua hii ni kweli

WW1, WW2 na kinachoendelea sasa Middle east vilipangwa mwaka 1871 kama barua hii ni kweli

Nimefuatilia sana majibu yako unavyomjibu mleta mada,kwanza kabisa nafahamu atakakuwa ni mtu aliyesoma wala siyo mbumbu flan hivi,kinachonisikitisha ni kwamba shule yake haina tofauti na wasomi wengi waliopo hapa Tanzania,hasa maprofesa wa Tanzania.

Kifupi ni kwamba,binadamu wa sasa si bora kabisa ukilinganisha na binadamu wa kale,maisha yamekuwa mafupi mno,maradhi yameongezeka sana,kufikisha miaka 50 ni ishu,kila mtu ni mgonjwa,mfano kama mtu hana HIV basi atakuwa anasumbuliwa na kisukari,kama hana kisukari ana uvimbe tumboni,kama hana uvimbe tumboni ana presha,kama hana presha ana vidonda vya tumbo,kama hana vidonda vya tumbo ana homa ya matumbo,UTI ,kama hana UTI ana malaria,kama hana malaria ana kansa ya tezi dume,fistula,watoto wenye utindio wa ubongo,vyakula vya asili vimepotoea na vingi vilivyopo ni feki hatari mtupu,kwa hiyo binadamu wa sasa ni dhaifu sana kimwili na hata kifikira,hii wala haihitaji kwenda shule sana ili kulitambua hilo.
Nimekupata vizuri mkuu....

Haya yote yanasababu wala hayapo hivi hivi tu na ni matokeo ya hawa viumbe ambao nimekuwa nikiwasema hapa maana wana lengo lao.....
 
Kama tumefanyiwa kama kwenye kitabu cha Plato The Republic, ama kama ni kweli kuna master puppeteers wanaotuchanganya akili na all thaat has been said kwenye huu uzi. kama ni kweli,
kwenye hukumu ya siku ya mwsho, ntakua na kosa gani wakati most of my choices were already limited by some men who thought they are mightier than God.

Why would God judge a blameless victim??
Nani ana nguvu kuliko Mungu?
 
Sio einstain tu mkuu kuna wajerumani Wanasayansi ambao ilibidi US waandae Special operation Katikati ya vita ww2. Kikosi maalumu kiliandaliwa kiwatafute popote walipo mafichoni ili waje kuwa hazina ya marekani. Matokeo yake 1969 Apollo ikatua Mwezini (ingawa hili huwa linachangamoto).
440px-Project_Paperclip_Team_at_Fort_Bliss.jpg

bumper8_launch-gpn-2000-000613.jpg

Matunda mazuri ya Operation Paperclip
Mungu wangu,unaijua vyemna operation paperclip mkuu?
 
Adam alikuwa wa kawaida sana. Jamaa anachanganya Umri na Akili au uwezo wa mwanadamu kubadili mazingira yamnufaishe.
Labda nikuulize swali rahisi sana tena sana....

Copy na original ni kipi kinakuwa bora?
 
Labda nikuulize swali rahisi sana tena sana....

Copy na original ni kipi kinakuwa bora?
Mkuu majuzi ile ulisema utaleta uzi hapa JF kuhusiana uwepo wa vatina na upapa kwamba unamchango gani juu ya maisha ya mwanadamu,nini hasa mission ya upapa na vatikan.

Kingine ningependa kukuuliza ni ni kwamba,Tanzania na dunia kwa ujumla sasa hivi tunashuhudia wimbi kubwa tena kubwa sana la wachungaji wanaoponya mgonjwa mbalimbali hii nini,makanisa yao ni ya uponyaji na miujiza na kuwaombea watu wapate utajiri hivi ni vitu gani?,je ? hawa ni manabii wa uongo?,hizi ni biashara? au tupo siku za mwisho?
 
