WW1, WW2 na kinachoendelea sasa Middle east vilipangwa mwaka 1871 kama barua hii ni kweli

WW1, WW2 na kinachoendelea sasa Middle east vilipangwa mwaka 1871 kama barua hii ni kweli

Mambo ya Mungu tusiyajadili na ma conspiracy theories....ni mazito kuliko uwezo wa akili zetu ...tuwe makini ingawa najua kwa hulka ya kibinadamu tutajiona tuko makini ....
 
Nimesoma michango yenu yote nahisi kupotea zaidi,hebu naomba kuuliza tu kwa wajuvi wa mambo.Mungu ndiye kaumba ulimwengu na vyote vilivyopo je kwanini ameruhusu huyu SHETANI amharibie kazi yake aliyoifanya? kumbuka hata shetani kaumbwa na mungu huyuhuyu.WHY asimtupe kwenye ziwa la moto binadamu wakaishi kwa amani.Vinginevyo kuna theory fulani itapata nguvu sana tunakoelekea.
 
Mkuu Eiyer we ni noma your genious mkuu vya mambo aisee nu vizuri kuyafahamu sana

Mseza Mkuu Uko vizuri Sana Mkuu umetupa elemi ya kutosha kama hamtojali basi vitu Kama vitabu hata vijarida kama kuna soft copy muwe mnatuwekea hapa tunapitia angalau tupate kidogo au hata vichwa au jina la kitabu
Nashukuru sàna

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hapa kuna mambo mengi na mitazamo mingi ila kinachotarajiwa sio kumaliza wakazi wa dunia. Hapana ni kuwaandaa wakazi wadunia wote watakaokuwepo juu ya kile kinachoitwa MAISHA BORA KABISA KWA KILA MWANADUNIA. Yaani ONE WORLD GOVERNMENT. ukifuatilia miaka ya zamani wafalme walitawala Dunia nzima bila kuwepo na vita vyovyote kikanda. lakini leo ni vita kila kona(probably planned to still minds of people to accept the pre-planned grobal proporsal). Haya mambo bado yapo kinadharia lakini siku yatakapo tokea tukiwa hai tutafanya informed decision. WW3 au War on Terror sio kwa ajili ya KUFANYA DEPOPULATION ila kuwashawishi wakazi wa dunia nzima juu ya mpango wa kuiunganisha iwe kitu kimoja, Na hapo kila raia wa dunia atakuwa na Option Moja kukubali au Kukataa na kubaki katika dilema hasa kama hauna imani dhabiti ya Mungu. Ila Asilimia ya kupinga inategemewa iwe ndogo maana tayari tunaandaliw a kupitia TV,MOVIES, SOCIAL MEDIA,CHurches, International forums and organizations, Schools and university Curriculums, Theatre centres, Entertainments etc, Yaani popote alipo mwanadamu amezingirwa na ushawishi wa kuprogram Ubongo kuchagua vya kupenda na vya kuchukia automatically. Automatic Grobal Mental Reprogramming. Haya tunayasema hayana haja sana kuaminiwa sasa ila ikitokea tusishangae sana kana kwamba ni wageni. Watu wanafuatilia trend hizi kwa Ku decode vitabu vya Daniel na Ufunuo japo sio kazi rahisi na kutia tick kila kinachotimia. Mambo haya yanafanywa na wanadamu purely. Kwa waamini na wafuatiliaji wa Bibilia kwa kusoma na kutafakari kuna suluisho kubwa tu la kuexist katika mazingira haya yanaoyoonekana ni ya kufikirika lakn ni busara kuacha chumba cha uhakika wa uwepo wake katika Ubongo ili yakitokea isiwe kama Suprise.
Mkuu hongera kwa kunyooka moja kwa moja kwenye shabaha.
 
