Kenya 2022 Yaliyojiri Uchaguzi Mkuu wa Kenya: William Ruto ashinda kiti cha Urais, apata 50.49% ya kura

Kenya 2022 Yaliyojiri Uchaguzi Mkuu wa Kenya: William Ruto ashinda kiti cha Urais, apata 50.49% ya kura

Kenya 2022 General Election
Wakati Watanzania tukifundishwa kwa vitendo somo la demokrasia na Wakenya nadhani huu mfumo wa Tv stations kuwa na ruksa ya kujumlisha matokeo na kuyatangaza hautufai Tanzania, naogopa TBC itasabanisha machafuko ambayo hatujawahi kuyaona.

Tutafute namna bora ya kupata matokeo ya kweli kabla ya tangazo rasmi la NEC.

TBC italeta maafa na machafuko makubwa Tanzania tukiadapt huu mfumo huru wa Kenya.
zile mbinu za Chadema kuwaambia wafuasi msiondoke kituoni hadi matokeo yabandikwe nadhani ipo kienyeji sana ,wenzetu wamestaarabika ,kura zimepigwa na wamekaa tu nje na mabox ya matokeo wanatuma matokeo na hakuna usumbufu ,hapa polisi wa ccm wangeforce hata kuvuruga wakiona kwenye kituo ccm inashindwa
 
Tanzania hatuwezi kukubali uchaguzi ukawa influenced na wahuni. Kenya hiyo ni failed state, kila mwenye vipesa anajiamulia tu.

Huku ni lazima CCM itengeneze serikali iwe kwa halali au haramu. Nakupa ukweli mchungu, umeze.

Iwe kwa halali au kwa haramu CCM ni lazima tuendelee kuongoza serikali.
Sasa hii uliyoandika ndo matatizo kuwa na akili matakoni badala ya kichwani
 
Tanzania hatuwezi kukubali uchaguzi ukawa influenced na wahuni. Kenya hiyo ni failed state, kila mwenye vipesa anajiamulia tu.

Huku ni lazima CCM itengeneze serikali iwe kwa halali au haramu. Nakupa ukweli mchungu, umeze.

Iwe kwa halali au kwa haramu CCM ni lazima tuendelee kuongoza serikali.

Nakusalimu kantriwaidi
 
Tanzania hatuwezi kukubali uchaguzi ukawa influenced na wahuni. Kenya hiyo ni failed state, kila mwenye vipesa anajiamulia tu.

Huku ni lazima CCM itengeneze serikali iwe kwa halali au haramu. Nakupa ukweli mchungu, umeze.

Iwe kwa halali au kwa haramu CCM ni lazima tuendelee kuongoza serikali.
Ndugu yangu kuwa na akiba ya maneno tafadhari. Kwa kauli zako ni sawa kabisa na kauli za yule bosi wa titanic. Lakini hakuamini macho yake siku anaona titanic yake ilivyokuwa inafukiwa na vilindi vya maji pasi na msaada wowote.

Na msingi mkubwa wa hao unaowasifia ni umbumbumbu wa wanaowaongoza. Sasa imagine siku hao mbumbumbu wakibumbuluka na wakati huo nyie kwa hio haram unayoitaja itakuwaje. Au wewe mwenzetu una pa kukimbilia?

Mnakula na vipofu, tafadhari msiwashike mikono. Acha kejeli na majivuno.
 
Ruto na Uhuru walikua marafiki kivipi? Ruto ndio alikua ana support mauaji ya Wakikuyu huku Kenyatta akidhamini vikundi vya Wakikuyu kuwachinja kabila la Ruto so walikua maadui kitambo. Kilichowaunganisha ni uchaguzi tu wa 2013 ila uadui umerudi kama zamani maana HAWAJAWAHI KUWA MARAFIKI.
Siasa za Kenya ni ngumu tangu zamani. Nakubali process zao za kupiga kura na kuhesabu kwa sasa ni nzuri na ziko open kuliko sisi lakini ukiingia kwa undani kuna makandokando mengi sana. Kuna mgombea mmoja wa ubunge ameua mtu kwa risasi na mpaka sasa hajulikani aliko. Ni mgombea wa ushirika wa Ruto na watu wanasema anasubiri Ruto ashinde ili ajitokeze akitegemea atalindwa na mamlaka. Yaani mtu hata urais hajaupata lakini tayari wameanza kuonyesha uongozi wa hovyo.
 
Ndugu yangu kuwa na akiba ya maneno tafadhari. Kwa kauli zako ni sawa kabisa na kauli za yule bosi wa titanic. Lakini hakuamini macho yake siku anaona titanic yake ilivyokuwa inafukiwa na vilindi vya maji pasi na msaada wowote.

Na msingi mkubwa wa hao unaowasifia ni umbumbumbu wa wanaowaongoza. Sasa imagine siku hao mbumbumbu wakibumbuluka na wakati huo nyie kwa hio haram unayoitaja itakuwaje. Au wewe mwenzetu una pa kukimbilia?

Mnakula na vipofu, tafadhari msiwashike mikono. Acha kejeli na majivuno.
Nimekupa ukweli mchungu, kuumeza ni hiari yako
 
Jamani sio kazi rahisi kupakua fomu 46,000 huku media house Zina wafanyakazi sio zaidi ya 20 kwenye kuhesabu kura!!

IEBC wenyewe hata kuhesabu hawajaanza afu lawama kwa vyombo vya habari?? Kwani wapi ni jukumu la vyombo vya habari kuhesabu na kutangaza Mshindi?
Basi waache kama hawawezi,ni rahisi kuwa chanzo cha fujo......maana wengi wanafuatilia Kwa njia ya vyombo hivyo
 
Hawa wagombea bendera fuata upepo wa chama cha Roots,Agano hizo kura 4 nne walizopata kwa diaspora zina ukweli!? Hapa huwa napata ukakasi au ni kuwa wakenya wamechoka na uongozi uliopo kiasi hata wasomi diaspora kutoka rwanda kuamua kuharibu kura zao 8 kwangu naziweka kwenye kundi la kura zilizoharibika.

Sent from my TECNO RC6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom