Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Uwanja wa Kambarage Shinyanga: Dkt. Magufuli asema Miaka 5 haitoshi, mpimeni kwa miaka 10

Uchaguzi 2020 Yaliyojiri Uwanja wa Kambarage Shinyanga: Dkt. Magufuli asema Miaka 5 haitoshi, mpimeni kwa miaka 10

Mwenye shinyanga yake Yuko kambarage, watu watauwana walivyojazana, kiwanja kimekuwa kidogo wengine wamekosa nafasi

Ama kweli JPM anatiisha
 
Watanzania tumeshuhudia maiti za watanzania wenzetu zikiokotwa kwenye fukwe zikiwa zimefungwa mawe na vyuma na nyingine zikiwa kwenye viroba.

Watanzania, tumeshuhudia wenzetu wakitekwa na kupotezwa, wafanyabiashra wakifilisiwa,.

Tumeona ndugu na jamaa zetu wakifunguliwa makesi makubwa na yasiyo na dhamana.

Huyu mtu hatufai kabisa.
Go to the point.
 
Nimeamini Lisu hajui hata kusoma yaliyoomo kwnye katiba Na sheria zetu.
MGAMBO ni askari msaidizi anayetambuliwa Na katiba yetu.
weka kifungu cha Katiba ya JMT inayosema hayo uliyoandika.
 

Leo kishindo cha awamu ya tano ambacho ni kishindo cha wasanii kitakuwepo uwanja wa Sabasaba Kambarage ambapo mgombea wa CCM ndugu John Pombe atakuwa jukwaani kunadi sera zake huku wasanii nane akiwemo Sholo Mwamba ambaye amempa shule kabambe ndugu Magufuli kucheza kiduku watakuwepo kutoa burudani ya hapa na pale.

Hizi kampeni bwana!
Imagine ndani ya mji mmoja anaanza Hashim Rungwe mnapiga bweche mnashiba, anafuatia Tundu Lissu mnakula madini na kisha anamalizia John Magufuli mnakula burudani kisha mnarudishwa makwenu.

Kwa hakika ingekuwa ni mserereko. NEC sikieni kilio chetu hiki kuhusu ratiba.

Burudani kwa wote!

Una akili ndogo kishenzi.... Silly.
 
Sisi Wanashinyanga tunamuuliza "Alikuwa wapi wakati ndugu zetu wanafukiwa kule Bulyanhulu"? Mbona hakuwahi kutoka kauli yoyote ya kusikitika? .
Lissu akiwa kijana ndiye aliyetupigania, huyu Msukuma mwenzetu alikaa kimya kama ugali
 
Mzee sauti imekauka..anatumia nguvu kubwa[SUB] sana kwenye kuzungumza.[/SUB]
 
PATROBAS KATAMBI- INJINI NDOGO YA CCM
Nimesikitika sana kuona Rais wangu leo anapigishwa magoti na yule mvuta bangi muimba kiduku.

Tafadhalini wahuni kama hawa wapelekeni kwenye kampeni za madiwani huko au za wabunge.

Ni lazima ifahamike Magufuli bado ni Rais wa nchi hata kama anaomba kura, sijapenda kabisa mvuta bangi mmoja kuwapigisha magoti viongozi eti anaendezha duwa huku anaimba singeli na viongozi wa dini wapo pale, msifumbie macho hawa wahuni wa Humphrey Polepole, hizi ni dili za Chakubanga, Dr Bashiru hakutaka kabisa kuwatumia hawa wahuni wakati TOT ipo na inapiga burudani live band na siyo yale magumashi ya play back za hawa Bongo fleva.
 
Back
Top Bottom