Wakati dunia ilipokuwa chini ya Mtawala mmoja mfano, Mesopotamia au Babylonian empire Chini ya mfalme Super Genius NEBUCHADNEZZAR dunia nzima ya wakati huo ilikuwa chini ya Mungu mmoja, Taratibu moja za dini, Mfumo mmoja wa kiuchumi,hata kama unafanya taratibu zako zako basi ufanye sirini usionekane. Na ilionekana ni rahisi sana kutawala dunia.
Ndio maana Wale jamaa watatu walioelezewa kwenye kitabu cha daniel walipogomea taratibu za dini wakati watu wote wa kila rangi kabila itikadi wakipiga magoti na kukubaliana Walitupwa ndani ya Moto. Na Ikaonekana kuwa na taratibu tofauti ni kama kuhatarisha amani. Na sasa kwa Mujibu wa wafuatiliaji wa mambo yajayo Dunia Inarudishwa kulekule babeli kwa kasi nzuri tu. Watu wa imani wanaamini Dunia inaelekezwa kwenye Vita ya Mwisho ambao Shetani na wafuasi wake wanakwenda kutumia SIlaha zao za mwisho za maangamizi Ila Mungu nae anaingilia kati kwa kwa walio wanyenyekevu kwake. Kwa lugha ya picha hiyo hali imeelezewa Ufunuo 18:2,3 Ila haita dumu muda mrefu Mungu anaingilia Kati na Huo ndio Mwisho wa Historia ya Ulimwengu. Huu ni Mtazamo wa kidini japo kuna Mitazamo mingi maana dunia hii huru tunajadili mambo Kidini, Kiuchumi, Kisiasa, Kimaendeleo na kila Mtazamo Unapingika na unakubalika. Kwa mtazamo wa Kidini Dunia hii kama ni Meli imekalibia Bandarini hakuna kurudi nyuma. Ila kisiasa na kiuchumi ngoja tuendelee kutatua matatizo yetu ta kila siku maana haya Mambo lazima yamuathiri kila mkazi wa dunia kaika nyanja zote za maisha yake ikitokea yametokea.
Umeweka darasa hauru ila mimi hapa naomba nifunge kwa kusema nachoamini mimi kuwa mtazamo wa kidini siku zote huwa right kuliko mtizamo mwingine wowote bila kupingana.

Hii mingine hugongana sana pia ina ukakasi mwingi sana.
 
Mkuu eiyer na mseza mkulu naona wote mna hoja nzito sana na zote zimekua msaada mkubwa kwetu kuweza kufahamu kiduchu kati ya mengi yaliyo ya siri.
Lakini naona mnashindwa kuelewana sehemu moja tu.
Mseza mkulu anadai kinachoendelea duniani kwa ujumla ikiwemo vita na mipango mingine ya siri ni mpango wa mwanadamu mwenyewe bila nguvu yoyote Ile kutoka nje ya ubinadamu, which is wrong.
Ukweli ni kwamba binadamu ni kama TV tu inayoendeshwa kwa remote control, nyuma ya yote haya Kuna nguvu ya ziada inayoratibu everything na kuhakikisha yanatimia kwa wakati, nae si mwingine ni muovu shetani kupitia mawakala wake, hivyo mseza mkulu sio kweli kwamba binadamu mwenyewe Ndio anapanga hichi kinachoendelea.

Na mkuu eiyer unadai Kuna vitu vinaitwa aliens, UFOs kiuhalisia hakuna vitu kama hivyo ni vitu vya kufikirika na kutengenezwa ili kuwatia hofu wanadamu ili iwe rahisi kwao kusimamisha NWO, kivipi... Aliens wamekua wakizungumziwa sana kwenye vyombo mbali mbali vya habari vikubwa duniani na pia kuandikwa sana kwenye vyanzo mbali mbali vya habari, Kuwa ni viumbe kutoka sayari nyingine na wana uwezo mkubwa sana wa kiakili na teknolojia yao ni ya hali ya juu sana, tunaaminisha haya kupitia movies mbali mbali kutoka Hollywood, yote hii ni kufanya akili zetu zione ni jambo la kawaida kwa viumbe hawa kutoka sayari nyingine, na ya kwamba kumbe duniani hatupo peke yetu!!! Kuna wageni toka sayari nyingine. Lakini ukweli ni kwamba si kweli ni vitu vya kutengenezwa tu, Ndipo hiyo siku itakapofika mpinga kristo atakapokua tayari kuja kuitawala dunia kupitia project ya blue beam light itakayokuwa displayed kwenye anga kutaonekana kama Kuna uvamizi wa hao aliens, na ili dunia tuweze kujikomboa dhidi ya huo uvamizi kutoka sayari nyingine tutalazimishwa kuungana kwa pamoja dunia nzima tuweze kumkabili adui kutoka sayari nyingine, ambapo kwa akili ya kawaida wengi wataona kweli Kuna ulazima wa kuungana ili kumkabili adui ambae kiukweli ni adui "fake" na hapo Ndipo wengi wataingia kwenye mtego wa NWO bila kutegemea na tayari Kuwa under one government, one currency, one religion na siku moja ya kuabudu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji445] [emoji445] [emoji445] [emoji444] [emoji444] only God can judge me[emoji444] [emoji444] [emoji443] [emoji443] [emoji445] [emoji445] [emoji445] [emoji441] [emoji441] RIP 2PAC

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tangu niliposoma na kujua alichokuwa anakimaanisha Plato kwenye kitabu chake cha Republic hasa kwenye story yake ya Allegory of the Cave ndiyo nilianza kuelewa kabisa hasa tunaishi kwenye dunia ya namna ipi....

