Yamenifika shingoni sijui la kufanya mimi

Yamenifika shingoni sijui la kufanya mimi

Wazee wengine nuksi tu kama wote ni wazaz halisi sepa kakae mbali kama ni mama wa kambo basi ndo sababu uzilazimishe kupendwa we kafanze yako wakizeeka hao itakuwa zamu yako kupeta nawe utakuwa umeshika mpini
Nimekuelewa mkuu
 
Asilimia 90 ya Wazazi wàpo hivyo.

Màtukio ya namna hiyo yanawapata Watu wengi Sana hasa kutoka bara la Afrika.

Mzazi anayetegemea kupata chochote Kwa Mtoto hana tofauti na mfanyabiashara.

Mungu pekee ndiye wakumtegemea, yeye hahitaji chochote kutoka kwako
Sawa ndugu yangu ubarikiwe nimekuelewa mkuu
 
Pole Sana Ila wazazi ni watu muhimu you need to respect them haijalishi wanaku-treat vipi.

Kama unapitia haya mambo

Financial broke
@clonical disease

Lazima hizi hali zitakufanya uwachukie WATU Sana .


Ushauri .

Be positive
Love ur parents
Jiandae kwa lolote don't afraid kuhusu kufa au kuishi.


Pambania Afya yako .

Umesema kuhusu sherehe, sherehe ni mambo madogo Sana in our life.


Pia jaribu kuwa giver na sio taker.
Ahsante sana mkuu ubarikiwe nimekuelewa sana
 
Kwa walionizidi umri shikamoni na kwa wa umri wangu habari zenu?

Kilichonileta mbele zenu ni hiki ndugu zanguni ni haya nayopitia na baba yangu licha ya kuwa na maswaibu yanayonisumbua kwa muda mrefu mpaka nashindwa kufanya kazi zangu kwa kuamua bali huwa najilazimisha ivoivo baada ya kuona ambao niliamini wanaweza simama na mimi kwenye haya nayopitia kuchukulia kawaida sana.

Siku moja hawa wazazi niliwaambia inabidi nienda hospitalini wakakaa kimya kwa kuwa nilikuwa nawajua nikajipanga hata kama hawatanisaidia pesa yoyote mimi ntaenda tu, siku ya kwenda ikafika nikajiaandaa wananiangalia tu.

Nikawa naenda hospital ya rufaa hiyo siku naye baba alikuwa anaelekea huko ila sio hospitalini tukawa tupo gari moja tukashuka tulivofika huka nikashangaa aniniuliza unaenda wapi nikamwambia hospitalini akakaa kimya tu tukaachana kila mtu akashika njia yake.

Cha kushangaza akarudi nyumbani na kuniacha huko alafu akaenda kumuulizia mama mimi apa nimeenda wapi?

Sikuona ata simu yake wala ya mama maana vipimo vyangu vilikuwa vinachukua sio chini ya siku 5 kulingana na tatizo langu lipo complicated sana. Basi ndugu zangu nikaendelea kuishi nao hivohivo wala si kusema kitu chochote.

ikatokea tena mda mwingine nataka niende hospital na wala nilikuwa siwategemei tena wakinisaidia sawa wasiponisaidia sawa lazma mimi mwenyewe nijipange kwanza hii time baba akanambia hela hana ila ambayo ipo anataka anunulie mashamba kwanza picha linaanza iyo tulipanga tutakuwa safar moja akaniacha.

Ila mi nilizoea toka niko shule nimefanyiwa mikwazo mingi sana nilienda chuo sikuwahi pewa ata 100 mbovu kabisa maana nauli toka nyumban had huko nilikuwa nasoma ilikuwa haipungui 40000,,,kuna kipindi niliwahi kaa njian wiki 2 kwa kujishikiza kwa dogo fulani ivi ndo nikafika huko chuo.

Hapo niligundua hata nikimaliza chuo sina msaada na huyu baba ikabidi kule chuo nijibane sana bas pesa niliopata kwa kusevu nikawekeza kule nyumbani.

