Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Cross examination ya huyu na jopo la utetezi ni paka j3 au j4 hawawezi kumuacha hivi hivi lazima wamchanganye hakane watu bila kujuaHuyu ndiye yule Masih tuliyekuwa tunasubili au tumsubili mwingine?
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16] Jopo la utetezi MUNGU awatangulie huyu ndio kiungo muhimu aulizwe,abanwe,alazimishwe kujibu.jibu la sijui lisiwepo kwenye msamiati wa Leo.
Na yeye ndo alikua kiongozi wao Ngerengere,Kwahiyo commando anaenda kuwasagia kunguni makomandoo wenzake
Daah hatar Sana, ngoja tumsikilize maelezo yake maana tusije muhukumu bure.Na yeye ndo alikua kiongozi wao Ngerengere,
Huyu ni yule kina Bwire walisema walimuona akipigwa kule TAZARA. Huenda amelazimishwa kutoa ushahidi wa mchongo kwa usalama wake.Daah hatar Sana, ngoja tumsikilize maelezo yake maana tusije muhukumu bure.
Huyu ndiye atakaemaliza mchezo mzima na bongo muvi itaishia hapo!!😎Ngoja naye tumsikie, ana mapya gani!
Akiulizwa yeye ni jinsia gani atsema ni "MKRISTO"Huyu inabudi Mawakili wa utetezi warnde nae mpaka ijumaa apigwe maswali mpaka akitoka hapo akiulizwa we ni jinsia ya kike aseme ndiyo
subiri kwenye Cross examination akikutana na Kibatala akiambiwa SHAHIDI NAKUKUMBUSHA UPO CHINI YA KIAPO, NAKUTAKA UJIBU .... Jibu NDIO au HAPANA ... atatoa tu sauti!!!Barakoa kubwa kavaa sema anaongea kama kalazimishwa.
yanayojiri yako wapii mbona umekwama??Salaam Wakuu,
Leo tarehe 24/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe inaendelea.
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
Kujua kesi ilipoishia soma: Yaliyojiri kesi ya Mbowe 24/01/2022: Shahidi wa 11, H4347 Goodluck amaliza ushahidi wake. Shahidi wa 12 kuendelea tarehe 26/01/2022
UPDATES
- Jaji ameingia Mahakamani
- Kesi inatajwa
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Ikikupendeza naitwa wakili Wa Serikali Robert Kidando nipo pamoja na wakili
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na wakili
- Pius Hilla
- Abdallah Chavula
- Jenitreza Kitali
- Nassoro Katuga
- Esther Martin
- Tulimanywa Majige
- Ignasi Mwinuka
- Jaji anaita Washitakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
- Nashon Nkungu
- John Mallya
- Dickson Matata
- Maria Mushi
- Khadija Aron
- Seleman Matauka
- Idd Msawanga
- Michael Lugina
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja Wakili Peter
Kibatala: Mheshimiwa Jaji na sisi tupo tayari Kuendelea.
Jaji: Anakuwa Shahidi namba Ngapi?
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Anakuwa Shahidi namba 12 Shahidi anakwenda kuitwa Shahidi anaingia Mahakamani, Mrefu Mwembamba, Mweupe Kidogo
Jaji: Majina yako
Shahidi: Naitwa Luteni Denis Urio
Jaji: Umri
Shahidi: Miaka 42
Jaji: Kabila
Shahidi: Mchaga
Jaji: Dini yako
Shahidi: Mkristo
Jaji: Kazi yako
Shahidi: Askari Wa Jeshi la Wananchi Tanzania.
Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama, kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa wa kweli, kweli tupu, Mungu Nisaidie Wakili wa Serikali.
Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shahidi Ataongozwa na Wakili Abdallah Chavula
Wakili wa Serikali Abdallah Chavula anqsimama na Kwenda Kwa ShahidiWakili wa Serikali: Shahidi nitakuwa nakuuliza Maswali, Ukijibu utakuwa unamjibu Mheshimiwa Jaji, Naomba Uongee kwa Sauti Ya Juu
Shahidi: Sawa
Wakili wa Serikali: Tukumbushe Majina yako
Shahidi: Naitwa Luteni Denis Leo Urio
Wakili wa Serikali: Mkazi wa Wapi?
