Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe 26 Jan 2022. Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio kuendelea kutoa ushahidi wake

Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe 26 Jan 2022. Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio kuendelea kutoa ushahidi wake

Hivi ndivyo inavyofahamika na watu wengi , kwamba Shahidi wa leo Luteni wa Jeshi la Wananchi aitwaye Denis Urio alikamatwa tangu mwaka jana na kuwekwa kizuizini hadi alipotolewa leo asubuhi kuja kutoa ushahidi wake Mahakamani .

Denis Urio ndiye anayetajwa kuwatafutia kazi ya Ulinzi akina Adamoo na wenzake ili wafanye ulinzi (VIP PROTECTION) kwa Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe .

Bila shaka Mahakama itaelezwa alikokuwa Urio kabla ya kuletwa Mahakamani na kama kwa hali hiyo ushahidi wake utaweza kupokelewa au la .
 
Katika makosa ambayo Mwenyezi Mungu ameyalaani ni pamoja na;
Kushuhudia uongo
Kutoa ushuhuda wa uongo
kutengeneza kesi za uongo ili kumuumiza mtu mwingine.
Fuatilieni watu wa namna hii utagundua kitu ktk maisha yao hasa uzee wao na familia zao utagundua kitu si cha kawaida ambapo ni laana na adhabu toka kwa Mungu kwa walichofanya kwa watu walioumbwa kwa mfano wa Mwenyezi Mungu
 
Salaam Wakuu,

Leo tarehe 24/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe inaendelea.

Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.

Kujua kesi ilipoishia soma: Yaliyojiri kesi ya Mbowe 24/01/2022: Shahidi wa 11, H4347 Goodluck amaliza ushahidi wake. Shahidi wa 12 kuendelea tarehe 26/01/2022

UPDATES

- Jaji ameingia Mahakamani

- Kesi inatajwa


Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Ikikupendeza naitwa wakili Wa Serikali Robert Kidando nipo pamoja na wakili
  • Pius Hilla
  • Abdallah Chavula
  • Jenitreza Kitali
  • Nassoro Katuga
  • Esther Martin
  • Tulimanywa Majige
  • Ignasi Mwinuka
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na wakili
  • Nashon Nkungu
  • John Mallya
  • Dickson Matata
  • Maria Mushi
  • Khadija Aron
  • Seleman Matauka
  • Idd Msawanga
  • Michael Lugina
- Jaji anaita Washitakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja Wakili Peter

Kibatala: Mheshimiwa Jaji na sisi tupo tayari Kuendelea.

Jaji: Anakuwa Shahidi namba Ngapi?

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Anakuwa Shahidi namba 12 Shahidi anakwenda kuitwa Shahidi anaingia Mahakamani, Mrefu Mwembamba, Mweupe Kidogo

Jaji: Majina yako

Shahidi: Naitwa Luteni Denis Urio

Jaji: Umri

Shahidi: Miaka 42

Jaji: Kabila

Shahidi: Mchaga

Jaji: Dini yako

Shahidi: Mkristo

Jaji: Kazi yako

Shahidi: Askari Wa Jeshi la Wananchi Tanzania.

Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama, kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa wa kweli, kweli tupu, Mungu Nisaidie Wakili wa Serikali.

Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shahidi Ataongozwa na Wakili Abdallah Chavula

Wakili wa Serikali Abdallah Chavula anqsimama na Kwenda Kwa Shahidi
Wakili wa Serikali: Shahidi nitakuwa nakuuliza Maswali, Ukijibu utakuwa unamjibu Mheshimiwa Jaji, Naomba Uongee kwa Sauti Ya Juu

Shahidi: Sawa

Wakili wa Serikali: Tukumbushe Majina yako

Shahidi: Naitwa Luteni Denis Leo Urio

Wakili wa Serikali: Mkazi wa Wapi?

Shahidi: Mkazi wa Ngerengere Morogoro

Wakili wa Serikali: Unafanya Shughuli gani

Shahidi: Ni Mwajiriwa wa Jeshi la Wananchi Tanzania

Wakili wa Serikali: Kituo Chako Cha Kazi ni wapi

Shahidi: Ni Ngerengere Morogoro

Wakili wa Serikali: Kituo Chako Kinafahamika kwa Jina gani?

