Pre GE2025 Yaliyojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA 23/9/2024
Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Chade
 

Attachments

  • 20240923_142737.jpg
    20240923_142737.jpg
    681.2 KB · Views: 1
1. Police wameshindwa kumpata Mbowe hadi amefika kwenye maandamano na kurekodiwa na vyombo vyote vya ndani na nje.

2. Jeshi la police limekuwa barabarani wakiwa na silaha na magari kwa siku 3 nchi nzima.

3. Watanzania wote wamejua chadema inaandamana na inazuiwa na serikali .

4. Watanzania wamefikishiwa ujumbe wa waliotekwa na waliupotezwa.

5. Serikakali imefikishiwa ujumbe, watanzania wanajua haki zao, ni watu wa amani, police wanatakiwa kuwalinda hata kwenye maandamano.
 

Attachments

  • 20240923_142000.jpg
    20240923_142000.jpg
    157.8 KB · Views: 1
Hali ilivyokuwa asubuhi ya leo jijini Dar es Salaam

Hali imerejea kuwa ya kawaida jijini Dar es Salaam baada ya polisi kuimarisha ulinzi katika maeneo mbalimbali ya jiji la kibiashara la Dar es Salaam nchini Tanzania wakati ambapo maandamano yaliyotangazwa na chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) yalikuwa yamepangwa kufanyika.
Polisi wakiwa na silaha na magari yenye maji ya kuwasha na gesi ya kutoa machozi walionekana katika maeneo kadhaa jambo ulinzi uliimarishwa Zaidi eneo la Magomeni ambako Chadema ilipanga kuanzia maandamano yao.
Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho Freeman Mbowe alikamatwa na Polisi eneo hilo la Magomeni Pamoja na bintiye Nicole, umbali wa wa takribani kilomita tatu kutoka katikati ya jiji. Bintiye Mbowe alichiwa huru baadaye. Mke wake Mbowe, Dkt Lilian pia alikamatwa wakati akielekea kazini, japo aliachiwa baadaye.

Kabla ya Mbowe kukamatwa, alifika eneo hilo akiwa na gari dogo, kisha kuanza kuzungumza na waandishi wa habari.
Viongozi wengine kadhaa wameripotiwa kukamatwa wakiwa kwenye kikao katika ofisi ya kanda ya chadema, akiwemo Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara, Benson Kigaila.
Septemba 11, 2024, Mbowe alitangaza kufanyika maandamano ya kulaani matukio ya watu kutekwa na mauaji, akiwemo kada wake, Ali Kibao. Hata hivyo, Jeshi la Polisi kupitia msemaji wake, David Misime lilitangaza kuyapiga marufuku.
Kwa mujibu wa Mbowe, wameamua kuweka mkazo suala hilo, baada ya maombi ya mahitaji, ikiwemo kutaka kujiuzulu kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Hamad Masauni, viongozi waandamizi wa ulinzi na usalama kama sehemu ya uwajibikaji.
Mbowe aliwaambia waandishi wa habari kuwa aliamua kuwa mstari wa mbele ili kuongoza maaandamano na kwamba kinachofanywa na vyombo vya dola dhidi ya upinzani ndiyo gharama ya dedmokrasi.
Mapema polisi walimkamata Makamu mwenyekiti Tundu Lissu, kwenye makazi yake eneo la Tegeta nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam baada ya kuizingira nyumba yake.
Baadaye kamanda wa pili Kanda maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro ilitangaza kuwashililia watu kumi na wanne (14) wakiwemo viongozi wa chama hicho Freeman Mbowe, Tundu Lissu na Godbless Lema.
Kwa mujibu wa taarifa ya polisi viongozi hao wamekamatwa wakiwa wanahamasisha kufanyika kwa maandamano ambayo hayana kibali.
"Taarifa rasmi tunazozitoa nikuwa watu hawa tunawashikilia na si kuwa wametekwa kama taarifa zinazozagaa, huko mtaani ulinzi umeendelea kuhamasishwa ili kuilinda amani tulionayo," ameeleza Muliro.
Polisi walisistiza kuwa hakuna kibali cha kufanya maandamano hivyo wataendelea kuwakamata wote wanaohamasisha maandano hayo.
Aidha polisi hawajaweka wazi ni lini watuhumiwa hao watapelekwa mahakamani.
Mwanasheria Rugemeleza Nshala, ambaye aliwahi kuwa rais wa chama cha wanasheria Tanganyika ameiambia BBC kuwa hatua ya polisi kuzuia maandamano si halali kwani Katiba ya Tanzania kuandamana na kutoa hisia zao na kupinga vitu vinavyoonekana kuwa kinyume ch Katiba.
“Ibara ya 26 (1) inaeleza kila raia anapaswa kuheshimu Katiba na sheria za nchi na kwamba watu wote akiwemo polisi na rais wameapa kuilinda Katiba na kwamba Ibara ya 8(1) ya Katiba inaeleza kuwa madaraka yanatoka kwa wananchi, hivyo watendaji wa vyombo vya dola wanaposhindwa kulinda haki za binadamu ikiwemo haki kubwa ya kushinda zote, haki ya maisha, kutoka na kushindwa kuzuia mauaji na watu kutekwa na kuzuia maandamano, huko ni kukwepa uwajibikaji” amebainisha Nshala.
Amefafanua kuwa hukumu ya Mahakama Kuu ya mwaka 1995 katika kesi ya Christopher Mtikila dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali jaji Kahwa Lugakingira alitoa msimamo wazi kuwa maandamano yatanatakiwa kusitishwa ama kuzuiwa iwapo tun kuna viashria vya wazi vya uvunjivu wa amani jambo ambalo anase kwa sasa hapakuwepo viahiria vya aina hiyo kwani chadema wana rekodi ya kuandamana kwa amani. Chanzo.BBC
 