Kimsingi,watu wote ambao leo tunawachukulia kama "majiniaz" walipata ujuzi waliokuwa nao kutoka mahali fulani,Mesopotamia huko.Pythagoras,Socrates,Galileo,Alexander the Great,Plato na hadi hawa akina Sir Francis Beacon na John Dee ni watu ambao walipata elimu hizi tofauti kabisa na wanafunzi wengine waliikuwa kwenye madarasa ya watu hawa....

Socrates aliwahi kumueleza mwanafunzi wake mmoja aitwaye Plato kwenye madarasa yao kwamba,elimu anayowapa ni elimu iliyoko kwenye makundi mawili.Kunsi la kwanza ni lile la kawaida ambalo wanapewa elimu ya kawaida kuhusu mafuzo waliyokuwa wanapewa na kundi la pili ni lile ambalo linapewa elimu maalum na nyeti ambayo hakupaswa kupewa mtu yoyote na ni elimu maalum ambayo ndiyo lengo kuu la wao kufundishwa....

Kwenye darasa maalum ambalo walipewa elimu maalum ambayo Socrates alimueleza Plato,miongopni mwa wanafunzi waliokuwemo ni Plato mwenyewe.Utaratiobu huu ambao Plato alielezwa na mwalimu wake ulikuwepo tangu Socrates mwenyewe alipopata ujuzi huo kutoka kwa Pythagoras na Plato aliendelea kuwa nao na hata wanafunzi wake waliofuatioa kama akina Alexander The Great waliendelea nao....

Hapa sasa dipo tunakuja kupata maana mbili za hadithi ya Allegory of the Cave inayopatikana kwenye kitabu cha Plato kiitwacho The Republic.....

Hadithi ile inazungumzia watu waliokuwa kwenye pango ambao walikuwa wamefungwa kwa minyororo kwenye miguu yao wakati huo huo nyuma yao kukiwa kuna mto unaowaka.Watu hawa waliishi kwenye pango hili kwa miaka mingi sana,wakiwa wameelekezea nyuso zao kwenye ukuta wa pango lile wakitazama vivuli vyao ukutani na waliamini ule ndiyo ulikuwa uhalisia [the dancing shadow became their reality]....

Kwao maisha na dunia ilikuwa ni ile waliyokuwa wakiiona kwenye pango lile.vivuli ndiyo mazingira yaliyowazunguka na huo ulikuwa ni ukweli mkubwa sana kwao....

Uhalisia ule ambao ulikuwa wazi kabisa kwenye macho yao ndiyo ulikuwa ukweli.Haikuwa rahisi kabisa kuja kumueleza mmoja wao au wote kwamba ule hukuwa uhalisia kwakuwa walikuwa wakiona kwa macho yao.Waliamini kila walichokuwa wakikiangalia kilikuwa ndicho halisi...

Bahati mbaya kabisa ni kwamba hawakujua kwamba uhalisia ule ulikuwa umetengenezwa tu,haukuwa halisi.Waliamini kila walichokuwa wanakiona ni halisi.Waliamini hakuna anayeweza kutengeneza kitu halafu kikaonekana kuwa halisi hadi siku mmoja wao alipokata mnyororo na kutoka nje na kuuona uhalisia halisi na kurudi ndani kuwafungua wenzake minyororo ile na wao kuja kuuona uhalisia ambao hata kwa bunduki wasingekubali kuwa upo kama mtu angeenda kuwaeleza hili.....

Ukiangalia au ukitaka kujua maana ya hadithihii ndipo utakuja kuona kile ambacho kinaendelea duniani.Plato aliwaeleza maana halisi ya hadithi hii watu wachache sana wanaitwa "the elect ones",watu ambao walikuwa wakielezwa haya kwa sababu maalaum ili waje kutawala dunia....

Kinachoendelea duniani leo sicho kilichopo kwenye uhalisia,siyo uhalisia bali ni uhalisia uliotengenezwa tu.Wengi na nadhani hata wewe unaamini kuna ugonjwa unaosababishwa na kirusi fulani kinachoitwa HIV,unaamini kuna ugonjwa unoitwa EBOLA unaoua kikatili kabisa,unaamini kuna mafua ya ndege,unaamini kuna watu wanaotishia maisha ya watu wanaoitwa magaidi,unaamini rais wa Marekani anachaguliwa na wapiga kura kidemokrasia,unaamini kuna uadui kati ya Marekani,China na Urusi,unaamini dunia ina watu wengi sana hivyo inaweza kuja kuleta matatizo hapo baadaye hivyo tunapaswa kutumia uzazi wa mpango.Unaamini kuwa dunia ina mabilioni ya miaka,Unaamini kuwa viwanda vinaharibu hali ya hewa na kuzababisha mvua kutonyesha na kuongeza joto duniani,fake relity ziko nyingi sana....