Umeeleza mengi, ila kuhusu hao jamaa chotara naona nikuache uendelee nao. Maana hata ulipoombwa utoe Muhutasari wa WHo are they, How are they going to impliment NWO, What is their purpose, Ni faida gani kwa Waliowaunga mkono watawapata. Mfano wa chotara mmoja anayeishi na watu dunai ya sasa Hadi kesho hujaweka muhutasari hawa hizo stori kwa maarifa macache ya punje ya mchanga uliyonayo kama ulivyotufahamisha. Goliath pamoja na wewe kumuhusisha na WANEPHILI/AU CHOTARA VYOVYOTE UTAKAVYO na Kwa maelezo yako tulitegemea Goliath awe na uwezo mkubwa wa kufikiri kuliko hata wale kaka zake daudi na wayahudi wote. Cha ajabu Goliath kuonyesha Utaahira wake alivua Helment wakati anapigana na mtu mwenye jiwe. Golath alikuwa mbumbumbu kuliko hata mwanadamu wa kawaida.

SWALI: Niwekee kitu ambacho unaamini mwanadamu hawezi kubuni hadi kubuniwe na HYBRID au ALIEN? Kama ni Kombola la SATAN 2(Sarmat intercontinental ballistic missile). Hizo Idea Nicola tesla alizidemnstrate kitambo sana hadi akataka kupewa tenda na British loyal navy awatengenezee long range missile kwa idea zake za Wireless transmission. Hicho kitu pia ni development ya kazi ya Wernher von Braun's ambae document zake nyingi zilikuwa smuggled US na USSR katika Espionage war at the eve of WW2.
Nimeshasema hapa ni kwa namna gani watakwenda kuisimamia na kuifanikisha hii NWO,naona una tatizo la kusahau mkuu....

Wanaowaunga mkono ni watu wasiojua ukweli wa wakifanyacho hawa isipokuwa wachache ambao wamezawadiwa maisha ya kibilionea hapa duniani.....

Hawa machotara wa Kishetani wanaishi kwa kificho sana ili wasijulikane na iwe siri na jambo lisiloweza kuaminika na hii ni sababu ya hata wewe kukana hapa.....

Hata hiki ulichokiandika hapa kumhusu Goliath kinaonesha ni namna ipi binadamu tuna tatizo la kufikiri.Kwanza Goliath alikuwa na urefu wa futi 15 na pengine zaidi,sijui kama hata unajua futi kumi na tano ni nini maana yake,alikuwa na uzito wa zaidi ya kilo 500,Daudi inakadiriwa alikuwa na futi 6 hadi 7,binadamu mwenye kiwango cha Goliath anaweza kutioshwa namna ipi na binadamu wa kawaida hata kwa akili ndogo tu ya kawaida? Hakukosea kutoa kofia ya kichwa kwaajili ya kujilinda maana alijua hata hilo jiwe la Daudi lisinge mdhuru hata kama Daudi angelirusha kwa nguvu gani,ni sawa nba wewe upigane na mtoto wa miaka 7,uitamsambaratisha tu hata kama atakuwa na mawe.Usichokijua tu ni kwamba jiwe la Daudi lilimuua Goliath kwasababu ya Mungu na siyo kwasababu lilikuwa na kasi na usito mkubwa,sijui ni kwanini huoni hili jambo la kawaida kabisa.....

Sijui kama unaweza kupna makosa ya swali lako la kutaka nikuoneshe kitu kimoja ambachpo binadamu hawezi kutengeneza.Hivi nikikuambia tu kuwa bibnadamu hawezi kutengeneza tarakilishi [computer] utawezaje kupinga hili kwa mfano? Hebui nijibu halafu nitakuonesha matatizo kwenye swali lako hili....
 
Mkuu majuzi ile ulisema utale uzi hapa JF kuhusiana uwepo wa vatina na upapa kwamba unamchango gani juu ya maisha ya mwanadamu,nini hasa mission ya upapa na vatikan.

Kingine ningependa kukuuliza ni ni kwamba,Tanzania na dunia kwa ujumla sasa hivi tunashuhudia wimbi kubwa tena kubwa sana la wachungaji wanaoponya mgonjwa mbalimbali hii nini,makanisa yao ni ya uponyaji na miujiza na kuwaombea watu wapate utajiri hivi ni vitu gani?,je ? hawa ni manabii wa uongo?,hizi ni biashara? au tupo siku za mwisho?
Sikusema nitaleta bali nilisema nitaangalia nitakapokuwa na muda nitafanya hivyo kwa siku za usoni mkuu.....