Kuna kipindi wakati nasoma nilijitahidi nikawekeza kwenye kitu cha msimu ile pesa baada ya kupatikana baba akaichukua huku akasema atanipa ndo ikawa mazima.

Wakati namaliza chuo wote wawili wakaniagiza simu kama nina balance niwanunulie simu watanipa ela nikifika nyumbani ikawa ndo bas tena wakati mi nilikuwa nawaza hizo ndo hela zitanisaidia ninavoingia mtaani hii yote nilikuwa najua nafanya wema kumbe najimaliza.

Life la mtaa likaanza sasa nikajiingiza kwenye moja ya zao kama mnavojua haya mazao yanataka mbolea sasa mimi nikamwomba uyu baba siku unaenda huko tutaenda wote nikaangalie mbolea maana kule bei nafuu kuliko sehemu ninakoishi nikafos maana iyo siku nayo alikuwa anataka kuniacha.

Nikaenda kutafuta zile mbolea na kuuliza bei na yeye nikamwambia akasema zimepanda zilikuwa haziuzwi hivyo, basi akaniambia kunamtu huwa namubebea anajumuaga labda tukaunganishe naye nikasema sawa bas inabidi uwasiliane naye kama inawezekana ili niwe na uhakika chenga zikawa nyingi kiufupi ikawa haeleweki bas nikamwambia mimi ntaenda kuchukua kwa bei nilizozikuta siku ukiwa unaenda uniambie akapata safari ya kwenda tena uko cha ajabu hata hajaniambia.

Hapa nina maswali sana kwani ipo wazi huyu baba yangu furaha yake ni kuniona nateseka hilo ameanza kitambo sema mi najishobokesha tu niliamini atabadilika hapa nawaza kumkimbia kabisa huku nikiumia hilo zao nimewekeza kwa miaka isiopungua mi5 ila naliacha iviivi kisa visa vya baba ambaye niliamini ndo anaweza kuwa nguzo yangu na mshauri ila ndo mtu wa kwanza kunipiga vita, niliamini atabariki kazi zangu ila imekuwa tofauti sana😭😭😭😭 sina mpango wa kuuza ayo maeneo ili niondoke ni bora nimkimbie na nimuachie ilo zao kama atakataa kuliendeleza acha life tu sina namna.

Hivi na nyie mmewahi yapitia haya nishaulini jamani nafanyaje jamani kunamda huwa nawaza nijitoe dunian kabisa.

Nina mengi haya ni machache sana . Yani hapa ninavoongea licha ya kupita huko shule ya msingi, sekondari, advance had chuo kikuu sijawahi fanyiwa sherehe hata moja ndugu zanguni naombeni ushauri wowote kulingana na maelezo ya hapo juu
Nilipofikia tu eti tatizo langu liko complicated sana nikaona ni bullshit!

Kama unataka ushauri sema hilo tatizo lako ni nini. Kama huwezi nenda kalale, Pumbafu!
 
Mara nyingi huwa naandika kuwa tatizo namba moja la waafrika ni ujinga...

Pindi waafrika watapoacha kukumbatia ujinga, hakika mambo mengi yatabadilika...

Ndugu mleta mada , acha ujinga...
Wewe una unaundugu na baba yangu hata yeye angeandika kama wewe
 
We piga chn huyo otherwise unajtafutia laana pga chn wote wawili tembea zako mi mzee nlishatemana naye kbs stak anijue na stak nimjue kila mtu apambane kivyake na nnahisi iktokea ametangulia uwenda kama taenda bs taenda kama mtu baki tu au staenda kbs. Pga chn kapambane kwngne badili namba waskupate kwsha.
Wewe utakuwa umenielewa vizur sana mkuu ahsante kwa kunitia moyo pia
 
Ndio wazazi wengi wa Kiafrika walivyo mkuu, sisi kule kwetu tunawaita
Wajerumani. Yani ni wazee wenye ukatili fulani hana muda wala
urafiki na watoto. Na mara nyingi ni wabinafsi na vitu vyao,

Wanataka ukatafute vitu vyako sio ufanye maendeleo kwenye
eneo lake. Hivyo bora uelewe tuu hivyo.