Tunaishi kwenye pango,vivuli vilivyotengenezwa na moto ndiyo uhalisia wetu,giza lililoko ndani ya pango ndiyo ukweli wetu.Minyoror inatufanya tuamini hivyo kwakuwa hatuwezi kutoka humo....

Sasa basi pango ni nini,minyororo ni nini?Moto na vivuli ni nini? Maana za haya yote utaweza kupata angalau clue kama utanisoma hapo juu kwa makini.Hapa ndipo tunapokuja kuamini kwamba vita vinasababishwa kwasababu tunazoambiwa,lakini kuna sababu za kweli ambazo hatuambiwi....

Tunaishi kwenye dunia ambayo ukipata hata nukta kidogo ya ukweli utaogopa....

Nimesema haya ili kukufanya mkuu MSEZA MKULU uangalie tena mara mbili sababu za vita ulivyovisema hapo kwenye mada yako ili uone kama hazina chumvi au uongo.....

Ashante......
Unaupeo mkubwa sana Nimepata elimu Kubwa sana katika hili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unaandika mambo kama vile una hakika nayo kabisa ....in short unasema Kanisa Katoliki ni mpango wa shetani ....hii ni kufuru ...hebu nitajie dhehebu au huduma ambayo link yake haijatokea Kanisa Katoliki (sijui kama unanielewa) .....Hata Biblia ni tunda la Kanisa Katoliki ....historia iliyonyooka ya Kanisa ipo ....tuache conspiracy ambazo ni kumpa tu utukufu shetani ....nguvu ya Kanisa Katoliki duniani miaka yote iwe ni kazi ya shetani? Sasa unabii wa Yesu juu ya Kanisa lake ungetimiaje? Au ndio hii kila mtu anaibuka akitafsiri biblia anavyojisikia? ....
Mkuu

Naona unanishutumu sana kuwa ninaandika kama vile nina uhakika wakati [kwa mtazamo wako] uhakika sina,hili ni kosa la kwanza kati ya makosa mengi tu kwenye maelezo yako....

Historia ya kanisa Katoliki naijua vizuri sana tu,ninajua kuhusu madhehebu mengine,lakini umenishangaza kwa kudhani kuwa ninadhani kuna dhehebu ambalo halijatokana na kanisa katoliki au kuna dhehebu safi.Mimi kusema shida ya kanisa katoliki hakuyafanyi makanisa au madhehebu mengine kuwa safi,yote yana uchafu wake na ni mbaya kweli kweli hivyo haya mawazo yako siyo sahihi kabisa....

Ninafahamu namna biblia ilivyopatikana,ufahamu wangu haujafungwa,sijaelewa kuwa,kama Kanisa katiloki ndilo lilihusika na upatikanaji wa Biblia ndiyo kunalifanya vipi kutokuwa na makosa jambo ambalo ni kawaida kabisa kwasababu linaongozwa na binadamu.Ninachoelewa mimi ni kwamba,kwakuwa linaongozwa na binadamu lina uchafu wake kama vile ambavyo sehemu yoyote inayoongozwa na binadamu inavyoweza kuwa na uchafu kwasababu ya udhaifu wa kibinadamu....

Nina uhakika na niandikayo wala sibahatishi,kuna mambo inawezekana huyajui kuhusu Kanisa hili lakini kutokuyajua kwako hakuwezi kuyaondoa jambo ambalo ni sawa sawa na mtu wa dhehebu lingine atakaposhindwa kujua ya dhehebu lake,kutokujua huko hakuyaondoi mabaya hayo....
 
Tangu niliposoma na kujua alichokuwa anakimaanisha Plato kwenye kitabu chake cha Republic hasa kwenye story yake ya Allegory of the Cave ndiyo nilianza kuelewa kabisa hasa tunaishi kwenye dunia ya namna ipi....

Kimsingi,watu wote ambao leo tunawachukulia kama "majiniaz" walipata ujuzi waliokuwa nao kutoka mahali fulani,Mesopotamia huko.Pythagoras,Socrates,Galileo,Alexander the Great,Plato na hadi hawa akina Sir Francis Beacon na John Dee ni watu ambao walipata elimu hizi tofauti kabisa na wanafunzi wengine waliikuwa kwenye madarasa ya watu hawa....

