Kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea leo katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo upande wa mashitaka utaleta shahidi mwingine.
Fuatilia hapa kujua kitakachojiri katika mchakato mzima wa kesi hiyo kwa siku ya leo 11/01/2021
==========
Watuhumiwa wote wamekwishawasili katika ukumbi wa mahakama tayari kuanza kwa kesi.
Jaji: Ameingia sasa
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa
Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe na wenzake
Wakili wa Serikali, Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
1. Pius Hilla
2. Abdallah Chavula,
3. Jenitreza Kitali,
4. Nasorro Katuga,
5. Esther Martin,
6. Ignasi Mwinuka
7. Tulimanywa Majige
Wakili Peter Kibatala anawatambulisha Mawakili Wa Utetezi
1.Jeremiah Mtobesya
2.Michael Mwangasa
3.Seleman Matauka
4.Nashon Nkungu
5.Alex Massaba
6.Michael Lugina
7.Maria Mushi
8.Hadija Aron
9.Dickson Matata
10.Jonathan Mndeme
11.Fredrick Kihwelo
12.John Malya
Jaji: anawait Washitakiwa 1,2,3 na 4 Wanasimama Kuitikia
Wakili wa Serikali: Kwa Upande wetu tuna shahidi Mmoja kwa Leo na tupo tayari Kuendelea Kwa Upande wetu tupo tayari kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Tupo tayari na sisi Kuendelea
Wakili wa Serikali: Mmoja anatoka Kwenda Kumuita Shahidi Nje ya Chumba Cha Mahakama Mahakama Ipo Kimya Kidogo
Shahidi anapita ni Mdada Kajitanda Buibui na Kavaa Barakoa Kubwa sana Kumziba Sura,
Jaji: Majina Yako
Shahidi: Anita Varelian Mtali
Jaji: umri Shahidi: 45yrs
Jaji: Kabila
Shahidi: Mchaga
Jaji: Shughuli Zako
Shahidi: Nafanya Biashara
Jaji: Dini yako
Shahidi: R. C
Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii Kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni kweli, kweli tupu Eeeh Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Shahidi Ataongozwa na Wakili Esther Martin
Wakili wa Serikali: Esther Ikumbushe Mahakama Majina yako
Shahidi: Anita Varelian Mtali
Wakili wa Serikali: Unaishi Wapi
Shahidi: Moshi, RAU madukani.
Jaji: Jina lako la Tatu sijalipata Vizuri ni Mtali.?
Shahidi: Mtaro
Wakili wa Serikali: Umeishi kwa Muda gani Rau
Shahidi: Miaka 08
Wakili wa Serikali: Unafanya Shughuli gani
Shahidi: Nafanya Biashara ya Kuuza Mbege
Wakili wa Serikali: Ulianza lini Biashara yako ya Mbege
Shahidi: Miaka 08 ninayo
Wakili wa Serikali: Mbali na Biashara yako ya Mbege una bishara gani Nyingine
Shahidi: Kuna Glocery, Stationary, Banda la Tigo Pesa na Kuna Sehemu ya Kutolea Movie
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama 05 Mwezi 08 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Sehemu yangu ya Biashara, Nikifanya Usafi
Wakili wa Serikali: Saa ngapi
Shahidi: Saa Saba Kasoro
Wakili wa Serikali: Ya Muda gani
Shahidi: Ya Mchana
Wakili wa Serikali : Kabla ya Kufika eneo lako la Biashara ulikuwa umetoka wapi?
Shahidi: Nilikuwa Nimetoka Nyumbani Nikaenda Saloon Kuosha Nywele
Wakili wa Serikali: Na Ulipotoka Saloon kuelekea sehemu yako Kufanya Usafi
Shahidi: Nilikuta Wakaka Watatu walikuwa wamekaa Mbele Yangu walikuwa wanakunywa na Kusajili Laini
Wakili wa Serikali: Walikuwa wanakunywa nini
Shahidi: Walikuwa wanakunywa Bia
Wakili wa Serikali: Hizo laini walikuwa wanasajili wapi
Shahidi: Kuna Vijana wanapitaga Mitaani Kusajili Laini
Wakili wa Serikali: Ukiwa unafanya Usafi kitu gani Kingine ulishuhudia
Shahidi: Kuna wakaka wawili walikuwa wanapitapita wakiongea na simu, Wanaenda wanarudi wakiongea na Simu
Wakili wa Serikali: Hao wanaopita ni tofauti na wale uliposema walikuwa wanakunywa Bia
Shahidi: Hapana ni walewale
Wakili wa Serikali: Kutoka Kwako Unapofanyia Kazi Mpaka Glocery ni Umbali gani
Shahidi: Kama Hatua 10
Wakili wa Serikali: Hapo Katikati sasa, Kati ya Glocery na ulipo, pana kitu gani
Shahidi: Pana uwazi
Wakili wa Serikali: Baada ya Muda kitu gani kilitokea
Shahidi: Wakati wanaongea na Simu Walitokea watu wawili wakaongea kwa sauti kali "Mpo chini ya Ulinzi Mnahusika na Mambo ya Kigaidi, chuchumaa Chini Mikono Juu"
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine ulisikia
Shahidi: Chuchumaa Chini Mnahusika na Mambo ya Kigaidi Wakili wa Serikali: Ni watu gani sasa hao
Shahidi: Ni Askari
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unafanya nini wakati huo
Shahidi: Nafanya Usafi
Wakili wa Serikali: Pana umbali gani kutoka Walipo na Mpaka Ulipokuwa unafanya Usafi
Shahidi: Hatua 05
Wakili wa Serikali: Ulisikia nini Kingine
Shahidi: Sikusikia Kingine zaidi ya Chuchumaa Chini Nyoosha Mikono Juu
Wakili wa Serikali: Walikuwa Askari wangapi
Shahidi: Wawili
Wakili wa Serikali: Hali ya Pale ilikuwaje
Shahidi: Ilikuwa ni Utulivu
Wakili wa Serikali: Nini Kilifuata
Shahidi: Walitokea Askari Wengine watatu wakawa wamefika eneo la Tukio
Wakili wa Serikali: Ongeza Sauti
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kiliendelea
Shahidi: Baada ya Kuwa Askari watano alitokea Mmoja akaniambia anaomba nisogee anahitaji Kuwafanyia Upekuzi
Wakili wa Serikali: Ni Askari gani huyo
Shahidi: Alinitambulisha anaitwa Askari Polisi Jumanne
Wakili wa Serikali: Ulifanya nini kujiridhisha?