Shahidi: Mkazi wa Ngerengere Morogoro
Wakili wa Serikali: Unafanya Shughuli gani
Shahidi: Ni Mwajiriwa wa Jeshi la Wananchi Tanzania
Wakili wa Serikali: Kituo Chako Cha Kazi ni wapi
Shahidi: Ni Ngerengere Morogoro
Wakili wa Serikali: Kituo Chako Kinafahamika kwa Jina gani?
Shahidi: 92 KJ Ngerengere
Wakili wa Serikali: Cheo Chako ni Kipi
Shahidi: Luteni wa Jeshi
Wakili wa Serikali: Majukumu yako ni Yapi
Shahidi: Ni Platoon Commander Kuongoza Askari Walio Chini yangu
Wakili wa Serikali: Unaongoza Askari Wangapi
Shahidi: Afisa Mmoja na Askari 30
Wakili wa Serikali: Ni Askari gani wanayofanya kazi Katika Kikosi cha KJ 92
Shahidi: Ni Wanajeshi Waliopata Mafunzo Maalum, Komando
Wakili wa Serikali: tuambie Wewe Umetumikia Jeshi Kwa Miaka Mingapi
Shahidi: Miaka 18
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama ulijiunga na Jeshi la Wananchi Tanzania Mwaka gani
Shahidi: Tarehe 16,June 2003
Wakili wa Serikali: Jeshi la Wananchi Tanzania lina Majukumu yepi
Shahidi: Lina Majukumu ya Ulinzi wa Mipaka dhidi ya Uvamizi Wa Ndani na Nje
Wakili wa Serikali: Jukumu lingine ni lipi
Shahidi: Kwenye Operation ya Ulinzi Wa Amani Kwenye Mataifa yenye Mgogoro
Wakili wa Serikali: Umesema Wewe ni Luteni wa Jeshi, Je Umekuwa Kwenye Nafasi hiyo kwa Miaka Mingapi
Shahidi: Kwa Miaka 6
Wakili wa Serikali: Umeeleza Mahakama Kwamba Miongoni Mwa Majukumu ya Jeshi ni Kuleta Amani Kwenye Mataifa Mengine, Ushiriki wako ni Vipi
Shahidi: Nimeshirriki Kulinda Amani 2011 Nchini Sudani, Na 2019 ni Sudan hiyo hiyo Jimbo la Darfur
Wakili wa Serikali: Tueleze Mahakama Kule Darfur ulipo enda Majukumu yako yalikuwa yepi
Shahidi: Kuhakikisha Wale Staff Officer (Wapatanishi) Ku Ensure Usalama wao Kwa Sababu Wao ni Unarmed Personnel
Wakili wa Serikali: Kuna Mtu anafahamika Kwa Jina la Khalfani Bwire Unamfahamu Vipi
Shahidi: Nina Mfahamu Kwa Muda Mrefu, Nili Mtrain, Nikifanya naye Kazi Kituo Kimoja cha 92 KJ
Wakili wa Serikali: Umemfahamu Kuanzia Mwaka gani
Shahidi: Kuanzia 2006 Mpaka 2009
Wakili wa Serikali: Wakati Unamfahamu, yeye alikuwa ana Jukumu gani
Shahidi: alikuwa Kiongozi Mdogo, anaongoza,Ni Section Commander, alikuwa anaongoza Watu 9
Wakili wa Serikali: Cheo Chake Kilikuwa ni Kipi
Shahidi: Rank ya koplo
Wakili wa Serikali: Unaposema Ulifahamiana naye kuanzia 2006 Mpaka 2009 umamaam gani
Shahidi: Ukomo wake Ulikuwa Mwaka 2019
Wakili wa Serikali: Nini Kilitokea Mpaka I kafika Ukomo wake
Shahidi: alifukuzwa Kazi Jeshini
Wakili wa Serikali: Kwa sababu Zipi afukuzwe Kazi
Shahidi: Kwa Utovu wa Nidhamu
Wakili wa Serikali: Wakati Mwaka 2019 anafukuzwa + kazi Wewe Ulikuwa wapi
Shahidi: Kwenye Operation Ya Peace Keeping, Sudan Jimbo la Darfur
Wakili wa Serikali: Ni wakati gani Ulikuja Kufahamu Kwamba Khalfani Bwire alifukuzwa Kazi kwa Utovu wa Nidhamu
Shahidi: Ni 2020 Mwezi March Baada ya Kutoka Darfur
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama ni Mazingira Yapi Ulifahamu Kwa Yeye Kufukuzwa Kazi Jeshini
Shahidi: Nilipata Taarifa hizo kutoka Kwa Administration Officer of the Unit
Wakili wa Serikali: Administration Officer ndiyo nani?