Socrates aliwahi kumueleza mwanafunzi wake mmoja aitwaye Plato kwenye madarasa yao kwamba,elimu anayowapa ni elimu iliyoko kwenye makundi mawili.Kunsi la kwanza ni lile la kawaida ambalo wanapewa elimu ya kawaida kuhusu mafuzo waliyokuwa wanapewa na kundi la pili ni lile ambalo linapewa elimu maalum na nyeti ambayo hakupaswa kupewa mtu yoyote na ni elimu maalum ambayo ndiyo lengo kuu la wao kufundishwa....

Kwenye darasa maalum ambalo walipewa elimu maalum ambayo Socrates alimueleza Plato,miongopni mwa wanafunzi waliokuwemo ni Plato mwenyewe.Utaratiobu huu ambao Plato alielezwa na mwalimu wake ulikuwepo tangu Socrates mwenyewe alipopata ujuzi huo kutoka kwa Pythagoras na Plato aliendelea kuwa nao na hata wanafunzi wake waliofuatioa kama akina Alexander The Great waliendelea nao....

Hapa sasa dipo tunakuja kupata maana mbili za hadithi ya Allegory of the Cave inayopatikana kwenye kitabu cha Plato kiitwacho The Republic.....

Hadithi ile inazungumzia watu waliokuwa kwenye pango ambao walikuwa wamefungwa kwa minyororo kwenye miguu yao wakati huo huo nyuma yao kukiwa kuna mto unaowaka.Watu hawa waliishi kwenye pango hili kwa miaka mingi sana,wakiwa wameelekezea nyuso zao kwenye ukuta wa pango lile wakitazama vivuli vyao ukutani na waliamini ule ndiyo ulikuwa uhalisia [the dancing shadow became their reality]....

Kwao maisha na dunia ilikuwa ni ile waliyokuwa wakiiona kwenye pango lile.vivuli ndiyo mazingira yaliyowazunguka na huo ulikuwa ni ukweli mkubwa sana kwao....

Uhalisia ule ambao ulikuwa wazi kabisa kwenye macho yao ndiyo ulikuwa ukweli.Haikuwa rahisi kabisa kuja kumueleza mmoja wao au wote kwamba ule hukuwa uhalisia kwakuwa walikuwa wakiona kwa macho yao.Waliamini kila walichokuwa wakikiangalia kilikuwa ndicho halisi...

Bahati mbaya kabisa ni kwamba hawakujua kwamba uhalisia ule ulikuwa umetengenezwa tu,haukuwa halisi.Waliamini kila walichokuwa wanakiona ni halisi.Waliamini hakuna anayeweza kutengeneza kitu halafu kikaonekana kuwa halisi hadi siku mmoja wao alipokata mnyororo na kutoka nje na kuuona uhalisia halisi na kurudi ndani kuwafungua wenzake minyororo ile na wao kuja kuuona uhalisia ambao hata kwa bunduki wasingekubali kuwa upo kama mtu angeenda kuwaeleza hili.....

Ukiangalia au ukitaka kujua maana ya hadithihii ndipo utakuja kuona kile ambacho kinaendelea duniani.Plato aliwaeleza maana halisi ya hadithi hii watu wachache sana wanaitwa "the elect ones",watu ambao walikuwa wakielezwa haya kwa sababu maalaum ili waje kutawala dunia....

Kinachoendelea duniani leo sicho kilichopo kwenye uhalisia,siyo uhalisia bali ni uhalisia uliotengenezwa tu.Wengi na nadhani hata wewe unaamini kuna ugonjwa unaosababishwa na kirusi fulani kinachoitwa HIV,unaamini kuna ugonjwa unoitwa EBOLA unaoua kikatili kabisa,unaamini kuna mafua ya ndege,unaamini kuna watu wanaotishia maisha ya watu wanaoitwa magaidi,unaamini rais wa Marekani anachaguliwa na wapiga kura kidemokrasia,unaamini kuna uadui kati ya Marekani,China na Urusi,unaamini dunia ina watu wengi sana hivyo inaweza kuja kuleta matatizo hapo baadaye hivyo tunapaswa kutumia uzazi wa mpango.Unaamini kuwa dunia ina mabilioni ya miaka,Unaamini kuwa viwanda vinaharibu hali ya hewa na kuzababisha mvua kutonyesha na kuongeza joto duniani,fake relity ziko nyingi sana....

Tunaishi kwenye pango,vivuli vilivyotengenezwa na moto ndiyo uhalisia wetu,giza lililoko ndani ya pango ndiyo ukweli wetu.Minyoror inatufanya tuamini hivyo kwakuwa hatuwezi kutoka humo....

