YEHODAYA
JF-Expert Member
- Aug 9, 2015
- 36,902
- 52,001
Watu tayari wameshaanza kufurika Uwanja wa Amani Zanzibar.
====
MWILI WA HAYATI DKT. MAGUFULI WAWASILI ZANZIBAR
Mwili wa Hayati Dkt. John Magufuli umewasili Visiwani Zanzibar ukitokea Makao Makuu ya Tanzania, Dodoma, ambapo shughuli ya kumuaga kitaifa ilifanyika jana Machi 22, 2021.
Mwili wa Dkt. Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, 2021 umepokelewa na Viongozi mbalimbali wakiwemo Rais Hussein Mwinyi wa Zanzibar na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa. Utapelekwa Uwanja wa Amaan ambapo utaagwa.
RAIS MWINYI: KIONGOZI KAMA DKT. MAGUFULI NI NADRA KUPATIKANA
Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi amesema Hayati Dkt. John Magufuli alikuwa mstari wa mbele katika kuimarisha maisha ya Watanzania kwa misingi ya Haki na Usawa bila kujali Dini, Kabila, Rangi au Jinsia.
Amesema, "Tumempoteza Mwana Mapinduzi mahiri wa karne ya sasa. Alikuwa Kiongozi mwenye uwezo na kipaji cha aina yake. Kiongozi kama yeye ni nadra sana kupatikana"
Katika hotuba yake, amemuelezea Dkt. Magufuli kama Kiongozi aliyejipambanua kwa uzalendo wa kweli, mtetezi wa wanyonge, mwenye kujivunia na kujionea ufahari Utanzania na Uafrika wake.
Amesema kifo chake kimeleta simanzi kwa Watanzania na wapenda Maendeleo katika bara la Afrika.
====
MWILI WA HAYATI DKT. MAGUFULI WAWASILI ZANZIBAR
Mwili wa Hayati Dkt. John Magufuli umewasili Visiwani Zanzibar ukitokea Makao Makuu ya Tanzania, Dodoma, ambapo shughuli ya kumuaga kitaifa ilifanyika jana Machi 22, 2021.
Mwili wa Dkt. Magufuli aliyefariki dunia Machi 17, 2021 umepokelewa na Viongozi mbalimbali wakiwemo Rais Hussein Mwinyi wa Zanzibar na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa. Utapelekwa Uwanja wa Amaan ambapo utaagwa.
RAIS MWINYI: KIONGOZI KAMA DKT. MAGUFULI NI NADRA KUPATIKANA
Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi amesema Hayati Dkt. John Magufuli alikuwa mstari wa mbele katika kuimarisha maisha ya Watanzania kwa misingi ya Haki na Usawa bila kujali Dini, Kabila, Rangi au Jinsia.
Amesema, "Tumempoteza Mwana Mapinduzi mahiri wa karne ya sasa. Alikuwa Kiongozi mwenye uwezo na kipaji cha aina yake. Kiongozi kama yeye ni nadra sana kupatikana"
Katika hotuba yake, amemuelezea Dkt. Magufuli kama Kiongozi aliyejipambanua kwa uzalendo wa kweli, mtetezi wa wanyonge, mwenye kujivunia na kujionea ufahari Utanzania na Uafrika wake.
Amesema kifo chake kimeleta simanzi kwa Watanzania na wapenda Maendeleo katika bara la Afrika.