Yanayofanyika viwandani Tanzania ni utumwa. Kazi ngumu, maslahi duni. Serikali haina mpango na wananchi wake, inachoangalia ni kodi tu

Someone out there woke up today thinking the government cares about them🤣🤣
Do you, https://jamii.app/JFUserGuide the gvt
 
Ngozi nyeusi tuna laana sana chief.
Kuna ajali za kutisha huko kwenye viwanda ,we acha tu , hata safety gears Tu ,Hamna
Kuna ajali nimewahi shuhudia mwanamke anagongwa na kuvunjwa mguu na yale meno ya fork lift za kubebea mizigo kutoka kwenye production line kwenda warehouse ,na hakupewa hata fidia au matibabu ya maana , ni ulemavu wa kudumu

Sent from my Nokia 6.2 using JamiiForums mobile app
 
Kule usalama wako ni juu yako kama shughuli inahatarisha usalama bora ukache tu , watu wana jidespose ktk heat kubwa ya mashine 12hrs mpaka maini yanaiva bora ukapike chapati kariakoo
 
Kusema kweli ninepita viwanda fulani hapo Matumbi, inasikitisha sana hali ilivyo........ Afya za wafanyakazi hazijazingatiwa kabisa
Unakuta watu wanameza vumbi na kugongwa na joto kali kwenye production plants kama mchwa mpaka ukiwaangalia moyo unaenda mbio unatamani kuzimia ,ila wao ndio mwanzo mwisho asubuhi saa mbili mpaka saa tatu usiku

Sent from my Nokia 6.2 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna mpango mzuri kama wa kuamua kulima asee unakuwa uhuru wa kujifanyia mambo yako kwa uhakika
 
Inasikitisha sana
Mkuu,ndiyo maana magonjwa kama cancer yanaspidi kubwa katika jamii yetu,kuna kiwanda cha sufuria hapo Matumbi staki kukitaja jina,hali ni mbaya sana, OSHA wakienda wanaishia kwenye management tu wanachukua bahasha bila hata kufanya ukaguzi
 
Ni balaa , tena hao maofisa wa OSHA ndio wazee wa rushwa , wazee wa kubeba vibahasha vya kaki


Sent from my Nokia 6.2 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…