Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na rushwa. Shauri kuendelea kesho Nov, 2, 2021

Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na rushwa. Shauri kuendelea kesho Nov, 2, 2021

Kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea leo katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo upande wa mashitaka utaleta shahidi mwingine.

Fuatilia hapa kujua kitakachojiri katika mchakato mzima wa kesi hiyo kwa siku ya leo 11/01/2021

==========

Watuhumiwa wote wamekwishawasili katika ukumbi wa mahakama tayari kuanza kwa kesi.

Jaji: Ameingia sasa

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa

Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe na wenzake

Wakili wa Serikali, Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
1. Pius Hilla
2. Abdallah Chavula,
3. Jenitreza Kitali,
4. Nasorro Katuga,
5. Esther Martin,
6. Ignasi Mwinuka
7. Tulimanywa Majige

Wakili Peter Kibatala anawatambulisha Mawakili Wa Utetezi
1.Jeremiah Mtobesya
2.Michael Mwangasa
3.Seleman Matauka
4.Nashon Nkungu
5.Alex Massaba
6.Michael Lugina
7.Maria Mushi
8.Hadija Aron
9.Dickson Matata
10.Jonathan Mndeme
11.Fredrick Kihwelo
12.John Malya

Jaji: anawait Washitakiwa 1,2,3 na 4 Wanasimama Kuitikia

Wakili wa Serikali: Kwa Upande wetu tuna shahidi Mmoja kwa Leo na tupo tayari Kuendelea Kwa Upande wetu tupo tayari kuendelea

Wakili Peter Kibatala: Tupo tayari na sisi Kuendelea

Wakili wa Serikali: Mmoja anatoka Kwenda Kumuita Shahidi Nje ya Chumba Cha Mahakama Mahakama Ipo Kimya Kidogo

Shahidi anapita ni Mdada Kajitanda Buibui na Kavaa Barakoa Kubwa sana Kumziba Sura,

Jaji: Majina Yako

Shahidi: Anita Varelian Mtali

Jaji: umri Shahidi: 45yrs

Jaji: Kabila

Shahidi: Mchaga

Jaji: Shughuli Zako

Shahidi: Nafanya Biashara

Jaji: Dini yako

Shahidi: R. C

Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii Kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni kweli, kweli tupu Eeeh Mungu nisaidie

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Shahidi Ataongozwa na Wakili Esther Martin

Wakili wa Serikali: Esther Ikumbushe Mahakama Majina yako

Shahidi: Anita Varelian Mtali

Wakili wa Serikali: Unaishi Wapi

Shahidi: Moshi, RAU madukani.

Jaji: Jina lako la Tatu sijalipata Vizuri ni Mtali.?

Shahidi: Mtaro

Wakili wa Serikali: Umeishi kwa Muda gani Rau

Shahidi: Miaka 08

Wakili wa Serikali: Unafanya Shughuli gani

Shahidi: Nafanya Biashara ya Kuuza Mbege

Wakili wa Serikali: Ulianza lini Biashara yako ya Mbege

Shahidi: Miaka 08 ninayo

Wakili wa Serikali: Mbali na Biashara yako ya Mbege una bishara gani Nyingine

Shahidi: Kuna Glocery, Stationary, Banda la Tigo Pesa na Kuna Sehemu ya Kutolea Movie

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama 05 Mwezi 08 2020 ulikuwa wapi

Shahidi: Sehemu yangu ya Biashara, Nikifanya Usafi

Wakili wa Serikali: Saa ngapi

Shahidi: Saa Saba Kasoro

Wakili wa Serikali: Ya Muda gani

Shahidi: Ya Mchana

Wakili wa Serikali : Kabla ya Kufika eneo lako la Biashara ulikuwa umetoka wapi?

