Nimekumbuka Kagame kipindi cha ugomvi wake na JK alishasema kuwa Membe anamsapoti JK katika vita yake dhidi ya Kagame kwa vile Mama Salma na mke wa Membe Dorcas wamezaliwa kijiji kimoja na kusoma shule na wamekuwa marafiki kwa muda mrefu. Nimekumbuka pia wakati wa uchaguzi wa viongozi wa NEC Mama Salma na Ridhiwani walimpigia kampeni sana Membe hadi akapita kwenye lile kundi la watu 10. Ninachokiona hapa ni mwendelezo wa JK kumuachia Membe madarakani ili alinde maslahi yake na familia na wala Membe siyo chaguo la wanaCCM bali ni chaguo la mwenyekiti wa CCM. Naamini ata Magufuli atakatwa tu JK anaona ata akikosa Membe bora ampe mwanamke Migiro au huyo mama mwingine ili asisumbuliwe baadae ila anajidanganya kwa vyovyote mipango yake itafeli watanzania wanataka rais wa kuwaletea mabadiliko wasipomuona ndani ya CCM wamtamfata UKAWA Dr. Slaa