Ishu ya wachungaji na kuponya maradhi ni ishu ya kinabii ambayo imeandikwa kwenye Biblia,hii haipo Tanzania tu bali dunia nzima....
 
Naomba nitoe muhutasari wa bandiko lote hili.
Ili twende sawa tutofautane kwa hoja jengefu. Nimetoa Msimamo na Uelewa wangu kuhusu Daniel 2, 7 kuwa ni vitu vinaendana. Msimamo huu ndio ulikuwa msimamo wa waprotestant wote kabla hawajachakachuliwa sasa wakiwemo waldenses, hussites, wycliff, martin luther, john gill, baptist theoregians, tyndale, na wengine wengi na mimi naungana nao mkono pasipo shaka. Ndio maana wao walienda mbali hadi kuziweka sanamu hizo makanisani na viongozi wao akiwemo na kiongozi wa Rumi enzi hizo kaisari. Luther alitamka wazi kabisa kuwa anti christ ni nani.

Picha.
N%C3%BCrnberg_Rathaus_(The_Town_Hall)_4.jpg


Sasa nikuombe kitu kimoja.
Eleza vyote unavofahamu kuhusu Daniel 2, 7 then nijue naongea na mtu anayeamini nini, naona kama unmarukaruka na kupita pembeni. Pia nitakueleza hata mwanzilishi wa hicho unachoamini maana nimeshapata mwangwi wake na kwa nini aliiweka hivyo.
Mwanzilishi wa ninachoamini? Kwanini unadhani kuna mwanzilishi tofauti na mimi mwenyewe? Sikumbuki kusoma mahali kuhusu hiki nilichokuambia,kama kuna mtu ana mtazamo kama wangu basi jua tu tumefikiria kitu kinachofanana na siyo kwamba nimetoa kwake....

Bahati mbaya naona hujui kuwa unabii hautegemei nani anaona nini,kitendo cha waprotestanti kuwa na msimamo huo hakuufanyi uwe sahihi.Nilianza kuona uongo wa hii fasiri ya unabii siku nyingi sana bila hata kupata ushawishi kutoka kwa mtu yoyote....

Nimekupa changamoto tu ya pembe kumi ambayo inaonesha matege ya hii fasiri yako lakini naona hutaki kabisa kunielewa na unataka nieleze Danieli 2 na 7 yote sijui kwa sababu ipi....

Wewe na wenzako mnasema kwamba pembe kumi ni ni yale mataifa [falme] kumi yaliyopatikana baada ya Rumi kuanguka [japokuwa hata hili nalo siyo sahihi na nilikueleza ni kwanini],nikakuambia kuwa unabii unasema pembe kumi siyo mataifa [falme] bali ni viongozi wa mnyama husika,lakini hili umeskip tu halafu unataka nikueleze tena.

Unasahau sana sijui au ni nini.....
 
Tangu niliposoma na kujua alichokuwa anakimaanisha Plato kwenye kitabu chake cha Republic hasa kwenye story yake ya Allegory of the Cave ndiyo nilianza kuelewa kabisa hasa tunaishi kwenye dunia ya namna ipi....

Kimsingi,watu wote ambao leo tunawachukulia kama "majiniaz" walipata ujuzi waliokuwa nao kutoka mahali fulani,Mesopotamia huko.Pythagoras,Socrates,Galileo,Alexander the Great,Plato na hadi hawa akina Sir Francis Beacon na John Dee ni watu ambao walipata elimu hizi tofauti kabisa na wanafunzi wengine waliikuwa kwenye madarasa ya watu hawa....

Socrates aliwahi kumueleza mwanafunzi wake mmoja aitwaye Plato kwenye madarasa yao kwamba,elimu anayowapa ni elimu iliyoko kwenye makundi mawili.Kunsi la kwanza ni lile la kawaida ambalo wanapewa elimu ya kawaida kuhusu mafuzo waliyokuwa wanapewa na kundi la pili ni lile ambalo linapewa elimu maalum na nyeti ambayo hakupaswa kupewa mtu yoyote na ni elimu maalum ambayo ndiyo lengo kuu la wao kufundishwa....

