Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe 26 Jan 2022. Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio kuendelea kutoa ushahidi wake

Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe 26 Jan 2022. Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio kuendelea kutoa ushahidi wake

Huyu ndiye yule Masih tuliyekuwa tunasubili au tumsubili mwingine?
😁😁😁😁 Jopo la utetezi MUNGU awatangulie huyu ndio kiungo muhimu aulizwe,abanwe,alazimishwe kujibu.jibu la sijui lisiwepo kwenye msamiati wa Leo.
 
Huyu ndiye yule Masih tuliyekuwa tunasubili au tumsubili mwingine?
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] Jopo la utetezi MUNGU awatangulie huyu ndio kiungo muhimu aulizwe,abanwe,alazimishwe kujibu.jibu la sijui lisiwepo kwenye msamiati wa Leo.
Cross examination ya huyu na jopo la utetezi ni paka j3 au j4 hawawezi kumuacha hivi hivi lazima wamchanganye hakane watu bila kujua
 
Barakoa kubwa kavaa sema anaongea kama kalazimishwa.
subiri kwenye Cross examination akikutana na Kibatala akiambiwa SHAHIDI NAKUKUMBUSHA UPO CHINI YA KIAPO, NAKUTAKA UJIBU .... Jibu NDIO au HAPANA ... atatoa tu sauti!!!
 
yanayojiri
Salaam Wakuu,

Leo tarehe 24/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe inaendelea.

Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.

Kujua kesi ilipoishia soma: Yaliyojiri kesi ya Mbowe 24/01/2022: Shahidi wa 11, H4347 Goodluck amaliza ushahidi wake. Shahidi wa 12 kuendelea tarehe 26/01/2022

UPDATES

- Jaji ameingia Mahakamani

- Kesi inatajwa


Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Ikikupendeza naitwa wakili Wa Serikali Robert Kidando nipo pamoja na wakili
  • Pius Hilla
  • Abdallah Chavula
  • Jenitreza Kitali
  • Nassoro Katuga
  • Esther Martin
  • Tulimanywa Majige
  • Ignasi Mwinuka
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na wakili
  • Nashon Nkungu
  • John Mallya
  • Dickson Matata
  • Maria Mushi
  • Khadija Aron
  • Seleman Matauka
  • Idd Msawanga
  • Michael Lugina
- Jaji anaita Washitakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja Wakili Peter

Kibatala: Mheshimiwa Jaji na sisi tupo tayari Kuendelea.

Jaji: Anakuwa Shahidi namba Ngapi?

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Anakuwa Shahidi namba 12 Shahidi anakwenda kuitwa Shahidi anaingia Mahakamani, Mrefu Mwembamba, Mweupe Kidogo

Jaji: Majina yako

Shahidi: Naitwa Luteni Denis Urio

Jaji: Umri

Shahidi: Miaka 42

Jaji: Kabila

Shahidi: Mchaga

Jaji: Dini yako

Shahidi: Mkristo

Jaji: Kazi yako

Shahidi: Askari Wa Jeshi la Wananchi Tanzania.

Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama, kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa wa kweli, kweli tupu, Mungu Nisaidie Wakili wa Serikali.

Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shahidi Ataongozwa na Wakili Abdallah Chavula

Wakili wa Serikali Abdallah Chavula anqsimama na Kwenda Kwa Shahidi
Wakili wa Serikali: Shahidi nitakuwa nakuuliza Maswali, Ukijibu utakuwa unamjibu Mheshimiwa Jaji, Naomba Uongee kwa Sauti Ya Juu

Shahidi: Sawa

Wakili wa Serikali: Tukumbushe Majina yako

Shahidi: Naitwa Luteni Denis Leo Urio

Wakili wa Serikali: Mkazi wa Wapi?

Shahidi: Mkazi wa Ngerengere Morogoro

Wakili wa Serikali: Unafanya Shughuli gani

Shahidi: Ni Mwajiriwa wa Jeshi la Wananchi Tanzania

Wakili wa Serikali: Kituo Chako Cha Kazi ni wapi

Shahidi: Ni Ngerengere Morogoro

Wakili wa Serikali: Kituo Chako Kinafahamika kwa Jina gani?