Shahidi: Mtu anaye fuatilia Maisha ya Askari Wote Kikosini na Maafisa ya Jeshi, Pia ni Kiongozi
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mahusiano yenu na Khalfani Bwire tangu 2006 Mpaka 2019 yalikuwaje
Shahidi: Yalikuwa ni Mahusiano Mazuri tu, Ya Kiongozi na afisa wake.
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mahusiano yenu baada ya Ajira Kukoma yalikuwaje
Shahidi: Bado nilikuwa naendelea Kuwasiliana naye, Mawasiliano ya Kawaida tu
Wakili wa Serikali: Shahidi Kuna Mtu anaitwa Adam Hassan Kasekwa ama Jina Lingine anaitwa Adamoo.
Shahidi: Nafahamiana naye toka Mwaka 2012 ndipo alipofika Kwenye Unit ya 92KJ alifika Kwenye Mafunzo, Nikam' train, aka' pass Maana nilimpokea Mimi.
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama, Huyu Adam Kasekwa ama Adamoo alifanya kazi Jeshini Kwenye 92 KJ alifanya kazi Mpaka Lini
Shahidi: Mpaka Mwaka 2018
Wakili wa Serikali: Nini Kilimsibu Mwaka huo 2018
Shahidi: Alifukuzwa Kazi Jeshini.
Wakili wa Serikali: Alifukuzwa Kazi Jeshini Kwa Sababu zipi
Shahidi: Kwa Utovu Wa Nidhamu
Wakili wa Serikali: Mpaka anafukuzwa Kazi Jeshini Kwa Utovu, Je alikuwa na Cheo gani
Shahidi: alikuwa Private Soldier.
Wakili wa Serikali: Unaposema Private Soldier Unamaanisha nini
Shahidi: Ni Askari ambaye hana Rank inayo kuwa Displayed, Ni Askari anayekuwa Chini ya Kiongozi Wake
Wakili wa Serikali: Wakati Adam Kasekwa anafukuzwa kazi Wewe Ulikuwa upo wapi
Shahidi: Nilikuwa Nipo Arusha.
Wakili wa Serikali: Ni wakati Gani Ulikuja Kufahamu Kwamba Adam Kasekwa kafukuzwa Kazi Jeshini
Shahidi: Baada ya Kurudi Kwenye Kituo Changu Cha Kazi Kutoka Arusha Kwenye Kozi
Wakili wa Serikali: Taarifa za Yeye Kufukuzwa Kazi Kwa Utovu Wa Nidhamu Wewe Ulizipata Wapi?
Shahidi: Administration Officer
Wakili wa Serikali: alikupatia Taarifa Hizo Mkiwa katika Mazingira gani
Shahidi: Ofisini Kwake
Wakili wa Serikali: Mazingira ya Mahusiano Baina ya Wewe na Adam Kasekwa yalikuwa Je Kipindi Kile Kabla ajafukuzwa Jeshi.
