Kenya 2022 Yaliyojiri Uchaguzi Mkuu wa Kenya: William Ruto ashinda kiti cha Urais, apata 50.49% ya kura

Kenya 2022 Yaliyojiri Uchaguzi Mkuu wa Kenya: William Ruto ashinda kiti cha Urais, apata 50.49% ya kura

Kenya 2022 General Election
TUME YAKANUSHA TAARIFA ZA MIFUMO YAKE KUDUKULIWA

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imewatoa hofu wananchi juu ya uwepo taarifa za mifumo yake ya Kura kudukuliwa

Mkurugenzi Mtendaji wa IEBC, Marjan Hussein Marjan amesema taarifa zinazoenea kuhusu tovuti ya matokeo kuingiliwa sio za kweli na amewakikishia Wakenya kuwa wamechukua hatua za kujilinda katika ngazi zote

Marjan amekiri kuwa wadukuzi walijaribu kufanya hivyo lakini mifumo ya IEBC haikuwa dhaifu, na kuongeza kuwa wamekuwa wakifuatilia mifumo yote ikiwa ni pamoja na mtandao, programu, hifadhidata na mfumo wa uendeshaji ili kuzuia majaribio yote ya udukuzi
 
kitendawiliiiiiiiiiiiiiiii.................tega.....nikuteg!!
Babu kazimia akiwa mdomo wazi...........

Jibu tafadhali..................
 
Ngoja tusaidiane ni a simple language na mfano, let's say kuna kura halali za urais 20,na katika kura hizi mgombea A kapata 12 ya kura halali zilizopigwa na mgombea B kapata kura 7 na mgombea C kapata kura 1,jumla ya kura zote itakua 12+7+1=20(hizi ni total ya kura halali zilizopigwa za urahisi na ndio 100%,ya kura zote),to be a winner ni LAZIMA uwe na kura 10(50% ya total vote(20)plus 1 vote yaani uwe na kura 11,sasa kwa katiba ya Kenya ya sasa ni lazima mshindi apate 50%ya kura zote halali (majority)plus 1,kuna hatari ya kufanya re run ya hawa top two.Tanzania unaweza kuwa president hata kama umepata 29%,ya total votes as far wengine wana below that!yaani A ana 10%,B ana 7%na C awe na 3%,ya total veto,huyu aliyepata 10%ya kura anaapishwa kuwa president
Tanzania ndio safi ni simple majority biashara inaisha
 
Yeah and within seconds unakimbilia humu kulalama na ajira za muda za sensa,!!
Nani alalame ? Ndugu yangu Demokrasia ni kitu kigumu sana ndio maana hata wakati Fulani chaguzi za Marekani zinaleta tatizo. Hata hawa wakenya bado ni shida tu. Mbona sasa TV zimezuiwa kwa muda kutoa taarifa ? Chezea Demokrasia weye.
 
Kwenye re-run wanabaki wagombea wawili tu kwa hiyo possibility ya kupata mshindi ni 99.99999999 % kwa sababu uwezekano wa kupata kura 50% plus 1 vote ni mkubwa.
Mkuu kwa mwenendo ulivyo Ruto anachukua nchi bila marudio ya upigaji kura! Kuna uwezekano team ya Raila walifanya uongo mwingi kupitia media house anzia majuzi kwenye utoaji wa taarifa
 
Mkuu kwa mwenendo ulivyo Ruto anachukua nchi bila marudio ya upigaji kura! Kuna uwezekano team ya Raila walifanya uongo mwingi kupitia media house anzia majuzi kwenye utoaji wa taarifa
Uongo unatoka wapi tena wkt matokeo yapo kwenye site ya uchaguzi kila mtu anaweza kujumlisha
 
Back
Top Bottom