Shahidi: Nilikuwa Nimetoka Nyumbani Nikaenda Saloon Kuosha Nywele

Wakili wa Serikali: Na Ulipotoka Saloon kuelekea sehemu yako Kufanya Usafi

Shahidi: Nilikuta Wakaka Watatu walikuwa wamekaa Mbele Yangu walikuwa wanakunywa na Kusajili Laini

Wakili wa Serikali: Walikuwa wanakunywa nini

Shahidi: Walikuwa wanakunywa Bia

Wakili wa Serikali: Hizo laini walikuwa wanasajili wapi

Shahidi: Kuna Vijana wanapitaga Mitaani Kusajili Laini

Wakili wa Serikali: Ukiwa unafanya Usafi kitu gani Kingine ulishuhudia

Shahidi: Kuna wakaka wawili walikuwa wanapitapita wakiongea na simu, Wanaenda wanarudi wakiongea na Simu

Wakili wa Serikali: Hao wanaopita ni tofauti na wale uliposema walikuwa wanakunywa Bia

Shahidi: Hapana ni walewale

Wakili wa Serikali: Kutoka Kwako Unapofanyia Kazi Mpaka Glocery ni Umbali gani

Shahidi: Kama Hatua 10

Wakili wa Serikali: Hapo Katikati sasa, Kati ya Glocery na ulipo, pana kitu gani

Shahidi: Pana uwazi

Wakili wa Serikali: Baada ya Muda kitu gani kilitokea

Shahidi: Wakati wanaongea na Simu Walitokea watu wawili wakaongea kwa sauti kali "Mpo chini ya Ulinzi Mnahusika na Mambo ya Kigaidi, chuchumaa Chini Mikono Juu"

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine ulisikia

Shahidi: Chuchumaa Chini Mnahusika na Mambo ya Kigaidi Wakili wa Serikali: Ni watu gani sasa hao

Shahidi: Ni Askari

Wakili wa Serikali: Ulikuwa unafanya nini wakati huo

Shahidi: Nafanya Usafi

Wakili wa Serikali: Pana umbali gani kutoka Walipo na Mpaka Ulipokuwa unafanya Usafi

Shahidi: Hatua 05

Wakili wa Serikali: Ulisikia nini Kingine

Shahidi: Sikusikia Kingine zaidi ya Chuchumaa Chini Nyoosha Mikono Juu

Wakili wa Serikali: Walikuwa Askari wangapi

Shahidi: Wawili

Wakili wa Serikali: Hali ya Pale ilikuwaje

Shahidi: Ilikuwa ni Utulivu

Wakili wa Serikali: Nini Kilifuata

Shahidi: Walitokea Askari Wengine watatu wakawa wamefika eneo la Tukio

Wakili wa Serikali: Ongeza Sauti

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kiliendelea

Shahidi: Baada ya Kuwa Askari watano alitokea Mmoja akaniambia anaomba nisogee anahitaji Kuwafanyia Upekuzi

Wakili wa Serikali: Ni Askari gani huyo

Shahidi: Alinitambulisha anaitwa Askari Polisi Jumanne

Wakili wa Serikali: Ulifanya nini kujiridhisha?

Shahidi: Alitoa Kitambulisho Akanionyesha

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilifanyika

Shahidi: Alimsimamisha Mmoja

Wakili wa Serikali: Kabla ya Kumsimamisha..?

Shahidi: Afande Jumanne alijipekua kuanzia Kifuani akatoa Mifuko Nje

Wakili wa Serikali: We ulikuwa na nani wakati huo

Shahidi: Dada Mmoja anaitwa Esther

Wakili wa Serikali: Kutoka Eneo la walioambiwa Wachuchumae Chini, palikuwa na Umbali gani?

Shahidi: Kama Hatua Mbili

Wakili wa Serikali: Kuna Kitu gani Kingine

Shahidi: Raia walikuwa wamekuja

Wakili wa Serikali: Kabla ya Raia Kusogea eneo hilo palikuwa na hali gani?

Shahidi: Palikuwa na Jua

Wakili wa Serikali: ahaa ahaaa yani hali ya pale ilikuwaje?

Shahidi: Palikuwa pametulia

Wakili wa Serikali: Ikaendelea nini?

Shahidi: Alimsimamisha Mmoja akamuuliza Unaitwa nani?

Wakili wa Serikali: Akajibu anaitwa nani?

Shahidi: Adam Kasekwa

Wakili wa Serikali: Akamwambia nini?

Shahidi: Akiwa amenyoosha Mikono Juu akamwambia Geuka, akageuka

Wakili wa Serikali: Baada ya Kugeuka

Shahidi: Askari Jumanne alianza Kumpekua Kuanzia Kichwani, Mabegani, Alipofika Kiunoni alikuta Kitu kigumu

Wakili wa Serikali: Alikikuta Upande gani

Shahidi: Kushoto

Wakili wa Serikali: Maeneo Gani?

