Yanayoendelea Zanzibar tusubiri majibu ya Wahanga na kuzaa gharika

Yanayoendelea Zanzibar tusubiri majibu ya Wahanga na kuzaa gharika

Zanzibar ni nchi ya kiislamu hivyo ni lazima ufuate sheria za kiislamu, hivyo kwa wale wanaokula mchana hadharani mwezi wa ramadhani lazima wapigwe bakora. katiba yao ndio isemavyo tofauti kabisa na katiba ya bara yenye ukiristo na uislamu
 
Allah anapodanganya;

9:30 Na Mayahudi wanasema: Uzeir ni mwana wa Mungu. Na Wakristo wanasema: Masihi ni mwana wa Mungu. Hiyo ndiyo kauli yao kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya walio kufuru kabla yao. Mwenyezi Mungu awaangamize! Wanageuzwa namna gani hawa! 30
 
Zanzibar ni nchi ya kiislamu hivyo ni lazima ufuate sheria za kiislamu, hivyo kwa wale wanaokula mchana hadharani mwezi wa ramadhani lazima wapigwe bakora. katiba yao ndio isemavyo tofauti kabisa na katiba ya bara yenye ukiristo na uislamu

Katiba yao ipi hiyo? ibara ya ngapi inasema Zanzibar ni nchi ya kiislamu? usipotoshe watu hapa mkuu.
 
Allah anapodanganya;

9:30 Na Mayahudi wanasema: Uzeir ni mwana wa Mungu. Na Wakristo wanasema: Masihi ni mwana wa Mungu. Hiyo ndiyo kauli yao kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya walio kufuru kabla yao. Mwenyezi Mungu awaangamize! Wanageuzwa namna gani hawa! 30

Hivi haya maneno ni ya nani na anamwambia nani? Na huyu Mungu anayeombwa awaangamize watu hawa ni Mungu yupi? Tangu lini Mayahudi wakawa na mtu wanayemwita "mwana wa Mungu"? Ezra hakuna kitabu chochote kinachomtambua kama "mwana wa Mungu". Wakati mwingine tumieni akili kuhoji. Sio mnaambiwa kwa mungu kuna danguro la mabikira, mnaamini tu.
 
Mbona uulizi kwanini makanisa mengi sana huko Tanzania Bara yanazuia kwa nguvu zote waumini kuingia na vimini wakti wa ibada? Je hujui kwa nini?


Pamoja na kuzuia lakini hawapigwi mkubwa wangu, kufunga ni nafsi yako na mungu wako kwann upate tabu na mtu anayekula?
 
Kwani zanzibar kufunga wameanza leo??

Ukristo zanzibar umeanza leo??

Tusisikie hayo mambo miaka yote tuje tuskue leo??

Hivi Kukaa bila kuwachokonoa waislam hamjiskii raha.

Hii id ya jason bourne nakumbuka Mods hapo awali walishawahi kuiuunganisha na Yericko Nyerere.

Hivi huyu jamaa anasumbuliwa na nin hasa??

Kutwa kucha kuanzisha ids za kijinga na kuanzisha mijadala isiyo na tija.

Mods angalieni hivi vitu baadae huja kusababisha taharuki zisizo na maana.

Hii post yako itaondolewa sasa hiviii.
 
Hivi polisi kazi yao ni nini?

Au ni ruhusu kupiga watu???

Leo ndiyo unatambua Polisi kazi yao ni kulinda wahalifu? Hasa wezi wa Mabilioni na kuacha kazi yao ya kulinda Usalama wa raia?

Wewe siku zote unasherekea Polisi kuacha majukumu yao na kufanya kazi ya Siasa kwa kuhakikisha Upinzani unakufa na viongozi wao wanabambikiwa kesi?

Mara ngapi wahalifu wanajitamba na mabomu yanalipuliwa ovyo huku polisi wakifanya siasa?
 
Kanisa haliendi mitaani na kuzuia watu kuvaa vimini. Msomi kama wewe mbona hili unalijua sana?

Mkienda Ulaya au USA na Ramadhani zenu, mnaona mabaya zaidi ya hayo ya Tanzania. Summer kama hii, watu wanakunywa pombe nje nje na hamlalamiki, Vimini nje nje na Vi-Tishrt vya kuchokoza. Mkifika tu Tanzania, mnajifanya mmekuwa watu wa dini. Mbona nchi kama Mali, Guinea, Senegal nk kwenye Waislaam wengi sana, hii kulazimishana haipo? Waliletewa sharia watu wa Mali, wakaipinga kwa nguvu zote. Wakadai kabisa, wao dini hakuna kulazimishana.

Fedha za mafuta zinasumbua watu. Nasubiri na sisi tuanze kuchimba na tuwe kama Angola - Misikiti (na Makanisa, Sinagogi ......) ni marufuku Tanzania. Halafu tutaona huyo Mungu, Jehovah, Budhah, Allah nk nk kama kweli atakufa. Mie naamini kuwa, yeye ana nguvu zaidi ha hahitaji kutetewa na kibinadamu alichokiumba mwenyewe na kukipa pumzi na leo kinajifanya eti kinaweza kumpigania Allh.


Mbona uulizi kwanini makanisa mengi sana huko Tanzania Bara yanazuia kwa nguvu zote waumini kuingia na vimini wakti wa ibada? Je hujui kwa nini?

 
U guys stop insulting each other,Tunakoelekea tunapoteza uzalendo,we fight for nothing coz in the end no one atakua mshindi.

wkt mwingine tunakaribisha lugha ambazo hata vitabu vyetu vyote vya dingpg visingeruhusu itumike for clarification!!

