Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais


Ina maana huko zinapigwa kura za ndiyo na hapana siyo za kutaja jina la unayempendekeza?
 
hivi wabongo hamna kazi ee, unaacha kujenga maisha unakaa kwenye TV kuangalia wengine wakitengeneza mpunga wao
 
mazingira ya kuwakata baadhi ya wagombea yalijengwa mapema,na viongozi waliopo serikarini....
kingunge hamna anachoongea amezeeka akili anashindwa kutofautisha chama na serikali! si ajabu anaempambia kakatwa tena.
 
Ina Maana hawamuoni Dk. Magufuli? wapuuzi sana hao NEC walio piga HAPANA.
 
heee!! eti rais kwa kuwa atakuwa amiri jeshi mkuu, lazima awe angalau amepitia hata MGAMBO!!!! Huyu mzee vipi??!!
 


Karata ya Mwanausalama dhaifu kama Membe ni risk kubwa sana kwa masilahi ya Taifa labda kwa masilahi ya familia ya JK.
Na kwa sababu ni sehemu ya Mtandao Ugombea wake nao ni hatari kwa uhai wa Chama-unajua ana maadui wangapi ndani ya Chama Chake.

Ni wazi Raisi pengine anategemea mazoea ya kutumia magoli ya mikono kama alivyodokeza Nape Nauye lakini muda mwingine ulazima wa kuangali hali halisi ni muhimu.




 
Kweli nimeamini kuwa mtu ukizeeka akili huwa zinarudi kwenye utoto.....maneno anayoyaongea huyu mzee ni kama mchawi aliyelishwa usembe....
Kwa kifupi mzee anaropoka....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…