1. Police wameshindwa kumpata Mbowe hadi amefika kwenye maandamano na kurekodiwa na vyombo vyote vya ndani na nje.

2. Jeshi la police limekuwa barabarani wakiwa na silaha na magari kwa siku 3 nchi nzima.

3. Watanzania wote wamejua chadema inaandamana na inazuiwa na serikali .

4. Watanzania wamefikishiwa ujumbe wa waliotekwa na waliupotezwa.

5. Serikakali imefikishiwa ujumbe, watanzania wanajua haki zao, ni watu wa amani, police wanatakiwa kuwalinda hata kwenye maandamano.
IMG-20240923-WA0050.jpg
 
No body is fearing international community, sisi ni nchi huru, hatupangiwi cha kufanya, tunapenda amani nchini sio mnatusumbua sumbua na maandamano tunashindwa hata kwenda mjin bana
 
Waandamanaji wa leo walikuwa polisi, mabango yalikuwa mitutu ya bunduki ya polisi na mic za waandishi wa habari

Kiongozi wa maandamano alikuwa Mh. Mbowe aliyefanikiwa kutoa hotuba kabla ya kutiwa nguvuni

Kimantiki ujumbe waliokusudia kuutoa umefika sehemu iliyokusudiwa na waliosaidia kuufikisha ni askari polisi na waandishi wa habari. Kufikisha ujumbe hilo ndio lengo kuu la maandamano yoyote yale duniani.

CHADEMA wanatakiwa kuwashukuru viongozi wa serikali na polisi kuwasaidia kufikisha ujumbe wao pengine kuliko ambavyo wangeandamana wenyewe tu bila hiki kilichotokea leo
 
Waandamanaji wa leo walikuwa polisi, mabango yalikuwa mitutu ya bunduki ya polisi na mic za waandishi wa habari

Kiongozi wa maandamano alikuwa Mh. Mbowe aliyefanikiwa kutoa hotuba kabla ya kutiwa nguvuni

Kimantiki ujumbe waliokusudia kuutoa umefika sehemu iliyokusudiwa na waliosaidia kuufikisha ni askari polisi na waandishi wa habari. Kufikisha ujumbe hilo ndio lengo kuu la maandamano yoyote yale duniani.

CHADEMA wanatakiwa kuwashukuru viongozi wa serikali na polisi kuwasaidia kufikisha ujumbe wao pengine kuliko ambavyo wangeandamana wenyewe tu bila hiki kilichotokea leo
Ahahahahaha! Mabingwa wa kuandamana nyuma ya keyboards at work! Ahahahahaha!!
 
tatizo la polisi na kiongozi wao ni ile kauli ya "samia must go" hiyo ndio wanaiogopa watu wasiitamke
 
Hali imeendelea kama ilivyokuwa, hakukuwa na tatizo lolote zaidi ya watu kukosa tu uhuru kutokana na virungubkuwa vingi mitaani
 
Ahahahahaha! Mabingwa wa kuandamana nyuma ya keyboards at work! Ahahahahaha!!
Linapokuja swala la kuandamana nchi hii inawaandamanaji maalum, ni swala la kuwa-switch tu muwaamrishe waandamane nchi nzima, mkoa mmoja au wilaya moja! Hawajawahi kushindwa hao. Hujaona leo walivyoandamana kwa magari, wengine kwa miguu na wengine wakiwa na mbwa tena wakiwa na sare zao safiii kabisa. Wako smart!
 
Back
Top Bottom