Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Rilaxx, alwayz najua "nje" huwa inamaanisha nchi za magharibi zenye wazungu, sasa kama wewe ulimaanisha Iraq never mind.Tafadhali, hakuna mahala katika mada yangu nimetanabaisha neno wazungu.
Nimesema kutoka nje.
Huko nje yaweza kuwa ni popote pale.
Nipo makuru apa karbu na ukumbi wa jk convection but not ccmWivu kwa Chadema?
Usiandike kwa wasiwasi.
Karibu Dodoma mkuu.
Sisi tunajimwambafwai tu ila angalau katika ukanda wote wa maziwa makuu tunaheshimika.
Tishio nnalolizungumzia si silaha wala mabomu ni mbinu za kawaida kabisa.
Wala si mpango kutoka nje bali kuna watu wenye maslahi binafsi wanaokitumia chama hicho kama platform ya harakati zao. Sihitaji kutaja majina. Pita mtandaoni utawaelewa
Mbona mbogamboga wanawanunua na kuwapa vyeo na kuwaacha makanjanja wenu wakipigwa vumbi tu kama hawana strategists?Chadema ni chama cha siasa chenye wanasiasa ambao si makini.
Ni chama kilichokusanya watu wanojiita wanasiasa lakini hawana mbinu za kuishi kwenye siasa.
Miaka mitano ilopita Chadema walipata shida na hawakuweza kujinafasi na serikali ambayo iliongozwa na raisi ambae hakuwa tayari kuvumilia vurugu iwe maneno au vitendo.
Sasa yupo raisi Samia Hassan huu ndo ulikuwa wakati wa Chadema kuketi chini na kupanga mikakati mipya ambayo itaendana na mwendo wa serikali ya sasa.
Nimewahi kusema mara nyingi kuwa Chadema haina wanasiasa makini ambao wanaweza kutofautisha siasa za vurugu na siasa makini za majibizano ya hoja kwa ustaarabu.
Pia nimewahi kusema kuwa Chadema imekosa wanamkakati au "strategists" ambao wataisaidia kuogelea kwenye bahari ambayo imejaa maji mengi ya CCM na vifaa vyake vyote bunge, mahakama, polisi, jeshi na mamlaka zingine.
Mwanamkakati kazi yake kubwa ni kutumia kampeni ambazo zitahakikisha wapiga kura wanabadili mawaqzo yao juu ya chama kingine na kuwa tayari kuwapa kura.
Kazi zingine ni kufanya kura za maoni kuona kama chama kinakubalika kwa wapiga kura na kwa asilimia ngapi, kutumia teknolojia na mitandao ya kijamii kusambaza ujumbe halisi wa kisiasa na pia kuendesha harambaee za kuchangisha mifumo ya chama ili kupata fedha za kujiendesha.
Ni hili suala namba tatu ndilo lingeiwezesha Chadema kujenga ofisi yake maalum ya makao makuu ambayo ingekuwa inatambulika rasmi badala ya kajumba ka pale Ufipa Street.
Siasa ambazo Chadema inaendesha sasa hivi za kudai katiba mpya haziwezi kuiyumbisha CCM hata kwa dawa.
Sanasana ni kwa wanasiasa wa Chadema na wafuasi wao kuketi chini na kupanga mbinu mpya badala ya maandamano ambayo ni dhahiri yatapata taabu kuruhusiwa na polisi.
Katiba ndo msingi wa sheria na hutoa mwongozo namna serikali inavyotenda shughuli zake za kila siku.
Hivyo katiba ya nchi ni muhimu na pia utaratibu mzima wa kutaka kuibadili pia ni muhimu.
Bado Chadema haiweki wazi kuwa yataka katiba mpya au mabadiliko ya katiba tulio nayo.
Lakini Chadema ingeweza kuketi na kushawishi ili kupata washirika kutoka CCM kwa maslahi ya taifa na kutaka katiba ifanyiwe marekebisho kuwa wabunge wasijiongeze mishahara kiholela.
Serikali ya awamu ya sita yapaswa kusikiliza dai la tume huru. hili dai ndo msingi wa vurugu zinazoweza kujitokeza hapa nchi ama leo au siku za usoni.