Mungu ipe mwongozo nchi ya tz na uwafumbue wa tz kwamba adui mkubwa ni ignorance na poverty.
 
Mbona uulizi kwanini makanisa mengi sana huko Tanzania Bara yanazuia kwa nguvu zote waumini kuingia na vimini wakti wa ibada? Je hujui kwa nini?


Kunatofauti kubwa sana kati ya kunyimwa kuingia kwenye kanisa(private place) ukiwa umevaa kimini na kuzuiwa kula kwa mamamtilie (public place) na kuwa assaulted kwa kuchapwa viboko. Shirikisha ubongo we mburula
 
wewe kama bado umelala wenzako wameamka,unalotakiwa kujua ni kuwa Zanzibar ni nchi yenye bunge lake,serikali yake na mipaka kamili na Kikwete akienda Zanzibar haina tofauti kama akienda Kenya

Haujajibu swali langu, nioneshe ni sehemu gani ya katiba ya Zanzibar inasema Zanzibar ni nchi ya kiislamu.
 
What goes around comes around?

Hii mitusi yote hapa ndani kwaajili ya nani hasa, come ooon guys calm down please

BACK TANGANYIKA
 
Zanzibar ni nchi ya kiislamu hivyo ni lazima ufuate sheria za kiislamu, hivyo kwa wale wanaokula mchana hadharani mwezi wa ramadhani lazima wapigwe bakora. katiba yao ndio isemavyo tofauti kabisa na katiba ya bara yenye ukiristo na uislamu

Tuambie kipengele gani cha katiba ya zanzibar kinasema uliyo yasema?
 
Mbona haijatokea gharika Tanganyika ambako wenye macho mekundu wanauliwa, au maalibino kukatwa viungo vya mwili na watu kuchunywa ngozi!!!????

Au katiba ya TZ inaruhusu haya? Na mbona hauyashangai haya na badala yake unakuja kushangaa watu wanaopigwa bakora ZNZ kwa kosa LA kula mchana wa mwezi wa Ramadhani!!??? Acha unafiki name kumbuka hicho kitabu chako unachokifuata kinasema ukitaka kutoa kibenza kwenye jicho la mwenzako basi anzia kutoa boriti kwenye jicho lako

Lakini sikushangai sana maana mfumo kristo ndivyo ulivyokulea kulifanya kubwa lolote lile ambalo waislamu watalifanya name kuliona dogo lolote lile ambalo wakristo watalifanya hata kama ni mapdri kulawiti watoto

Hata masheh na ma ustaadh,wanaofundisha madrasa,wanabaka pia,mfano tukio lililotokea LINDI,TUNDURU,jibu hoja sio kuleta cheap politics
 
Kwani zanzibar kufunga wameanza leo??

Ukristo zanzibar umeanza leo??

Tusisikie hayo mambo miaka yote tuje tuskue leo??

Hivi Kukaa bila kuwachokonoa waislam hamjiskii raha.

Hii id ya jason bourne nakumbuka Mods hapo awali walishawahi kuiuunganisha na Yericko Nyerere.

Hivi huyu jamaa anasumbuliwa na nin hasa??

Kutwa kucha kuanzisha ids za kijinga na kuanzisha mijadala isiyo na tija.

Mods angalieni hivi vitu baadae huja kusababisha taharuki zisizo na maana.

Waialam na wakristo wana haki ya kula mchana nje kama waislam walivyo na haki ya kufuturu nje kama sheria zinafuatwa tanzania. Alie chapwa anaweza kwenda maakamani kuishitaki serekali kwa hili
 
ivi kuna tatizo gani zanzibar ikiwa nchi ya kiislamu

Hakuna tatizo.Isipokuwa wamuachie Mungu anayeweza kuhukumu kwa haki kuwahukumu wale wanaomkosea kwa vile ni Mungu pekee anaye weza kuhukumu kwa haki na si binadamu ambae ni mkosaji kama binadamu mwenzake.
 
Naungana na mtoa hoja kwamba hawa wajinga wachache wanaotia doa uislam kwa vitendo vilivyo nje ya mafundisho ya uislam serikali ni lazima iwaangalie na kuwadhibiti kwani wanakotupeleka ni kwenye vilio na kusaga meno.hali ya chuki za kidini na kisasi ikishamiri ktk jamii yetu ya kitanzania kitachofuata ni mauaji ya kimbari.lakini waislam lazima tujifunze kuishi kwa kuvumiliana na siyo kujifanya mahakimu wa kila jambo ktk hii dunia.tukihukumu sisi mungu atafanya kazi gani?tuache kuwa wa kwanza kuanzisha machafuko ambayo baadae yana-back fire upande wetu tunabaki kulalama kama ilivyotokea huko jamhuri ya afrika ya kati.
Kuhusu kufunga wako watu ambao hawana sifa ya kufunga kama vile wagonjwa,wasafiri,watoto nk,hawa wote lazima wale chakula.lakini pia kufunga saumu pamoja na maana zingine ni kujizuia kula na sio kukataza wengine wanaostahili kula wasile,wataishije sasa?mgonjwa hata kama ni muislam anatakiwa ale ndipo atumie dawa,msafiri hana ndugu anahitaji ale munafunga migahawa!mtoto mdogo anahitaji ale,mwanamke aliye ktk hedhi pia hatakiwi kufunga,sasa kuzuia watu hawa kula kwa kuwapiga na kuwafanyia vurugu hayo siyo mafundisho ya islam.ifike wakati serikari iache siasa katika mambo yanayotishia usalama wa nchi na iwaadhibu wahuni hawa bila huruma.
 
Back
Top Bottom