Yaliyojiri katika Chaguzi Ndogo: Uchaguzi wa ubunge jimbo la Dimani na madiwani Tanzania Bara

Yaliyojiri katika Chaguzi Ndogo: Uchaguzi wa ubunge jimbo la Dimani na madiwani Tanzania Bara

CCM, Sio vyema kujisifu kwa ushindi kwenye chaguzi zinazoendeshwa kihuni namna hii?

Hivi CCM hamuoni aibu kusema mmeshinda kwenye chaguzi zilizotamalaki figisu figisu za wazi namna hii?
Mimi nafikiri umefika watu wakakataa kushiriki upigaji kura kabisa, vinginevyo uchaguzi ujao ccm itawapunguza wapinzani kwa wizi wa kura kwa sababu wanasaidiwa na polisi ambao ni wanaccm wenzao.
 
Uchaguzi wa Jimbo la dimani hadi sasa ni machafuko matupu, mawakala wa cuf wametolewa kwenye vyumba vya kupiga kura kwa sababu ya KUGUNDUA na KUHOJI mambo yafuatayo:

Wamegundua baadhi ya masanduku yamejazwa kura ambazo zimeshatiwa tiki kwa mbunge wa ccm

Wamegundua kuwa kuna watu hawamo ndani ya daftari la kupiga kura ila wamekuja kupiga kura na walipo pinga MAWAKALA WETU, (kaa Mujib wa Sheria na Kanuni za Sheria za Uchaguzi) JESHI LA POLISI waliwakunja na kuwatoa Nje

Chumba number 6 imegundilikana kwamba masunduku yote yamejazwa kura

MAPANDIKIZI NI MENGI YAKILINDWA NA KUSINDIKIZWA NA JESHI LA POLISI.

Mazombi waanza kupiga watu maeneo ya fuoni kituo cha kibondeni
Hali ikoje kwa sasa mkuu
 
Makamanda ina maana leo mmekuwa wavivu hata kutupa matokeo ya kata au kituo kimoj? Basi hata ya jimbo la Arumeru mnatunyima makamanda wenzenu? kwakweli mbona mnatuangusha makamanda? au hamkushiriki kabisa?
 
CCM inaongoza Maeneo mbalimbali ya Nchi kuanzia Ubunge Zanzibar na chaguzi ndogo za huku Bara. Imani ya Wananchi kwa Serikal Yao na Chama cha Mapinduzi imerejea

Matokeo ya uchaguzi yanafahamika toka muda ulipotangazwa uchaguzi, leo ni kuuhadaa tu ulimwengu kwamba kuna demokrasia. Matokeo yote yanatakiwa ccm ishinde ili kuonyesha kwamba wananchi wana imani sana na ccm. Kwa hiyo wala hakuna cha kushangilia hapo mshindi ameshachaguliwa na tume.
 
*MATOKEO YA CHAGUZI NDOGO NCHINI:SOMO KWA UPINZANI?*

: *ubunge jimbo la Dimani CCM Imeshinda kwa kishindo kura 4408 na cuf 1204..*

*Kata ya Ng'hambi Wilaya Mpwapwa CCm1306 chadema 812*

*Matokeo Ya jumla ngarenanyuki. Ccm 1615 chadema 764 cuf 11*.

*Kahama Tumeshinda kwa kura 539ccm na342 chadema*

*K/ndege Morogoro CCM 1384 cdm 1189 cuf 218*

*Mkoa wa Mwanza kata zote 2 tumeshinda kwa kishindo! Malya (Kwimba), na Kahumulo (Sengerema)*

*Kata ya Kwani muleba kati ya vituo 26. Ccm inaongoza vituo 20 kwa kura 526...Bado matokeo ya vituo 6*
 
Kwa nini ukawa hawajaweka mgombea mmoja kama mwaka 2015?
Mfano k/ndege wangeshinda ukawa
 
Matokeo ya uchaguzi yanafahamika toka muda ulipotangazwa uchaguzi, leo ni kuuhadaa tu ulimwengu kwamba kuna demokrasia. Matokeo yote yanatakiwa ccm ishinde ili kuonyesha kwamba wananchi wana imani sana na ccm. Kwa hiyo wala hakuna cha kushangilia hapo mshindi ameshachaguliwa na tume.

Sasa Kama Mlijua hayo kwanini mlishiriki UchaguZi ? Tushawazoea hamtupi shida!
 
Awamu ya magufuli imezika kabisa misingi ya muasisi wa taifa hili wa haki na usawa. Na kinachoonekana wazi ndani ya taifa la Tanzania ni kiu ya kiwango kikubwa ya kumwaga damu.
Tukifika hapo ndo adabu na heshima itapatikana kila mtu atamuona mwenzie anafaa na niwamuhimu

Sent from my HUAWEI LUA-L21 using JamiiForums mobile app
 
Sasa Kama Mlijua hayo kwanini mlishiriki UchaguZi ? Tushawazoea hamtupi shida!

Mimi sijashiriki ila nilitoa angalizo kwa wapinzani kuliko kupoteza raslimali muda na fedha kushiriki uchaguzi wa tume isiyokubalika ni kupoteza muda. Pia niliwataka ili kuweka mazingira ya kuwa na tume huru ya uchaguzi hiyo 2020 ni kuanza kususia hizi chaguzi ndogo kwani matokeo yake yatatangazwa kuendana na hofu ya watawala. Hayo matokeo wala hayanishangazi bali ninawashangaa wapinzani wamepata wapi muda na fedha za kupoteza?
 
*MATOKEO YA CHAGUZI NDOGO NCHINI:SOMO KWA UPINZANI?*

: *ubunge jimbo la Dimani CCM Imeshinda kwa kishindo kura 4408 na cuf 1204..*

*Kata ya Ng'hambi Wilaya Mpwapwa CCm1306 chadema 812*

*Matokeo Ya jumla ngarenanyuki. Ccm 1615 chadema 764 cuf 11*.

*Kahama Tumeshinda kwa kura 539ccm na342 chadema*

*K/ndege Morogoro CCM 1384 cdm 1189 cuf 218*

*Mkoa wa Mwanza kata zote 2 tumeshinda kwa kishindo! Malya (Kwimba), na Kahumulo (Sengerema)*

*Kata ya Kwani muleba kati ya vituo 26. Ccm inaongoza vituo 20 kwa kura 526...Bado matokeo ya vituo 6*

[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Back
Top Bottom