Ya Adani na Wachina: Hii ndiyo sababu kuu inayofanya Wanasiasa wetu wawachukie Wazungu

Ya Adani na Wachina: Hii ndiyo sababu kuu inayofanya Wanasiasa wetu wawachukie Wazungu

Kusema kweli ili tuendelee tunawahitaji sana Wazungu kuliko hawa wachina na wahindi wanaojenga miradi ya hovyo iliyo chini ya kiwango tena kwa pesa nyingi ambazo zinaenda kutumika kama Rushwa kuwanufaisha wachache.
Tatizo ni nyinyi wenye miradi mnataka 10% Mchina hana tatizo
 
Nakubaliana na wewe isipokuwa kuchoma nyumba hicho kitu sahau watanzania mazuzu.
 
Unakumbuka enzi za Magufuli hadi HISA za Barrick ziliporomoka sana huko duniani baada ya ile report kutoka? Barrick pia wamekua wanalalamikiwa huko huko Ulaya kwa madhambi wanayo yafanya Africa na America kusini. Wazungu wamenyooka, Wahindi na Wachina HAPANA
Wote wale wale tu wazungu wenyewe wanatoa hongo kuoata tenda.
Hukuona ile report ya malipo ya barick yasiyo kuwa na maelezo hapa nchini.
 
Eti "Wanasiasa wanachukia wazungu"

Hebu tuwekee makala yeyote ile au matamshi ikionyesha/yakionyesha Wanasiasa wa Tanzania wakiwa wanawachukia wazungu??


Uzi kama huu huwa una lengo la kuwachonganisha Waafrika na Wahindi na Wachina.

Piganeni wenyewe huko, msituingize Waafrika kwenye vita zenu na fikra za Ubeberu. Rushwa or Not
 
Pamoja na yote Mzungu ni mtu aliyenyooka sana!

Mzungu kawekeza sana kwenye suala la utawala bora ambapo kupitia utawala bora amejenga Taasisi na mifumo imara sana zinazosimamia mambo na kuhakikisha yanaenda bila shida.

Kunyooka huku kwa Mzungu ndiko kumefanya sasa aanze kupoteza sana Africa. Hii ni kwa sababu Viongozi wa Afrika wanapenda sana Rushwa. Kupenda Rushwa kwa Viongozi wa Afrika ndiko kumefanya kwa sasa bara la Africa kuongoza kwa uwekezaji wa Wachina na Wahindi.

Mchina na Mhindi ni watu wanaoamini kuwa ili jambo lake liende lazima atoe Rushwa. Endapo siku ikitokea ukafanyika uchunguzi huru wa namna kandarasi za Wachina na Wahindi zinavyopatikana hapa Tanzania na Afrika nawaambia wananchi wetu wanaweza choma nyumba zote za Viongozi wetu sio tu Tanzania bali Afrika nzima.

Waendesha Mashtaka wa Marekani kufungua Mashtaka dhidi ya tajiri wa kihindi Adani ni funzo kubwa kwetu kuwekeza kwenye katiba bora inayojenga na inayosimamia mifumo imara. Mifumo isiyotoa nafasi kwa rushwa na kuhakikisha fedha zote za walipakodi zinatumika kwa maendeleo ya wananchi tu na sio kuwanufaisha wachache.

Hapa Tanzania Adani kapewa sehemu ya Bandari yetu. Huwezi sikia hata siku moja PCCB wakifanya uchunguzi. Na kamwe hatutosikia. Hii ni kwa sababu Adani ameingia Tanzania kupitia Ofisi namba moja.

Sio mara ya kwanza kwa mzungu kuonyesha umuhimu wa Mifumo na Taasisi imara kwenye utawala bora. Tanzania tulishawahi rudishiwa chenji yetu ya Rada baada ya Wazungu kugundua kuwa kampuni zao zilitupiga na wakazibana zikarudisha kweli.

Kuna kipindi Bandarini Wazungu waligundua kuna kampuni zao zilitoa Rushwa kupata tenda za kufunga mifumo ya tehama kwenye Bandari yetu. Ila pamoja na Ile kampuni kubanwa nchini mwao hapa kwetu hatujasikia hadi leo wahusika wakifikishwa Mahakamani.

Kusema kweli ili tuendelee tunawahitaji sana Wazungu kuliko hawa wachina na wahindi wanaojenga miradi ya hovyo iliyo chini ya kiwango tena kwa pesa nyingi ambazo zinaenda kutumika kama Rushwa kuwanufaisha wachache.

Najua huu uzi hautapata wachangiaji wengi kwa sababu Watanzania wengi ni mazuzu. Hawaelewi unyeti wa kodi zao na wanawaona wanasiasa kama miungu ambao wanaweza fanya chochote na hela zao bila kuhojiwa au kufanywa chochote.
View attachment 3158628

Ipo siku

Lord denning
Qatar
Umezungumza ukweli wa 100%, na hii unayoona viongozi wanaingia kwa chaguzi za wizi, njia zote chafu ni ili kulinda maslahi yao yanayopatikana kwa njia ya rushwa. Na kwenye rushwa hizi wanakula viongozi wa kisiasa na wa vyombo vya dola, ili kulindana katika madaraka.
 