Kuna dalili zote zionyeshazo kuwa nguvu kubwa kutoka nje ya nchi ipo nyuma ya hizi kelele za katiba mpya au tume huru.
Suala ni je ni kelele za msingi au ni nguvu tu ya kutaka kuhakikisha CCM inaondolewa madarakani?
Kabla ya uchaguzi wa 2015 CCM ilikuwa imefikiriwa katika majukwaa ya kimataiofa kuwa ni chama kilichohitaji kuondoka kupisha chama kingine ambacho kingekuja na mawazo mapya.
Ni pale CCM ilipompata hayato John Magufuli na baada ya miezi sita ya kwanza ndipo majukwaa hayo yalipobaini kuwa CCM huenda imejigawa ila ni ileile.
Kelele za Katiba mpya au tume huru ya uchaguzi hazitaisha leo.
Ila katiba mpya si rahisi kuipata bila kuwepo kura ya maoni ambayo ndo itatoa mwanga kuwa wananchi wanataka nini.
Hivyo kwa maoni yangu naona Chadema na wanaharakati wote wanapaswa kupigania kuwepo kura ya maoni.
Pia kuhusu tume huru ni kwamba ni lazima wabunge wa upinzani bungeni wawe na ushawishi wa kuweza kuleta bungeni wazo la kuundwa kwa tume huru ya uchaguzi ambayo ndo itasimamia zoezi la uchaguzi nchini na kuhakiksha vyama vyote vya siasa vinahakikiwa vyanzo vya0o vya fedha.
Ili zoezi la uchaguzi lipate heshima ni lazima kuwepo tume huru ya uchaguzi ambayo pia itasimamiwa na Bunge kupitia kamati ya siasa.
Katika hali ya sasa ni vigumu sana kupata tume huru ya uchaguzi endapo wabunge wa upinzani hawazidi theluthi mbili ya wabunge.
Idadi kadhaa ya wabunge wakija na hoja na wakazidi theluthiu mbili hiyo huwa ni shida tayari na ni lazima wazo lao lisikilizwe.
Ndo maana mwaka 1993 Marehemu Njelu Kasaka ambae alikuwa mbunge wa jimbo la Lupa huko Chunya akiongoza kundi la wabunge 55 kudai serikali tatu na serikali ya Tanganyika alizimwa na hayati Mwalimu Nyerere kwa kuwa tu ndie alikuwa mlezi wa chama na hoja yake ya kupinga hoja ya serikali tatu ilikuwabaliwa tu kwa kilichoonekana ushawishi wa kisiasa badala ya hali halisi.
Hivyo kwa maoni yangu napendekeza Chadema wajikite katika kujiandaa kuchukua majimbo ambayo yatawasaidia kuongeza idadi ya wabunge kule bungeni ambao wanaweza kuweka hoja yenye nguvu.
Hivi ndivyo chama cha MCP cha Malawi kilivyojipanga kukitoa madarakani chama cha DPP na ikawa hivyo. MCP walihakikisha wanapata wabunge wengi zaidi ili kuweza kuunda serikali na bunge.
Serikali isipuuzie hizi harakati za Chadema maani hii ni mikakati ya muda mrefu katika kuhakikisha nchi inaingia kwenye matatizo endapo matakwa yao hayatatimizwa.
Watanzania tunasifika kwa woga na upole kiasi cha kushindwa kuhioji hata uhandisi jamii unoendelea hivi sasa wa kuhakikisha miradi ya maendeleo inadhurika na isiendelee.
Katika duru za usalama, uhandisi jamii waweza kutafsiriwa kuwa ni kitendo cha kumshawishi mtu kufanya kitendo ambacho kitanufaisha au kutonufaisha maslahi yake.
Mtu au watu hao ni pamoja na matarishi, makatibu muhtasi au mamesenja na maafisa masijala.
Nina imani serikali yetu itakuwa makini na itatumia busara katika kujadiliana na Chadema ambao sasa hivi wamekuja kwa kasi.
Pia sina shaka na mazee na mkuu wao Mabeyo na wanakamati wengi ambao bado wanatatizwa na kinachoendelea.
Mungu ibariki Tanzania.
Mimi si mwanachama wa CCM au mfuasi wake.
