Yajue masuala mbalimbali kuhusu Biashara ya kuuza Juisi ya matunda ya aina mbalimbali

Yajue masuala mbalimbali kuhusu Biashara ya kuuza Juisi ya matunda ya aina mbalimbali

Shostiee fika hapa kariakoo utapata juicers na dispencers na extracors za juice aina nyingi bei ya kushindana. bishara hiyo ni nzurilakini uwepo mwenyewe, laa sivyo utaibiwa sana !

Asante shost angu wa ukweli, nashukuru sana japo sipo dar kwa sasa, nikija Dar nitaziangalia pia. Nashukuru kwa ushauri ndugu yangu. Tupo pamoja
 
Kama uko Dar es Salaam jaribu kutembelea siku moja Chuo cha D.I.T pale uone, kuna jamaaa ana kamtaji seems ni kadogo sana ila anapiga hela ya ajabu sana kwa kuuza "FRUITS" yaani ile mixture ya matunda yaliyopondwa pondwa na kuchanganywa kwa pamoja bila kuyasaga.

Jamaa anapiga sana pesa maana ubunifu wake ni mzuri na watu wananunua ile kitu for luxury tu na out of curiosity lakini ukishanunua huwezi kuacha maana ni matunda fresh na ameyachanganya kwa ubunifu mzuri.

Ukipata sehemu yenye mkusanyiko wa watu wengi ukawa unauza hio kitu unatoka maana seems watu wanapenda sana hii "fruit" kuliko matunda magumu au juisi iliyosagwa, any way ni idea tu unaweza kuifanyia kazi kabla ya kuifanyia impelementation

Mkuu, kweli jamii forum ni darasa tosha, nimepata elimu nzuri sana na kiukweli mmenitia moyo sana wanajf, Nakushukuru sna mkuu kwa kunitia moyo katika hili.

Natamani nimpate huyo mjasi mwenzangu anijuze mbinu alizoanza nazo ila ndo hivo nipo mbali, acha nipambane kwanza kwa huku, then siku nikienda dar, nitajaribu kwakweli kuonana naye, ni vizuri kujifunza kwa waliofanikiwa mkuu. Nakushukuru mno na tena. Tupo pamoja
 
Hii Biashara inalipa sana ukiwa sio bahili kwa wafanyakazi wako. Wengi inawashinda kwa kutowajali wahusika. Unatakiwa kwanza uwe msafi na pia jaribu kuwa unaibadilisha ladha ili isiwe common.

Na kama unaweza basi tengeneza za aina tofauti. Mfano Dar matunda ni mengi sana. Niliwahi kuifanya hii mtaani ilikuwa inatoka licha ya changamoto za kutorejeshwa chupa.

Unaweza kuwa unatengeneza Juice ya ina moja, mfano ya Ukwaju, Avocado, Stafeli (hii unaweza kuuza mpaka ukachanganyikiwa), na pia unaweza kufanya ya kuchanganya.

Juice ya Stafeli ni nzuri sana kama vile ya avodaco,ni bora uuze ghali upate faida kidogo ila ubora uwe mzuri. Watu wengi wanafanya Juices za kuchanganya, Embe, Peshen, Nanasi, Tangawizi kidgo, nk, kwakuwa ni rahisi na pia mchananyiko wake unatoa faida kubwa. Lakini tambua kwamba baadhi ya Juice za kujitegemea pia nazo zina faida pia. Hapo watu wanakimbia labda wingi, mfano Stafeli au avocado inabidi liwe lakutosha na huifanya iwe juice nzito kiasi.

Muhimu ni kwamba walipe wafanyakzi wako vizuri itakulipa na mungu atakuongezea. Kuna mama nilimuona Ilala anauza lakini anawadhulum wafanyakazi wake balaa, Mungu hawezi kukubariki kwa kutaka faida kubwa.Utakuta unafanya baada ya muda unafunga biashara au utatafuta Mganga.

Pia ukipata pesa nunua hata Pikipiki zile ndogo uweke Tenga nyuma ili uwe unachukua mzigo mwenye Pale Buguruni mida ya Jioni matunda yanamwaga karibu ya Bure. Kuliko kumpa Carry ambapo lazima atakubana. Mtaji ukikua nunua Carry unakuwa unapiga mzigo mwenyewe.

Hata Mbuyu ulianza kama Spinach
 
Naomba Kuuliza Je machine na manual ya kutengeneza juice ya miwa naweza kuipata kwa bei gani? & ya umeme nayo inaweza oatikana kwa bei gani?

shukrani kwa wote
 
Salam sana wakuu.

Nilipo nimeona fursa ya kuanzisha biashara ya natural juice na popcorn..nataka kujua vitu vitu vifuatavyo
-Bei ya popcorn machine
-Bei ya blender kubwa
--Bei ya juice machine ile ya kuuzia
-Bei ya blender kubwaa ya kutengeneze hizo juice
-Vifungashio vya ki..sasa napata wapi
Na chochote cha kunisaidia
 
Kaka napita na haraka.
WEewe kichwa.
Hii biashara ukikomaa inalipa ile mbaya.Ninaposema kulipa ile mbaya kulingana na nature yake.
Nakushari kama upo Dar nenda pale Kariakoo,viu vyote hivyo vipo.
Maana hapa hata ukishauriwa ni kwamba aina zote ulizotaja hapo juu zina Size kulingana na ujazo wake.

Kwa kujazia hapo,nakushauri
-Tafuta mashine ya Juice ila ya Port mbili hadi tatu,ili iwe rahisi kuuza juice za aina zaidi ya moja.
-Najua hapo utahitaji Freezers
-Ongezea kwa kuuza Fresh fruites,usiuze zile za kiswahili sana za papai telee,matangao ya kutupia halafu unakoroga,huo ni uji sio Fruite. Uza ile ya vipande kwa mfumo wa packing na mfumo wa kula hapo hapo.Hii inalipa sana mkuu,Dar matunda mengi sana ila ndio mkoa wa watu wanoongoza kwa uvivu wa kujimenyea matunda wao wenyewe.

-Nakushauri katika biashara hii usiweke Juice za viwandani,kwanza ni kujaza Banda bila sababu,pili faida yake inaweza kuathiri mapato ya upande wa pili. Tambua kwamba kitu chochote unachoweka kwenye freezer au fridge lazima kupata baridi kitumie moto,na fridge au freezer hufanyakazi kulingana na idadi ya vitu vilivyomo ndani yake ili compressor iweze kuvuta umeme.Sasa biashara za faida ya shilingi 50 na zinahitaji umeme katika mfumo unaotaka kuanza wewe zitakugharimu bila kujua.

-Hakiisha fremu yako ya biashara isiwe kijiwe,watu wengie wenye kupenda kutumia kwenye mabanda hayo,huwa wanapenda kuona banda ni rafiki wa mteja na sio banda kama kijiwe cha kumnyima uhuru mteja.

-La zaidi,ukipata Mashine ya Ice cream na ukawa umepeta mafunzo ya utengenezaji wake basi hapo miguu juu.
Ila hesabu ya mashine hii ni ndefu sana,3.5 - 5m size ya kawaida outlets mbili

Nikumbuka lingine nitakuja
 
mi naomba tuwe patners katika hili. nilishawahi kufanya biahsra hii... kuna machine moja inatengeneza juice kukamua na kufreze yenyewe... inauzwa laki nane lakini ilikuwa ya kichina ghafla ikaharibika.... na kushindwa kupona na pesa ingine nikawa sina so nikakosa space ile. vipi wewe ushapata sehemu ya kuweka. ni pm pia
 
Mkuu Fanya Uni PM na Mimi.
mi naomba tuwe patners katika hili. nilishawahi kufanya biahsra hii... kuna machine moja inatengeneza juice kukamua na kufreze yenyewe... inauzwa laki nane lakini ilikuwa ya kichina ghafla ikaharibika.... na kushindwa kupona na pesa ingine nikawa sina so nikakosa space ile. vipi wewe ushapata sehemu ya kuweka. ni pm pia
 
Wadau naomba msaada kujua kiasi cha mtaji kinachotakiwa kuanzisha biashara ya kuuza matunda mchanganyiko pamoja na changamoto zake pia
 
Safi Sana mkuu uko na wazo kama langu nimetamani kuanza kuanzisha hii kitu kama upo dar Tuwasiliane tupeane mawazo
 
Nibiashara nzuri na pia hata ukiwa na mtaji mdogo waweza Fanya na kukuingizia kipato kizuri Tu. Changamoto ni chache ikiwemo kupata mzunguko mkubwa na pia kuchagua matunda yaliyo bora, upatikanaji wa matunda kwa hapo Dar naweza sema ni rahisi hivyo kazi kwenu vijana.
 
Iko poaaa sna tu mi hapa nilipo kina jamaaa zangu wanauza maisha sio haba wanapata pesaaa
 
Ninampango wa kuanzisha fresh juice kwa kutumia baiskeli ya miguu mitatu kwa kuzungukia wateja!

Nina mpango wa kuiuza juisi hii siku za weekend,hasa nikilenga kuuzuia mashabiki wa ligi ya uingereza na zinginezo ktk kumbi zinazoonesha mpira!

Nina mpango wa kubandika stickers za timu za ligi mbalimbali ktk glasi za wateja! Mathalani shabiki wa arsenal akipenda anaweza serviwa juice yenye sticker ya Giroud!

Na pia kujaribu kubandika picha za wachezaji ktk baiskeli yangu,misimamo ya ligi,top scorers,kupiga nyimbo za timu,na other infos!

Pia kutoa free juices kwa mashabiki watakaojibu maswali ya mpira,hasa ligi ya simba na yanga!
Naomba ushauri jinsi ya kuboresha wazo hili?
 
Back
Top Bottom