Yajue maisha ya Mbinguni, yana raha isiyo na kifani

Huyo ni roho mtakatifu anawaka kila mahali 😂😂
da!! ila huyu mwamba aliyepiga picha mbinguni kiboko!!!....alifikaje huko bila kukamatwa na mwamba malaika MICHAEL???,,,,mwanangu jamaa noma,,ananyatia hadi MBINGU na anaipiga picha?????,,,,sasa huyu si hatari sana??,,,kama ameweza kuingia mbinguni na kupiga picha si anaweza kuingia IKULU huku anapiga ULUZI?
 
Hao walishakufa, kwa tuliopo duniani wote tunafuata tuliyoyakuta walioleta hawawezi kuamka maana walishakuwa mavumbi miaka mingi sana.
Tatizo mambo mengi ya historia huathiriwa

Dini zinazid kuathiriwa Kwa kasi sana had sisi tumefikia kudanganyana waziwazi had kizazii kingine mambo yattaazid kuharibika
 
Mkuu Setfree naomba dadavua hapa panapo nitatiza Mimi binafsi
  • Hakuna njaa wala kiu – Ufunuo 7:16
  • Hatutakula kwa jasho. Tutakula matunda, bure – Ufunuo 2:7
Asiyekuwa na njaa hahitaji kula eventually hatoenda chooni mana hajala chochote.

Kama mbinguni hakutakuwa na njaa kwanini tule matunda? Kwanini tushiriki karamu kubwa pamoja na Yesu kristo?
 
Hakuna mbinguni au motoni, ni mchongo tu. Kama kweli mbingu ipo ni kwa nini mtu usikubali kufa ili uende huko? Ndugu zangu, hakuna maisha mazuri zaidi ya haya, jaribu tu kuboresha maisha yako kabla ya kuyeyuka.
 
Waliotuketea dini sikumoja waamke watuambie ukweli Jamani
Hasa hawa,wanayumba sana.

Yohana 9:2
Wanafunzi wake wakamuuliza, “Mwalimu, ni nani aliyetenda dhambi; ni huyu mtu au wazazi wake hata azaliwe kipofu?”
 
Mbingu ipo hapahapa duniani
Mkuu, epuka huo mtazamo wa Atheists. Biblia inatufundisha waziwazi kuwa mbingu ipo; ni makao ya Mungu na ni mahali ambapo waaminio watakwenda kuishi.

Biblia inataja mbingu mara nyingi kuwa ni mahali halisi tofauti na dunia.

Mwanzo 1:1 – “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.” Mstari huo unaonyesha kuwa mbingu sio sehemu ya dunia, bali ni mahali tofauti.

Yesu pia alisema, "Katika nyumba ya Baba yangu mna makao mengi...nakwenda kuwaandalia mahali... ili nilipo, nanyi muwepo." (Yohana 14:2-3). Hapo Yesu anaelezea mbingu kuwa ni mahali halisi ambako waaminio watakwenda.

Mbingu sio sehemu ya dunia. Kama mbingu ingekuwa hapa hapa duniani, Yesu asingesema kuwa "Nakwenda kuwaandalia mahali."(Yohana 14:2). Maandiko yanaonyesha wazi kuwa Yesu alipaa kwenda mbinguni(Matendo 1:9-11). Na pia Yesu asingesema atarejea tena duniani, kama mbingu ingekuwa hapa hapa.

Biblia inatupa ufunuo wa watu walioiona Mbingu.
Paulo anasema alipelekwa hadi "mbingu ya tatu" (2 Wakorintho 12:2), akionyesha kuwa kuna viwango vya mbingu na kwamba ipo sehemu iliyo tofauti na dunia.
Stefano alipopigwa kwa kutupiwa mawe, aliona "mbingu zimefunguka" na Yesu akiwa mkono wa kuume wa Mungu (Matendo 7:55-56).

Usidanganywe na raha za kitambo za hapa duniani ukafikiri ndiyo mbingu yenyewe. Mbinguni hakuna raha ya kitambo. Ni raha tupu milele yote.
 
Raha ikwapi hapo wakati hakutakuwa na wali maharage
Kama unafurahia wali maharage, basi mbinguni kuna zaidi ya wali maharage kwakuwa aliyeumba wali na maharage Mbinguni ndiyo makao yake. Anatuandalia vyakula vitamu zaidi.
 
Tatizo wanaosimulia mbinguni pazuri, wanaogopa kufa😆😆😆 hampendi kwenda kula raha!?
Mtu wa rohoni haogopi kufa. Kufa ni faida na kuishi ni Kristo. Kumbuka habari za Stefano. Alishtakiwa kwa uongo. Wakati anajitetea mbele ya wazee wa baraza, walimsagia meno kwa hasira. Hakuogopa vitisho vyao kuwa watamuua, badala yake alifurahi na kuwaambia anaona mbingu zimefunuliwa(Matendo 7:55-56).
 
Nani kakuambia huo mtazamo ni wa Atheists? Je wana hati miliki ya hayo maneno?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…