Shahidi: 92 KJ Ngerengere

Wakili wa Serikali: Cheo Chako ni Kipi

Shahidi: Luteni wa Jeshi

Wakili wa Serikali: Majukumu yako ni Yapi

Shahidi: Ni Platoon Commander Kuongoza Askari Walio Chini yangu

Wakili wa Serikali: Unaongoza Askari Wangapi

Shahidi: Afisa Mmoja na Askari 30

Wakili wa Serikali: Ni Askari gani wanayofanya kazi Katika Kikosi cha KJ 92

Shahidi: Ni Wanajeshi Waliopata Mafunzo Maalum, Komando

Wakili wa Serikali: tuambie Wewe Umetumikia Jeshi Kwa Miaka Mingapi

Shahidi: Miaka 18

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama ulijiunga na Jeshi la Wananchi Tanzania Mwaka gani

Shahidi: Tarehe 16,June 2003

Wakili wa Serikali: Jeshi la Wananchi Tanzania lina Majukumu yepi

Shahidi: Lina Majukumu ya Ulinzi wa Mipaka dhidi ya Uvamizi Wa Ndani na Nje

Wakili wa Serikali: Jukumu lingine ni lipi

Shahidi: Kwenye Operation ya Ulinzi Wa Amani Kwenye Mataifa yenye Mgogoro

Wakili wa Serikali: Umesema Wewe ni Luteni wa Jeshi, Je Umekuwa Kwenye Nafasi hiyo kwa Miaka Mingapi

Shahidi: Kwa Miaka 6

Wakili wa Serikali: Umeeleza Mahakama Kwamba Miongoni Mwa Majukumu ya Jeshi ni Kuleta Amani Kwenye Mataifa Mengine, Ushiriki wako ni Vipi

Shahidi: Nimeshirriki Kulinda Amani 2011 Nchini Sudani, Na 2019 ni Sudan hiyo hiyo Jimbo la Darfur

Wakili wa Serikali: Tueleze Mahakama Kule Darfur ulipo enda Majukumu yako yalikuwa yepi

Shahidi: Kuhakikisha Wale Staff Officer (Wapatanishi) Ku Ensure Usalama wao Kwa Sababu Wao ni Unarmed Personnel

Wakili wa Serikali: Kuna Mtu anafahamika Kwa Jina la Khalfani Bwire Unamfahamu Vipi

Shahidi: Nina Mfahamu Kwa Muda Mrefu, Nili Mtrain, Nikifanya naye Kazi Kituo Kimoja cha 92 KJ

Wakili wa Serikali: Umemfahamu Kuanzia Mwaka gani

Shahidi: Kuanzia 2006 Mpaka 2009

Wakili wa Serikali: Wakati Unamfahamu, yeye alikuwa ana Jukumu gani

Shahidi: alikuwa Kiongozi Mdogo, anaongoza,Ni Section Commander, alikuwa anaongoza Watu 9

Wakili wa Serikali: Cheo Chake Kilikuwa ni Kipi

Shahidi: Rank ya koplo

Wakili wa Serikali: Unaposema Ulifahamiana naye kuanzia 2006 Mpaka 2009 umamaam gani

Shahidi: Ukomo wake Ulikuwa Mwaka 2019

Wakili wa Serikali: Nini Kilitokea Mpaka I kafika Ukomo wake

Shahidi: alifukuzwa Kazi Jeshini

Wakili wa Serikali: Kwa sababu Zipi afukuzwe Kazi

Shahidi: Kwa Utovu wa Nidhamu

Wakili wa Serikali: Wakati Mwaka 2019 anafukuzwa + kazi Wewe Ulikuwa wapi

Shahidi: Kwenye Operation Ya Peace Keeping, Sudan Jimbo la Darfur

Wakili wa Serikali: Ni wakati gani Ulikuja Kufahamu Kwamba Khalfani Bwire alifukuzwa Kazi kwa Utovu wa Nidhamu

Shahidi: Ni 2020 Mwezi March Baada ya Kutoka Darfur

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama ni Mazingira Yapi Ulifahamu Kwa Yeye Kufukuzwa Kazi Jeshini

Shahidi: Nilipata Taarifa hizo kutoka Kwa Administration Officer of the Unit

Wakili wa Serikali: Administration Officer ndiyo nani?