Shahidi: Alitoa Kitambulisho Akanionyesha
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilifanyika
Shahidi: Alimsimamisha Mmoja
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kumsimamisha..?
Shahidi: Afande Jumanne alijipekua kuanzia Kifuani akatoa Mifuko Nje
Wakili wa Serikali: We ulikuwa na nani wakati huo
Shahidi: Dada Mmoja anaitwa Esther
Wakili wa Serikali: Kutoka Eneo la walioambiwa Wachuchumae Chini, palikuwa na Umbali gani?
Shahidi: Kama Hatua Mbili
Wakili wa Serikali: Kuna Kitu gani Kingine
Shahidi: Raia walikuwa wamekuja
Wakili wa Serikali: Kabla ya Raia Kusogea eneo hilo palikuwa na hali gani?
Shahidi: Palikuwa na Jua
Wakili wa Serikali: ahaa ahaaa yani hali ya pale ilikuwaje?
Shahidi: Palikuwa pametulia
Wakili wa Serikali: Ikaendelea nini?
Shahidi: Alimsimamisha Mmoja akamuuliza Unaitwa nani?
Wakili wa Serikali: Akajibu anaitwa nani?
Shahidi: Adam Kasekwa
Wakili wa Serikali: Akamwambia nini?
Shahidi: Akiwa amenyoosha Mikono Juu akamwambia Geuka, akageuka
Wakili wa Serikali: Baada ya Kugeuka
Shahidi: Askari Jumanne alianza Kumpekua Kuanzia Kichwani, Mabegani, Alipofika Kiunoni alikuta Kitu kigumu
Wakili wa Serikali: Alikikuta Upande gani
Shahidi: Kushoto
Wakili wa Serikali: Maeneo Gani?
Shahidi: Niliona ni Bastola
Wakili wa Serikali: Ulijuaje kama ni Bastola?
Shahidi: Afande Jummane alituambia ni Bastola
Wakili wa Serikali: Halafu
Shahidi: akatuonyesha namba
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni namba gani.?
Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Zilikuwa kwenye nini
Shahidi: Kwenye Bastola
Wakili wa Serikali: Wakati anakuonyesha Bastola Adam alikuwa wapi?
Shahidi: Alikuwa amesimama
Wakili wa Serikali: Ukiona na nini Kingine
Shahidi: Risasi 03
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi, alipofika Upande wa Kulia akakuta Vitu vidogo vidogo Kwenye Karatasi ya Nailon akasema inasadikiwa ni Madawa ya Kulevya ila itajulikana Mbele.
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ngapi Shahidi: 58
Wakili wa Serikali: ikawaje
Shahidi: Aliendelea Kumpekua akamkuta na Simu Ndogo aina ya Itel
Wakili wa Serikali: Hiyo simu akaifanyaje
Shahidi: Akatoa laini akakuta namba akaziandika
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo aliendelea na nini
Shahidi: Akamwambia Naomba fomu, .......akaleta fomu
Wakili wa Serikali: fomu ngapi
Shahidi: Zilikuwa Mbili
Wakili wa Serikali: Akafanya nini sasa Kwenye ile Fomu
Shahidi: Kaandika Vitu alivyokuwa amempekua
Wakili wa Serikali: Umesema palikuwa na fomu Mbili, fomu ya kwanza akijaza nini
Shahidi: fomu ya kwanza alijaza Bastola, Risasi na Laini
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni laini gani
Shahidi: Laini ya Voda na Airtel
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumalizia fomu ya kwanza
Shahidi: alichukua fomu Nyingine
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kujaza Fomu Nyingine
Shahidi: Alipomaliza Kujaza akampa akasaini na Baadae akasaini yeye alipo maliza Kusaini.