Wewe kama upo mikoa ya kusini sijui ni Mtwara au Lindi nyie si
Mjomba ana nguvu sana ulishaongea na mjomba?
Hataki kuwasikia ndugu za mama yangu yani yeye ni mtu wa kulaumu sana huwa nasikia anasema et wanamdharau
 
Viashiria havipo kabisa mkuu
Pia ni wewe mwenyewe ndio unajua ukweli. Nikuulize je wazazi wako wana viashiria vya kuwa washirikina? Nimeona mikasa kama hii ya wazazi kukataa watoto na kuwa wakatili sana kwa watoto wao wengi wa wazazi hawa unakuta ni wachawi na wamejaribu kuwashawishi watoto wao wawe wachawi ila wamekataa sasa wazazi wanawatesa ili kuwashinikiza wakubali.
 
oya dogo
hapo hauna wazaz aiseee hap ni wachawi yani kiufup wanatabia za wachaw maana hata mama mzaz huwa hawez kumfanyia mtoto wake wa kumzaa hivo hata kama utamkosea nn yan hawez kabsa sasa hao unaokaa nao huenda walkuzaa baat mbaya na hawana mpango na ww kwaio kua makn na hata uo ugonjwa huenda wanaujua ndo mana hawakup sapot upone
kwaio dogo tembea fanya mamb yako haina haja ya kuongea nao na kutia uluma amua maamuz magumu we mwanaume toka magetoni
kwanza nashangaa umemalza chuo ela umepata et bado unakaa nyumban yan we jamaa ni mfnyu. wa akili na degree yako
ama hapo kwenu ondoka kabsa na kajtafute hao wenyewe watakufata aiseeee
kaaa nao mbali sio wema kwako hata kama walkuzaa au huenda bmkubwa wako japo aliolewa akachepuka faza akajua sasa katka.kutunza heshima akaamua kuvunga ndo mana au almkuta mamako na ujauzto nn
sema kikubwa jitafute na je hauna ndugu kwan mbona unahangaika huku jf akat ndugu zako wapo upande wa mamako na babako emb watafute uwaulze juu yako toka utoto wako mpaka sasa wana kipi wanafaam pia uulize juu ya wazaz wako kwa wao huwa wanawafaam vp toka huko mwanzon mpaka sasa
ACHA KUTIA ULUMA DUNIA YA SASA HAINA HURUMA NA VJANA WANYONGE KAMA WW
JARBU KUJFUNZA NJIA NGUMU YA MAISHA NA UKFANKIWA N WW UKSHINDWA PIA N WW WAO NDO KWANZA UKISHNDWA WATAENDELEA KUKUCHAWIA UKFANIKIWA WATAKUJA NA BADO WATATAKA KUKUDIDIMIZA
Kwaio amua acha kulialia we wakiume
Nimekuelewa sana mkuu,,,mama yangu ndo huwa anafanyia vitu mpaka nashangaa na kubaki bila majibu,,,naweza nikapika labda nikatumia nyanya za ndani anakuja analalama na kuniambia uwe unanunua za kwako,,,vitu vyake siwezi nikavichukua kirahis bas mimi saiz nshabaki namwambia mungu tu aje anijalie niwe na uwezo wa kuvinunua huenda hiyo kauli ya kusema ninunue vyakwangu utaacha
 
Hapo mwisho kwenye hujawahi kufanyiwa sherehe nimecheka sana.
Nikirudi kwenye mada,binafsi nimepitia hali kama yako,mzee wangu hajawahi kunipa senti kumi yake licha ya kuwa alikuwa mwalimu mwenye mshahara.
Alipostaafu 2006 akaniambia anataka anipe 5m nifanyie mtaji kwasababu hajawahi kunisadia.Hakunipa chochote ni porojo.