Shahidi: Mtu anaye fuatilia Maisha ya Askari Wote Kikosini na Maafisa ya Jeshi, Pia ni Kiongozi

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mahusiano yenu na Khalfani Bwire tangu 2006 Mpaka 2019 yalikuwaje

Shahidi: Yalikuwa ni Mahusiano Mazuri tu, Ya Kiongozi na afisa wake.

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mahusiano yenu baada ya Ajira Kukoma yalikuwaje

Shahidi: Bado nilikuwa naendelea Kuwasiliana naye, Mawasiliano ya Kawaida tu

Wakili wa Serikali: Shahidi Kuna Mtu anaitwa Adam Hassan Kasekwa ama Jina Lingine anaitwa Adamoo.

Shahidi: Nafahamiana naye toka Mwaka 2012 ndipo alipofika Kwenye Unit ya 92KJ alifika Kwenye Mafunzo, Nikam' train, aka' pass Maana nilimpokea Mimi.

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama, Huyu Adam Kasekwa ama Adamoo alifanya kazi Jeshini Kwenye 92 KJ alifanya kazi Mpaka Lini

Shahidi: Mpaka Mwaka 2018

Wakili wa Serikali: Nini Kilimsibu Mwaka huo 2018

Shahidi: Alifukuzwa Kazi Jeshini.

Wakili wa Serikali: Alifukuzwa Kazi Jeshini Kwa Sababu zipi

Shahidi: Kwa Utovu Wa Nidhamu

Wakili wa Serikali: Mpaka anafukuzwa Kazi Jeshini Kwa Utovu, Je alikuwa na Cheo gani

Shahidi: alikuwa Private Soldier.

Wakili wa Serikali: Unaposema Private Soldier Unamaanisha nini

Shahidi: Ni Askari ambaye hana Rank inayo kuwa Displayed, Ni Askari anayekuwa Chini ya Kiongozi Wake

Wakili wa Serikali: Wakati Adam Kasekwa anafukuzwa kazi Wewe Ulikuwa upo wapi

Shahidi: Nilikuwa Nipo Arusha.

Wakili wa Serikali: Ni wakati Gani Ulikuja Kufahamu Kwamba Adam Kasekwa kafukuzwa Kazi Jeshini

Shahidi: Baada ya Kurudi Kwenye Kituo Changu Cha Kazi Kutoka Arusha Kwenye Kozi

Wakili wa Serikali: Taarifa za Yeye Kufukuzwa Kazi Kwa Utovu Wa Nidhamu Wewe Ulizipata Wapi?

Shahidi: Administration Officer

Wakili wa Serikali: alikupatia Taarifa Hizo Mkiwa katika Mazingira gani

Shahidi: Ofisini Kwake

Wakili wa Serikali: Mazingira ya Mahusiano Baina ya Wewe na Adam Kasekwa yalikuwa Je Kipindi Kile Kabla ajafukuzwa Jeshi.

Shahidi: Yalikuwa Mazuri tu

Wakili wa Serikali: VIpi Baada ya Yeye Kufukuzwa Kazi na Kuondoka Jeshini yalikuwaje

Shahidi: Yalikuwa Mazuri

Wakili wa Serikali: Shahidi Kuna Mtu Naitwa Mohammed Abdilah Ling'wenya Unamfahamu Vipi

Shahidi: Namfahamu Nilifanya naye Kazi Kituo Kimoja

Wakili wa Serikali: Kituo Gani hicho

Shahidi: 92 KJ

Wakili wa Serikali: umeanza Kufanya naye Kazi huyo Mohammed Ling'wenya kuanzia Mwaka gani Mpka Mwaka gani