Naangalia siasa za nchi yetu kutokea upande ulio huru.
CCM wanaangalia kitu chaitwa potential kutoka kwa haohao mbogamboga.Mbona mbogamboga wanawanunua na kuwapa vyeo na kuwaacha makanjanja wenu wakipigwa vumbi tu kama hawana strategists?
Hawapo na ndio maana mliwanunua akina Joshua Nasari na kuwabandika vyeo fasta.CCM wanaangalia kitu chaitwa potential kutoka kwa haohao mbogamboga.
CCM ina hazina ya strategists ni wengi mno.
Chadema ina safari ndefu na ngumu sana huko mbele.
Ila vurugu na maandamano si suluhisho na matatizo hayo.
Mimi ni mpenda mabadiliko na ni mwanaharakati.Wala huhitaji kusema ww ni nani, inawezekana huna kadi ya ccm kwakuwa haina maana kubwa kwenye majukumu yako ya siku kwa siku. Lakini uko wazi peupe kiitikadi.
Kama ni kupewa hela na wazungu, kuanzia serikali, taasisi mbalimbali hadi watu binafsi wanapewa wala sio siri. Huo ukumbi wa ccm hapo Dodoma ccm wamejengewa na wachina, ndio maana tender karibia zote wanawapa, huku viongozi wakilamba 10% zao kila mradi. Labda utafute wasiojua lolote ndio uwaambie hiyo propaganda mfu.Siwezi kuzijata hapa kuna kanuni kadhaa zinanizuia.
Aliyezifikisha hapa siasa za Tanzania ni ccm baada ya kupoteza mvuto kwa wananchi.Mimi ni mpenda mabadiliko na ni mwanaharakati.
Nilikuwa pamoja na akina BAK hapa enzi zetu.
Ningekuwa na uwezo wa kuanzisha chama ningefanya hivyo.
Ila siasa za Tanzania zilipofikia kwa sasa ni hatari sana.
Wachumia tumbo sio strategists wa lolote. Sifa za bandia na nguvu zote za ccm ziko kwenye nguvu ya rais kwa kutumia state machinery. Ccm mwenyekiti wake akipoteza cheo cha urais, TLP Itakuwa afadhali kuliko ccm.CCM wanaangalia kitu chaitwa potential kutoka kwa haohao mbogamboga.
CCM ina hazina ya strategists ni wengi mno.
Chadema ina safari ndefu na ngumu sana huko mbele.
Ila vurugu na maandamano si suluhisho na matatizo hayo.
KIjana Joshua nasari ana akili sana na ana potential.
NIlimsoma uzuri pale London nilipokutana nae akiwa masomoni na kumsaili.
10% si suala geni hata huko nje wanafanya hizi deals na hata waligunduliwa huzimwa kimyakimya.Kama ni kupewa hela na wazungu, kuanzia serikali, taasisi mbalimbali hadi watu binafsi wanapewa wala sio siri. Huo ukumbi wa ccm hapo Dodoma ccm wamejengewa na wachina, ndio maana tender karibia zote wanawapa, huku viongozi wakilamba 10% zao kila mradi. Labda utafute wasiojua lolote ndio uwaambie hiyo propaganda mfu.
Siwezi kuzijata hapa kuna kanuni kadhaa zinanizuia.
10% si suala geni hata huko nje wanafanya hizi deals na hata waligunduliwa huzimwa kimyakimya.
Ndo maana hata pale UK waziri wa afya akawapa hizo tendes rafiki zake kusambaza vifaa vya PPE na kadhalika.
Ila Chama cha Boris ni chama kama vingine tu hufanya mambo kama CCM zabuni kutolewa kwa kujuana na kadhalika.
Cha msingi kama wanavyosisitiza ni kuona maendeleo yanafanyika kama huduma za afya, mashule na huduma za jamii.
Ila wenzetu pia wao wameendelea zaidi kwa kuwa kila mwananchi analipa kodi kuanzia ule ya maendeleo ya unapoishi Council au Municipal Tax hadi kodi ya mapato.
Sisi Tanzania bado hatujafikia huko si wananchi wote wanalipa kodi.
Wafanya biashara wengi wamekataa kulipa kodi sasa maendeleo yatapatikana vipi?