Wakili wa Serikali: alimpa nani
Shahidi: Alimpa Adam
Wakili wa Serikali: baada ya fomu ya kwanza nini kiliendelea
Shahidi: alichukua Fomu Nyingine
Wakili wa Serikali: alijaza nini
Shahidi: alijaza vile Vikete vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vingapi Vilikuwa Vingapi
Shahidi: Vilikuwa 58
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: akampa Adam asome alafu asaini na sisi akamtupa tusaini
Wakili wa Serikali: Wewe na nani..?
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada Kumalizia nini kilifuata
Shahidi: akamuita Mwingine
Wakili wa Serikali: huyo Mwingine anaitwa nani
Shahidi: Mohamed Abdulahi Ling'wenya
Wakili wa Serikali: akamwambia nini
Shahidi: asimame ageuke, Baada ya kugeuka akaanza Kumpekua
Wakili wa Serikali: alianzaje Kumpekua
Shahidi: Kichwani Mikononi
Wakili wa Serikali: ilikuwaje
Shahidi: Upande wa Kulia alikuta na Vikete Vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi
Shahidi: 25
Wakili wa Serikali: akafanyeje
Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua
Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua
Shahidi: alikuta Simu aina ya Tecno
Wakili wa Serikali: Rangi gani
Shahidi: Nyeusi
Wakili wa Serikali: akafanya nini
Shahidi: akapekua akakuta kuna laini
Wakili wa Serikali: laini gani
Shahidi: Hallotel
Wakili wa Serikali: baada ya Kupata simu akafanyeje
Shahidi: akazitoa zile Laini, Akampa yule Mwingine akazishika
Wakili wa Serikali: Na Yeye Akaendelea na nini
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi
Wakili wa Serikali: hizo laini alikuwa anafanya nazo nini?
Shahidi: Alimpa Askari wa Pembeni akazishika
Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi
Shahidi: Aliendelea na Upekuzi lakini hakukuta kitu Kingine
Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi
Shahidi: aliomba fomu Mbili
Wakili wa Serikali: fomu ya Kwanza alijaza nini
Shahidi: alijaza vile Vikete Vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi
Shahidi: 25
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Alimpa akasema akasaini
Wakili wa Serikali: Nani Yeye, afande Jumanne?
Shahidi: Ndiyo na Baadae Mohamed
Wakili wa Serikali: na baadae
Shahidi: tukasaini sisi
Wakili wa Serikali: Wewe na nani
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: Ile fomu Nyingine akajaza Simu na laini Nyingine
Wakili wa Serikali: Za Mtandao gani
Shahidi: Airtel na Hallotel
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Alimpa Mohamed asome kisha akasaini
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: afande Jumanne alituomba na sisi tusome Kisha tusaini
Wakili wa Serikali: Wewe na nani
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada ya Upekuzi
Shahidi: walivalishwa Pingu
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: afande Jumanne akatuomba tuelekee Kituoni
Wakili wa Serikali: Hao walivalishwa Pingu walikuwa ni akina nani
Shahidi: Adam na Mohamed
Wakili wa Serikali: baada ya kuvalishwa Pingu..?
Shahidi: Wakaelekea kwenye Magari, Barabarani
Wakili wa Serikali: Palikuwa na Askari wangapi
Shahidi: Watano
Wakili wa Serikali: Walikuwa wamebeba nini
Shahidi: Wawili walikuwa wamebeba Bunduki
Wakili wa Serikali: Hali ya hewa eneo lile ilikuwaje
Shahidi: ilikuwa imetulia
Wakili wa Serikali: Hali ya hewa ilikuwaje
Shahidi: Kulikuwa na Jua na Mwanga
Wakili wa Serikali: Mlichukua Muda gani kwenye lile eneo Mpaka Mnamaliza Zoezi
Shahidi: Kama Dakika 45
Wakili wa Serikali: Baada ya Kufanya Upekuzi Kuna Vitu Vilipatikana na Kwamba Kuna fomu zilijazwa Sasa fomu ukiziona hapa utaweza Kuzitambua?
Wakili wa Serikali: sasa bada ya Kumalizia Mkaelekea kituoni, kituo gani..?
Shahidi: Central Moshi
Wakili wa Serikali: baada ya Kufika police central
Shahidi: Tuliandika Maelezo
Wakili wa Serikali: Maelezo ya nini
Shahidi: Kitu gani Kilichofanyika ......
Wakili wa Serikali: Tukianza na fomu ya Adam utaitambuaje
Shahidi: Kwa vitu vilivyoaandikwa, Jina langu na sahihi yangu
Wakili wa Serikali: Kulikuwa na nini Kingine Bastola
Wakili wa Serikali: Kingine
shahidi: Palikuwa na Risasi
Wakili wa Serikali namba gani Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba nimpe fomu aweze Kuitambua
Wakili wa Serikali: Shika hii Karatasi iangalie kwa Makini
Shahidi: Ndiyo yenyewe
Wakili wa Serikali: Yenyewe nini
Shahidi: Fomu niliyo saini