Shahidi: Kuanzia Mwaka 2010 Mpaka Mwaka 2017

Wakili wa Serikali: Nini Kilitokea Mwaka 2017

Shahidi: alifukuzwa Kazi Kwa Utovu Wa Nidhamu

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Mpaka anafukuzwa Kazi, alikuwa ana Cheo gani Katika Jeshi

Shahidi: Alikuwa ni Private Soldier

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Unaposema Private Soldier Unamaanisha nini

Shahidi: Ni Askari Mwenye Cheo Cha Mwisho chini

Wakili wa Serikali: VIpi Kuhusiana na Mahusiano yenu

Shahidi: Tulikuwa na Mahusiano Mazuri

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Baada ya Yeye Kufukuzwa Kazi Kwa Utovu Wa Nidhamu, Mahusiano yenu yalikuwaje

Shahidi: Yaliendelea Kuwa Kama alipokuwa Kazini

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama wakati Mohammed Ling'wenya anafukuzwa kazi Wewe Ulikuwa Wapi

Shahidi: Nilikuwa Kwenye Kazi Maalum

Wakili wa Serikali: Ni Wakati Gani Ulikuja Kupata Ufahamu, kuwa Mohammed Ling'wenya amefukuzwa kazi

Shahidi: Baada ya Kurudi Kwenye Kituo Changu Cha Kazi, kutoka kwa Administration Officer

Wakili wa Serikali: Huyo Administration Officer alikupatia Taarifa Hizo Mkiwa katika Mazingira Yepi

Shahidi: Tukiwa Ofisini

Wakili wa Serikali: Unasema Unamfahamu Khalfani Bwire Je akiwa Miongoni Mwetu unaweza Kumtambua

Shahidi: Ndiyo naweza Kumtambua

Wakili wa Serikali: Sababu ipi itakufanya Umtambue

Shahidi: Nimefanya naye Kazi zaidi Ya Miaka 10, lakini pia Body Morphology

Wakili wa Serikali: Mtu huyo Yupo wapi

Shahidi: aliyepo Mbele yangu, Tunatizamana, Yupo Jirani na Magereza

Wakili wa Serikali: Pia Umemtaja Adam Kasekwa Maarufu Kama Adamoo, Je Unaweza Kumtambua

Shahidi: Ndiyo naweza Kumtambua

Wakili wa Serikali: Ni sababu Zipi hasa zitafanya Umtambue

Shahidi: Nimefanya naye Kazi zaidi Ya Miaka 5 lakini pia na Body Morphology Yake

Wakili wa Serikali: Hebu tuonyeshe Mtu huyo Yupo wapi

Shahidi: Ni Wapili Kutoka Kulia Mwa Khalfani Bwire

Wakili wa Serikali: tuambie Mwingine unaye Msema ni Mohammed Abdilah Ling'wenya, na Yeye Vipi Unaweza Kumtambua

Shahidi: Ndiyo naweza Kumtambua

Wakili wa Serikali: Sababu Ipi Itakufanya umtambue

Shahidi: Nimefanya naye Kazi zaidi Ya Miaka 5, pia Body Morphology yake, Tatu ana Makovu Usoni na Mkononi.

Wakili wa Serikali: Hapa Yupo wapi

Shahidi: Ni watatu Kutoka Upande Wa Kulia wa Bwire

Wakili wa Serikali: Shahidi isaidie Mahakama, Unasema Adam Kasekwa Na Mohamed Ling'wenya Walikuwa ni Private Soldier, Je pale Jeshini Walikuwa na Majukumu Yapi

Shahidi: Wao Ni watendaji wa Shughuli za Kijeshi

Wakili wa Serikali: Huyu Khalfani Hassan Bwire, Adam Hassan Kasekwa, Mohammed Abdilah Ling'wenya wakati wa Utumishi wao Wa Jeshi Pale 92 KJ Makazi yao yalikuwa wapi?