Kwenye darasa maalum ambalo walipewa elimu maalum ambayo Socrates alimueleza Plato,miongopni mwa wanafunzi waliokuwemo ni Plato mwenyewe.Utaratiobu huu ambao Plato alielezwa na mwalimu wake ulikuwepo tangu Socrates mwenyewe alipopata ujuzi huo kutoka kwa Pythagoras na Plato aliendelea kuwa nao na hata wanafunzi wake waliofuatioa kama akina Alexander The Great waliendelea nao....

Hapa sasa dipo tunakuja kupata maana mbili za hadithi ya Allegory of the Cave inayopatikana kwenye kitabu cha Plato kiitwacho The Republic.....

Hadithi ile inazungumzia watu waliokuwa kwenye pango ambao walikuwa wamefungwa kwa minyororo kwenye miguu yao wakati huo huo nyuma yao kukiwa kuna mto unaowaka.Watu hawa waliishi kwenye pango hili kwa miaka mingi sana,wakiwa wameelekezea nyuso zao kwenye ukuta wa pango lile wakitazama vivuli vyao ukutani na waliamini ule ndiyo ulikuwa uhalisia [the dancing shadow became their reality]....

Kwao maisha na dunia ilikuwa ni ile waliyokuwa wakiiona kwenye pango lile.vivuli ndiyo mazingira yaliyowazunguka na huo ulikuwa ni ukweli mkubwa sana kwao....

Uhalisia ule ambao ulikuwa wazi kabisa kwenye macho yao ndiyo ulikuwa ukweli.Haikuwa rahisi kabisa kuja kumueleza mmoja wao au wote kwamba ule hukuwa uhalisia kwakuwa walikuwa wakiona kwa macho yao.Waliamini kila walichokuwa wakikiangalia kilikuwa ndicho halisi...

Bahati mbaya kabisa ni kwamba hawakujua kwamba uhalisia ule ulikuwa umetengenezwa tu,haukuwa halisi.Waliamini kila walichokuwa wanakiona ni halisi.Waliamini hakuna anayeweza kutengeneza kitu halafu kikaonekana kuwa halisi hadi siku mmoja wao alipokata mnyororo na kutoka nje na kuuona uhalisia halisi na kurudi ndani kuwafungua wenzake minyororo ile na wao kuja kuuona uhalisia ambao hata kwa bunduki wasingekubali kuwa upo kama mtu angeenda kuwaeleza hili.....

Ukiangalia au ukitaka kujua maana ya hadithihii ndipo utakuja kuona kile ambacho kinaendelea duniani.Plato aliwaeleza maana halisi ya hadithi hii watu wachache sana wanaitwa "the elect ones",watu ambao walikuwa wakielezwa haya kwa sababu maalaum ili waje kutawala dunia....

Kinachoendelea duniani leo sicho kilichopo kwenye uhalisia,siyo uhalisia bali ni uhalisia uliotengenezwa tu.Wengi na nadhani hata wewe unaamini kuna ugonjwa unaosababishwa na kirusi fulani kinachoitwa HIV,unaamini kuna ugonjwa unoitwa EBOLA unaoua kikatili kabisa,unaamini kuna mafua ya ndege,unaamini kuna watu wanaotishia maisha ya watu wanaoitwa magaidi,unaamini rais wa Marekani anachaguliwa na wapiga kura kidemokrasia,unaamini kuna uadui kati ya Marekani,China na Urusi,unaamini dunia ina watu wengi sana hivyo inaweza kuja kuleta matatizo hapo baadaye hivyo tunapaswa kutumia uzazi wa mpango.Unaamini kuwa dunia ina mabilioni ya miaka,Unaamini kuwa viwanda vinaharibu hali ya hewa na kuzababisha mvua kutonyesha na kuongeza joto duniani,fake relity ziko nyingi sana....

Tunaishi kwenye pango,vivuli vilivyotengenezwa na moto ndiyo uhalisia wetu,giza lililoko ndani ya pango ndiyo ukweli wetu.Minyoror inatufanya tuamini hivyo kwakuwa hatuwezi kutoka humo....