Sasa basi pango ni nini,minyororo ni nini?Moto na vivuli ni nini? Maana za haya yote utaweza kupata angalau clue kama utanisoma hapo juu kwa makini.Hapa ndipo tunapokuja kuamini kwamba vita vinasababishwa kwasababu tunazoambiwa,lakini kuna sababu za kweli ambazo hatuambiwi....

Tunaishi kwenye dunia ambayo ukipata hata nukta kidogo ya ukweli utaogopa....

Nimesema haya ili kukufanya mkuu MSEZA MKULU uangalie tena mara mbili sababu za vita ulivyovisema hapo kwenye mada yako ili uone kama hazina chumvi au uongo.....

Ashante......
 
eiyer
habari hii inatisha! Je kila aingiaye kwenye utawala katika Marekani, Urusi, China na sasa Korea Kaskazini wanazifahamu hizi habari?
 
Hili la kujiona wanajua wakati hawajui ni tatizo lingine kubwa kweli kweli na ni changamoto ngumu sana kwa watu kujifunza.Wakati naanza kuyafuatilia haya mambo huku kwetu hayakuwepo kabisa,kuna wakati unajikuta unakaa kimya tu huku ukiwa unaumia tu....

Haya mambo yalipoingia hapa nchini na watu kuyaingilia kwa sifa ndiyo matokeo ya ujuaji usiokuwa na maana,mtu anajua vitu "vya kawaida" lakini anaona anajua mengi sana,ukikosoa unaonekana wewe mjuaji,unajikalia kimya tu...

Karibu sana mkuu unipe maujuzi zaidi....
Mkuu haya mambo niyakufikirisha na ukiwaza kwa makini ni ukweli mtupu lakini wanaochukulia mambo kirahisi hawawezi kuamini.
Ni ukweli kuwa wapo watu wanaondesha dunia na kupanga dunia iende vipi ,pia inavyoonekana hizi secret societies chimbuko lake ni moja au viongozi wao wa juu ni kitu kimoja,kuna sehemu kwenye mabandiko yaliyopita ulisema skulls & bones ni wanajihusisha vyuo,Freemason wanajihusisha na mambo ya imani,je hata haya tunayoyaita ni vitabu vitakatifu tuna uhakika gani kwamba may be ni conspiracy za hao majamaa?iwapo Pindar ni yupo Vatican na kitabu kitakatifu kinachotumika ndo hiki at the same time yeye ni kati ya wakuu wa illuminati.

Ni kweli kwamba kuna vitu binadamu hakupaswa kufahamu lakini akafunuliwa na huyu jamaa mwenye busara,ingawa biblia inasema shetani ni mwongo ila ni kama aliyoeleza kwenye bustani ya eden ni kweli na hajamdaganya mtu maana tunda alilosema kweli ilimfunua ufahamu wa kujua mema na mabaya.

Ukifuatilia hawa watu illuminati na Freemason wanamchanganyiko wa dini mbali mbali na kwenye ceremony initiations biblia ni kati ya vitabu vinavyotumika kufanya viapo kwa wale ambao ni wakristo,na pia ukiangalia hata codes za kupanda madaraja ya degree zao zinasemekana zipo ndani ya biblia,sasa tuamini vipi kwamba hivi vitabu vitakatifu hawajahusika ?isije ikawa ni mwendelezo wa hawa majamaa kutuingiza mkenge
 
Mkuu haya mambo niyakufikirisha na ukiwaza kwa makini ni ukweli mtupu lakini wanaochukulia mambo kirahisi hawawezi kuamini.
Ni ukweli kuwa wapo watu wanaondesha dunia na kupanga dunia iende vipi ,pia inavyoonekana hizi secret societies chimbuko lake ni moja au viongozi wao wa juu ni kitu kimoja,kuna sehemu kwenye mabandiko yaliyopita ulisema skulls & bones ni wanajihusisha vyuo,Freemason wanajihusisha na mambo ya imani,je hata haya tunayoyaita ni vitabu vitakatifu tuna uhakika gani kwamba may be ni conspiracy za hao majamaa?iwapo Pindar ni yupo Vatican na kitabu kitakatifu kinachotumika ndo hiki at the same time yeye ni kati ya wakuu wa illuminati.

Ni kweli kwamba kuna vitu binadamu hakupaswa kufahamu lakini akafunuliwa na huyu jamaa mwenye busara,ingawa biblia inasema shetani ni mwongo ila ni kama aliyoeleza kwenye bustani ya eden ni kweli na hajamdaganya mtu maana tunda alilosema kweli ilimfunua ufahamu wa kujua mema na mabaya.

