Yanayoendelea sasa hivi nchini ni hatari kwa uhai wa chama kilichopo madarakani na baadhi ya viongozi waliopo Serikalini

Yanayoendelea sasa hivi nchini ni hatari kwa uhai wa chama kilichopo madarakani na baadhi ya viongozi waliopo Serikalini

Samia wakati madudu yanafanyika alikuwa wapi?
Kama unamjua vizuri magufuli sitarajii uulize maswali ya aina hiyo.
Yani maovu ya magufuli.kutotaka kuweka hadharani report za Cag,akampokonya cheo Assad kisa alisema ukweli.akamweka mtu kwa sharti aseme tu kile anachokotaka yeye,mtu anaisemea mahakama kwamba muhukumu huyu mwachie huyu..

Madhambi ya magu mnataka kumbebesha mama wa watu wakati ukute hakushiriki hata maamuzi..

Tafuta jingine
 
Mama samia asingeweza kufanya lolote vinginevyo wangemtundulisuu mapema ...


Harafu mtoa mada usikaze ubongo mjinga wewe ,inamaana ulikuwa huoni yanayowakuta watendaji wake wanaoenda kinyume na yeye ....


Mfano cag aliyepita assad ..

Huyo magu alijitengenezea bomu mwenyewe wacha limlipukie huko huko aliko ...
Kwahiyo kujiuzulu alishindwa kama alikuwa hakubaliani na maovu?
 
Angeanzaje kumsema mhishimiwa mkuu wa malaika na alivyokua anasumbuliwa na maukimwi angeweza hata kumvua shungi hadharani, hatakiwi kujiudhulu anatakiwa aumuongezee ulinzi CAG ili aendelee kuanika madudu ya hata hao aliowateua tujue tu rangi zao halisi unafiki haukaagi muda unajitokeza fasta tu kama ilivyo sasa
 
Kama unamjua vizuri magufuli sitarajii uulize maswali ya aina hiyo.
Yani maovu ya magufuli.kutotaka kuweka hadharani report za Cag,akampokonya cheo Assad kisa alisema ukweli.akamweka mtu kwa sharti aseme tu kile anachokotaka yeye,mtu anaisemea mahakama kwamba muhukumu huyu mwachie huyu..

Madhambi ya magu mnataka kumbebesha mama wa watu wakati ukute hakushiriki hata maamuzi..

Tafuta jingine
Makamu wa rais asiyeshirikishwa na akabaki madarakani bila kujiuzulu,anafaa kuwa rais?
 
JAMANI MAMBO YA KUNYWA VIROBA ASUBUHI SIO SAHIHI...MH SAMIA AJIUZURU KWA LIPI ALIKUWA MAKAMU WA RAISI NA YUPO WAZIRI MKUU AMABAYE NDIYE MTANDAJI NA CHIEF SECRETARY ....MAMA CHAPA KAZI ACHANA NA WASIOJIELEWA
 
Kwa ufisadi mkubwa ulioibuliwa na CAG uliofanyika awamu ya tano, makamu wa Rais wa kipindi hicho anakuwaje msafi ilihali ndiye aliyekuwa mtendaji wa karibu zaidi na Rais?

Tukiacha siasa, ni dhahiri kabisa haya yote yametendeka kutokana na uzembe wa mwendazake na wasaidizi wake akiwemo Rais wa sasa.

Msemakweli ni mpenzi wa Mungu.
Sijui, ila nasikia harufu ya "chembe chembe za chuki binafsi hapa". Dawa sio kwa uongozi wa sasa kujiuzulu, ila DAWA ni kuchukua hatua stahiki, muafaka na kwa muda sahihi DHIDI ya WATUHUMIWA WOTE, yaani wapewe nafasi ya kujibu hoja hizo za CAG hata kama wako nje ya mfumo wa uongozi na serikali. Kuwajibishwa NI LAZIMA kwa misingi, taratibu, kanuni na sheria za nchi.
 
Angeanzaje kumsema mhishimiwa mkuu wa malaika na alivyokua anasumbuliwa na maukimwi angeweza hata kumvua shungi hadharani, hatakiwi kujiudhulu anatakiwa aumuongezee ulinzi CAG ili aendelee kuanika madudu ya hata hao aliowateua tujue tu rangi zao halisi unafiki haukaagi muda unajitokeza fasta tu kama ilivyo sasa
Hapo unabashiri tu, lakini mtu aliye imara kujiuzulu hawezi kushindwa.
 
Kwani wewe hautaki ukweli usemwe?, haya ndio madhara yakuhodhi kila kitu wewe uwe raisi wewe uwe mtunga sera wewe wewe uwe mshauri wewe uwe mfuatiliaji ili baadae wewe wewe upewe sifa. Sasa tunasema hivi na madudu yote apewe yeye.

Watanzania tumepigwa sanaa
 
Kumbuka raisi Samia alikuwa makamu wa raisi ktk serikali hiyo inayosemekana kuwa ilifanya ufisadi mkubwa, waziri mkuu pia na bila kuwasahau baadhi ya mawaziri ambao pia wapo ktk serikali hii mpya ya mama Samia. Ikiwa shutuma hizi zitaendelea na hao niliowataja hapo hawatojiuzulu nyazifa zao serikalini, basi 2025 CCM ijiandae kwa anguko kubwa, japo wengi hawalioni hili
Makamu qa Rais hana Say kwaio lawama zinaendelea kwenda kwa Mwendazake
 
Zabayanga Naye Alikuwa TRA Baadaye Wizara Ya Fedha Na Mipango Sasa Hivi Ndiyo Anazurura Kule Hombolo
😅😀
 
Back
Top Bottom