Sasa basi pango ni nini,minyororo ni nini?Moto na vivuli ni nini? Maana za haya yote utaweza kupata angalau clue kama utanisoma hapo juu kwa makini.Hapa ndipo tunapokuja kuamini kwamba vita vinasababishwa kwasababu tunazoambiwa,lakini kuna sababu za kweli ambazo hatuambiwi....

Tunaishi kwenye dunia ambayo ukipata hata nukta kidogo ya ukweli utaogopa....

Nimesema haya ili kukufanya mkuu MSEZA MKULU uangalie tena mara mbili sababu za vita ulivyovisema hapo kwenye mada yako ili uone kama hazina chumvi au uongo.....

Ashante......
JAMAA yangu uko sawa kabisa minyororo tulofungwa ni migumu kukatika hatakama wakija watu kutukatia ningunu sana hata kutoka kwenda kwenye uhalisia WA mambo, nilifuatilia story za mossad kuua wahusika WA kundi LA kigaidi kimya kimya na kusambaratisha kinu cha nyuklia, chanza cha kujua kua Syria inajenga kinu ni pale walipokata minyororo na kupuuzia kuwa treni iliyoripuka north Korea nilikuwa imebeba petrol, wasingechunguza wasingejua mambo halisi, mfano mwingine kama nwaba jf alivosema inawezekanaje MTU kuuwawa saremajevo halafu dunia ianzishe mapigano makubwa namba ile? Bado Plato nawenzake nitawaheshim mpaka kufa. Pia hongera kwa kukata myororo nami WA kwangu nilishaukata kitambo. Nice day
 
Mungu wangu,unaijua vyemna operation paperclip mkuu?
Exodus 20:7 reads: "Thou shalt not take the name of the LORD thy God in vain; for the LORD will not hold him guiltless that taketh his name in vain." (KJV).
Kuwa makini mkuu haukuwa na sababu ya kushutka hivyo.
Uperation paperclip ipo inajulikana na wahusika wanajulikana, Kama wewe unaifahamu yako ya kinjama za ALLIEN uiweke hapa ifukuliwe. Mbona unatumia nguvu kubwa kuliko mada mezani
 
Labda nikuulize swali rahisi sana tena sana....

Copy na original ni kipi kinakuwa bora?
Inategemea.
Mfano Copy ya karatasi sio Copy ya Mwanadamu.
Unaweza kusema ni Kopi lkn Mungu anasema
Psalm 139:13 For You formed my inward parts; You wove me in my mother's womb.
Jeremiah 1:5
Before I formed thee in the belly I knew thee, and before thou camest forth out of the womb I sanctified thee; I have appointed thee a prophet unto the nations.

Isaiah 44:24 Thus says the Lord, your Redeemer,
who formed you from the womb

Unaweza kukubali kuwa wewe ni Nth copy ya Adam lakni wengine Tuliumbwa na Mungu Tumboni mwa mama zetu.
Hakuna excuse
 
Nimeshasema hapa ni kwa namna gani watakwenda kuisimamia na kuifanikisha hii NWO,naona una tatizo la kusahau mkuu....

Wanaowaunga mkono ni watu wasiojua ukweli wa wakifanyacho hawa isipokuwa wachache ambao wamezawadiwa maisha ya kibilionea hapa duniani.....

Hawa machotara wa Kishetani wanaishi kwa kificho sana ili wasijulikane na iwe siri na jambo lisiloweza kuaminika na hii ni sababu ya hata wewe kukana hapa.....

Hata hiki ulichokiandika hapa kumhusu Goliath kinaonesha ni namna ipi binadamu tuna tatizo la kufikiri.Kwanza Goliath alikuwa na urefu wa futi 15 na pengine zaidi,sijui kama hata unajua futi kumi na tano ni nini maana yake,alikuwa na uzito wa zaidi ya kilo 500,Daudi inakadiriwa alikuwa na futi 6 hadi 7,binadamu mwenye kiwango cha Goliath anaweza kutioshwa namna ipi na binadamu wa kawaida hata kwa akili ndogo tu ya kawaida? Hakukosea kutoa kofia ya kichwa kwaajili ya kujilinda maana alijua hata hilo jiwe la Daudi lisinge mdhuru hata kama Daudi angelirusha kwa nguvu gani,ni sawa nba wewe upigane na mtoto wa miaka 7,uitamsambaratisha tu hata kama atakuwa na mawe.Usichokijua tu ni kwamba jiwe la Daudi lilimuua Goliath kwasababu ya Mungu na siyo kwasababu lilikuwa na kasi na usito mkubwa,sijui ni kwanini huoni hili jambo la kawaida kabisa.....