Shahidi: Walikuwa Wa naishi huko, Khalfani Bwire Ngerengere, Adam Kasekwa alikuwa Anaishi Chalinze katika Utaratibu Wa Misbehave

Wakili wa Serikali: Hapana Usiende Huko

Shahidi: Na Mohamed Ling'wenya na Yeye Chalinze

Wakili wa Serikali: Unasema Kwamba Mwaka 2011 ulikuwa Darfur, Je katika Wenye Cheo Cha Private Soldier nani Uliyekuwa naye

Shahidi: Sikumbuki

Wakili wa Serikali: Unaposema Ukumbuki unamaanisha nini

Shahidi: Sina Kumbukumbu Ka Nilikuwa na Mmoja wapo.

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama pale Darfur Ulipokuwa Unaishi Kwenye ile Nyumba yako Ulikuwa Unaishi na Nani

Shahidi: Tulikuwa tunaishi Viongozi Watupu

Wakili wa Serikali: Na Mwaka 2012 pale Darfur Pia Mwenye Cheo Cha Private, nani ulikuwa naye

Shahidi: Sikumbuki.

Wakili wa Serikali: Mtu anaitwa Freeman Mbowe Wewe Unahusiana naye Vipi

Shahidi: Tulifahamiana naye Mwaka 2008 Mpaka 2020

Wakili wa Serikali: Unaweza Kusema ni Mazingira Gani yaliyopelekea Nyinyi Kufahamiana.

Shahidi: Mwaka 2008 Freeman Mbowe anilipigia Simu akaniita Kwa Majina yangu

Wakili wa Serikali: Unaweza Kueleza Mahakama Ilikuwa Tarehe Ngapi

Shahidi: Siwezi Kukumbuka hiyo Tarehe

Wakili wa Serikali: Shahidi Irejee Mahakama tena, Unasema alikupigia Simu lini

Shahidi: Mwaka 2008

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Ilikuwa Tarehe Ngapi na Mwezi gani

Shahidi: Sikumbuki Tarehe Wala Mwezi

Wakili wa Serikali: alikupigia Simu, wewe si yako ilikuwa ya Namba gani

Shahidi: ilikuwa 0754612518

Wakili wa Serikali: Unaweza Kukumbuka na Yeye namba yake iliyokupogoa ilikuwa namba gani

Shahidi: Ilikuwa Mtandao Wa Airtel, ila namba Sikumbuki

Wakili wa Serikali: alikueleza nini

Shahidi: alipiga Simu akauliza Wewe ni Denis Urio, Nikamwambia Yes ndiyo Mimi, akasema ni Askari wa Jeshi la Wananchi, Nikamwambia Ndiyo, akajitambulisha, Kwa Sababu Namfahamu Nikamuamkia.

Wakili wa Serikali: Kwa Sababu Unamfahamu Ukamuamkia, Ulikuwa Unamfahamu Vipi

Shahidi: Alikuwa anaonekana Kwenye Vyombo Vya Habari, Haikuwa Jina geni, I Amana anafahamika

Wakili wa Serikali: Baada ya wewe Kumpa Salamu nini Ulifanya

Shahidi: alikuwa ana confirm Profile Yangu.

Wakili wa Serikali: Unamaanisha Nini

Shahidi: alikuwa nauliza wewe si Denis Urio Nikasema Ndiyo, ni Mtu wa Kilimanjaro basi Mimi Ndugu yako, Ndipo Uhusiano Ulianza

Wakili wa Serikali: Hebu Iambie Mahakama Namba yako ya Simu alitoa Wapi

Shahidi: Sifahamu alipoitoa.

Wakili wa Serikali: Yeye alikueleza, Ni wapi ametoa Namba yako

Shahidi: aliniambia Kuwa Mbona Unafahamu, Kwa Mtu Kupata Namba ya Simu Siyo Tatizo, Usiwe na Wasiwasi

Wakili wa Serikali: Ni Kitu gani kilipelekea Mpaka Yeye Kusema Kuwa Mbona Unafahamika Sana.

Shahidi: Ni pale Nilipo taka Kujua amepata wapi Namba Yangu

Wakili wa Serikali: Hebu tuambie Sasa Hayo Maneno ni Wakati gani alikutamkia

Shahidi: Mara ile ya Kwanza Kuwasiliana, Nikiwa natumia Mtandao Wa Voda yeye akitumia Mtandao Wa Airtel.