Shahidi: Niliona ni Bastola

Wakili wa Serikali: Ulijuaje kama ni Bastola?

Shahidi: Afande Jummane alituambia ni Bastola

Wakili wa Serikali: Halafu

Shahidi: akatuonyesha namba

Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni namba gani.?

Shahidi: A5340

Wakili wa Serikali: Zilikuwa kwenye nini

Shahidi: Kwenye Bastola

Wakili wa Serikali: Wakati anakuonyesha Bastola Adam alikuwa wapi?

Shahidi: Alikuwa amesimama

Wakili wa Serikali: Ukiona na nini Kingine

Shahidi: Risasi 03

Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea

Shahidi: Akaendelea na Upekuzi

Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea

Shahidi: Akaendelea na Upekuzi, alipofika Upande wa Kulia akakuta Vitu vidogo vidogo Kwenye Karatasi ya Nailon akasema inasadikiwa ni Madawa ya Kulevya ila itajulikana Mbele.

Wakili wa Serikali: Zilikuwa ngapi Shahidi: 58

Wakili wa Serikali: ikawaje

Shahidi: Aliendelea Kumpekua akamkuta na Simu Ndogo aina ya Itel

Wakili wa Serikali: Hiyo simu akaifanyaje

Shahidi: Akatoa laini akakuta namba akaziandika

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo aliendelea na nini

Shahidi: Akamwambia Naomba fomu, .......akaleta fomu

Wakili wa Serikali: fomu ngapi

Shahidi: Zilikuwa Mbili

Wakili wa Serikali: Akafanya nini sasa Kwenye ile Fomu

Shahidi: Kaandika Vitu alivyokuwa amempekua

Wakili wa Serikali: Umesema palikuwa na fomu Mbili, fomu ya kwanza akijaza nini

Shahidi: fomu ya kwanza alijaza Bastola, Risasi na Laini

Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni laini gani

Shahidi: Laini ya Voda na Airtel

Wakili wa Serikali: Baada ya Kumalizia fomu ya kwanza

Shahidi: alichukua fomu Nyingine

Wakili wa Serikali: Kabla ya Kujaza Fomu Nyingine

Shahidi: Alipomaliza Kujaza akampa akasaini na Baadae akasaini yeye alipo maliza Kusaini.

Wakili wa Serikali: alimpa nani

Shahidi: Alimpa Adam

Wakili wa Serikali: baada ya fomu ya kwanza nini kiliendelea

Shahidi: alichukua Fomu Nyingine

Wakili wa Serikali: alijaza nini

Shahidi: alijaza vile Vikete vidogo Vidogo

Wakili wa Serikali: Vingapi Vilikuwa Vingapi

Shahidi: Vilikuwa 58

Wakili wa Serikali: baada ya hapo

Shahidi: akampa Adam asome alafu asaini na sisi akamtupa tusaini

Wakili wa Serikali: Wewe na nani..?

Shahidi: Mimi na Dada Esther

Wakili wa Serikali: baada Kumalizia nini kilifuata

Shahidi: akamuita Mwingine

Wakili wa Serikali: huyo Mwingine anaitwa nani

Shahidi: Mohamed Abdulahi Ling'wenya

Wakili wa Serikali: akamwambia nini

Shahidi: asimame ageuke, Baada ya kugeuka akaanza Kumpekua

Wakili wa Serikali: alianzaje Kumpekua

Shahidi: Kichwani Mikononi

Wakili wa Serikali: ilikuwaje

Shahidi: Upande wa Kulia alikuta na Vikete Vidogo Vidogo

Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi

Shahidi: 25

Wakili wa Serikali: akafanyeje

Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua

Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua

Shahidi: alikuta Simu aina ya Tecno

Wakili wa Serikali: Rangi gani

Shahidi: Nyeusi

Wakili wa Serikali: akafanya nini

Shahidi: akapekua akakuta kuna laini

Wakili wa Serikali: laini gani

Shahidi: Hallotel

Wakili wa Serikali: baada ya Kupata simu akafanyeje

Shahidi: akazitoa zile Laini, Akampa yule Mwingine akazishika

Wakili wa Serikali: Na Yeye Akaendelea na nini

Shahidi: Akaendelea na Upekuzi

Wakili wa Serikali: hizo laini alikuwa anafanya nazo nini?