Ukifuatilia hawa watu illuminati na Freemason wanamchanganyiko wa dini mbali mbali na kwenye ceremony initiations biblia ni kati ya vitabu vinavyotumika kufanya viapo kwa wale ambao ni wakristo,na pia ukiangalia hata codes za kupanda madaraja ya degree zao zinasemekana zipo ndani ya biblia,sasa tuamini vipi kwamba hivi vitabu vitakatifu hawajahusika ?isije ikawa ni mwendelezo wa hawa majamaa kutuingiza mkenge
Sijajua kama Pindar anapatikana Vatican ila ninafahamu ndiye mkuu wa Illuminati...

Kuhusu vitabu vya dini ni kwamba kuna dini ambazo ni product ya hawa "watu" lakini kuna moja tu ambayo siyo.Jambo hili siyo rahisi moja kwa moja kama wengine wanavyoweza kudhania,ni gumu sana.....

Shetani hakuwa mkweli pale Eden kwa asilimia 100 bali kwa sehemu tu.Lakini pia Mungu hakuwahi kusema kisichokuwepo,alipowaeleza Adam na Hawa matokeo ya ulaji wa tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya ilikuwa ni kweli...

Mungu hakukataa kuwa Adam na Hawa walifumbuliwa macho,lakini Mungu hakutaka wawe hivyo kwasababu hawakuumbwa namna hiyo.Hawakuumbwa kuweza kuhimili uwezo wa kujua meam na mabaya na matokeo yake tunayaona kila uchao.Shetani hakuishia hapo tu bali aliendelea kuwafundisha mengine yaliyosababisha mengi sana na ya hatari.....

Binadamu walifundishwa elimu ya nyota,walifundishwa namna ya kutoa ujauzito,walifundishwa namna ya kutengeneza silaha za moto,walifundishwa elimu ya anga,fizikia na nyingine ambazo binadamu hakupaswa kujua....

Kwenye rituals zao na initiations kuna biblia na vitabu vingine vya dini zingine,kila kitabu kiko pale kwaajili ya kazi maalum na siyo kama wengi wanavyodhani....

Nirahisi sana mtu kuhusisha jambo fulani na kitu kingine lakini kuthibitisha ni suala lingine kabisa mkuu.....
 
Tangu niliposoma na kujua alichokuwa anakimaanisha Plato kwenye kitabu chake cha Republic hasa kwenye story yake ya Allegory of the Cave ndiyo nilianza kuelewa kabisa hasa tunaishi kwenye dunia ya namna ipi....

Kimsingi,watu wote ambao leo tunawachukulia kama "majiniaz" walipata ujuzi waliokuwa nao kutoka mahali fulani,Mesopotamia huko.Pythagoras,Socrates,Galileo,Alexander the Great,Plato na hadi hawa akina Sir Francis Beacon na John Dee ni watu ambao walipata elimu hizi tofauti kabisa na wanafunzi wengine waliikuwa kwenye madarasa ya watu hawa....

Socrates aliwahi kumueleza mwanafunzi wake mmoja aitwaye Plato kwenye madarasa yao kwamba,elimu anayowapa ni elimu iliyoko kwenye makundi mawili.Kunsi la kwanza ni lile la kawaida ambalo wanapewa elimu ya kawaida kuhusu mafuzo waliyokuwa wanapewa na kundi la pili ni lile ambalo linapewa elimu maalum na nyeti ambayo hakupaswa kupewa mtu yoyote na ni elimu maalum ambayo ndiyo lengo kuu la wao kufundishwa....

Kwenye darasa maalum ambalo walipewa elimu maalum ambayo Socrates alimueleza Plato,miongopni mwa wanafunzi waliokuwemo ni Plato mwenyewe.Utaratiobu huu ambao Plato alielezwa na mwalimu wake ulikuwepo tangu Socrates mwenyewe alipopata ujuzi huo kutoka kwa Pythagoras na Plato aliendelea kuwa nao na hata wanafunzi wake waliofuatioa kama akina Alexander The Great waliendelea nao....

Hapa sasa dipo tunakuja kupata maana mbili za hadithi ya Allegory of the Cave inayopatikana kwenye kitabu cha Plato kiitwacho The Republic.....

Hadithi ile inazungumzia watu waliokuwa kwenye pango ambao walikuwa wamefungwa kwa minyororo kwenye miguu yao wakati huo huo nyuma yao kukiwa kuna mto unaowaka.Watu hawa waliishi kwenye pango hili kwa miaka mingi sana,wakiwa wameelekezea nyuso zao kwenye ukuta wa pango lile wakitazama vivuli vyao ukutani na waliamini ule ndiyo ulikuwa uhalisia [the dancing shadow became their reality]....