Wakili wa Serikali: Shahidi hebu tuambie Baada ya Siku hiyo kuwasiliana Mawasiliano yenu yalikuwaje

Shahidi: Tulikuwa tunaendelea Kuwasiliana, Iwe Kwa Kunisalimia alikuwa ananitumia Ujumbe wa Kuni wish hata Kama Kuna Sikukuu au Event Yoyote

Wakili wa Serikali: Mlimkuta ana kwa ana Lini

Shahidi: Tukikutana Ana Kwa Ana Mwaka 2012

Wakili wa Serikali: Unaweza Kueleza Mahakama Mwaka huo 2012 Ilikuwa ni Tarehe Ngapi na Mwezi Gani

Shahidi: Siwezi Kukumbuka Tarehe Wala Mwezi

Wakili wa Serikali: Shahidi nikirudishe Nyuma, Umeeleza Awali Kwamba 2011 ulikuwa Darfur Nchi Sudan, Je Ulirejea Nchi Mwaka Gani

Shahidi: Nili rejea Mwaka 2011 Mwezi wa 10

Wakili wa Serikali: Ilikuwa Tarehe Ngapi

Shahidi: Siwezi Kukumbuka Siku wala Tarehe.

Wakili wa Serikali: Ni Mazingira Yepi Yalipelekea Ninyi Mwaka 2012 Kukutana

Shahidi: Mwaka 2012 nikiwa Maeneo Ya Mgulani (Saba Saba) Nilipokea Simu ya Mheshimiwa Mbowe Kama Ilivyo Kawaida yake akaniambia Upo wapi, Nikamwambia Nipo Maeneo Ya Mgulani (sabasaba).

Wakili wa Serikali: alikueleza nini

Shahidi: Alini uliza nipo Wapi, Nikamuelekeza Location nilipo

Wakili wa Serikali: Location Maana yake ni nini

Shahidi: Eneo nilipo

Wakili wa Serikali: Endelea

Shahidi: aliniambia Kuwa Kuna Kitu anataka Tuongee, Je tunaweza Kuonana? Nikamuuliza Wewe Upo wapi akasema Yupo Mikocheni Cassa Motel

Jaji: Unaweza Kutaja Spelling zake

Shahidi: CASA Sikumbuki Vizuri

Wakili wa Serikali: Wewe Ukamwambia Nini

Shahidi: Sijui Mikocheni Vizuri, Wala Mahala Ilipo

Wakili wa Serikali: Ulifanya Nini sasa

Shahidi: Baada ya kumwambia Siyo Mwenyeji aliambiwa niende Kituo Cha Tax Ni Mwambie Dereva Yoyote yule anipeleke CASA Motel

Wakili wa Serikali: Baada ya Kupewa hayo Maelekezo, Maamuzi yako yalikuwa ni nini

Shahidi: Nilienda Kwa Dereva Tax, Nikamwambia Anipeleke CASA Motel, nikaweza Kufika CASA Motel

Wakili wa Serikali: Hicho Kituo Cha Tax Ulicho enda Kutafuta Tax ni Kituo Cha Wapi

Shahidi: Ni Saba Saba Mbele Kidogo Kama Unaenda Kwa Aziz Ally Wilaya Ya Temeke.

Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Hiyo Safari yako ya CASA hotel Ilikuwaje

Shahidi: Nili weza Kufika, Nikampigia Simu akapokea, akauliza nimefika Wapi, Nikamwambia Nimeshafika

Wakili wa Serikali: Taratibu Jaji anaandika..

Wakili wa Serikali: endeleaaaa

Shahidi: akanielkeza Pale CASA Motel Kuna Vitu Kama Vimepangwa Kuna watu walikuwa wamekaa Mbali Mbali Ka Wanne hivi, Baada ya Kufika akaniuliza huyu anadai TSh ngapi Nikamwambia TSh 20

Wakili wa Serikali: Baada ya Kumwambia Ikawaje

Shahidi: Alilipa hiyo Tsh 20.