Kwa hiyo wazungu hawatoi rushwa na hawali rushwa?
Hakuna paliposemwa Wazungu hawatoi Rushwa, wanatoa ila kutokana na nchi zao kuwa na mifumo imara ya checks and balance wanaogopa sana kutoa Rushwa na ndo mana Viongozi wa Kitanzania na Afrika kwa ujumla hawawapendi
 
Magulification must go on to root out the scourge of Corruption in the African Continent.

Lead by Big Wazungu, Wahindi na Waarabu Cooperation. And Big Companies.
 
Ndio anapindisha hivyo. Wazungu wamekula Rushwa kutoka kwa Adani, anawasingizia Waafrika.

Wazungu ni watoa Rushwa na wala rushea namba moja Duniani. piga ua
Elewa mada acha kukurupuka.

Mbona imeelezwa kuhusu walivyotupiga kwenye manunuzi ya Rada kipindi cha Mkapa?

Uzi unazungumziq namna walivyokuwa na mifumo thabiti ya cheks and balances kiasi ambacho hata kampuni zao zimekuwa zikiogopa sana kutoa Rushwa.

Mzungu akitoa Rushwa kuna mfumo wa kumchunguza kwenye nchi yake. Na anaweza kubanwa na mpaka kuchukuliwa hatua. Hili limewafanya waogope sana kutoa Rushwa hivi karibuni
 
Umeishia darasa la ngapi?
Eti "Wanasiasa wanachukia wazungu"

Hebu tuwekee makala yeyote ile au matamshi ikionyesha/yakionyesha Wanasiasa wa Tanzania wakiwa wanawachukia wazungu??


Uzi kama huu huwa una lengo la kuwachonganisha Waafrika na Wahindi na Wachina.

Piganeni wenyewe huko, msituingize Waafrika kwenye vita zenu na fikra za Ubeberu. Rushwa or Not
 
Umezungumza ukweli wa 100%, na hii unayoona viongozi wanaingia kwa chaguzi za wizi, njia zote chafu ni ili kulinda maslahi yao yanayopatikana kwa njia ya rushwa. Na kwenye rushwa hizi wanakula viongozi wa kisiasa na wa vyombo vya dola, ili kulindana katika madaraka.
Kwa Viongozi ipo hivi km ulikua haujui kwenye masuala ya Uchaguzi ngoja nikutoe tongotongo mfano chama A kipo madarakani km chama tawala halafu chama B kipo km chama pinzani, sasa ikitokea mgombea wa chama B ana nguvu kuliko mgombea wa chama A yaan wananchi wanamkubari sana mgombea wa chama B ambae yupo upinzani na kwenye sanduku la kura kweli wote wakampigia mgombea wa chama B ambae ni wa chama pinzani, nikuambie kitu kinachofanywa na viongozi wa Afrika ni kwamba Mwananchi hana haki wao viongozi waliopo madarakani ndio wenye haki kwa hio ikitokea wapiga kura wakampigia kura zote mgombea wa chama pinzani wanatumia nguvu ya Dola kumuweka mtu wao wanaemtaka wao kwa kumtumia msimamizI wa kutangaza matokeo ya uchaguzi wanachompa ni security tu kwamba ukitangaza tutakulinda viongozi na Wananchi hawana haki kwa hio wataamua waende wakashtaki wanapopajua maana wakienda mahakamani ndio km unaenda kushtaki kesi ya nyani kwa ngedere
 
Umedadavua hilo vipi? Takataka Babako, mamako, Mjomba wako, nyanya yako na familia yako yote. Koma kuwaita watu weusi takataka. Shenzi wahead



Wahindi ndio watoa Rushwa moja hapa Tanzania-warudishwe makwao-na ndio maana nasema tungo'oke kwenye Jumuiya ya Madola ambayo ndio inayowapa hawa Wahindi Trade Advantage.

Jiridhie na Treaty ya Waingereza baada ya kushindwa kuwarudisha wahindi makwao baada ya kuwatumia kama watumwa wa kujenga reli zao Duniani.

Wamasai wanafanya nini? Wakurya wanafanya nini? Kama sio kutoa elimu kwa vijana wao tangia wakiwa wadogo?
Mapovu hayakusaidii chochote, utendaji wetu ni takataka kama wewe umechukulia kuwa wewe ni takataka hayo ni matatizo yako binafsi.

Sisi tunayo matatizo yetu mengi tu, inferiority complex zetu zinatudanganya kwamba kila mtu ni adui ya maendeleo yetu wakati adui wa kwanza ni hulka zetu wenyewe.
 
Back
Top Bottom