Sijui kama unaweza kupna makosa ya swali lako la kutaka nikuoneshe kitu kimoja ambachpo binadamu hawezi kutengeneza.Hivi nikikuambia tu kuwa bibnadamu hawezi kutengeneza tarakilishi [computer] utawezaje kupinga hili kwa mfano? Hebui nijibu halafu nitakuonesha matatizo kwenye swali lako hili....
Kwa nini machotara wa kishetani wenye uwezo mdogo kuliko maraika wake waishi kificho, wakati Maraika wa shetani Mapepo wanafurushwa kila kukicha makanisani? Huoni kama unajipotosha.


Dimensions za Goliath unazitoa kwenye vitabu gani maana kama ni Bibilia haisemi Uzito wake, Pia hizo futi 15 za urefu (6 feet 9 inches .
wakati huo huo takwimu za dunia mtu anayeshilikilia record ya ulefu duniani siku za hivi karibuni ni Robert Pershing Wadlow (USA) aliyekuwa 8 ft 11.1 in. Urefu ambao hata huyo goliath alikuwa mfupi sana.
 
Mwanzilishi wa ninachoamini? Kwanini unadhani kuna mwanzilishi tofauti na mimi mwenyewe? Sikumbuki kusoma mahali kuhusu hiki nilichokuambia,kama kuna mtu ana mtazamo kama wangu basi jua tu tumefikiria kitu kinachofanana na siyo kwamba nimetoa kwake....

Bahati mbaya naona hujui kuwa unabii hautegemei nani anaona nini,kitendo cha waprotestanti kuwa na msimamo huo hakuufanyi uwe sahihi.Nilianza kuona uongo wa hii fasiri ya unabii siku nyingi sana bila hata kupata ushawishi kutoka kwa mtu yoyote....

Nimekupa changamoto tu ya pembe kumi ambayo inaonesha matege ya hii fasiri yako lakini naona hutaki kabisa kunielewa na unataka nieleze Danieli 2 na 7 yote sijui kwa sababu ipi....

Wewe na wenzako mnasema kwamba pembe kumi ni ni yale mataifa [falme] kumi yaliyopatikana baada ya Rumi kuanguka [japokuwa hata hili nalo siyo sahihi na nilikueleza ni kwanini],nikakuambia kuwa unabii unasema pembe kumi siyo mataifa [falme] bali ni viongozi wa mnyama husika,lakini hili umeskip tu halafu unataka nikueleze tena.

Unasahau sana sijui au ni nini.....
pembe kumi sijaskip ila wewe ndio umekoswa ujasiri wa kuelezea tafsiri zako kwanza kama nilivyokuomba ili tuongeze kina cha mahojiano na mjadala. kusema ni mawazo yako pia ni rahisi ila wafuatiliaji wa haya mambo wananyamaza maana wenda unafumba macho mchana ionekane ni giza kumbe mchana kweupe. Naomba usikate kona nielezee daniel 2, 7 kwa mtazamo wako. Nilitegemea maelezo page hata mbili umekimbia kwa unaza kutafuta vichaka vya kujifichia. Uwe huru funguka tu hatutafuti mshindi bali ni kupeana mawazo mbadala
 
Exodus 20:7 reads: "Thou shalt not take the name of the LORD thy God in vain; for the LORD will not hold him guiltless that taketh his name in vain." (KJV).
Kuwa makini mkuu haukuwa na sababu ya kushutka hivyo.
Uperation paperclip ipo inajulikana na wahusika wanajulikana, Kama wewe unaifahamu yako ya kinjama za ALLIEN uiweke hapa ifukuliwe. Mbona unatumia nguvu kubwa kuliko mada mezani
Sijataja bure jina la Mungu hapo kwakuwa sinalitaja jina lake Mungu....
 