Shahidi: Alimpa Askari wa Pembeni akazishika

Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi

Shahidi: Aliendelea na Upekuzi lakini hakukuta kitu Kingine

Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi

Shahidi: aliomba fomu Mbili


Wakili wa Serikali: fomu ya Kwanza alijaza nini

Shahidi: alijaza vile Vikete Vidogo Vidogo

Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi

Shahidi: 25

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo

Shahidi: Alimpa akasema akasaini

Wakili wa Serikali: Nani Yeye, afande Jumanne?

Shahidi: Ndiyo na Baadae Mohamed

Wakili wa Serikali: na baadae

Shahidi: tukasaini sisi

Wakili wa Serikali: Wewe na nani

Shahidi: Mimi na Dada Esther

Wakili wa Serikali: baada ya hapo

Shahidi: Ile fomu Nyingine akajaza Simu na laini Nyingine

Wakili wa Serikali: Za Mtandao gani

Shahidi: Airtel na Hallotel

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo

Shahidi: Alimpa Mohamed asome kisha akasaini

Wakili wa Serikali: baada ya hapo

Shahidi: afande Jumanne alituomba na sisi tusome Kisha tusaini

Wakili wa Serikali: Wewe na nani

Shahidi: Mimi na Dada Esther

Wakili wa Serikali: baada ya Upekuzi

Shahidi: walivalishwa Pingu

Wakili wa Serikali: baada ya hapo

Shahidi: afande Jumanne akatuomba tuelekee Kituoni

Wakili wa Serikali: Hao walivalishwa Pingu walikuwa ni akina nani

Shahidi: Adam na Mohamed

Wakili wa Serikali: baada ya kuvalishwa Pingu..?

Shahidi: Wakaelekea kwenye Magari, Barabarani

Wakili wa Serikali:
Palikuwa na Askari wangapi

Shahidi: Watano

Wakili wa Serikali:
Walikuwa wamebeba nini

Shahidi:
Wawili walikuwa wamebeba Bunduki

Wakili wa Serikali:
Hali ya hewa eneo lile ilikuwaje

Shahidi:
ilikuwa imetulia

Wakili wa Serikali:
Hali ya hewa ilikuwaje

Shahidi:
Kulikuwa na Jua na Mwanga

Wakili wa Serikali: Mlichukua Muda gani kwenye lile eneo Mpaka Mnamaliza Zoezi

Shahidi: Kama Dakika 45

Wakili wa Serikali: Baada ya Kufanya Upekuzi Kuna Vitu Vilipatikana na Kwamba Kuna fomu zilijazwa Sasa fomu ukiziona hapa utaweza Kuzitambua?

Wakili wa Serikali:
sasa bada ya Kumalizia Mkaelekea kituoni, kituo gani..?

Shahidi: Central Moshi

Wakili wa Serikali: baada ya Kufika police central

Shahidi: Tuliandika Maelezo

Wakili wa Serikali: Maelezo ya nini

Shahidi: Kitu gani Kilichofanyika ......

Wakili wa Serikali: Tukianza na fomu ya Adam utaitambuaje

Shahidi: Kwa vitu vilivyoaandikwa, Jina langu na sahihi yangu

Wakili wa Serikali:
Kulikuwa na nini Kingine Bastola

Wakili wa Serikali:
Kingine

shahidi:
Palikuwa na Risasi

Wakili wa Serikali namba gani Shahidi: A5340

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba nimpe fomu aweze Kuitambua

Wakili wa Serikali: Shika hii Karatasi iangalie kwa Makini

Shahidi:
Ndiyo yenyewe

Wakili wa Serikali: Yenyewe nini

Shahidi:
Fomu niliyo saini
Yaani majibu ya kutunga yana furahisha sana. Unaona kabisa majibu ya ajabu ajabu.
 
Usimjibu mpumbavu kipumbavu, usije ukafanana naye. Mjibu mpumbavu kama ustahilivyo upumbavu wake, asije akajiona kuwa mwenye hekima zaidi. Kumtuma mpumbavu ujumbe, ni kama kujikata miguu au kujitafutia shida. Methali mdomoni mwa mpumbavu, ni kama miguu ya kiwete inayoninginia. Kumpa mpumbavu heshima, ni kama kufunga jiwe kwenye kombeo. Mpumbavu anayejaribu kutumia methali, ni kama mlevi anayejaribu kungoa mwiba mkononi. Mtu amwajiriye mpumbavu au mlevi, ni kama mpiga upinde anayejeruhi kila mtu. Mpumbavu anayerudiarudia upumbavu wake, ni kama mbwa anayekula matapishi yake. Wamwona mtu ajionaye kuwa mwenye hekima? Nakuambia mpumbavu ni nafuu kuliko huyo.
 
