Yanayoendelea ndani ya uongozi wa CCM na serikali yanatafakarisha

Yanayoendelea ndani ya uongozi wa CCM na serikali yanatafakarisha

Mtakuja kutuambia. Hii Secretariat ya Nchimbi ni mbovu kuwahi kutokea. Ni zaidi ya ile ya Wilson Mkama. Picha linaanza wanafanya kazi na kutoa hotuba kama vile ni watumishi wa umma(civil servants). Wamegeuka wasemaji wa maafisa masuhuli na Mawaziri katika maeneo tofauti tofauti. Nadhani hili limechangiwa pia name ukweli kwamba wengi wao wamezoea kuwa watendaji katika maeneo kadha waliopita.
Makonda ndiye anajua na alijua kutafsiri maana halisi ya chama cha siasa, chama tawala na maana ya chama kuunda serikali.

Chama tawala hakipaswi kujiunga katika mlolongo wa Government Bureaucratic system but it should commands the system. Nchimbi and Co. ndio kwanza wameanza ziara ya kwanza lkn kwa jicho la tatu, wanafanya kazi kama bureaucrats wa serikali.

Wanashindwa kutafsiri majukumu yao kwa niaba ya chama. Wanashindwa kutafsiri supremacy ya chama over the govt system. Wanashindwa kukaa upande wa Wananchi ama kuvaa viatu vya wananchi. Wasipobadilika, itakuja kuwa Secretariat Mbovu kuwahi kutokea ndani ya chama cha mapinduzi.
Siku zote chama kinatakiwa kuwa na wananchi ili wakiunge mkono. Kwa kuwashawishi wananchi, chama chaweza kubadilisha team yake serikalini kutokana na hoja za wananchi.
Hata hivyo, kwa sababu ya siasa za uchawa wa kutafuta teuzi, chama tawala, watumishi wa serikali na vyombo vya dola huimba mapambio ya kusifu na kuabudu.
Utamaduni huu utabadilika pole pole kama wakiwepo viongozi wanaoona mbali (kwa vyama vyote).
Siasa lazima zijengwe kwa hoja zenye mantiki badala ya uchawa (wawepo watu wafuasi wa viongozi, siyo chawa, ambao wanaweza kujenga hoja).
 
Leo hii ukimuweka hapa Nchimbi na Makonda ktk sanduku la kura na uwaache wapige kampeni, Makonda atashinda mchana kweupe. Ninyi na akina Nchimbi msichokielewa ni kuwa Tanzania ya sasa siyo ile ya miaka ya tisoni! Na kumbuka, Dkt Magufuli alitembea kila sehemu ya hii nchi wakiwa na Dkt Samia.

Dkt Magufuli alikuwa sikio la kila mtanzania kila pahala alipotembelea na Dkt Samia alipendwa sana na watanzania baada ya msiba ila yeye ndiye aliyeharibu kwa kujionesha kiasi kwamba leo hii ukienda vijijini wanajua yeye ndiye aliyehusika na kifo na hilo mtu pekee aliyeanza kufuta hayo mawazo alikuwa Makonda.

Kibaya ya manchojidanganya nikudhani kura zinapigwa na watu wa mjini, hahaha hapana. Sisi wa mwenye mitandao siyo wapiga kura na mtu kama Mange na kundi lake siyo wapiga kura kabisa. Na ukitaka kujua Makonda anapendwa tizama alivyokuwa anajaza watu na wanamlilia.

Dkt Nchimbi na kundi lake ni kama sikio la kufa, maana wangeusoma mchezo walipaswa kuona namna nzuri ya kuendelea kumtumia Makonda CCM Kujisafisha na kuondokana na dhana potofu inayoendelea mtaani ya CCM kumuua Dkt Magufuli ili ufisadi uendelee.

Walimuuaje?
 
Ustaarabu wa Nchimbi uko wapi, tatizo lako ni uchawa. Hivi. Unajua kwanini Nchimbi alitupiwa ubalozini,, badala ya kudili na mtu angedili na matatizo yaliyopo.

Sasa hivi yupo busy kupanga Safi na kufikiriabinu chafu za ushindi. Nchimbi historia yake ya siasa imejaa makandokando mengi hivyo Hana usafi wowote wa kuanza ksifia.

Halafu jamaaa hana mvuto halafu yupo kama chizi fulan hivi

Zile nywele zake ni nyingi halaf zina mvi utasema ni nzi wamepandiana

Now hakuna anaefuatilia tena mambo ya uenezi
Ni kama umepoa

Makonda ilikuwa ni lazima uingie insta kusia leo kasema nn
 
Kwa ufahamu na akili yako ni pumba. Lakini unaweza kupingana na nature?

Unafikiri shetani naye hafanyi miujiza? Unadhani shetani hatendi na kuleta matokeo? Je, kwa kuwa analeta matokeo unadhani anaweza kuchukua nafasi ya Mungu?

And remember this. Two wrongs can't make right..!

Forget about Germany, New Zealand, India, Liberia and other nations. Makosa ya wengine hayawezi kutupa uhalali sisi nasi kufanya makosa kama hayo!
Wewe mpuuzi tu, Rais wako ni Samia Suluhu Hassan, kubali au kataa.

Shetani una uhakika gani hayupo hata hapo unapoishi nyumbani kwako?.

Usijihesabie sana haki ukiwa bado unapumua pumzi ya bure anayotupa Mungu.
 
Kwa nini Mh Nchimbi anaonyesha vita ya waziwazi kabisa hivi?! Hii si sawa kiuongozi, inaonyesha udhaifu. Kila wanapopita wanamtupia dongo Makonda. Wakati wao wanatakiwa kukinadi na kukijenga chama!
CCM hii ya sasa inatafakarisha mno! Nchimbi na Makala wako bize kumpiga madongo Makonda huku Kinana na wengineo wako bize wanapambana na Mwendazake utafikiri hao wanaowatupia madongo siyo/hawakuwa wanaCCM wenzao. Muda mzuri wa kunadi sera na mafanikio ya chama kwa wapiga kura unapotezwa kwa kuelezea ugomvi wao na personal grievances - tena kuelekea kwenye chaguzi! Si waitane waonyane huko halafu wakitoka huku nje waonyeshe umoja? Inashangaza sana!🖐
 
CCM hii ya sasa inatafakarisha mno! Nchimbi na Makala wako bize kumpiga madongo Makonda huku Kinana na wengineo wako bize wanapambana na Mwendazake utafikiri hao wanaowatupia madongo siyo/hawakuwa wanaCCM wenzao. Muda mzuri wa kunadi sera na mafanikio ya chama kwa wapiga kura unapotezwa kwa kuelezea ugomvi wao na personal grievances - tena kuelekea kwenye chaguzi! Si waitane waonyane huko halafu wakitoka huku nje waonyeshe umoja? Inashangaza sana!🖐
Kosa ni la CCM wenyewe kumpa nafasi Magufuli ya kuongoza nchi, hakukubaliana na wanachama wengi wenye kuziamini hulka za Kikwete. Mtifuano upo kati ya school of thoughts mbili zinazopingana ndani ya CCM.
 
Back
Top Bottom