Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

Membe rais amina salum makamu magufuli waziri mkuu makamba waziri mambo ya nje migiro spika wa bunge

Maelezo yako yana ukweli flani, yani hiyo safu iliyopangwa hapo ni kama inaelekea maandalizi ya mgawanyo wa majukum mapema.
 
[h=1]Dodoma kumekucha, Lowassa nje, matano yajulikana[/h]
SHARE
BOOKMARK
PRINTEMAILRATING




 
Kwa katiba yetu hii, Mgombea Urais akitoka upande mmoja wa Muungano, lazima Mgombea Mwenza atoke upande mwingine. Kwa maana hii, Kama Membe atakuwa Rais, hawezi kumpendekeza Magufuli kuwa Mgombea Mwenza.

Membe ana kazi kubwa ya kufanya ili kuwashawishi wajumbe hasa ikichukuliwa Timu Lowassa watafanya linalowezekana ili asipate kura za kutosha.

Kama ulivyosema, Asha Migiro ana nafasi iliyo sawa na Magufuli kutokana na mazingira yalivyo.

Mimi nadhani Makamba Jnr anaandaliwa kimkakati katika uchaguzi wa 2025!

Timu Lowassa pamoja na mbwembwe zote huku wakiwatisha wajumbe wa Kamati Kuu wamejikuta wako nje.

Nini hatima ya Lowassa katika siasa za CCM?

Hii ndiyo CCM ambayo ina wenyewe!

Nilipoiona jana hii Taarifa ya Habari kutoka Channel ten nikafahamu Timu Lowassa inatapatapa kwa vile wamefahamu mtu wao amekatwa!

[video]https://youtu.be/Y2etAsrvNv0[/video]

Ni kweli betting yangu ilikuwa on the money!
 
Angalau sasa Amani itapatikana.
Tuone patakapochimbika na mchimbaji no nani!!!
 

Makamba...?kweli wewe una mtindio wa Ubongo kama yeye mwenyewe,pytuuuu tema na tapika kabisa
 
jamani makongoro.....he was ma best...but najua one day Yes
 
Nauona mwanzo wa mpasuko mkubwa ndani ya ccm unakuja miezi michache ijayo.
mimi na wadau wengine ndio tunautaka kwa udi na uvumba huo mpasuko.kutokuwepo kwake kuna sababisha dubwasha,nyonya damu,chinja chinja CCM liendelee kupumua.ukawa daima.
 
Watanzania hawatadhubutu. Wote waliokatwa watanyamaza kimya. Ingekuwa Kenya tungeteta vinginevyo
 
Ila si ilidaiwa kwamba wameahirisha kikao chao mpaka kesho .....

Kikao cha NEC ndio kilisogezwa kesho (Jumamosi)...

Kikao cha kamati kuu kiliendelea hadi usiku mnene na majibu ya watano walioteuliwa hayakutajwa (Nape akataja kuwa yatatajwa kutapopambazuka)...

Lakini baadaye kidogo majina matano yakaanza kusambaa na chanzo kikiwa ni page ya twitter ya CCM...
 
Hata siamini kilicho tokea, ila nimefurahi fisadi lowasa katemwa. TUONE KAMA PATACHIMBIKA AU LA.

SASA NDIO TUTAJUA LOWASA NA CCM NANI ZAIDI.
 
Yaani hata bila ya aibu tena mchana kweupe na kwa mbeleko kubwa kabisa,hapa ndio atampandisha zaidi Mori Mmasai.

Rais ajaye ataongoza kwa tabu sana nchi hii. Kwanza uchumi umeporomoja, deni la taifa limepaa, hujakaa sawa ukigeuka huku unakutana na kuporomoka kwa shilingi dhidi ya dola ya kimarekani, kabla hujapumzika unakuta maisha ya wananchi yamekua magumu zaidi, wakati unatafakari nini ufanye unamkuta bwana mamvi kaunda kambi rasmi ya upinzani ndani ya ccm na kabla hujakaa sawa mtaani ajira hakuna, bidhaa zimepanda bei, etc. etc. Matatizo juu ya matatizo. Pole sana mheshmiwa rais mtarajiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…