Shahidi: 92 KJ Ngerengere

Wakili wa Serikali: Cheo Chako ni Kipi

Shahidi: Luteni wa Jeshi

Wakili wa Serikali: Majukumu yako ni Yapi

Shahidi: Ni Platoon Commander Kuongoza Askari Walio Chini yangu

Wakili wa Serikali: Unaongoza Askari Wangapi

Shahidi: Afisa Mmoja na Askari 30

Wakili wa Serikali: Ni Askari gani wanayofanya kazi Katika Kikosi cha KJ 92

Shahidi: Ni Wanajeshi Waliopata Mafunzo Maalum, Komando

Wakili wa Serikali: tuambie Wewe Umetumikia Jeshi Kwa Miaka Mingapi

Shahidi: Miaka 18

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama ulijiunga na Jeshi la Wananchi Tanzania Mwaka gani

Shahidi: Tarehe 16,June 2003

Wakili wa Serikali: Jeshi la Wananchi Tanzania lina Majukumu yepi

Shahidi: Lina Majukumu ya Ulinzi wa Mipaka dhidi ya Uvamizi Wa Ndani na Nje

Wakili wa Serikali: Jukumu lingine ni lipi

Shahidi: Kwenye Operation ya Ulinzi Wa Amani Kwenye Mataifa yenye Mgogoro

Wakili wa Serikali: Umesema Wewe ni Luteni wa Jeshi, Je Umekuwa Kwenye Nafasi hiyo kwa Miaka Mingapi

Shahidi: Kwa Miaka 6

Wakili wa Serikali: Umeeleza Mahakama Kwamba Miongoni Mwa Majukumu ya Jeshi ni Kuleta Amani Kwenye Mataifa Mengine, Ushiriki wako ni Vipi

Shahidi: Nimeshirriki Kulinda Amani 2011 Nchini Sudani, Na 2019 ni Sudan hiyo hiyo Jimbo la Darfur

Wakili wa Serikali: Tueleze Mahakama Kule Darfur ulipo enda Majukumu yako yalikuwa yepi

Shahidi: Kuhakikisha Wale Staff Officer (Wapatanishi) Ku Ensure Usalama wao Kwa Sababu Wao ni Unarmed Personnel

Wakili wa Serikali: Kuna Mtu anafahamika Kwa Jina la Khalfani Bwire Unamfahamu Vipi

Shahidi: Nina Mfahamu Kwa Muda Mrefu, Nili Mtrain, Nikifanya naye Kazi Kituo Kimoja cha 92 KJ

Wakili wa Serikali: Umemfahamu Kuanzia Mwaka gani

Shahidi: Kuanzia 2006 Mpaka 2009

Wakili wa Serikali: Wakati Unamfahamu, yeye alikuwa ana Jukumu gani

Shahidi: alikuwa Kiongozi Mdogo, anaongoza,Ni Section Commander, alikuwa anaongoza Watu 9

Wakili wa Serikali: Cheo Chake Kilikuwa ni Kipi

Shahidi: Rank ya koplo

Wakili wa Serikali: Unaposema Ulifahamiana naye kuanzia 2006 Mpaka 2009 umamaam gani

Shahidi: Ukomo wake Ulikuwa Mwaka 2019

Wakili wa Serikali: Nini Kilitokea Mpaka I kafika Ukomo wake

Shahidi: alifukuzwa Kazi Jeshini

Wakili wa Serikali: Kwa sababu Zipi afukuzwe Kazi

Shahidi: Kwa Utovu wa Nidhamu

Wakili wa Serikali: Wakati Mwaka 2019 anafukuzwa + kazi Wewe Ulikuwa wapi

Shahidi: Kwenye Operation Ya Peace Keeping, Sudan Jimbo la Darfur

Wakili wa Serikali: Ni wakati gani Ulikuja Kufahamu Kwamba Khalfani Bwire alifukuzwa Kazi kwa Utovu wa Nidhamu

Shahidi: Ni 2020 Mwezi March Baada ya Kutoka Darfur

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama ni Mazingira Yapi Ulifahamu Kwa Yeye Kufukuzwa Kazi Jeshini

Shahidi: Nilipata Taarifa hizo kutoka Kwa Administration Officer of the Unit

Wakili wa Serikali: Administration Officer ndiyo nani?