Nilipambana biashara hapa na pale nikanunua daladala route ya Mwenge _Bagamoyo mwaka 2008.
Hapo ndoto yangu ya kusoma ikarudi,nikajisomesha QT namshukuru Mungu nilitoboa kote,2012 nikaingia chuo kikuu na mkopo nikapata (BAED)
Baada ya kumaliza chuo nikapata kazi ,nikafundisha miaka 3 nikaacha kwasababu sikuona kama ndoto zangu zitatimia kwenye kada ya ualimu,hivyo nikarejea kwenye biashara.

Wakati wote huo mzee wangu amejiweka mbali na mimi hata nikimpigia simu anaongea ile kimachale haraka haraka ili nisimuombe kitu kumbe hajui niko vizuri wakati huo.

Point ambayo ndio tuliagana rasmi na sidhani kama nitapiga u turn, ni wakati nataka kuoa,nikamtaarifu kwa heshima tu akasema ni jambo jema tuko pamoja atanipa ushirikiano nk.Kinyume chake hakufanya chochote hata kwenda ukweni alipiga chenga akidhani kwamba nitamuambia atoe mahari (kama ilivyo desturi ya kwetu )
Kutoka hapo hatuwasiliani kabisa zaidi ya miaka 3 sasa.Habari zangu anasikia kwa ndg zangu,kijana kajenga ghorofa pale,kijana kanunua gari ya mbunge 😂 nk.Roho inamuuma lakini hawezi kuniambia nimsaidie amepigika mbaya.

Nimetoa huo ushuhuda mrefu kuwatia moyo wale wote wanaopitia hali ya kukataliwa na wazazi hasa baba zao, wapambane kana kwamba mzazi alishafariki.Hiyo hasira ya kukataliwa igeuze kichocheo cha kuchapa kazi kwa bidii na ubunifu ili siku moja uwaoneshe kwamba walibet vibaya
Imenitachi sana hii mkuu,,,kwa sasa mi mwenyewe Napambana kama mungu atajalia sitaki anitolee mahali kabisa maana mi hata nikiona mia yake huwa nahis mtego huu badala ya kufurahia hii baraka toka kwa mzazi
 
Nilipofikia tu eti tatizo langu liko complicated sana nikaona ni bullshit!

Kama unataka ushauri sema hilo tatizo lako ni nini. Kama huwezi nenda kalale, Pumbafu!
Sawa mkuu mimi sio mtu wa kupanic ata siku moja hili unaloliandika ni dogo sana kwangu na najua katika maisha watu kama nyie mpo hahaha kwaiyo tuishi tu ila nashukuru nimekutana na wewe
 
Ushauri mbaya sana huu mkuu.
Sio kila mzazi au mzee ana uelewa wa kukaa na wewe chini mkazungumza hayo yote.
Usikute hayo maongezi akachukulia kama matusi kwake.
Na lazima iwe ivo mkuu hapa utakuwa umeongeza matatizo tu
 
Kaka kuna wewe na kuna yeye mzee.
Mzee wako ni mtu mzima anatambua nini anachofanya,sio kwamba haoni anachofanya na hajui anachofanya.
Sasa unaumiaje juu ya mtu ambaye anatambua anachofanya!??
Wewe jipange ukishajipanga chomoka nenda unapopajua utaanzisha maisha yako kwa utaratibu sahihi.
Ila ukiondoka usiwatusi wala usiwavunjie adabu,ondoka kiadabu tu.
Ahsante mkuu nimeupokea ushauri wako ubarikiwe
 
sherehe sio kitu cha kulalamikia am 30's sijui sherehe yoyote ile mpaka saiv sio basidei mahafari au ndugu yake na hayo
Silalami hata mimi hivi vitu ni vidogo sana kwangu ni sikuwah kuwalaum ila naona wamevuka mipaka ndo mana nahusianisha
 
Back
Top Bottom