Wakili wa Serikali: Wakati yoye Haya Unayosema Kuanzia Kupigana Simu Mpaka Unafika CASA Hotel Ilikuwa ni Majira yapi

Shahidi: Ilikuwa Kuanzia Saa Saba Mchana Mpaka Alasiri

Wakili wa Serikali: Pale Mlipoliwa Mmekaa na Kukutana naye, Mwingine nani Mliye kuwa Mmekaa naye

Shahidi: Hapakuwa na Mtu Mwingine zaidi yangu Mimi na Yeye

Wakili wa Serikali: Ieleze Mahakama Sasa, Nini Mlichozungumza Wakati Mmekutana

Shahidi: Mambo Makubwa matatu, Kutaka Kujua Mimi ni Nani, nafanya kazi gani, Nina Cheo gani?

Wakili wa Serikali: Kwenye Hayo Madodoso wewe Ulimjibu nini

Shahidi: Mimi ni +Rank gami Majibu niliyompa, Nilimwambia Mimi Sina Rank

Wakili wa Serikali: Ulipomueleza Wewe huna Rank Ulikuwa Unamanisha Nini

Shahidi: Nilimwambia Mimi Sina Cheo Chochote.

Wakili wa Serikali: Kwanini Ulimueleza hayo

Shahidi: Kwa sababu aliniuliza Swali

Wakili wa Serikali: Lingine lipi ulilomjibu

Shahidi: Nilimjibu nafanya kazi Mkoani Morogoro, na Nyumbani ni wapi nilimwambia Mimi Nyumbani ni Mkoani Kilimanjaro, Wilaya ya Moshi Vijijini.

Wakili wa Serikali: Kingine Kipi

Shahidi: Akitaka Kujua Msimamo Wangu dhidi ya Vyama Vya Upinzani

Wakili wa Serikali: Kwenye hilo la Msimamo Wako Majibu yako Yalikuwa ni Yepi

Shahidi: Nilimwambia Kwa Mujibu wa Kazi yangu Siruhusiwi Kufungamana na Chama Chochote
OH SERIKALI HAINA MASHAIDI WALA USHAHIDI
 
Kwenye hii kesi shahidi anaandaliwa kama anaenda kufanya NECTA wakati hujui Kibatala atatoa maswali kwenye topic ya Geometry? Algebra? hujui akiomba kielelezo namba fulani swali linalofuata shahidi anachanganyikiwa kwamba atumie calculator au four figure table, shahidi akienda kwenye desa/kibuti anatoa majibu ya swali la kwanza kumbe aliulizwa swali la tatu........
Nyie pigeni porojo tu ila Mbowe anafungwa tena kwa ushahidi usio na mashaka
 
Urio ndo anajua kila kitu anaweza kuchomoa waya ndo itakuwa mwisho wa kesi
 
OH SERIKALI HAINA MASHAIDI WALA USHAHIDI

IMG_8886.jpg

Wawalinde maana hawakawii kujinyonga hao...
 
Huyu ndio shahidi wa muhimu kuliko wote, huyu ndio atamaliza kesi yote.
 
Wakili wa Serikali: Lingine lipi mililozungumza

Shahidi: Alini uliza Juu ya Makampuni ambayo yangeweza Kufunga Mfumo Wa Mawasiliano Kwenye Ofisi zao, na Kama Jeshini Kuna Makampuni yaliyofunga Mawasiliano Jeshini. Nilipo Muuliza Kwanini anataka Kufanya kazi na Makampuni Yaliyofunga Mawasiliano Jeshini, Akajibu Kuwa anataka Kufuatilia Mawasiliano ya Viongozi Wenzie Wanaotoa Siri Nje ya Chama.

Wakili wa Serikali: ieleze Mahakama Baada ya Kuku uliza Juu ya Swala hilo, Majibu yako Yalikuwa ni nini

Shahidi: Nilimshauri aende Kwenye Taasisi za Elimu ya Juu ndiyo atapata Suluhu ya Tatizo lake Wakili wa Serikali Nini Kiliendelea Sasa Baada ya Hapo.
fix tupu, looh
 
Back
Top Bottom