Shahidi: Mtu anaye fuatilia Maisha ya Askari Wote Kikosini na Maafisa ya Jeshi, Pia ni Kiongozi

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mahusiano yenu na Khalfani Bwire tangu 2006 Mpaka 2019 yalikuwaje

Shahidi: Yalikuwa ni Mahusiano Mazuri tu, Ya Kiongozi na afisa wake.

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mahusiano yenu baada ya Ajira Kukoma yalikuwaje

Shahidi: Bado nilikuwa naendelea Kuwasiliana naye, Mawasiliano ya Kawaida tu

Wakili wa Serikali: Shahidi Kuna Mtu anaitwa Adam Hassan Kasekwa ama Jina Lingine anaitwa Adamoo.

Shahidi: Nafahamiana naye toka Mwaka 2012 ndipo alipofika Kwenye Unit ya 92KJ alifika Kwenye Mafunzo, Nikam' train, aka' pass Maana nilimpokea Mimi.

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama, Huyu Adam Kasekwa ama Adamoo alifanya kazi Jeshini Kwenye 92 KJ alifanya kazi Mpaka Lini

Shahidi: Mpaka Mwaka 2018

Wakili wa Serikali: Nini Kilimsibu Mwaka huo 2018

Shahidi: Alifukuzwa Kazi Jeshini.

Wakili wa Serikali: Alifukuzwa Kazi Jeshini Kwa Sababu zipi

Shahidi: Kwa Utovu Wa Nidhamu

Wakili wa Serikali: Mpaka anafukuzwa Kazi Jeshini Kwa Utovu, Je alikuwa na Cheo gani

Shahidi: alikuwa Private Soldier.

Wakili wa Serikali: Unaposema Private Soldier Unamaanisha nini

Shahidi: Ni Askari ambaye hana Rank inayo kuwa Displayed, Ni Askari anayekuwa Chini ya Kiongozi Wake

Wakili wa Serikali: Wakati Adam Kasekwa anafukuzwa kazi Wewe Ulikuwa upo wapi

Shahidi: Nilikuwa Nipo Arusha.

Wakili wa Serikali: Ni wakati Gani Ulikuja Kufahamu Kwamba Adam Kasekwa kafukuzwa Kazi Jeshini

Shahidi: Baada ya Kurudi Kwenye Kituo Changu Cha Kazi Kutoka Arusha Kwenye Kozi

Wakili wa Serikali: Taarifa za Yeye Kufukuzwa Kazi Kwa Utovu Wa Nidhamu Wewe Ulizipata Wapi?

Shahidi: Administration Officer

Wakili wa Serikali: alikupatia Taarifa Hizo Mkiwa katika Mazingira gani

Shahidi: Ofisini Kwake

Wakili wa Serikali: Mazingira ya Mahusiano Baina ya Wewe na Adam Kasekwa yalikuwa Je Kipindi Kile Kabla ajafukuzwa Jeshi.

Shahidi: Yalikuwa Mazuri tu

Wakili wa Serikali: VIpi Baada ya Yeye Kufukuzwa Kazi na Kuondoka Jeshini yalikuwaje

Shahidi: Yalikuwa Mazuri

Wakili wa Serikali: Shahidi Kuna Mtu Naitwa Mohammed Abdilah Ling'wenya Unamfahamu Vipi

Shahidi: Namfahamu Nilifanya naye Kazi Kituo Kimoja

Wakili wa Serikali: Kituo Gani hicho

Shahidi: 92 KJ

Wakili wa Serikali: umeanza Kufanya naye Kazi huyo Mohammed Ling'wenya kuanzia Mwaka gani Mpka Mwaka gani

Shahidi: Kuanzia Mwaka 2010 Mpaka Mwaka 2017

Wakili wa Serikali: Nini Kilitokea Mwaka 2017

Shahidi: alifukuzwa Kazi Kwa Utovu Wa Nidhamu

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mpaka anafukuzwa Kazi, alikuwa ana Cheo gani Katika Jeshi

