Uchaguzi 2020 Yaliyojiri kwenye Kampeni za Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu mikoa ya Kigoma na Kagera

Uchaguzi 2020 Yaliyojiri kwenye Kampeni za Mgombea Urais wa CHADEMA, Tundu Lissu mikoa ya Kigoma na Kagera

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CHADEMA, Tundu Lissu Jana ameingia Kigoma kwa kishindo kikuu.

Alilakiwa na Maelfu Elfu ya watu waliojipanga majiani huku wakitandika mikeka chini shujaa huyo wa karne hii apite juu yake.

Akihutubia umati mkubwa unaokadiriwa kuwa na watu zaidi ya Elfu 30 katika viwanja vya Community Centre Lissu alisema alichokishuhudia Kigoma ni kwamba wananchi wameamua kuondoa utawala wa kidhalimu na kuweka utawala utakaojali #UTUHAKINAMAENDELEOYAWATU#

Tundu Lissu alisema Chadema kinatambua mchango mkubwa unaotolewa na Zitto Kabwe ambaye ni mzaliwa wa Mkoa huo.Lissu aliuambia umati huo Chadema na ACT ni kitu kimoja katika uchaguzi huu na kwamba wananchi wamchague mgombea anayeweza kuitoa CCM madarakani ambaye ana ushawishi Hoja na anayeungwa mkono na watu.

Huku wakimjibu kwa kelele za Shangwe wananchi hao walipaaza sauti na kusema ni Zitto Kabwe watakayemchagua kuwa mbunge wao na kura zote za Urais wataelekeza kwa Tundu Lissu

Awali Lissu aliwaambia wananchi hao kwamba wakati anaumwa alipata Salaam kutoka kwa watu wa Kigoma walizomtuma kijana wao Zitto Kabwe.

Mara baada ya kuhutubia Shujaa huyo akisindikizwa Kifalme na umati mkubwa uliokuwa ukiimba Rais Rais Rais mpaka Hotelini kwake.

Siku moja kabla ya Tundu Lissu Kuwasili Kigoma Kiongozi wa ACT Zitto Kabwe alitoa tangazo rasmi la kunikaribisha mkoani humo na kuwataka wananchi kumpokea kwa Shangwe
 
Wakuu habari za Jumapili , kama kawaida yetu leo tena tunaendelea kuwaletea taarifa za mbeba maono Mh Lissu , ambapo leo yuko Kigoma na baadaye atatinga Mkoa wa Kagera

Endelea kubaki hapahapa JF kwa taarifa za uhakika .

Mgombea Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Tundu Lissu ataendelea na  ( 640 X 640 ).jpg


=======
UPDATES 1

Kazuramimba - Uvinza

Subpost 3 - Mgombea Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Tundu Lissu le ( 360 X 640 ).jpg
Subpost 2 - Mgombea Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Tundu Lissu le ( 360 X 640 ).jpg
Subpost 1 - Mgombea Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Tundu Lissu le ( 359 X 640 ).jpg
 
I swear before God and Man! Kuna usiku niliota kitu cha namna hii.

Usiku wa majuzi wiki iliyopita niliota Lissu kambwaga Magufuli kwenye uchaguzi huu wa 2020.
Kazi iliyobaki kwa Lissu ni kulinda ushindi wake na ndilo jukumu la watanzania.
 
Kazi kubwa sana inafanyika
Yale mambo ya kusema eti CCM inabebwa na taasisi za serikali pamoja na majeshi yake inabidi yakome mwaka huu. Hivyo vyombo vinakuwa na nguvu vinapokabiliana na mtu mmoja mmoja aliyehitilafiana na haki. Lakini kama ni umma unaodai haki, hapatatosha! Na mwaka huu hakuna kumwachia Mungu hata tone la uonevu.
 
I swear before God and Man! Kuna usiku niliota kitu cha namna hii.

Usiku wa majuzi wiki iliyopita niliota Lissu kambwaga Magufuli kwenye uchaguzi huu wa 2020.
Kazi iliyobaki kwa Lissu ni kulinda ushindi wake na ndilo jukumu la watanzania.
Endelea kuota, angalia tu usikojoe!
 
I swear before God and Man! Kuna usiku niliota kitu cha namna hii.

Usiku wa majuzi wiki iliyopita niliota Lissu kambwaga Magufuli kwenye uchaguzi huu wa 2020.
Kazi iliyobaki kwa Lissu ni kulinda ushindi wake na ndilo jukumu la watanzania.
This is the remaining concern! A great one! Lisu keshashinda. Je watamtangaza? Nini kifanyike LEO (na si kesho) ili atangazwe? Mwanahabari Huru
 
Back
Top Bottom