Yaliyojiri Ikulu Dar: Rais Magufuli amtaka CAG Kichere kutojifanya Muhimili mwingine, amwambia anaweza kuondolewa hata akiwa na mwaka mmoja

Yaliyojiri Ikulu Dar: Rais Magufuli amtaka CAG Kichere kutojifanya Muhimili mwingine, amwambia anaweza kuondolewa hata akiwa na mwaka mmoja

Kama Charles Kicheere ana akili nzuri, angeikataa kazi hii ya CAG. Naona atapata shida sana kwenye awamu zitakazokuja baada ya Magufuri. Amepewa nafasi kwenda kukiuka misingi ya u-CAG

Hivi zitakuwepo kweli awamu zingine?
Na ikiwepo tuombe lisijetoka jiwe kikaja kiazi.
 
jaji mfawidhi,

Kuna utofauti kati ya kipindi na Miaka. Katiba imesema miaka ila imetoa nafasi kwa sheria kuangalia kuweka umri wowote unaofaa... Sheria imeweka vipindi wa utawala wa CAG na haijaweka ulazima wa kuteuliwa tena. phrase 'shall be eligible' humaanisha kuwa na vigezo stahiki (having necessary quality/satisfy requirements)

Therefore katika kipindi cha pili CAG anaweza kuwa na vigezo stahiki lakini sio lazima ateuliwe tena. huenda unachoweza kukimbia mahakamani kukichallenge ni legality ya kifungu cha 6(2) cha Sheria ya Hesabu za Umma juu ya vipindi hivyo viwili. Katiba imetaja miaka na sio vipindi.
 
Hivi zitakuwepo kweli awamu zingine?
Na ikiwepo tuombe lisijetoka jiwe kikaja kiazi.
Hata asipotoka kwa sanduku la kura atatoka kwa njia ambayo Mungu mwenyewe anajua. Hawezi kuiacha Tanzania kwenye mkono ya shetani.
 
Tutaona sasa sheria na Katiba ipi yenye nguvu. Maana tunaambiwa "when the law(s) contradict(s) with the constitution the constitution the constitution shall prevail"
 
Ni vyema kama umetambua kuwa Mfumo wa Uongozi wa JPM ni Data za upishi upishi na ujanja ujanja. Nakuhakikishia ripoti inayofuata itaonyesha faida kubwa sana kwenye mashirika ya UMMA. Tutasahau kabisa kuwa ATCL itamaliza kupata hasara mwaka 2023
kocha yoyote akiona mchezaji performance yake huwa anatoa anaweka mwingine ndicho kilichotokea hamna kingine ili apate matokeo mazuri ashinde mechi
 
Nasikia Assad kapata bonge la mkataba serikali ya Sweden
 
Influenza,

Rais anasema hawezi kupewa mamlaka ya kuteua akakosa mamlaka ya kutengua. Tumwulize anaweza kutengua uteuzi wa jaji mkuu ama jaji yoyote wa mahakama kuu?
 
Hivi Dodoma kashindwa kabisa kwenda uko? Nashindwa kuelewa kabisa ilikuwa ni siasa au mkakati nilitegemea mambo kama aya yafanyike Dodoma maana juzi tu kasema kashaamia uko.

Kwa hiyo wewe Technically unataka kumpangia rais shughuli zake? Kwa nini usingeuliza sababu? Mtakalia kuropokaropoka tu humu JF.
 
" Kwa CAG mpya nakutakia kazi njema, usije ukaenda huko ukajifanya na wewe ni mhimili, mihimili ni mitatu tu na umeiona hapa, na katika kiapo chako nilikuwa nakisikiliza nafasi yako ni Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, kwahiyo mwenye Serikali yupo "- @MagufuliJP #MwananchiUpdates

Hebu tujadili zaidi.
 
Sasa kajiteulia wa kulinda wizi wao wa kuchukua pesa BOT muda wowote kama ilivyokuwa kwa marehemu Mobutu Sese Seko wa Congo.

Grow up and be respectful to your president, huwezi kumlinganisha na huyo kichaa. Kuweni na shukrani na democracy ambayo ameileta JPM na kukuza uchumi wa Tanzania. JK mlimwita Vasco Da Gama na mnafahamu Hazina hakukuwa na fedha alipoondoka hata vifaranga vyake vilikuwa na biashara huyu anafanya juhudi za kufufua uchumi mnaanza tena hadithi za Abunuwasi na Bulicheka.
 