Shahidi: Yalikuwa Mazuri tu
Wakili wa Serikali: VIpi Baada ya Yeye Kufukuzwa Kazi na Kuondoka Jeshini yalikuwaje
Shahidi: Yalikuwa Mazuri
Wakili wa Serikali: Shahidi Kuna Mtu Naitwa Mohammed Abdilah Ling'wenya Unamfahamu Vipi
Shahidi: Namfahamu Nilifanya naye Kazi Kituo Kimoja
Wakili wa Serikali: Kituo Gani hicho
Shahidi: 92 KJ
Wakili wa Serikali: umeanza Kufanya naye Kazi huyo Mohammed Ling'wenya kuanzia Mwaka gani Mpka Mwaka gani
Shahidi: Kuanzia Mwaka 2010 Mpaka Mwaka 2017
Wakili wa Serikali: Nini Kilitokea Mwaka 2017
Shahidi: alifukuzwa Kazi Kwa Utovu Wa Nidhamu
Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mpaka anafukuzwa Kazi, alikuwa ana Cheo gani Katika Jeshi
Shahidi: Alikuwa ni Private Soldier
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Unaposema Private Soldier Unamaanisha nini
Shahidi: Ni Askari Mwenye Cheo Cha Mwisho chini
Wakili wa Serikali: VIpi Kuhusiana na Mahusiano yenu
Shahidi: Tulikuwa na Mahusiano Mazuri
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Baada ya Yeye Kufukuzwa Kazi Kwa Utovu Wa Nidhamu, Mahusiano yenu yalikuwaje
Shahidi: Yaliendelea Kuwa Kama alipokuwa Kazini
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama wakati Mohammed Ling'wenya anafukuzwa kazi Wewe Ulikuwa Wapi
Shahidi: Nilikuwa Kwenye Kazi Maalum
Wakili wa Serikali: Ni Wakati Gani Ulikuja Kupata Ufahamu, kuwa Mohammed Ling'wenya amefukuzwa kazi
Shahidi: Baada ya Kurudi Kwenye Kituo Changu Cha Kazi, kutoka kwa Administration Officer
Wakili wa Serikali: Huyo Administration Officer alikupatia Taarifa Hizo Mkiwa katika Mazingira Yepi
Shahidi: Tukiwa Ofisini
Wakili wa Serikali: Unasema Unamfahamu Khalfani Bwire Je akiwa Miongoni Mwetu unaweza Kumtambua
Shahidi: Ndiyo naweza Kumtambua
Wakili wa Serikali: Sababu ipi itakufanya Umtambue
Shahidi: Nimefanya naye Kazi zaidi Ya Miaka 10, lakini pia Body Morphology
Wakili wa Serikali: Mtu huyo Yupo wapi
Shahidi: aliyepo Mbele yangu, Tunatizamana, Yupo Jirani na Magereza
Wakili wa Serikali: Pia Umemtaja Adam Kasekwa Maarufu Kama Adamoo, Je Unaweza Kumtambua
Shahidi: Ndiyo naweza Kumtambua
Wakili wa Serikali: Ni sababu Zipi hasa zitafanya Umtambue
Shahidi: Nimefanya naye Kazi zaidi Ya Miaka 5 lakini pia na Body Morphology Yake
Wakili wa Serikali: Hebu tuonyeshe Mtu huyo Yupo wapi
Shahidi: Ni Wapili Kutoka Kulia Mwa Khalfani Bwire
Wakili wa Serikali: tuambie Mwingine unaye Msema ni Mohammed Abdilah Ling'wenya, na Yeye Vipi Unaweza Kumtambua
Shahidi: Ndiyo naweza Kumtambua
Wakili wa Serikali: Sababu Ipi Itakufanya umtambue
Shahidi: Nimefanya naye Kazi zaidi Ya Miaka 5, pia Body Morphology yake, Tatu ana Makovu Usoni na Mkononi.
Wakili wa Serikali: Hapa Yupo wapi
Shahidi: Ni watatu Kutoka Upande Wa Kulia wa Bwire
Wakili wa Serikali: Shahidi isaidie Mahakama, Unasema Adam Kasekwa Na Mohamed Ling'wenya Walikuwa ni Private Soldier, Je pale Jeshini Walikuwa na Majukumu Yapi
Shahidi: Wao Ni watendaji wa Shughuli za Kijeshi
Wakili wa Serikali: Huyu Khalfani Hassan Bwire, Adam Hassan Kasekwa, Mohammed Abdilah Ling'wenya wakati wa Utumishi wao Wa Jeshi Pale 92 KJ Makazi yao yalikuwa wapi?
Shahidi: Walikuwa Wa naishi huko, Khalfani Bwire Ngerengere, Adam Kasekwa alikuwa Anaishi Chalinze katika Utaratibu Wa Misbehave
Wakili wa Serikali: Hapana Usiende Huko
Shahidi: Na Mohamed Ling'wenya na Yeye Chalinze