Shahidi: Alikuwa ni Private Soldier

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Unaposema Private Soldier Unamaanisha nini

Shahidi: Ni Askari Mwenye Cheo Cha Mwisho chini

Wakili wa Serikali: VIpi Kuhusiana na Mahusiano yenu

Shahidi: Tulikuwa na Mahusiano Mazuri

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Baada ya Yeye Kufukuzwa Kazi Kwa Utovu Wa Nidhamu, Mahusiano yenu yalikuwaje

Shahidi: Yaliendelea Kuwa Kama alipokuwa Kazini

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama wakati Mohammed Ling'wenya anafukuzwa kazi Wewe Ulikuwa Wapi

Shahidi: Nilikuwa Kwenye Kazi Maalum

Wakili wa Serikali: Ni Wakati Gani Ulikuja Kupata Ufahamu, kuwa Mohammed Ling'wenya amefukuzwa kazi

Shahidi: Baada ya Kurudi Kwenye Kituo Changu Cha Kazi, kutoka kwa Administration Officer

Wakili wa Serikali: Huyo Administration Officer alikupatia Taarifa Hizo Mkiwa katika Mazingira Yepi

Shahidi: Tukiwa Ofisini

Wakili wa Serikali: Unasema Unamfahamu Khalfani Bwire Je akiwa Miongoni Mwetu unaweza Kumtambua

Shahidi: Ndiyo naweza Kumtambua

Wakili wa Serikali: Sababu ipi itakufanya Umtambue

Shahidi: Nimefanya naye Kazi zaidi Ya Miaka 10, lakini pia Body Morphology

Wakili wa Serikali: Mtu huyo Yupo wapi

Shahidi: aliyepo Mbele yangu, Tunatizamana, Yupo Jirani na Magereza

Wakili wa Serikali: Pia Umemtaja Adam Kasekwa Maarufu Kama Adamoo, Je Unaweza Kumtambua

Shahidi: Ndiyo naweza Kumtambua

Wakili wa Serikali: Ni sababu Zipi hasa zitafanya Umtambue

Shahidi: Nimefanya naye Kazi zaidi Ya Miaka 5 lakini pia na Body Morphology Yake

Wakili wa Serikali: Hebu tuonyeshe Mtu huyo Yupo wapi

Shahidi: Ni Wapili Kutoka Kulia Mwa Khalfani Bwire

Wakili wa Serikali: tuambie Mwingine unaye Msema ni Mohammed Abdilah Ling'wenya, na Yeye Vipi Unaweza Kumtambua

Shahidi: Ndiyo naweza Kumtambua

Wakili wa Serikali: Sababu Ipi Itakufanya umtambue

Shahidi: Nimefanya naye Kazi zaidi Ya Miaka 5, pia Body Morphology yake, Tatu ana Makovu Usoni na Mkononi.

Wakili wa Serikali: Hapa Yupo wapi

Shahidi: Ni watatu Kutoka Upande Wa Kulia wa Bwire

Wakili wa Serikali: Shahidi isaidie Mahakama, Unasema Adam Kasekwa Na Mohamed Ling'wenya Walikuwa ni Private Soldier, Je pale Jeshini Walikuwa na Majukumu Yapi

Shahidi: Wao Ni watendaji wa Shughuli za Kijeshi

Wakili wa Serikali: Huyu Khalfani Hassan Bwire, Adam Hassan Kasekwa, Mohammed Abdilah Ling'wenya wakati wa Utumishi wao Wa Jeshi Pale 92 KJ Makazi yao yalikuwa wapi?

Shahidi: Walikuwa Wa naishi huko, Khalfani Bwire Ngerengere, Adam Kasekwa alikuwa Anaishi Chalinze katika Utaratibu Wa Misbehave

Wakili wa Serikali: Hapana Usiende Huko

Shahidi: Na Mohamed Ling'wenya na Yeye Chalinze
yanayojiri yako wapii mbona umekwama??
 
Huyu waliona wasingizie siku ya jana hawezi kufika Ili siku nzima amezeshwe desa la kuja Lutema Leo!
Haya,tusubiri tuone!
Shahidi huyu ni muhimu sana kwenye hii kesi!
 
Back
Top Bottom