Kwa nini machotara wa kishetani wenye uwezo mdogo kuliko maraika wake waishi kificho, wakati Maraika wa shetani Mapepo wanafurushwa kila kukicha makanisani? Huoni kama unajipotosha.
Makanisani wanafurushwa mapepo na siyo malaika za Shetani,kuna tofauti kati ya malaika walioasi na na mapepo...

Dimensions za Goliath unazitoa kwenye vitabu gani maana kama ni Bibilia haisemi Uzito wake,
Nina vyanzo vingi sana tena sana,hata nikikupa huamini maana naona wewe umefunga akili yako kwenye kijibox ambapo hutaki kutoka humo...
Pia hizo futi 15 za urefu (6 feet 9 inches .
wakati huo huo takwimu za dunia mtu anayeshilikilia record ya ulefu duniani siku za hivi karibuni ni Robert Pershing Wadlow (USA) aliyekuwa 8 ft 11.1 in. Urefu ambao hata huyo goliath alikuwa mfupi sana.
Mkuu una matatizo gani?

Mimi nimesema "futi" nikitumia kiswahili nikimaanisha urefu, na siyo "feet" kwa maana unayotaka wewe kuionesha hapo,lakini cha ajabu na wewe umetumia neno lile lile kwa kiswahili ulipotumia "futi 8 kwa kuandika kwa kifupi ft,sijui una tatizo gani tu...

Ulichokifanya ni sawa na mtu aje hapa akukosoe kwa kuchanganua ft zako kwa feet kama ulivyochukua "futi" nilizotoa kisha akafanya tena kama wewe kwa kusema ft 8 ni sawa na feet 4 kisha akuletee lijamaa huko mtaani kwao lenye futi 6 akikukosoa kuwa haupo sahihi...

Sijui kama unaelewa ninachoandika hapa...

Kimsingi hueleweki kabisa...
 
pembe kumi sijaskip ila wewe ndio umekoswa ujasiri wa kuelezea tafsiri zako kwanza kama nilivyokuomba ili tuongeze kina cha mahojiano na mjadala. kusema ni mawazo yako pia ni rahisi ila wafuatiliaji wa haya mambo wananyamaza maana wenda unafumba macho mchana ionekane ni giza kumbe mchana kweupe. Naomba usikate kona nielezee daniel 2, 7 kwa mtazamo wako. Nilitegemea maelezo page hata mbili umekimbia kwa unaza kutafuta vichaka vya kujifichia. Uwe huru funguka tu hatutafuti mshindi bali ni kupeana mawazo mbadala
Haya mkuu nimekimbia....
 
Makanisani wanafurushwa mapepo na siyo malaika za Shetani,kuna tofauti kati ya malaika walioasi na na mapepo...


Nina vyanzo vingi sana tena sana,hata nikikupa huamini maana naona wewe umefunga akili yako kwenye kijibox ambapo hutaki kutoka humo...

Mkuu una matatizo gani?

Mimi nimesema "futi" nikitumia kiswahili nikimaanisha urefu, na siyo "feet" kwa maana unayotaka wewe kuionesha hapo,lakini cha ajabu na wewe umetumia neno lile lile kwa kiswahili ulipotumia "futi 8 kwa kuandika kwa kifupi ft,sijui una tatizo gani tu...

Ulichokifanya ni sawa na mtu aje hapa akukosoe kwa kuchanganua ft zako kwa feet kama ulivyochukua "futi" nilizotoa kisha akafanya tena kama wewe kwa kusema ft 8 ni sawa na feet 4 kisha akuletee lijamaa huko mtaani kwao lenye futi 6 akikukosoa kuwa haupo sahihi...

Sijui kama unaelewa ninachoandika hapa...

Kimsingi hueleweki kabisa...
Goliath 2. 06m Robert wadlow 2.72m
Goliath miaka zaidi ya 3000 iliyopita na huyu mdau kuzaliwa juzi tu asubuhi 22.2.1918.
Kama bibilia kwako ni ndani ya box basi uko sahihi kama vizio vya Goliath na mapepo kutokuwa Malaika wa Shetani umevitoa nje ya Box uko sahihi. Lkn kama ni bibilia nimerahisiha vipimo vya Goliath, hilo la mapepo kutakuwa majini na fallen angels endelea kuamini nje ya box.
 
Back
Top Bottom