Huo Ndio ukweli

CAG sio muhimili wa serkali ila ni mfanyakazi wa serkali

Huyu CAG Mstaafu aliingizwa kichwa na wanasiasa wachumia tumbo akajiona Ndio mwamba

Akapumbumzike alee wajukuu
 
Tutaona sasa sheria na Katiba ipi yenye nguvu. Maana tunaambiwa "when the law(s) contradict(s) with the constitution the constitution the constitution shall prevail"
Inabidi ikatafutwe tafsiri ya kimahakama na baada ya hapo ndipo mabadiliko yafanywe kuputia Bunge.
 
Nafuatilia mnyukano wa kikatiba na kisheria unaoendelea baada ya Rais kuteua CAG mpya.

Huyo CAG mpya ni ACPA 1450 ila sio active member 1.7.2019, kama sio active member anakosa sifa. Hebu chungulia hapa ujionee: Orodha ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu |BODI YA TAIFA YA WAHASIBU NA WAKAGUZI WA HESABU TANZANIA (NBAA).

Aliyekuwa hafai TRA Sasa ameteuliwa kuwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali! Yajayo yanafurahisha!!
Raia wanauliza sasa Mahesabu yake akiwa TRA ana uhalali wa kuyakagua?
Je, matumizi ya ofisini akiwa RAS Njombe atakuwa na uhalali wa kuyakagua?
Hakuna rangi hatutaona at this Regime

Taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Prof. Mussa Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano kwenye nafasi hiyo. Lakini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (ambayo ndio sheria mama) haelezi hicho kinachoitwa "kipindi cha miaka mitano"

Katiba inaeleza kuwa CAG atakoma utumishi wake atakapotimiza umri wa miaka 60. Yani akifikisha umri wa miaka 60 anapumzika bila kujalisha ametumikia nafasi hiyo kwa muda gani. Iwe miezi miwili, miaka nane, au miaka kumi.

Ndio maana maCAG wote waliotangulia wameongoza ofisi hiyo kwa vipindi tofauti. Mzee Mohamed Aboud aliongoza kwa miaka 27 tangu 1969 hadi 1996. Thomas Kiama akaongoza kwa miaka 9 tangu 1996 hadi 2005. Ludovick Utouh akaongoza kwa miaka 8 tangu 2006 hadi 2014. Sasa hii kauli ya kusema Assad amemaliza kipindi chake cha "miaka mitano" imetoka wapi?

Matakwa ya kikatiba ni umri wa miaka 60, unless aondolewe kwa kushindwa kutimiza majukumu yake. Na ikitokea hivyo Katiba imeweka utaratibu wa kumuondoa kwa kuunda tume.

Lakini taarifa ya Ikulu inaeleza Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano. Je hiki kipindi cha miaka mitano Ikulu wamekitoa wapi? Kwenye sheria ipi? Kama ipo sheria hiyo ipo ni batili maana inapingana na katiba.

Na kwa kawaida unapotokea mgogoro kati ya sheria na katiba, basi Katiba ndiyo inayoshika hatamu (When a state law conflicts with a Constitution, then constitution prevails because constitution rules supreme above all state laws).
_
Prof.Assad amezaliwa tar.06 October mwaka 1961. Kwa sasa ana umri wa miaka 58. Atafikisha umri wa miaka 60 October 06 mwaka 2021. Hivyo nadhani kwa mujibu wa KATIBA Assad alipaswa kustaafu nafasi yake ya CAG akifikisha umri huo, na si kwa hiki kinachoitwa "miaka mitano". I stand to be corrected. Hoja hujibiwa kwa hoja, sio bunduki.!

1.0 Kwa mazingira haya hana sifa ya kuwa auditor kwa kuwa amesajiliwa na NBAA kama mhasibu na sio auditor. Auditor kwa sheria ilivyo anaweza akawa mhasibu ila mhasibu sio auditor. Ina maana auditor ni superior kuliko mhasibu.

2.0 Hayuko kwenye active members wa 1.7.2019 yaani (2018/2019). Hivyo hana Certificate of Practice hata ya uhasibu ya 2018/2019.

Nimeona kuna migawanyiko ya hoja, upande wa kusifu na kuabudu unaongonzwa na VIBAKA wa Lumumba wao wanatetea uteuzi huu kwakutumia Sheria iliyoanzisha hiyo Ofisi( The National Audit Act 2008) inayo-specify 5 years terms na umri ni 65 year. Na kwamba hapa Rais ndipo katumia.

Upande wa kundi jadidi lenye akili na weledi, lenye busara na hekima ya nera una hoja za kikatiba sio za kisheria. Ikulu imeeleza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Prof.Mussa Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano kwenye nafasi hiyo.