Kwao maisha na dunia ilikuwa ni ile waliyokuwa wakiiona kwenye pango lile.vivuli ndiyo mazingira yaliyowazunguka na huo ulikuwa ni ukweli mkubwa sana kwao....

Uhalisia ule ambao ulikuwa wazi kabisa kwenye macho yao ndiyo ulikuwa ukweli.Haikuwa rahisi kabisa kuja kumueleza mmoja wao au wote kwamba ule hukuwa uhalisia kwakuwa walikuwa wakiona kwa macho yao.Waliamini kila walichokuwa wakikiangalia kilikuwa ndicho halisi...

Bahati mbaya kabisa ni kwamba hawakujua kwamba uhalisia ule ulikuwa umetengenezwa tu,haukuwa halisi.Waliamini kila walichokuwa wanakiona ni halisi.Waliamini hakuna anayeweza kutengeneza kitu halafu kikaonekana kuwa halisi hadi siku mmoja wao alipokata mnyororo na kutoka nje na kuuona uhalisia halisi na kurudi ndani kuwafungua wenzake minyororo ile na wao kuja kuuona uhalisia ambao hata kwa bunduki wasingekubali kuwa upo kama mtu angeenda kuwaeleza hili.....

Ukiangalia au ukitaka kujua maana ya hadithihii ndipo utakuja kuona kile ambacho kinaendelea duniani.Plato aliwaeleza maana halisi ya hadithi hii watu wachache sana wanaitwa "the elect ones",watu ambao walikuwa wakielezwa haya kwa sababu maalaum ili waje kutawala dunia....

Kinachoendelea duniani leo sicho kilichopo kwenye uhalisia,siyo uhalisia bali ni uhalisia uliotengenezwa tu.Wengi na nadhani hata wewe unaamini kuna ugonjwa unaosababishwa na kirusi fulani kinachoitwa HIV,unaamini kuna ugonjwa unoitwa EBOLA unaoua kikatili kabisa,unaamini kuna mafua ya ndege,unaamini kuna watu wanaotishia maisha ya watu wanaoitwa magaidi,unaamini rais wa Marekani anachaguliwa na wapiga kura kidemokrasia,unaamini kuna uadui kati ya Marekani,China na Urusi,unaamini dunia ina watu wengi sana hivyo inaweza kuja kuleta matatizo hapo baadaye hivyo tunapaswa kutumia uzazi wa mpango.Unaamini kuwa dunia ina mabilioni ya miaka,Unaamini kuwa viwanda vinaharibu hali ya hewa na kuzababisha mvua kutonyesha na kuongeza joto duniani,fake relity ziko nyingi sana....

Tunaishi kwenye pango,vivuli vilivyotengenezwa na moto ndiyo uhalisia wetu,giza lililoko ndani ya pango ndiyo ukweli wetu.Minyoror inatufanya tuamini hivyo kwakuwa hatuwezi kutoka humo....

Sasa basi pango ni nini,minyororo ni nini?Moto na vivuli ni nini? Maana za haya yote utaweza kupata angalau clue kama utanisoma hapo juu kwa makini.Hapa ndipo tunapokuja kuamini kwamba vita vinasababishwa kwasababu tunazoambiwa,lakini kuna sababu za kweli ambazo hatuambiwi....

Tunaishi kwenye dunia ambayo ukipata hata nukta kidogo ya ukweli utaogopa....

Nimesema haya ili kukufanya mkuu MSEZA MKULU uangalie tena mara mbili sababu za vita ulivyovisema hapo kwenye mada yako ili uone kama hazina chumvi au uongo.....

Ashante......
Asante cc Eiyer inabid nitafute hiki kitabu
 
Point yangu ya pili ni kwamba,references za mijadala yetu sote inatokana na kitabu biblia ambacho binafsi naamini hawa jamaa wanaweza kuwa wameisha distort ukweli kwa kiwango cha kutosha ndio maana mijadala yetu inakuwa haiishi kama duara. Mungu aliposema ya kwamba tutafute maarifa,alijua kutakuwa na hidden truth kuhusu yeye na uumbaji.
Biblia imekuwa kama Keepleft without outlet
 
Bwana wee hawa watu wawil eiyer na mseza mkulu wapo smart sana. Nimefurahishwa sana na kutolewa ujinga kwa kiasi kikubwa na eiyer na hili lisingewezekana bila maswal na mtazamo wa mseza mkulu. Tunameng ya kujifunza kutoka kwenu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom