November 4 , 2019
Dar es Salaam, Tanzania
Majaji 12 wapya wa Mahakama Kuu walioteuliwa, wala viapo vyao leo katika Ikulu ya Dar es Salaam nchini Tanzania mbele ya Mh. Rais John Pombe Joseph Magufuli.
Walioteuliwa ni;
Dkt. Zainabu Diwa Mango, Kabla ya uteuzi huu Dkt. Zainab Diwa Mango alikuwa Wakili wa Serikali Mkuu katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.
Edwin Elias Kakolaki, Kabla ya uteuzi huu Edwin Elias Kakolaki alikuwa katika Ofisi ya Kupambana na Kuzuia Dawa za Kulevya Nchini.
Dkt. Deo John Nangela, Kabla ya uteuzi huu Dkt. Deo John Nangela alikuwa katika Ofisi ya Tume ya Ushindani (Fair Competition Commission – FCC).
Fredrick Kapela Manyanda, Kabla ya uteuzi huu Fredrick Kapela Manyanda alikuwa katika Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.
Elizabeth Yoeza Mkwizu, Kabla ya uteuzi huu Elizabeth Yoeza Mkwizu alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani.
Augustine Karichuba Rwizile, Kabla ya uteuzi huu Augustine Karichuba Rwizile alikuwa Naibu Msajili wa Mahakama.
Ephery Sedekia, Kabla ya uteuzi huu Ephery Sedekia alikuwa Katibu wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Attorney General – AG).
Angaza Mwaipopo, Kabla ya uteuzi huu Angaza Mwaipopo alikuwa katika Ofisi ya Rais, Ikulu.
Joachim Charles Tiganga, Kabla ya uteuzi huu Joachim Charles Tiganga alikuwa Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Kassim Ngukali Robert, Kabla ya uteuzi huu Kassim Ngukali Robert alikuwa katika Ofisi ya Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu cha Wizara ya Fedha na Mipango.
Said Mashaka Kalunde, Kabla ya uteuzi huo, Said Mashaka Kalunde alikuwa katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Angela Antony Bahati, Kabla ya uteuzi huo, Angela Antony Bahati alikuwa Katibu Msaidizi wa Tume ya Kurekebisha Sheria.
Maneno ya Jaji Mkuu wa Tanzania:
Jaji Mkuu wa Tanzania awataka Majaji walioapishwa kufuata Sheria Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma, amewataka Majaji 12 wa Mahakama Kuu walioteuliwa na baadaye kuapishwa na Rais John Magufuli, kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria na kamwe wasifanye upendeleo.
Akizungumza wakati wa hafla ya kuwaapisha Majaji hao pamoja na viongozi wengine Ikulu jijini Dar es salaam, Jaji Mkuu amesisitiza kuwa Majaji hawana Polisi wa kuwachunga, hivyo vi vema wakajichunga wenyewe na kujitathmini kila wakati wakifanya kazi zao.
Jaji Mkuu amesema kuwa mashauri bado ni mengi yanayohitaji kufanyiwa kazi haraka, hivyo ni vema wakahakikisha wanayafanyia kazi na kuhakikisha hukumu zinatoka kwa wakati.
Amemshukuru Rais Magufuli kwa kuiongezea Mahakama Kuu Majaji 12, na kuongeza kuwa kwa sasa Mahakama Kuu itakuwa na Majaji 78 kutoka 66 waliokuwepo hapo awali. Amesema kuwa kwa ongezeko hilo, Jaji mmoja wa Mahakama Kuu kwa sasa itakua na uwezo wa kushughulikia mashauri 220 kwa mwaka, badala ya mashauri 518 ambayo walikuwa wakiyashughulikia kabla ya ongezeko la Majaji hao 12.
Halfa ya kuwaapisha Majaji hao pamoja na viongozi wengine, pia imehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, - Job Ndugai.