Wakili msomi Emmanuel Chengula anafafanua kwa kusema kwamba, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (ambayo ndio sheria mama) haelezi hicho kinachoitwa "kipindi cha miaka mitano"

Katiba inaeleza kuwa CAG atakoma utumishi wake atakapotimiza umri wa miaka 60. Yani akifikisha umri wa miaka 60 anapumzika bila kujalisha ametumikia nafasi hiyo kwa muda gani. Iwe miezi miwili, miaka nane, au miaka kumi.

Ndio maana maCAG wote waliotangulia wameongoza ofisi hiyo kwa vipindi tofauti. Mzee Mohamed Aboud aliongoza kwa miaka 27 tangu 1969 hadi 1996. Thomas Kiama akaongoza kwa miaka 9 tangu 1996 hadi 2005. Ludovick Utouh akaongoza kwa miaka 8 tangu 2006 hadi 2014. Sasa hii kauli ya kusema Assad amemaliza kipindi chake cha "miaka mitano" imetoka wapi?

Matakwa ya kikatiba ni umri wa miaka 60, unless aondolewe kwa kushindwa kutimiza majukumu yake. Na ikitokea hivyo Katiba imeweka utaratibu wa kumuondoa kwa kuunda tume.

Lakini taarifa ya Ikulu inaeleza Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano. Je hiki kipindi cha miaka mitano Ikulu wamekitoa wapi? Kwenye sheria ipi? Kama ipo sheria hiyo ipo ni batili maana inapingana na katiba.

Na kwa kawaida unapotokea mgogoro kati ya sheria na katiba, basi Katiba ndiyo inayoshika hatamu (When a state law conflicts with a Constitution, then constitution prevails because constitution rules supreme above all state laws).
_
Prof.Assad amezaliwa tar.06 October mwaka 1961. Kwa sasa ana umri wa miaka 58. Atafikisha umri wa miaka 60 October 06 mwaka 2021. Hivyo kwa mujibu wa KATIBA alipaswa kustaafu nafasi yake ya CAG akifikisha umri huo, na si kwa hiki kinachoitwa "miaka mitano".

Kumbuka, Kicheere alitumbuliwa June 8, 2019 baada ya kutuhumiwa na wafanyabiashara kuwafanyia bugudha na kuua biashara zao, Alikuwa kamishna wa TRA. Leo kateuliwa kuwa CAG!

Nchi ina maigizo mengi hii. Bahati mbaya wanaoigiziwa hawajui lolote. Charles Kicheere alitumbuliwa kwa tuhuma za uzembe katika usimamizi wa TRA na kubugudhi wafanyabiashara sasa ameteuliwa anakwenda kuwa Msimamizi wa uadilifu katika mifumo ya fedha na UKAGUZI.

Mtu aliyeonekana kupwaya TRA (Kicheere) anapewa sasa kwenda kusimamia UKAGUZI wa mahesabu ya serikali. Kusimamia ukusanyaji wa mapato alishindwa, tukaaminishwa hivyo, ataweza kweli kudhibiti na kukagua HESABU za umma? Anyways, tuendelee kuona maajabu!

Wakili Chengula amemaliza kwakusema, I stand to be corrected.!

Katika hatua nyingine, Mbunge Zitto Kabwe ameongeza utata wa uteuzi wa CAG mpya kuonyesha kuwa hana sifa ya kushika ofisi hiyo kubwa ya umma iliyoanzishwa na katiba ya nchi sio na sheria,

Zitto anasema, "Charles Kicheere hana sifa za kuwa CAG kwa mujibu wa Katiba. Hana record ya ku-practice Auditing. Rais Alipomwondoa Kicheere TRA alimsema kuwa hajui kazi. Leo anampatia kazi kubwa hii huku akiwaacha 4 Deputies CAG. Uteuzi huu ni wa kuficha wizi (miradi mikubwa)"

CAG Musa Asad ameonekana kushangazwa na uteuzi huo na amenukuliwa na chombo cha habari kuwa hata taarifa hizo na yeye yuko katika majukumu ya kiutendaji. Hapa ndipo mkanganyiko unapozidi.

Kwa maoni yangu, nawauliza, ni lini utawala huu uliwahi kufuata sheria na katiba ya nchi kwa 100% katika utendaji wake? Mnakumbuka kesi ya uteuzi wa AG?
Umejitahidi kufafanua lakini huyo Magufuli keshaamua hivyo, ingewezekana mtu kuombewa mauti ningewashauri mumuombee lakini ndio hivyo tena.
 
Back
Top Bottom