Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Katika Mapokezi ya Tundu Lissu na Mkutano Mkubwa wa Hadhara Geita Mjini

Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Katika Mapokezi ya Tundu Lissu na Mkutano Mkubwa wa Hadhara Geita Mjini

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
Mgombea Urais kupitia Chadema Tundu Lissu yupo Mkoani Geita akiendeleza kampeni zake za kuingia Ikulu.

Lissu aliyewasili mkoani Geita hapo Jana na kupata mapokezi yaliyovunja Rekodi ya Tanzania katika mji wa Katoro Jimbo la Busanda.

Mkoa wa Geita ni nyumbani kwa mgombea wa CCM John Magufuli Lakini shauku ya wananchi kumuunga mkono mgombea wa Chadema inakitia hofu kubwa chama tawala Cha CCM.

Lissu aliwasili usiku mjini Geita na kulakiwa na halaiki kubwa ya watu wanaokadiriwa kufikia elfu 10

Umati wa huo wa watu ulimsindikiza mpaka Hotelini alikofikia na ulikesha nje ya Hoteli hiyo kwa kile walichodhani wanamlinda Rais wao.

Mapokezi ya Lissu Geita ni salaam tosha kwa chama tawala na mgombea wake kwamba Zama zao zinaelekea ukingoni

Molemo Media itawaletea yatakayojiri katika mkutano wa Hadhara mjini Geita

Video ya kwanza chini inaonyesha mapokezi yake ya Jana alipotua kwa Mara ya kwanza mkoani Geita Jimbo la Busanda.

Yaliyojiri Jioni Hii
Kama ilivyotarajiwa Lissu amewasili kwa kishindo kikubwa mjini Geita.Umati wa watu uliomlaki umesababisha achelewe kuingia viwanjani.

Akimwaga sera kwa wananchi mkombozi huyo wa Tanzania ameendelea kuhubiri sera yake ya Uhuru Haki Na Maendeleo ya Watu.

Lissu ameendelea kulaani ukandamizaji dhidi ya Wafanyakazi wa Tanzania ikiwemo kutokuongezewa mishahara kwa miaka mitano na kupitishwa kwa sheria Haramu dhidi ya Mafao ya Wafanyakazi kwa kuondoa Fao la Kujitoa na kupunguza Mafao ya wastaafu.Lissu amesema akiingia madarakani uonevu huo utakuwa umefikia mwisho.


IMG-20200924-WA0007.jpg
 

Attachments

  • VID-20200924-WA0086.mp4
    19.9 MB
  • VID-20200924-WA0081.mp4
    24.1 MB
  • VID-20200924-WA0078.mp4
    4.6 MB
Nitakwenda. Sababu mbili zinazonifanya niende japo sikuwa na mpango tokea mwanzo wa kampeni Ni.
1. Taarifa zinabaniwa. Mfano TBC 1 hawajisumbui hata kutoa taarifa japo ya dakika moja kuhusu mkutano wa Lisu. Na DSTV hawana Cha ITV Wala StarTV. Hivyo TBC 1 ndiyo channel pekee ya Habari ndani ya dish.

2. Kuna mgombea alisema picha za mikutano ya Lisu ni edit ya zile za 2015. Nami nikiwa Tomaso, siamini mpaka nipapase, nakwenda ku-verify kama kweli Wana CHADEMA huwa Wana edit picha wanazotuma mtandaoni, au huwa Ni za kweli.

Nikishaona na kumsikiliza, nitabaki na uamuzi ndani yangu wa kura yangu nimpigie nani tarehe 28/10.
 
Nakuhakikishia hakuna Kura itakayoibiwa mwaka huu.Mlizoea Sasa mmekutana na Mwamba msidhani ni Lowassa huyu
Ndio hakuna itakayoibwa ila, hamtakaa mpite uchaguzi huu. Amini usiamini.
 
Unaota.

Hutaamini kitakachotokea October 28, 2020.
Mwaka huu tumeleta mwamba atakayewahenyesha ole wenu mjaribu kuiba kura! Safari hii hatuibiwi kiboya, tukishinda lazima mtangaze! Magufuli usicheze na uchaguzi huu utaishia the Hague, Simon Sirro usicheze na uchaguzi huu utaishia the Hague, Kaijage na Mahera msicheze na uchaguzi huu utaishia the Hague!!
 
Meko hana chake uchaguzi wa mask's huu. Yaani kama huko kwao hawamtaki, unadhani ni wapi watamchagua huyu dhalimu.
Ni kama vile yaliomkuta Mbowe hai.

Kama ni same same. Inawezekana.

Ila huu mwaka hapiti mpinzani labda kwa next years.
 
Mwaka huu tumeleta mwamba atakayewahenyesha ole wenu mjaribu kuiba kura! Safari hii hatuibiwi kiboya, tukishinda lazima mtangaze! Magufuli usicheze na uchaguzi huu utaishia the Hague, Simon Sirro usicheze na uchaguzi huu utaishia the Hague, Kaijage na Mahera msicheze na uchaguzi huu utaishia the Hague!!
Hio ni ndoto nyingine.

Mtafanya nini hata mkiibiwa na mlivyowaoga.
 
Back
Top Bottom