Huyu asubirie maswali mafumu toka kwa Kibatara na wenzake.

Huyu lazima aombe poa. Muda utafika tu.
Huyu anatanyooshwa leo
IMG-20211101-WA0002.jpg
IMG-20211101-WA0001.jpg
 
Walikuwa wanakunywa hapo hapo wanaongea na simu wakiwa wanatembea duh! Hivi mawakili wa sirikali hawaoni haya kupeleka mashaid wa dizaini hii

Kutoka alipo hadi eneo la tukio ni kama hatua 2 hivi, lakini Anita anaendelea na usafi..!!
 
Anita kwa uongo huo, unajilaani wewe na kizazi chako !! acha kabisa kutoa ushahidi wa urongo kwa mambo ambayo mshitakiwa hakutenda, ni laana mbaya sana unajitafutia, hizi Serikali za nchi zinapita tu ila laana itakuwa ndani yako na uzao wako, walio karibu na wewe wakwambie mapema...
Wewe umejuaje wa uongo, ulikuwa eneo la tukio..acha ushabiki huu ushahidi upo wazi kuliko hata ule Sabaya wa kuunga unga na gundi
 
Makamani hapa wakili wa serikali Esther Martin anaupiga mwingi sana


Shahidi: Wakati wanaongea na Simu Walitokea watu wawili wakaongea kwa sauti kali "Mpo chini ya Ulinzi Mnahusika na Mambo ya Kigaidi, chuchumaa Chini Mikono Juu"

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine ulisikia

Shahidi: Chuchumaa Chini Mnahusika na Mambo ya Kigaidi Wakili wa Serikali: Ni watu gani sasa hao

Shahidi: Ni Askari

Wakili wa Serikali: Ulikuwa unafanya nini wakati huo

Shahidi: Nafanya Usafi

Wakili wa Serikali: Pana umbali gani kutoka Walipo na Mpaka Ulipokuwa unafanya Usafi

Shahidi: Hatua 05

Wakili wa Serikali: Ulisikia nini Kingine

Shahidi: Sikusikia Kingine zaidi ya Chuchumaa Chini Nyoosha Mikono Juu

Wakili wa Serikali: Walikuwa Askari wangapi

Shahidi: Wawili

Wakili wa Serikali: Hali ya Pale ilikuwaje

Shahidi: Ilikuwa ni Utulivu

Wakili wa Serikali: Nini Kilifuata

Shahidi: Walitokea Askari Wengine watatu wakawa wamefika eneo la Tukio

Wakili wa Serikali: Ongeza Sauti

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kiliendelea

Shahidi: Baada ya Kuwa Askari watano alitokea Mmoja akaniambia anaomba nisogee anahitaji Kuwafanyia Upekuzi
 
Wewe umejuaje wa uongo ..ulikuwa eneo la tukio..acha ushabiki huu ushahidi upo wazi kuliko hata ule Sabaya wa kuunga unga na gundi
Tutajie was sabaya umeungwaungwa vipi wakati hata huyo mtoto was mwisho was humour unamokaaa anajua kwamba sabaya alikuwa jambazi.

Muuza mbege ni askari na ni malaya sana.

Sent from my SM-N9150 using JamiiForums mobile app
 
Kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea leo katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo upande wa mashitaka utaleta shahidi mwingine...
Mbowe et al anapelekewa moto
 
Hii kesi iwe fundisho kwa vyama vingine ambavyo badala ya kufanya kazi za siasa, vinajigeuza kuwa Genge la kihalifu.
inapaswa kujitathimini kila wakati.
Ni MUNGU yupi unaye mwabudu katika kanisa la WA-ADVENTIST WASABATO?Jumamosi ulikuwa kanisani kufanya nini?Kwanini unashuhudia jirani yako uongo?

Vyeo vya CCM, fedha za CCM na fahari zote za CCM kwanini zikutenge na MUNGU wa kweli.Unatofauti gani na wakala wa shetani ndani ya kanisa letu la SDA?
 
Back
Top Bottom